OLS
JF-Expert Member
- Oct 12, 2019
- 419
- 666
Leo nimeingia katika website ya tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora (THBUB) nimeona kwa kipindi cha 2015 hadi 2022 hawajawahi kutoa tamko la kulani mauaji ya raia yaliyowahi kutokea nchini ikiwemo mauaji ya Akwilina, na raia kadhaa kule Zanzibar kipindi cha uchaguzi.
Hata hivyo imeonesha kuwa Tume imelaani mara mbili mauaji ya polisi yaliyowahi kutokea nchini kwa kipindi cha mwaka 2015 hadi 2020. Hii inanipa maswali kuhusu tume ya haki za binadamu na utawala bora kama ina maana pana ya kuhusu mambo wanayosimamia au wapo kwa ajili ya watumishi wa serikali.
Hata hivyo imeonesha kuwa Tume imelaani mara mbili mauaji ya polisi yaliyowahi kutokea nchini kwa kipindi cha mwaka 2015 hadi 2020. Hii inanipa maswali kuhusu tume ya haki za binadamu na utawala bora kama ina maana pana ya kuhusu mambo wanayosimamia au wapo kwa ajili ya watumishi wa serikali.