Kwanini tulidanganywa Obama ni Mkenya?

Feb 18, 2017
63
62
#DUNIAYAKO No.1
Tuliambiwa kijana anaitwa Obama, kijana mweusi kutoka Afrika Mashariki, Kenya. We! Utachekwa. Muulize aliyekuwa makamu wa raisi Dick Cheney atakuambia Obama ni nani, mbele ya macho ya wapiga kura watu hawa wawili aliyekuwa makamu wa rais Dick Cheney na raisi wa Marekani kwa tiketi ya Democratic, Barack Obama wanamitizamo tofauti yenye mawazo na nadharia zinazo pingana, lakini nyuma ya mapazia jamaa hawa ni ndugu wanashirikiana babu mmoja.

Mke wa Cheney alipokuwa anahojiwa na MSNBC alisema kuwa wakati anafanya utafiti wa kukusanya taarifa mbalimbali juu ya kitabu chake kipya anacho kiandaa kinachokwenda kwa jina la ‘Blue Skies, No Fences’ amegundua kuwa mume wake na kijana wa Democratic wanashirikiana babu wa vizazi nane vilivyopita. Anasema mwana mama huyo,

“Hii ni hadithi ya ajabu kwa wa-Marekani kwamba babu mmoja, mtu anayetokea Maryland anaweza kuwa ndiyo sababu wa mkondo wa familia ambayo imechukua njia tofauti kama familia ya Dick na Obama”.

Lakini mtu huyu mweusi Obama anayo undugu wa damu na mtu mweupe na mmoja wa viongozi mashuhuri kwenye serikali za Marekani.

Obama na Cheney wanauhusiano kupitia kwa Mareen na Duvall waliyehamia kutoka Ufaransa mnamo karne ya 17. Lakini kijana huyu anayetajwa kama mtu mweusi haishii hapo kwa Cheney peke yake, Obama ni ami (mtoto wa mjomba/shangazi) wa 11 wa rais aliye muachia kiti hicho, W. Bush, wanarithishana wapendavyo. Bush na Obama wanashirikiana ndugu walio ishi Massachusetts karne ya 17, mababu na bibi hao

wakubwa ni Samuel Hinckley na Sarah Soole, kwa hiyo kama ilivyo damu ya Bush na ya Obama nayo inarudi mpaka kwa Malkia wa Uingereza naye anaibeba mpaka kwa Firauni wa misri, naye anairudisha nyuma mpaka katika Babylon ya kale. Obama ni kijana mwingine aliyekuja kuipigisha hatua ajenda kubwa kuliko.

Tizama Hapo Bush na watu ambao anayo husiana nao kwa damu, imeitwa demokrasia lakini ukweli systeam ni ile ile ya kifalme, lazima uwe na damu hiyo ndiyo unakuwa rais, na siyo kura ndiyo inakuchagua.

Uchunguzi uliofanywa kwenye kitengo maalum cha kuchambua koo za familia na mahusiano yao kidamu kinachoitwa The New England Historic Genealogic Society kilikuja na hadithi ile ile pale kilipo zichunguza familia za waliokuwa wagombea watatu kwenye kinyang’anyiro cha kiti cha urais cha Marekani. Uchunguzi huo ulionesha kuwa Obama si kwamba ana undugu na Bush peke yake na aliyekuwa makamu wake wa rais lakini pia undugu wake unaungana na aliyekuwa waziri mkuu wa Uingereza Winston Churchill.

Uchunguzi huo pia unamuonganisha aliyekuwa mgombea mwenza wa Obama, Hillary Clinton na muimbaji maarufu wa muziki wa pop Madonna ambaye naye kafanya kazi nzuri za kimasonia kwenye nyimbo zake nyingi. Wakati huo huo Obama na mcheza filamu maarufu wa Hollywood, Brad Pitt wanashea mjomba mmoja aliyekufa mwaka 1769. Brad Pitt naye anatumiwa vizuri na Freemason katika kazi zake mbalimbali za filam, wakati huo huo rafiki wa kike wa Pitt ambaye naye ni mcheza filamu Angelina Jolie anahusiana na mjomba wa tisa wa Hillary Clinton ambaye alifariki mwaka 1718.

Kila kitu kinafuata mtandao kama alivyosema mwana masonia mwingine Bill Gates, kama tulivyoona watu hawa hawaowani kiholela. John McCain yeye na aliyekuwa mke wa raisi aliyemaliza muda wake Laura Bush wanashea mjomba mmoja, mmjomba wa sita kwenye mkondo wa ukoo huo.

Mchunguzi wa familia hizi bwana Christopher Child, anasema kuwa Obama anauhusiano pia na walio kuwa marais wa Marekani kama George H. W Bush, Gerald Ford, Lyndon Johson, Harry Truman na aliyekuwa kamanda wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe ndani ya Marekani Robert Lee.

Hillary kwa upande wa mama yake yeye ni Mfaransa mwenye asili ya Canada, ambapo anaunganishwa na waimbaji wengine wawili Celine Dion na Aanis Morissette. Wakati Obama mama yake ni mtu mweupe kutoka Kansas.

Sipendi nikuchoshe sana mdau wetu tukutane post inayofuata, tuangalie nikweli oboma ni mkenya au tulidanganywa? #Duniayako

Ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni, hii ni dugu moja bhanah!

Sehemu ya Pili

Sehemu ya Tatu
 
Mi sijaelewa maana ninachokiona hapo ni late miaka ya 1700 kurudi nyuma sasa kipindi hicho leo Unasemaje ni mjomba wa fulani wkt vizazi karibia 7+ vimeshapita?
 
hivyo vitabu vya ajabuajabu ni njia tu ya kuwapiga pesa wajinga, ukitafuta undugu wa watu miaka 300 iliyipita basi unaweza kukuta wasukuma wote ni ndugu.
Huo undugu wa miaka dahari unatusumbua akili kutafakari tunachojua Obama asili yake ni Kogelo Kenya awe aliununua kabla hajazaliwa ili aje kuwa Rais wa Marekani au ilikuaje sisi hayatuhusu. Mambo ya kuanza kuchoshana na upembuzi yakinifu yanatumaliza damu tu.
 
Back
Top Bottom