Red Giant
JF-Expert Member
- Mar 9, 2012
- 15,658
- 20,889
Nimerudi tena na hii hoja dhidi ya matumizi ya kiingereza kama Lugha ya kujifunzia.
Umewahi soma riwaya za kiingereza na kiswahili? Kama umewahi, utagundua kuwa utatumia muda mrefu sana kusoma riwaya ya kiingereza kuliko ya kiswahili. Riwaya ya kiswahili unayoweza kusoma kwa siku mbili, ikiwa kwa kiingereza unaweza tumia siku kumi na zaidi. Kusoma machapisho ya kiingereza kunaumiza sana akili kuliko kusoma ya Kiswahili.
Na kujiumiza huku hakuna manufaa yoyote, mfano kama ni maarifa ya shule unaweza yapata yaleyale kwa kiingereza na kwa kiswahili. Mateso haya yanafanya watoto wengi wakate tamaa ya kuendelea na sekondari, wafeli, wasijisomee textbooks, na waishie kukariri. Inasemwa kuwa ni 15% ya wanafunzi wa sekondari ndiyo wanaelewa kiingereza kiasi cha kuweza kuitumia kama lugha ya kujifunzia.
Kosa kubwa kwenye elimu yetu ni kutumia kiingereza kama lugha ya kujifunzia. Na ndilo tatizo namba moja la elimu yetu. Tukirekebisha mambo yote, lakini bado tukiendelea kujifunza kwa kutumia lugha tusiyoielewa, hatutaelimika.
Nimewahi sema kuwa, kwa kuendelea kutumia kiingereza kama lugha ya kujifunzia, tunakuwa kama mtu aliyepotea njia lakini anaona uvivu kurudi nyuma.
Kwanini hatutumii kiswahili kama lugha ya kujifunzia katika ngazi zote za elimu?
Umewahi soma riwaya za kiingereza na kiswahili? Kama umewahi, utagundua kuwa utatumia muda mrefu sana kusoma riwaya ya kiingereza kuliko ya kiswahili. Riwaya ya kiswahili unayoweza kusoma kwa siku mbili, ikiwa kwa kiingereza unaweza tumia siku kumi na zaidi. Kusoma machapisho ya kiingereza kunaumiza sana akili kuliko kusoma ya Kiswahili.
Na kujiumiza huku hakuna manufaa yoyote, mfano kama ni maarifa ya shule unaweza yapata yaleyale kwa kiingereza na kwa kiswahili. Mateso haya yanafanya watoto wengi wakate tamaa ya kuendelea na sekondari, wafeli, wasijisomee textbooks, na waishie kukariri. Inasemwa kuwa ni 15% ya wanafunzi wa sekondari ndiyo wanaelewa kiingereza kiasi cha kuweza kuitumia kama lugha ya kujifunzia.
Kosa kubwa kwenye elimu yetu ni kutumia kiingereza kama lugha ya kujifunzia. Na ndilo tatizo namba moja la elimu yetu. Tukirekebisha mambo yote, lakini bado tukiendelea kujifunza kwa kutumia lugha tusiyoielewa, hatutaelimika.
Nimewahi sema kuwa, kwa kuendelea kutumia kiingereza kama lugha ya kujifunzia, tunakuwa kama mtu aliyepotea njia lakini anaona uvivu kurudi nyuma.
Kwanini hatutumii kiswahili kama lugha ya kujifunzia katika ngazi zote za elimu?