Kwanini tulidanganywa Obama ni Mkenya?

Upuuzi mtupu.

Fanya ya maana. Obama muda wake kwisha.

Nadhani Trump, Magufuli na Duterte wanakutana kwenye mababu.
 
KWANINI TULIDANGANYWA OBAMA NI MKENYA.

#DUNIAYAKO No.2
Muandishi wa habari ambaye ni mchanguzi na mtafiti bwana Wayne Madsen kwa kupitia vyanzo mbalimbali vya CIA ameweza kugundua uhusiano baina ya CIA na watu muhimu katika maisha ya Barack Obama na mama yake, baba yake, bibi yake na baba wake wa kambo.

Tukianza na 'baba' yake na Obama ni kwamba alikuwa ni mmoja wa watu kadhaa waliotumiwa na CIA kwa ajili ya kusimamia mpango ambao utazuia siasa za ukomunisti kutoka China na muungano wa Sovieti usiingie Kenya na Afrika Mashariki kwa ujumla. Kennedy Foundation ilikuwa ikitoa pesa walizo ziita za ‘msaada’ kwa ajili ya kuwasomesha wanafunzi kutoka nchi za Afrika. September 12, mwaka 1960 Shirika la habari la Reuters kutoka London liliripoti kuwa mango unao itwa airlift ambapo fedha za Kennedy Foundation kwa ajili ya kuwasomesha watoto wa kiafrika Ulaya na Amerika si chochote bali ni mpango wa CIA kwa ajili ya kutoa mafunzo na kuwaanda vijana wa baadae wa kiafrika watakao tumika kwenye mapambano ya kisiasa dhidi ya China na Umoja wa Kisovieti kuzuia ushawishi wa kikomunisti kulimeza bara la Afrika.

Kinara na kibaraka wa Marekani hapa Afrika Mashariki katika mpango huu wa Airlift alikuwa ni bwana Tom Mboya ambaye alikuwa ni kiongozi wa chama cha KANU. Mboya alimchagua Baba yake na Obama kuwa kwa ajili ya kupata scholarship katika chuo cha Hawaii nchini Marekani ambapo huko ndiko alipokutana na mzazi mwenzake kwa Obama Dunham.

Jina kubwa ndani ya Kenya mpaka Marekani. Tom Mboya.

Tom Mboya alipokea dola za Marekani 100,000 kama msaada kwa ajili ya Airlift kutoka kwenye Kennedy Foundation na hii ni baada ya kukataa kiasi kama hicho kutoka US State Department na hii ni kwasababu fedha hizo ambazo zingeonekana zinatoka moja kwa moja kwenye serikali ya Marekani zingewaamsha walio lala kuwa Mboya ni kabaraka na ajenti wa CIA nchini Kenya lakini hizi za Kennedy Foundation ni wachache wangejua kuwa ni fedha kutoka kwenye mfuko mwingine wa suruali moja.[9]

Mboya akiwa na Kennedy, alitumiwa vizuri wakati wa utawala huo kuhakikisha viongozi wa Afrika hawajiungi na ukomonisti, divide and rule kama kawaida.

Airlift iliyoandaliwa na kupangiliwa na Mboya mnamo mwaka 1959 ilijumuisha wanafunzi kutoka Kenya, Uganda,Tanganyika, Zanzibar, Northern Rhodesia, Southern Rhodesia na Nyasaland. Baba yake na Obama hakuwa ni miongoni mwa wanafunzi wa mwanzo kudhaminiwa na Kennedy Foundation kupitia mpango wa Airlift ila ni miongoni mwa waliofuata baada ya hapo.

Kazi ya Mboya na wenzake ni kuhakikisha kuwa wanafunzi, vijana na viongozi wengine wa kiserikali ni vyama vya siasa hawajiungi na siasa za mrengo wa kushoto, siasa za ukomunisti. Hivyo Mboya alikuwa ni mtu mhimu sana kwa CIA. Katika mkutano wa mara ya pili uliofahamika kama All-African People’s Conference (AAPC) uliofanyika Tunisia Mboya alitumika kama tochi ya kuwamulika viongozi wote waliohudhuria kuona misimamo yao ya kisiasa na ikiwa kama ni wafuasi wa siasa za mrengo wa kushoto.

Tom Mboya ndiye aliyemuonganisha mtu ambaye anatajwa kama baba yake Obama kwenye mtandao wa kuwaandaa vijana wa Afrika kufuata maono ya Magharibi.

Katika mkutano huo kwenye ripoti ya CIA inaeleza kuwa palitokea msuguano na kutokuelewana kukali baina ya waziri mkuu wa Ghana Kwame Nkurumah na Tom Mboya. Mkutano wa mwanzo pia wa AAPC inadai ripoti hiyo kuwa Tom Mboya aliifanya kazi yake vyema ya kuwamulika viongozi hao na kupeleka ripoti kwa wakubwa zake.

Ni katika mkutano wa kwanza Mboya ndipo alimchagua baba yake na Obama kwenda kupata scholarship kupitia Kennedy foundation kwenye kivuli cha Airlift. Hivyo baba yake na Obama alikuwa akiaandaliwa kuwa ajenti wa CIA kwa ajili ya kufanya kazi sawa na ya Mboya.

Nkurumah alikuja kupinduliwa mwaka 1966 kwa msaada wa CIA na vijana wake iliyo waandaa kupitia mpango wa Airlift hapana shaka vijana wa Tom Mboya nikimaanisha Obama Sr. walikuwa na mkono kwenye kazi hii. Mwaka mmoja baadae mapinduzi mengine yalifanyika Indonesia ya kumpindua Sukarno kwa msaada wa CIA. Je unamjua mmoja wa waliohusishwa na mapinduzi hayo? Ni Ann Dunham, mama yake na rais Obama.

Inasemekana Mboya aliuwawa mwaka 1969 na maajenti wa kichina ambao walikuwa wakishirikiana na serikali ya Kenya kuondoa ushawishi wa Marekani nchini humo. Baada ya kifo cha Mboya kila ubalozi jijini Nairobi ulipeperusha bendera yake nusu mlingoti ispokuwa ubalozi wa China. Ushawishi wa Mboya kwenye serikali ya Kenya uliendelea muda mrefu hata baada ya kifo chake na hasa muda ambao Obama Sr. akiwa hai.

Dunham mama yake na Obama aliacha masomo katika chuo kikuu cha Huwaii mnamo mwaka 1960 wakati akiwa ni mjamzito wa mimba ya Barack Obama. Baba yake an Obama aliondoka Huwaii mwaka 1962 na kwenda kusoma Havard. Dunaham na Baba wa Obama walitalikiana mwaka 1964. Mwishoni mwa mwaka 1961 Dunham alirejea masomoni katika Chuo cha Washington akiwa na mtoto mchanga aliyeitwa Barack Obama.

Mwaka 1963 mpaka mwaka 1966 Dunham alirudi tena katika chuo cha Hawaii. Mwaka 1965 Dunhama aliolewa na Lolo Soetoro ambaye akawa ni baba wa kambo kwa Obama. Soetoro aliondoka na kuelekea Indonesia mnamo July 20, mwaka 1965 kama miezi mitatu hivi kabla ya uasi uliosimamiwa na CIA dhidi ya Surkano kufanyika. Ni wazi kuwa Soetoro aliitwa Indonesia na CIA kwa ajili ya kusaidia uwasi huo dhidi ya Sukarno ambao uligharimu maisha ya watu milioni moja wa Indonosia.

(Kennedy, Ton mbuya, Barack Wote watatu vifo vyao vinasemwa kuwa na mkono wa mtu nyuma yake)

Fuatilia post hii ya Oboma utajua mengi uliyofichwa katika histoiria yake. Tutajitahidi kila Siku kutoa post moja.

Tukutane post ijayo

Maoni yako ni muhimu.
Inawezekana hukuelewa tu,uliambiwa Obama ana asili ya Kenya na sio Kenyan ktk maelezo yako umekiri kwamba baba yake Barack ni mkenya,then sioni ulipodanganywa. Kwa wakati ule dunia ndivyo ilivyokuwa,ama uende east-communism(CHINA,USSR) ama west-capitalism(USA,WESTERN EUROPE) au usifungamane na upande wowote na katika mifumo hiyo yote miwili mikubwa hakuna wenye uzuri kwetu Afrika pengine afadhali magharibi. Kumbuka mmoja katika hiyo ulishakufa!
 
1. Kwa sera za uraia wa Marekani: ukizaliwa Marekani ni Mmarekani; kwahiyo Barack Obama ni Mmarekani mwenye asili ya Kenya.
2.Sera za Uraia wa Kenya zinasemaje? Mkenya akizaliwa nje ya Kenya, let say azaliwe Tanzania, atakuwa Mkenya au Mtanzania.
NB: Huenda Marekani wanamtambua Obama kama Mmarekani kwa sera zao na Wakenya wanamtambua Obama kama Mkenya kwa sera zao.
 
wengine walidanganywa kua obama ni muislamu.
Suala la dini siyo la kiasili, ni imani. Originally, baba wa Barack Obama alikuwa ni Muislam (kama sikosei ni "Hussein Obama" na mama wa Barack Obama ni mkiristo(u). Suala la dini yake halifuati dini ya baba wala mama. Anaweza Mkristo, Muislam au Idolator, au dini nyingine yoyote.
LABDA WEWE MWENZETU UMEBAINI UKWELI NI UPI? BARACK OBAMA NI DINI IPI?
 
KWANINI TULIDANGANYWA OBAMA NI MKENYA.

#DUNIAYAKO3
Obama Sr. anatajwa kama ndiye baba yake na Obama, LAKINI kwa herufi KUBWA, kuna ambaye anaye tajwa kama ndiye hasa baba yake na Obama na siyo Obama Sr.

Kama huyaamini macho yako, basi iko shida kubwa. Mwenye macho haambiwi tazama, jamani ni yupi baba wa Obama kati ta Barack Obama na Frank Davis?

Mama yake na Obama, Ann alipokuwa na miaka 17 alikuwa ni mfuasi wa sera za kimaksi (Marxism) na ndivyo alivyo kuwa baba yake mzazi pia. Kipindi hicho alikuwa ni rafiki na mtu aliyeitwa Frank Marshall Davis, mwanamama Ann akawa ana mahusiano ya kingono na wanaume wawili, yaani Frank Marshall Davis na Obama Sr. Katika kipindi cha mahusiano na wanaume hawa wawili ndipo alipo pata ujauzito wa Barck Obama.

Ann akasema ujauzito huo ni wa Mkenya mfuasi wa Makzist ndiye aliyempatia ujauzito huo, na ambaye jina lake ni Barck Obama au Barack Sr.

Kwanini basi Obama na wale wote qwanao ujua huu ukweli waliamua kunyamaza juu ya hili na kumsingizia Mkenya kuwa yeye ndiye Baba?

Lakini unapo mtizama Obama Sr. Na Obama Jr. Huoni hata kwa mbali kwamba wanafanana au kuhusiana kwa lolote, lakini ukimtazama Barack Jr. Na Frank M Davis, pumzi zitakuishia, ni copy right ya mwenzake.

Wanasema mtoto wa kukataliwa anakopi kila kitu, ndivyo alivyo fanya Obama kwa Davis. Chako chako tu, hata ukatae vipi. Tizama pua ya Davis na Obama, tizama midomo yao, tizama masikio, tizama bapa la uso na kope za macho yao, linganisha vitu hivyo na huyo jamaa wa Kenya! Kha!

Naweza kuendelea zaidi na zaidi juu ya baba yake Obama kuwa siyo Obama Sr. Bali ni Frank M. Davis, kwa kukusaidia pitia kumbukumbu hizi, tafuta kitabu kilicho andikwa naDavid Maraniss kinacho kwenda kwa jina la Barack Obama: The Story, tembele wovuti huu

THE ASTUTE BLOGGERS: Search results for STANLEY ANN DUNHAM

na huu

Obama & Hitler From No Where: Thats How Rothschild Likes It.

Mwaka 1967 Dunham alielekea Indonesia akiwa na Obama, kipindi hicho alianza kufundisha some la kingereza kwenye ubalozi wa Marekani Jakarta ambapo pia ilikuwa ni eneo lenye vituo vikubwa vya CIA. Mama yake na Obama alikuwa akifundisha somo la kingereza kwa ajili ya USAID ambayo nayo ni moja ya taasisi zinazotumiwa na CIA kama kivuli cha kufunikia kazi zao mbalimbali katika nchi tofauti tofauti.

USAID ndani ya Indonesia ilikuwa ni kivulicha shughuli za CIA. Dunham pia alikuwa akifanya kazi na mashirika ya Ford Foundation, World Bank, Asian Development Bank, Asian Development Bank, Bank Rakyat.

Mwaka 1971 USAID ilitoa fungu kwenye kile kilicho fahamika kama ‘Centre for Vietnam Studies’ katika chuo kikuu cha kusini cha Illinois ambacho kilishutumiwa kuwa ni miongoni mwa vivuli ambavyo CIA inavitumia kufichia kazi zake chafu.

Shirika hilo la USAID lilitoa fungu kwa mradi mwingine ulio fahamika kama Midwest Universities Consortium for International Activities (MUCIA) ambao ulihusisha vyuo vya Illinois, Wisconsin, Minnesota, Indiana na Michigan State ambavyo navyo vilishutumiwa na CIA kwa ajili ya kufanikisha miradi yake ukiwemo ule wa ‘agricultural education’ nchini Indonesia, na ‘miradi’ mingine kwenye nchi za Afghanistan, Mali, Nepal, Nigeria, Thailand, na Vietnam Kusini. Madai haya yalikuja mwaka 1971 mwaka ambao Ann Dunham alikuwa akifanya kazi kwenye shirika la USAID nchini Indonesia.

Julai 10 mwaka 1971, New York Times liliripoti kuwa USAID na CIA wanashutumiwa kwa kupoteza dola za Marekani bilioni 1.7 zilizotumika vibaya katika mpango uliofahamika kama Civil Operations.

Niambie inahitaji tarumbeta na safari za kwenda kwa bibi Kenya kuthibitisha Davis ndiyo baba wa Obama?

Kula pozi kwanza upate nguvu ya kusoma post ijayo.
FB_IMG_1544694817638.jpeg
FB_IMG_1544694792780.jpeg
FB_IMG_1544694829361.jpeg
 
huyu mama lazima aliangalia CV za wanaume akaona ya MJALUO wa kenya iko poa zaidi
 

Attachments

  • o.png
    o.png
    36 KB · Views: 25
  • f.png
    f.png
    29.4 KB · Views: 21
1. Kwa sera za uraia wa Marekani: ukizaliwa Marekani ni Mmarekani; kwahiyo Barack Obama ni Mmarekani mwenye asili ya Kenya.
2.Sera za Uraia wa Kenya zinasemaje? Mkenya akizaliwa nje ya Kenya, let say azaliwe Tanzania, atakuwa Mkenya au Mtanzania.
NB: Huenda Marekani wanamtambua Obama kama Mmarekani kwa sera zao na Wakenya wanamtambua Obama kama Mkenya kwa sera zao.
teh teh teh Jokate naye ni mmarekani?
 
Back
Top Bottom