Kwanini Tanzania na Watanzania hawependi kutoa msaada, je ni roho mbaya au laana?

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
Heshima kwenu wakuu,

Ili Tanzania na watanzania tufanikiwe lazima tujenge utamaduni wa kutoa. Vinginevyo tutasikia maendeleo kwenye TV. Nchi ya Tanzania haina Taasisi ya kiserikali hata moja ya kutoa misaada. Hata maandiko yamesema.

Ukweli ni kwamba Watanzania walio wengi hata kwa umoja wao kama nchi, hawana roho ya hisani. Yaani kutoa msaada na kujitolea.

Kwanini hatuna utashi wa kutoa misaada pale kwenye matatizo. Kidogo tunajitahidi kwenye misiba kwenda kuzika wapendwa wetu. Je, msaada lazima utoe kwa mtu unaye mfahamu?

Mfano:

Tanzania kulitokea tetemeko kule Kagera, lakini Serikali iligoma kuwasaidia wahanga lakini kenya waliweza saidia kwa kuleta mahindi ambayo sijui yaligawiwaje.

Kuna sehemu kuna ukame wananchi hawana chakula lakini serikali haisaidii.

Tuna watoto yatima wengi lakini ukiacha watu wa dini, na taasisi mbalimbali, huwezi kuona mtanzania wa kawaida anapeleka mchicha, maharage, mahindi nk. Anadai hana kitu.

Ombaomba barabarani Tanzania ukiangalia unakuta wanarushiwa mia mia mbovu hadi mia mbili. Halafu anatoka hapo anaenda kunywa bia za elfu 50.

Mtaani Tanzania kuna wasomi wengi, wanashinda wamekaa vijiweni. Huwezi kusikia wanaenda kujitolea sehemu ambazo elimu yao inahitajika.

Kuna watu wana nguvu, lakini hawawezi kwenda kujitolea kujenga, kutengeneza miundombinu ya kijamii.

Hii roho mbaya ya Watanzaniabna Serikali yao inatoka wapi?

Wamarekani wanashika nafasi ya pili kama watu wenye kuongoza katika kutoa misaada kwa wenzao. Mtu anayehesabika hutoa misaada ni yule anayesadia mtu mwenye shida ambaye mtoa msaada hamfahamu, anayechangia pesa za hisani, au anayejitolea kufanya kazi bila malipo. Nafasi ya kwanza ulimwenguni inashikwa na raia wa Myanmar.

Kwenye orodha niliyoipitia ambayo ni matokeo ya utafiti ya kampuni ya Gallup, Kenya inashika nafasi ya 12, Uganda ya 26, na Tanzania inashika nafasi ya 57 kwa matokeo ya utafiti wa mwaka 2016.

Ni rahisi kusema kuwa Wamarekani wana uwezo mkubwa wa fedha kuliko Watanzania, kwa hiyo ukweli kwamba pesa za hisani zipo nyingi zaidi nchini Marekani si suala la kushangaza.

Lakini hoja ya aina hiyo inapuuzia ukweli kwamba moyo wa kutoa au wa kujitolea hauna uhusiano wowote na utajiri. Moyo wa kujitolea ni uamuzi unaoongozwa na jinsi gani mtu mmoja amepima tatizo lililopo mbele yake na kuamua kuchukua hatua kupunguza tatizo hilo kwake au kwa jamii inayomzunguka.

Kila mara tunafikiwa na maombi ya kuwa miongoni mwa wale wanaochangia kumaliza matatizo kadha wa kadha. Na, hali inaporuhusu, kila mara tunafanya uamuzi wa kusaidia au kutosaidia.

Mara kwa mara napokea kadi ya kuchangia sherehe ya aina moja au nyingine, na tabia iliyojengeka miongoni mwetu ni kuwa asiyechangia sherehe hizo anajipambanua kama mtu ambaye hapendi kushirikiana na wanajamii wenzake.

Kwa hiyo baadhi ya Watanzania tunachangishana mamilioni ya pesa kwa madhumuni ya kuandaa sherehe kubwa na karamu za vyakula, vinywaji, na muziki kwa siku moja.

Na kwa siku zilizosalia ndani ya mwaka tunaitisha vikao kujadili matatizo mbalimbali ambayo yanatukabili ndani ya jamii zetu.

Kwenye sensa ijayo ingefaa kuwauliza Watanzania wanachangia kiasi gani cha pesa kwenye sherehe kila mwaka ili tukae kutafakari kama hayo mabilioni ya pesa yasingeweza kuleta manufaa makubwa zaidi kama yangeelekezwa kwenye kuboresha elimu, au afya zetu, au kwenye miradi ya kutunza na kuhifadhi mazingira.

Wapo watakaosema kuwa ni serikali ndiyo inayopaswa kuhakikisha kuwa raia wake wanapata huduma zote za jamii. Kinadharia utaratibu ni huo, lakini ukichunguza hali halisi utabaini kuwa hata kwenye nchi tajiri serikali inahitaji mashirika yasiyo ya kiserikali kushirikina nayo kuziba mapengo ya huduma mbalimbali za jamii.

Watu wenye asilia ya India ndo wanatuokoa katika kutoa misaada na kujitolea. Wanasiasa wanatoa misaada lakini nia kubwa inakuwa nibkwa manufaa yao ya kisiasa ndo maana hawatoi misaada kimya kimya.
 
Heri kutoa kuliko kupokea, unapopenda misaada utabaki mtumwa wa akusaidiaye milele.
Wengi wanapenda kuchangia harusi ili wapate sifa na wakale.
Huo sio utoaji.
Kibiblia ukiona nchi hajali yatima wala wazee ni laana.
Tuna yatima wengi mtaani hadi wamegeuka ombaomba na vibaka sababu hatuwajali.
Wazee wetu wamegeuka ombaomba sababu hatuna utamaduni mzuri wa kulea wazee kama taifa.
Hii ni laana
 
Kwanza shiba kisha fikiria wengine wakati nchi zilizoendelea 40% ya chakula wanachozalisha kinaishia jalalani(Wizara ya biashara ya Brazil,2009)

Sisi na siasa yetu ya ujamaa mwaka '75 ukame ikabidi tuombe chakula kwa wale tuliokuwa tunawaita mabeberu au tufe wote. Leo jiwe anatangaza vita na mabeberu kinachotokea ata misaada hawatoi. Tunaaminishwa eti sisi tutakuwa ma-donor tutatowa misaada na tutakopesha wengine(ANAYEAMINI HAYA YA JIWE NI KICHAA). Mwisho wa siku tunaanza kukopa kwa hao hao mabeberu same shit different day
 
Heshima kwenu wakuu,

Ili Tanzania na watanzania tufanikiwe lazima tujenge utamaduni wa kutoa. Vinginevyo tutasikia maendeleo kwenye TV. Nchi ya Tanzania haina Taasisi ya kiserikali hata moja ya kutoa misaada. Hata maandiko yamesema.

Ukweli ni kwamba Watanzania walio wengi hata kwa umoja wao kama nchi, hawana roho ya hisani. Yaani kutoa msaada na kujitolea.

Kwanini hatuna utashi wa kutoa misaada pale kwenye matatizo. Kidogo tunajitahidi kwenye misiba kwenda kuzika wapendwa wetu. Je, msaada lazima utoe kwa mtu unaye mfahamu?

Mfano:

Tanzania kulitokea tetemeko kule Kagera, lakini Serikali iligoma kuwasaidia wahanga lakini kenya waliweza saidia kwa kuleta mahindi ambayo sijui yaligawiwaje.

Kuna sehemu kuna ukame wananchi hawana chakula lakini serikali haisaidii.

Tuna watoto yatima wengi lakini ukiacha watu wa dini, na taasisi mbalimbali, huwezi kuona mtanzania wa kawaida anapeleka mchicha, maharage, mahindi nk. Anadai hana kitu.

Ombaomba barabarani Tanzania ukiangalia unakuta wanarushiwa mia mia mbovu hadi mia mbili. Halafu anatoka hapo anaenda kunywa bia za elfu 50.

Mtaani Tanzania kuna wasomi wengi, wanashinda wamekaa vijiweni. Huwezi kusikia wanaenda kujitolea sehemu ambazo elimu yao inahitajika.

Kuna watu wana nguvu, lakini hawawezi kwenda kujitolea kujenga, kutengeneza miundombinu ya kijamii.

Hii roho mbaya ya Watanzaniabna Serikali yao inatoka wapi?

Wamarekani wanashika nafasi ya pili kama watu wenye kuongoza katika kutoa misaada kwa wenzao. Mtu anayehesabika hutoa misaada ni yule anayesadia mtu mwenye shida ambaye mtoa msaada hamfahamu, anayechangia pesa za hisani, au anayejitolea kufanya kazi bila malipo. Nafasi ya kwanza ulimwenguni inashikwa na raia wa Myanmar.

Kwenye orodha niliyoipitia ambayo ni matokeo ya utafiti ya kampuni ya Gallup, Kenya inashika nafasi ya 12, Uganda ya 26, na Tanzania inashika nafasi ya 57 kwa matokeo ya utafiti wa mwaka 2016.

Ni rahisi kusema kuwa Wamarekani wana uwezo mkubwa wa fedha kuliko Watanzania, kwa hiyo ukweli kwamba pesa za hisani zipo nyingi zaidi nchini Marekani si suala la kushangaza.

Lakini hoja ya aina hiyo inapuuzia ukweli kwamba moyo wa kutoa au wa kujitolea hauna uhusiano wowote na utajiri. Moyo wa kujitolea ni uamuzi unaoongozwa na jinsi gani mtu mmoja amepima tatizo lililopo mbele yake na kuamua kuchukua hatua kupunguza tatizo hilo kwake au kwa jamii inayomzunguka.

Kila mara tunafikiwa na maombi ya kuwa miongoni mwa wale wanaochangia kumaliza matatizo kadha wa kadha. Na, hali inaporuhusu, kila mara tunafanya uamuzi wa kusaidia au kutosaidia.

Mara kwa mara napokea kadi ya kuchangia sherehe ya aina moja au nyingine, na tabia iliyojengeka miongoni mwetu ni kuwa asiyechangia sherehe hizo anajipambanua kama mtu ambaye hapendi kushirikiana na wanajamii wenzake.

Kwa hiyo baadhi ya Watanzania tunachangishana mamilioni ya pesa kwa madhumuni ya kuandaa sherehe kubwa na karamu za vyakula, vinywaji, na muziki kwa siku moja.

Na kwa siku zilizosalia ndani ya mwaka tunaitisha vikao kujadili matatizo mbalimbali ambayo yanatukabili ndani ya jamii zetu.

Kwenye sensa ijayo ingefaa kuwauliza Watanzania wanachangia kiasi gani cha pesa kwenye sherehe kila mwaka ili tukae kutafakari kama hayo mabilioni ya pesa yasingeweza kuleta manufaa makubwa zaidi kama yangeelekezwa kwenye kuboresha elimu, au afya zetu, au kwenye miradi ya kutunza na kuhifadhi mazingira.

Wapo watakaosema kuwa ni serikali ndiyo inayopaswa kuhakikisha kuwa raia wake wanapata huduma zote za jamii. Kinadharia utaratibu ni huo, lakini ukichunguza hali halisi utabaini kuwa hata kwenye nchi tajiri serikali inahitaji mashirika yasiyo ya kiserikali kushirikina nayo kuziba mapengo ya huduma mbalimbali za jamii.

Watu wenye asilia ya India ndo wanatuokoa katika kutoa misaada na kujitolea. Wanasiasa wanatoa misaada lakini nia kubwa inakuwa nibkwa manufaa yao ya kisiasa ndo maana hawatoi misaada kimya kimya.
Yaani toka nichangie maafa ya tetemeko Kagera halafu michango yetu ikaliwa na WAHESHIMIWA kabisa, sifikirii siku za hivi karibuni kutoa msaada, INAUMA sana yaani MHESHIMIWA kabisa!!!! na baada ya kuzila wacha aje kutusimanga wee! mpaka leo sina hamu!
 
Umeongea kitu kimoja kikubwa sana wachache watakuelewa, big up bro.

Kiukweli kwenye suala la kujitolea Watz hatuna kabisa moyo huo badala yake tunapenda zaidi kupokea.

Mfano wa ombaomba na watoto wa mitaa ni mzuri, hua nashangaa wana ndoa wanaishi miaka 20 kwenye ndoa bila kua na mtoto wanabaki kunung'unika na kulia ajabu vituo vya kulea watoto yatima kuna watoto wa kila sampuli lakini kulea mtoto sio wake anaona ni hasara kubwa.

Kweli vijana badala ya kushinda vijiweni wangeweza kwenda mahospital na kusaidia wagonjwa kuna wagonjwa wengi hawana ndugu na wapo katika hali mbaya wanahitaji kuogeshwa, kufuliwa na hata kufanyishwa mazoezi.

Hii kitu inapaswa ibadilike kwenye mioyo yetu, tunasikitisha sana.
 
Mbona nilisikia Juzi yule mwanamama aliyefiwa na mtoto Kenya( muna love)
amepokea msaada mpaka laini yake ya simu imeblock kuendelea kupokea pesa?

Au Watu wanachagua matukio
Cha ajabu hao hao wanaotoa hizo hela utakuta hajawahi kumpa mzee hata elfu moja
Wengi hawana utamaduni wa kutoa sadaka na ndio inatutafuna kila kukicha.

Watu 30 wanaweza kuchangia na kuchimba kisima lakini utafikiri wakitoa watafilisika hawajui wanatengeneza mazuri yao
 
Cristiano Ronaldo hana tattoo mwilini mwake, sababu ni kwamba yeye ni mchangaji wa damu. Pia huyu dogo anatoa misaada mbalimbali kwa taasisi mbalimbali za afya duniani. Kwanini Mungu asimuongezee utajiri na kila aina ya baraka.

Watanzania siku zote tunajiandaa kulalamika, kutukana, kusimanga na upuuzi mwingine wa aina hizo. Tunahukumu haraka sana kana kwamba tuna kila haki ya kuwashusha thamani wengine, halafu mtu anashangaa kwanini umaskini unatuganda.
 
Wabongo wanapenda sana mtelemko, hata ukiangalia kwenye jamii zetu, wengi wanadharau na kuchagua kazi, ukiwakuta vijiweni kazi kupiga porojo tu na kuwalaumu wengine, hata ukimsaidia leo hata jiongeza atarudi kesho na kesho na kesho tens
Kifupi wabongo hawabebeki hata kwa mbeleko ya chuma
 
Tanzania na watanzania tufanikiwe lazima tujenge utamaduni wa kutoa.
Naunga mkono hoja, kutoa ni moyo na sii utajiri.

Kwenye kutoa, kuna kanuni ya kitu kinaitwa "the money mystique" inasema "the more you give, the more you get".

Matajiri No.1-4 wa Tanzania ni watu wenye asili ya Bara Hindi, angalia wanavyosaidia, not necessarily masikini.

Mimi ni shahidi, enzi za ujana, kwenye yale mambo yetu yale, kuna wakati nilikuwa na foleni hadi Feri, maisha yalikuwa ni matanuzi, starehe na matumizi ya kuhudumia, fedha nazo zilikuwa zinatiririka.Sasa nimebadilika niko zero grazing, fungu nalo limekata!.

Natoa wito kwa Watanzania wenzangu, tujenge wa kujitolea ili pia tupate.

P.
 
misaada 8n
Naunga mkono hoja, kutoa ni moyo na sii utajiri.

Kwenye kutoa, kuna kanuni ya kitu kinaitwa "the money mystique" inasema "the more you give, the more you get".

Matajiri No.1-4 wa Tanzania ni watu wenye asili ya Bara Hindi, angalia wanavyosaidia, not necessarily masikini.

Mimi ni shahidi, enzi za ujana, kwenye yale mambo yetu yale, kuna wakati nilikuwa na foleni hadi Feri, maisha yalikuwa ni matanuzi, starehe na matumizi ya kuhudumia, fedha nazo zilikuwa zinatiririka.Sasa nimebadilika niko zero grazing, fungu nalo limekata!.

P.
misaada inatolewa na watu siyo serikali.
huduma zote hufanywa na watu wanaojitoa siyo serikali.
watanzania roho za kwanini zinawasumbua.
pwaaaa kila mtu kama mchawi vile.
 
Back
Top Bottom