Kwanini tunaendelea kujivuta kuhusu chanjo za Corona? Tunahitaji tubembelezwe kuhusu kuyathamini maisha yetu wenyewe?

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
36,564
44,221
Watu wameanza kupatawa na mashaka ya kuja wimbi la tatu la COVID 19. Kwa sabubu kamati ya Rais kuhusu CORONA ilikwisha pendekeza chanjo ziletwe na kila anayetaka achanjwe kwa hiari yake ni vyema Wizara ya Afya ikatangaza kuwaita pamoja wadau muhimu haraka iwezekanavyo ili kuweka mpango mkakati wa pamoja katika kuagiza chanjo na kuzifikisha kwa wananchi wahitaji.

Jambo hili halipaswi kuendelea kucheleweshwa kwa sababu tutapoteza watu wengi kwa vifo bila sababu hasa wezee ambao wako katika hatari kubwa ya kifo endapo watapata hivi virusi. Kila uhai mmoja una thamani kubwa na kila dakika tunayochelewa kuleta hizo chanjo tuko katika ukingo wa kumpoteza mtu mmoja zaidi.

Tayari tumeona nchi nyingine jinsi chanjo zilivyoleta ufanisi ndani ya muda mfupi na kuokoa maisha ya mamilioni ya watu. Tutakuwa watu wa ajabu sana kama tutaka tubembelezwe hata kuhusu kuyathamini maisha yetu wenyewe.Tunaweza kufanya vyema.
 
Kuna vijana wanaipinga hii chanjo lakini Mimi naumia sana.

Mimi ni kijana ila kiukweli wanaoumia na huu ugonjwa ni wazee.

Sasa hawana access ya Internet na mtu wa kuwasemea huku ila ukweli wanahitaji hiyo chanjo.

Inasikitisha sana kuwa na taifa la wapinga kila kitu.

Vijana tuache siasa kwenye kila jambo wazee wapewe kinga wanaotaka popote walipo.
 
Kama mpaka sasa hamzingatii kujilinda na corona kwa maana ya kuchukua tahadhari ndio mnapiga hesabu za chanjo na kuona ndio muokozi? Huko Marekani baadhi ya sehemu wanatoa hadi zawadi kwa watakao chanjwa ili kuhamasisha watu kuchanjwa sasa huku ambako sasa hivi tu hatuoni umuhimu wa kuchukua tahadhari za kujikinga na corona ndio mnafikiri hata hizo chanjo zikija ndio tutaona umuhimu wa kuchanjwa na sie kuwa kama hizo nchi zengine?
 
Unaelewa maana ya chanjo za ugonjwa kama hizo za ndui na polio ulizochanjwa kwa msada wa mabeberu ulipokuwa mchanga?
Kama mpaka sasa hamzingatii kujilinda na corona kwa maana ya kuchukua tahadhari ndio mnapiga hesabu za chanjo na kuona ndio muokozi? Huko Marekani baadhi ya sehemu wanatoa hadi zawadi kwa watakao chanjwa ili kuhamasisha watu kuchanjwa sasa huku ambako sasa hivi tu hatuoni umuhimu wa kuchukua tahadhari za kujikinga na corona ndio mnafikiri hata hizo chanjo zikija ndio tutaona umuhimu wa kuchanjwa na sie kuwa kama hizo nchi zengine?
 
Unaelewa maana ya chanjo za ugonjwa kama hizo za ndui na polio ulizochanjwa kwa msada wa mabeberu ulipokuwa mchanga?
Swali lako linahusiana vp na nilichoeleza? mbona sizungumzii masuala ya mabeberu sasa sijui umeleta hoja ya mabeberu kwa sababu ipi? Au unafikiri mimi napinga chanjo hapa?
 
Watu wameanza kupatawa na mashaka ya kuja wimbi la tatu la COVID 19. Kwa sabubu kamati ya Rais kuhusu CORONA ilikwisha pendekeza chanjo ziletwe na kila anayetaka achanjwe kwa hiari yake ni vyema Wizara ya Afya ikatangaza kuwaita pamoja wadau muhimu haraka iwezekanavyo ili kuweka mpango mkakati wa pamoja katika kuagiza chanjo na kuzifikisha kwa wananchi wahitaji.

Jambo hili halipaswi kuendelea kucheleweshwa kwa sababu tutapoteza watu wengi kwa vifo bila sababu hasa wezee ambao wako katika hatari kubwa ya kifo endapo watapata hivi virusi. Kila uhai mmoja una thamani kubwa na kila dakika tunayochelewa kuleta hizo chanjo tuko katika ukingo wa kumpoteza mtu mmoja zaidi.

Tayari tumeona nchi nyingine jinsi chanjo zilivyoleta ufanisi ndani ya muda mfupi na kuokoa maisha ya mamilioni ya watu. Tutakuwa watu wa ajabu sana kama tutaka tubembelezwe hata kuhusu kuyathamini maisha yetu wenyewe.Tunaweza kufanya vyema.
Hilo wimbi la tatu linawapata waliochanjwa, halituhusu sisi mbona kichwa chako kizito namna hiyo 😡! Mfyuuuuuu 😡!
 
Watu wameanza kupatawa na mashaka ya kuja wimbi la tatu la COVID 19. Kwa sabubu kamati ya Rais kuhusu CORONA ilikwisha pendekeza chanjo ziletwe na kila anayetaka achanjwe kwa hiari yake ni vyema Wizara ya Afya ikatangaza kuwaita pamoja wadau muhimu haraka iwezekanavyo ili kuweka mpango mkakati wa pamoja katika kuagiza chanjo na kuzifikisha kwa wananchi wahitaji.

Jambo hili halipaswi kuendelea kucheleweshwa kwa sababu tutapoteza watu wengi kwa vifo bila sababu hasa wezee ambao wako katika hatari kubwa ya kifo endapo watapata hivi virusi. Kila uhai mmoja una thamani kubwa na kila dakika tunayochelewa kuleta hizo chanjo tuko katika ukingo wa kumpoteza mtu mmoja zaidi.

Tayari tumeona nchi nyingine jinsi chanjo zilivyoleta ufanisi ndani ya muda mfupi na kuokoa maisha ya mamilioni ya watu. Tutakuwa watu wa ajabu sana kama tutaka tubembelezwe hata kuhusu kuyathamini maisha yetu wenyewe.Tunaweza kufanya vyema.
Unajua hayo matumaini uliyoyaweka ndio hufanya wengine kuuliza kuwa mbona baadhi ya zenye chanjo bado wanathiriwa sana na corona? na jibu huwa kiwango cha waliyochanjwa ni kidogo sana ukilinganisha population yao, kwahiyo muhimu kujua ni vp hizo chanjo zikija zitaleta ufanisi na sio kuwa na chanjo halafu tukawa bado tunaanza kuulizana mbona watu wanakufa.
 
Kuna vijana wanaipinga hii chanjo lakini Mimi naumia sana.

Mimi ni kijana ila kiukweli wanaoumia na huu ugonjwa ni wazee.

Sasa hawana access ya Internet na mtu wa kuwasemea huku ila ukweli wanahitaji hiyo chanjo.

Inasikitisha sana kuwa na taifa la wapinga kila kitu.

Vijana tuache siasa kwenye kila jambo wazee wapewe kinga wanaotaka popote walipo.
WImbi la tatu halihusu wazee pekee- Virusi vinazidi kubadilika. Vikipata nafasi ya kustawi (kama hapa TZ) vitabadilika zaidi. Soma ile thread Africa (+Tanzania) could face vaccine-resistant Covid
 
Watu wameanza kupatawa na mashaka ya kuja wimbi la tatu la COVID 19. Kwa sabubu kamati ya Rais kuhusu CORONA ilikwisha pendekeza chanjo ziletwe na kila anayetaka achanjwe kwa hiari yake ni vyema Wizara ya Afya ikatangaza kuwaita pamoja wadau muhimu haraka iwezekanavyo ili kuweka mpango mkakati wa pamoja katika kuagiza chanjo na kuzifikisha kwa wananchi wahitaji.

Jambo hili halipaswi kuendelea kucheleweshwa kwa sababu tutapoteza watu wengi kwa vifo bila sababu hasa wezee ambao wako katika hatari kubwa ya kifo endapo watapata hivi virusi. Kila uhai mmoja una thamani kubwa na kila dakika tunayochelewa kuleta hizo chanjo tuko katika ukingo wa kumpoteza mtu mmoja zaidi.

Tayari tumeona nchi nyingine jinsi chanjo zilivyoleta ufanisi ndani ya muda mfupi na kuokoa maisha ya mamilioni ya watu. Tutakuwa watu wa ajabu sana kama tutaka tubembelezwe hata kuhusu kuyathamini maisha yetu wenyewe.Tunaweza kufanya vyema.
Haya kachukue buku yako
 
Hilo wimbi la tatu linawapata waliochanjwa, halituhusu sisi mbona kichwa chako kizito namna hiyo 😡! Mfyuuuuuu 😡!
Hii habari unapata wapi? Haina ukweli hata kidogo. Ni watu gani wanaorudia uvumi bila msingi?
Wimbi la tatu linaanza sasa kuumia Afrika (ambako chanjo ziko hache mno) na kushambulia pia vijana
 
Kama mpaka sasa hamzingatii kujilinda na corona kwa maana ya kuchukua tahadhari ndio mnapiga hesabu za chanjo na kuona ndio muokozi? Huko Marekani baadhi ya sehemu wanatoa hadi zawadi kwa watakao chanjwa ili kuhamasisha watu kuchanjwa sasa huku ambako sasa hivi tu hatuoni umuhimu wa kuchukua tahadhari za kujikinga na corona ndio mnafikiri hata hizo chanjo zikija ndio tutaona umuhimu wa kuchanjwa na sie kuwa kama hizo nchi zengine?
Kwa hiyo tusubiri tu hadi watu wanaanza kuanguka barabarani kama pale Uhindi?
Hekima au ujinga?
 
Kwa hiyo tusubiri tu hadi watu wanaanza kuanguka barabarani kama pale Uhindi?
Hekima au ujinga?
Hujanielewa. Huo wakati unaouzungumzia huko India walikuwa na chanjo ila walikuwa wanakufa, unafikiri sababu nini?
 
Watu wameanza kupatawa na mashaka ya kuja wimbi la tatu la COVID 19. Kwa sabubu kamati ya Rais kuhusu CORONA ilikwisha pendekeza chanjo ziletwe na kila anayetaka achanjwe kwa hiari yake ni vyema Wizara ya Afya ikatangaza kuwaita pamoja wadau muhimu haraka iwezekanavyo ili kuweka mpango mkakati wa pamoja katika kuagiza chanjo na kuzifikisha kwa wananchi wahitaji.

Jambo hili halipaswi kuendelea kucheleweshwa kwa sababu tutapoteza watu wengi kwa vifo bila sababu hasa wezee ambao wako katika hatari kubwa ya kifo endapo watapata hivi virusi. Kila uhai mmoja una thamani kubwa na kila dakika tunayochelewa kuleta hizo chanjo tuko katika ukingo wa kumpoteza mtu mmoja zaidi.

Tayari tumeona nchi nyingine jinsi chanjo zilivyoleta ufanisi ndani ya muda mfupi na kuokoa maisha ya mamilioni ya watu. Tutakuwa watu wa ajabu sana kama tutaka tubembelezwe hata kuhusu kuyathamini maisha yetu wenyewe.Tunaweza kufanya vyema.
Mie siyataki hayo machanjo yenu.
 
Nadhani mambo ya chanjo yabaki kuwa maamuzi binafsi. Wanaona umuhimu wake watapewa hizo chanjo. Watanzania wengi wana akili za humu humu na diamond wao. Huwezi kuwaambia kitu wakakubali kama wewe si msanii wa miziki yao ya mambo Yao...
 
Tatizo lako mwandishi, uko Copenhagen halafu unaandika Masuala ya Dar. Umeona wapi mzee aliyekufa kwa COVID-19 kwa mwezi huu? Rudi nyumban tule maisha achana na propaganda za Capitalists.
 
Akili ndogo bwana haina uwezo wa kufikiri watu waliokufa duniani ni karibia millioni nne wakati Afrika ambako hata hizo chanjo waliochanjwa ni kidogo sana, watu waliokufa ni takribani laki mbili tu.

Akili ya matope inataka tutumia mbinu za wale waliokufa wengi,badala ya kutulia kujiuliza kwanini hakuna vifo vyingi Afrika? Nini kimeiokoa?
Nchi zilizochanjwa kama Uganda ndo zinaanza kuteswa tena na mlipuko.
 
Hujanielewa. Huo wakati unaouzungumzia huko India walikuwa na chanjo ila walikuwa wanakufa, unafikiri sababu nini?
Walikuwa wamefikia asilimia ndogo tu. Haidhuru kama chanjo iko katika nchi fulani hadi imefika kwenye mwili wa mtu husika. Ukitoa chanjo kwa watu milioni 50 Tanzania, umehaangamiza ugonjwa. Milioni 50 pale Uhindi ni asilimia 5 za wananchi tu, haisiadii sana.
 
Walikuwa wamefikia asilimia ndogo tu. Haidhuru kama chanjo iko katika nchi fulani hadi imefika kwenye mwili wa mtu husika. Ukitoa chanjo kwa watu milioni 50 Tanzania, umehaangamiza ugonjwa. Milioni 50 pale Uhindi ni asilimia 5 za wananchi tu, haisiadii sana.
Na point yangu ipo hapo kwenye kutofikia lengo na huku hamzingatii kuchukua tahadhari.
 
Watu wameanza kupatawa na mashaka ya kuja wimbi la tatu la COVID 19. Kwa sabubu kamati ya Rais kuhusu CORONA ilikwisha pendekeza chanjo ziletwe na kila anayetaka achanjwe kwa hiari yake ni vyema Wizara ya Afya ikatangaza kuwaita pamoja wadau muhimu haraka iwezekanavyo ili kuweka mpango mkakati wa pamoja katika kuagiza chanjo na kuzifikisha kwa wananchi wahitaji.

Jambo hili halipaswi kuendelea kucheleweshwa kwa sababu tutapoteza watu wengi kwa vifo bila sababu hasa wezee ambao wako katika hatari kubwa ya kifo endapo watapata hivi virusi. Kila uhai mmoja una thamani kubwa na kila dakika tunayochelewa kuleta hizo chanjo tuko katika ukingo wa kumpoteza mtu mmoja zaidi.

Tayari tumeona nchi nyingine jinsi chanjo zilivyoleta ufanisi ndani ya muda mfupi na kuokoa maisha ya mamilioni ya watu. Tutakuwa watu wa ajabu sana kama tutaka tubembelezwe hata kuhusu kuyathamini maisha yetu wenyewe.Tunaweza kufanya vyema.
Bado wanaogopa kivuli cha JPM. Jirani Kenya ile delta variant imeshapiga hodi inaua vibaya sn na gonjwa pandikizi la fungus, baadhi ya wagonjwa hunyofolewa jicho kubusuru uhai!

Sent from my G80 using JamiiForums mobile app
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom