Kwanini Tanzania inashindwa kuzalisha tena wachezaji ambao ni "University Graduates" kama akina Engineer Leodgar Tenga? Tunakwama wapi kama taifa?

Infantry Soldier

JF-Expert Member
Feb 18, 2012
15,893
16,317
Footballers with degrees: Kompany, Mata & 10 players who went to university | Goal.com

Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa Jamiiforums. Mimi mdogo wenu (Last Born) Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty. Eti ndugu zangu watanzania;

Kwanini Tanzania inashindwa kuzalisha tena wachezaji ambao ni "University Graduates" kama akina Engineer Leodgar Chila Tenga pamoja na ndugu Mohamed Mbwana Bakari "Junior"? Tunakwama wapi kama taifa?

Ninasikia huyu Mbwana Mohammed Bakari "Junior" alikuja kuwa boss mkuu (Commissioner General) wa idara ya uhamiaji hapa nchini baada ya kuacha kucheza soccer.

Ukijaribu kuangalia kwa haraka haraka katika kikosi cha timu ya taifa ya Soccer ya Tanzania (Taifa Stars) utakuta mchezaji mwenye elimu ya juu ni form six tu.

Kwanini vilabu vya soccer/michezo hapa kwetu havitoi msisitizo kwa wachezaji wao kujiendeleza kielimu ilhali inajulikana fika ya kuwa mchezaji hata kama akiwa ni tajiri sana akisoma anakuwa katika nafasi nzuri ya kusimamia vema mali zake?

OUR MOTTO: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.

Maoni ya mdau
Infantry Soldier,

Nafikiri ni mifumo ya upatikanaji wa hao wachezaji kubadilika...Mathalani mashindano kama Umitashumta na Umiseta hayatoi vipaji vyenye muendelezo(kielimu na kimichezo) lakini pia Serikali kupitia taasisi zake/wizara hazina sera au Watekeleza Sera madhubuti.
 
Infantry Soldier,

KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.[/QUOTE]Nafikiri ni mifumo ya upatikanaji wa hao wachezaji kubadilika...Mathalani mashindano kama Umitashumta na Umiseta hayatoi vipaji vyenye muendelezo(kielimu na kimichezo) lakini pia Serikali kupitia taasisi zake/wizara hazina sera au Watekeleza Sera madhubuti.
 
Huyo tenga na mbwana ilitokea tu kama kunguru kumnyea binaadamu. si kana kwamba eti enzi hizo kulikuwa na vipanga kunako soka. Na ili kulithibitisha hili ebu nitajie graduate wengine japo watatu mbali na hao wawili! Siku zote mpira wake masela😀 haruna moshi,kelvin yondani,juma nyoso etc.
 
Mbali na mata na huyo kompany hao wengine wakuokoteza labda Socrates. Mpira wake masela mkuu. Ikitokea graduate ujue hiyo kunguru kumnyea binaadamu
Sasa mzee baba, hauoni kuwa mchezaji tajiri akisoma anakuwa katika nafasi nzuri sana ya kusimamia vema mali zake?
 
Nyumbani ukiacha shule ucheze mpira ni kipigo, shule ukitega kisa kuna mechi mtaani ukibainika kipigo... ukijigawa huku na huku basi unakuwa average tu kila sehemu!
 
Back
Top Bottom