Kwanini tunampongeza na kumsifia hata sisi wafuasi wa Vyama pinzani?

Mtu akiwa Rais hata kwa kupindua nchi Ni Rais huyo,

Akiwa Rais kwa kuchaguliwa kidemokrasia Ni Rais huyo,
Akiwa Rais kwa kuiba kura ni Rais huyo.

Mtu aliyekalia kiti Cha Urais Ana Upanga wenye ncha Kali,Ana Maamuzi .

Hivyo akifanya mambo mazuri yanawafikia wote wasio wapinzani na wapinzani,
Akifanya mambo mabaya yanawapata watu wote wapinzani na wasio wapinzani.

Kwa muktadha huu sisi Watanzania kwa pamoja bila kujali chama tulipata mateso sawa kwa miaka mitano iliyopita,na Sasa mama anatuletea faraja Watanzania wote wanaCCM na ambao sio Wana CCM.

Hivyo nafuu ya mateso tunayoipata tuna Haki ya kumpongeza,Kwa sababu anafanya vizuri kuliko yule Bingwa.
Akikosea tutamkosoa,sisi wapinzani sio wanafiki.

Tukipinga mnasema kila kitu tunapinga,
Tukisifu au kupongeza mnasema tumekwisha.

Hata hivyo Leo hii ukija uchaguzi Mkuu Mimi Lee nitaikataa CCM na mambo yake yote,
Na fahari zake zote,
Na hila zake zote.

Tunaomba katiba nzuri na mpya,
Tuanomba tume huru ya uchaguzi,
Tunaomba Uhuru wa shughuli za kisiasa.
Tunaomba kuepuka gharama za u haguzi mama abadikishe Katina pasiwepo na uchaguzi 2025 kwani tunamkubali wote hata sisi wa upinzani
 
Nyie ni bendera fuata upepo!
Mtu hawezi kutekeleza baadhi ya Mambo aliuoyapigia kelele siku zote za kampeni Genius Tundu Lisu,halafu leo mama anatekeleza tusimppngezekweli?,
Alipigia kelele Kodi za kibabe,Samia katoa suluhisho,
Alipigia kelele ukwapuaji fedha kwenye akaunti za wafanyabiashara Samia katoa suluhisho,
Tundu Lisu kapigia kelele wafanyabiashara na wawekezaji kukimbia kwa sababu za unyanyasaji,Samia katoa suluhisho,
Tundu Lisu kapigia kelele kufungiwa vyombo vya habari,Samia katoa suluhisho,
Sasa Kama haya Genius Tundu Lissu aliyapigia kelele wakati wa kampeni na Mama leo anayafanyia kazi tuache kimsifu kweli kwa faida ya Taifa?
Wewe Taga najua unateseka Jiwe kafutika yeye na Mambo yake yote kwa Kasi ya 5G.
 
Anatekeleza ilani yetu na maono yetu kwa asilimia 110
Tena umenikumbusha haya yote anayoyatekeleza Ni Yale Genius Lissu alikua anayapigia kelele wakati wa Kampeni.
Kweli aisee.
Genius Lissu alipigia kelele
Vyombo vya habari kufungiwa na yule mwovu,
Alipigia kelele Kodi kukusanywa kibabe,
Alipigia kelele wafanyabiashara kufa kijiua kuhamisha biashara na fedha zao kupigwa kwenye akaunti,
Hakuana uovu Genius Lisu aliacha kukemea.
Kwa hiyo mama anatekeleza hoja Za CDM.
Yule mwovu aligoma,Sasa utaachaje kumpongeza Samia?
 
Wasukuma mnaumia sana Mama akipata uungaji mkono toka kwa Wapinzani,tunajua kabisa mnayo movement yenu ya kumhujumu Mama lakini kamwe hamtafanikiwa mashetani wakubwa nyie.
Washindwe. Mama kamtanguliza MUNGU hivyo ana haraka zote na wala hajajipa nafasi ya MUNGU kuwa yeye hakosei ndio akikosea anarekebisha bila kuona aibu anajua ye ni binadamu tu na sio mkamilifu.na atafanikiwa kwakuwa anaenda kuruhusu kukosolewa Ili kujirekebisha
 
Ni punguani peke yake ndiye anaweza kumsifia Mama kwa sababu bado anaongoza nchi kwa kutumia zile sheria kandamizi za Magufuli.Nchi huwa inaongozwa kwa mujibu wa sheria na wala siyo kwa maneno matamu na ahadi za matumaini.Kuongoza nchi kwa maneno matamu na ahadi za matumaini wakati sheria ni mbovu na kandamizi hilo huwa ni changa la macho!
Ameshasema sheria kandamizi zote zipitiwe upya
 
Mie ni Chadema damu damu lakini KAMWE sitaona aibu yoyote kumpongeza Mama yetu pale atakapofanya mazuri na kumkosoa pale atakapovurunda.
Mama hata mwezi hajamaliza lakini tayari tunasikia kauli zenye utofauti mkubwa sana na zile za dhalimu jiwe. Mwenyezi Mungu ashukuriwe 🙏🏾
By the way Mama anaonekana aliyoyafanyia kazi hadi Sasa niYale yote yaliyopigiwa kelele na Genius Tundu Lissu wakati wa Kampeni.
Ambapo gaidi yule aligoma kabisa kuwaondoa,Sasa Mama wa watu kawa muungwana,Sasa kwa Nini tisimsifie?
Kama Ni ilani ya CCM mbona alipokuwepo mwovu yule hakurekebisha?
 
M
Kwa UFINYU wa akili yako kumbuka Tanzania ni yetu SOTE si Tanzania ya Magufuli. Fungua akili yako.
Mkuu hivi vijamaa vina roho mbaya Sana,vijitu hivi ndio vilikua vinawaza kumchoma Genius Lisu sindano ya sumu halafu kwa pamoja kabisa Tena kwa moyo mkunjufu kabisa hadharani vikashangilia.

Na vile vikubwa vyao kile bungeni vilikubaliana kabisa Zito akionekana nchini auwawe vyote kwa pamoja mbele ya kamera na hansadi ikinukuu pamoja na spika vikakubaliana kwa pamoja kwa kupiga makofi ndiooo zito afeeee.

Hivi vijamaa Sasa hivi vinaishi kwa mashaka kuliko tulivyoishi sisi wenye mawazo mbadala.
Tuviombee msamaha kwa Samia.
Mfano hai Ni kile kibwana,kikuu Cha Vijiccm.
 
Ni punguani peke yake ndiye anaweza kumsifia Mama kwa sababu bado anaongoza nchi kwa kutumia zile sheria kandamizi za Magufuli.Nchi huwa inaongozwa kwa mujibu wa sheria na wala siyo kwa maneno matamu na ahadi za matumaini.Kuongoza nchi kwa maneno matamu na ahadi za matumaini wakati sheria ni mbovu na kandamizi hilo huwa ni changa la macho!
Ndugu yangu tutafika huko,tunampa muda,akichemka wewe mwenyewe Ni shahidi hatujawahi kushindwa kumpinga mwovu yoyote hapa Tanzania.
Je Tanzania hii paliwahi Kutokea Mtu katili kumshinda Jiwe?
Je hakukosolewa?
Nakuhakikishia huko tuendako hizo sheria kandamizi zinafutwa tu.
Yeye mwenyewe Maza Ana la kujifunza,anaona Kama kufanya kidogo hivi napata uungwaji mkubwa hivi Tanzania nzima,wanaCCM na wapinzani wamefungana kwa pamoja kunipongeza,je nikienda kinyume si watanilaani na kunichukia kabisa?
Akiwaza hivyo itabidi awe mwaminifu kw a ahadi zake.
 
Tunaomba kuepuka gharama za u haguzi mama abadikishe Katina pasiwepo na uchaguzi 2025 kwani tunamkubali wote hata sisi wa upinzani
Hapana itakua sio demokeasia,hata kwenye mfumo wa chama kimoja kiongozi huyo mmoja hupigiwa kura tena,baada ya miaka Fulani I'll kuhakikisha kukubaliwa kwake ama Kama Kuna mabadiliko ya watu wanaomkubali au wanaomkataa.
Kuendeleza bila kuchaguliwa Ni ufalme au umalkia.
 
19 Reactions
Reply
Back
Top Bottom