Kwanini tunakufa?

Dah,nilikuwa wapi muda wote huu kuja kutoa majibu sahihi?

Iko hivi, binadamu anapokufa hawezi kufufuliwa kama gari kifufuliwavyo kwasababu, mwili wa binadamu na viumbe hai wengine wana mpangilio ufuatao katika miili yao,

Seli› Tishu› Ogani› Sistimu(mfumo)› kiumbe hai

Na hiyo oganaizesheni hapo juu zinategemeana kila moja,yaani moja ikishindwa kufanya kazi inaathiri ufanyaji kazi wa kingine,

Mfano: Moyo ukifeli kusukuma damu, kuna seli zitakosa chakula,oksijeni n.k hivyo kufanya hizo semi kufa, na ikumbukwe pia kuna seli za aina mbalimbali, seli za ubongo, seli za Neva, seli za kwenye mapafu,figo,INI,utumbo, tumbo n.k hivyo kushindwa kwa Moyo kusukuma damu kutasababisha seli hizo zote kukosa chakula na oksijeni hivyo kupelekea hizo seli kufa.
Kwa maana hiyo mtu akifa kwa tatizo la moyo kushindwa kufanya kazi maana yake sehemu nyingine za mwili zimefeli pia, hivyo hata ukibadilisha moyo bado haitaweza kumfufua kwasababu kuna seli zingine za mwili zitakua hazifanyi kazi.
Hii inatofautiana na gari, gari inaweza ikafa injini lakini sehemu zingine ziko njema hivyo ukiweka injini nyingine gari inarudi kuwa nzima.

Bila shaka utakua umeelewa kwanini hatuwezi fufuliwa kama gari baada ya kufa
 
Kwakuwa sisi wanadamu tunae aliyetuumba bila shaka kufa sio mwisho wa maisha yetu bali kuna maisha baada ya kufa

Kama mwana damu anapotengeneza kifaa kikiharibika anaweza kukitengeneza na sisi wanadamu aliyetuumba anaweza kuturudisha siku ikifika

Kwa hiyo kwanini tunakufa sababu tunataka tukamiliashe hatuwa alizotupangia Muumba wetu

MUUMBA AMETUPANGIA WANADAMU.
*¤ Tuzaliwe
*¤ Tuishi kwa muda wowote tuliopangiwa
*¤ Tufe ili tuishi katika maisha ya barzah
*¤ Tufufuliwe ili tuhukumiwe kwa matendo yetu
*¤ Mwisho tuishi tena maisha ya Milele ikiwa peponi/Motoni
 
Habari wana jamvi, natumai wote mu wazima na mimi kwa upande wangu ni mzima na bukheri wa afya.

Kama heading inavyosema hapo, nataka kujua ki undani zaidi kwanini tunakufa? Na kwanini binadamu akifa anashindwa kufufuliwa, kama tatizo lilikuwa ni figo kufeli kwanini baada ya kufa marehemu akiwekewa figo nyingine hafufuki?

Maana katika maisha ya kawaida kitu kikiharibika kabisa kama vile gari kikiwekewa kitu kipya kinapona na kinarudia hali yake ya mwanzoni.
Refer to biology class, topic known as carrying capacity. Two, there is the principle of aging also known as depreciation in machines. Even if you replace machine parts to keep it functioning, you cannot do that for eternity. It comes a time when even the machine dies off.
 
Kama unakula kwa nini usinye
Kama kuna kuvaa kwa nini tusivue
Kama kuna kushika lazima kuna kuachia
Kama kuna ingiza lazima kuna kutoa
Kama kuna kuzaliwa lazima kuna kufa
Sasa usiulize kwa nini kuna kufa .
 
kaka swala la kwann tunakufa ni gumu kiimani ni rahis tu tuliumbwa ili tuje tutekeleze amr ambazo mungu aliziweka na tumtukuze pamoja na kumsifu yeye
hii mungu ametupa uhai kama mtihan ajue n nani atafanya mema
kibinadam kuanzia siku mimba inatungwa selli huanza kuzalishwa by mulitiplication effect mpaka pake mtu anapofikia ukubwa anmbapo sell zinazozalishwa huwa sawa na seli ambazo hufa kipind hiki mtu huwa haendelei kukua ni lazima mtua afe hata jkama hajaumwa au kupata ajali koz mtu anapoanza kuzeeka inamaana selli za mwili hufa kwa wing kuliko zinavyozalishwa hili swala likiendelea ni lazma baadae linaleta matatizo katika organs na mtu hukumbwa na matatizo lazma afe
kisayans tunakufa ili ile kitu inaitwa ecosystem ifikie lengo na lengo la ecosystem ni kumaintain a balance katika na viumbe mazingira yao
na kiiman tunakufa ila tupate malipo ya yale tuliyofanya hapa duniani
ila kaka swali linakuja kisayans kwann binadam anashindwa kukontrol kifo ingawa tunaendelea kisayans ila bado hatuwez kujiokoa kutokana na kifo lazma tufe ingawa dawa za kila ugonjwa zipo matibabu ya kila matatizo yapo kwa nn binadam asiish bila kifo kwa nn tunazeeka ni kweli hatuwez kumaintain uzalishwaj wa sell ndani ya miil yetu kupitia vyakula na madawa ya kisasa
ok kuna mambo ukihoj saana utaona there is alimit of human power and thinking
 
Kama ambavyo binadam amepewa uwezo wa kuliumba na kulitengeneza gari likatembea na kubeba mizigo vivyo hiyo gari hilo halina uwezo wa kulitengeneza gari lingine likatembea,ndivyo mungu alivyoona inapendeza kuwepo na mipaka,simple theory of nature(almighty state is for almighty God only)!
 
Tunakufa kwa sababu seli hai zetu zinafika mda zinachoka na hufa.

Kwa nini sayansi haiwezi kufufua watu? Mpaka hapa tulipofikia bado sayansi haijaweza kumfufua binadamu na niseme wazi tu kuwa sina hakika kama sayansi itaweza kumfufua mtu au la katika wakati ujao.
Hakika haitaweza
 
nje ya bibilia Hakuna Jibu la kweli mkuu.
Yote haya yalianza miaka zaidi ya 6000 hapo mashariki ya kati maeneo ya Iraq. Karibu na mto tigris ilipokaa bustani nzuri
ya Eden. Kwingine kote utadanganywa. Na summary yake ipo kitabu cha mwanzo 1,2,3.

Ukielewa vizuri ndio utauliza maswali mapya.
1:Kwa nini Kiyama?
2:Kwa nini kondoo/ndama alichinjwa mtu akimkosea Mungu?
3:Kwa nini Yesu Afe?
4:Ni nini Dawa ya kifo?
5:Kuna kufa mara ngapi? Kwa nini hupaswi kuogopa kifo hiki tunachokiona sasa (Temporal death)?
Umenena vyema
 
Tunakufa kwa sababu hatuamini kuwa kufa kupo,Sikh tukiamini kuwa kufa kupo hatutokufa kamwe.
 

Similar Discussions

10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom