Kwanini Tanzania inaitwa Nchi ya Dunia ya Tatu?

kumusoma

JF-Expert Member
Feb 3, 2014
566
889
Nchi nyingi za kiafrika ikiwemo Tanzania zinaitwa ni nchi za dunia ya tatu au zisizoendelea kwa sababu zifuatazo:.
  1. Rais kushindwa uchaguzi kwa kupata kura chache,lakin yeye ndio anakuwa Rais wa nchi.
  2. Mtu mwenye akili timamu kuendesha gari au pikipiki au baiskeli usiku bila kuwasha taa.
  3. Kufaulu mitihani darasa la saba bila kujua kusoma na kuandika.
  4. Kuteuliwa kuwa mkuu wa wilaya au mbunge bila kujua kusoma na kuandika.
  5. Kuua watu kwa pistol au bunduki hadharani ,lakin unaachiwa huru kuwa huna hatia.
  6. Rais kuteua watoto wote , ambao baba zao walishawahi kuwa viongoz na kuwapa uwazir bila kuzingatia uwezo wao.
  7. Mtu mwenye akili timamu kusimamisha gari yake barabarani na kujisaidia haja ndogo bila wasiwasi.
  8. Mabinti au vijana wengi kumaliza vyuo huku hawajui walichosomea.
  9. Ukijuana tu na Rais au wazir mkuu au makamo wa Rais unateuliwa kuwa mkuu wa mkoa au wazir bila kuzingatia weledi wako.
  10. Ajali kuwa nyingi barabarani na kugharimu maisha ya watu wengi huku wakuu wa Polisi wakizidi kupandishwa vyeo.
  11. Watumishi wote waliofukuzwa kwa kuwa na vyeti fake ,kulipwa mafao yao.
  12. Wazir wa nishati kusimama bila aibu na kutaja sababu za uongo za kukatika kwa umeme kila siku.
 
Andika haliakisi uhalisia wa tanzania kuitwa nchi ya dunia ya tatu ila linaangazia udhaifu na utashi wa kisiasa. Maana hasa ya nchi ya dunia ya tatu ni nchi ambazo hazina maendeleo ukilinganisha na nchi zinazoitwa nchi za dunia ya kwanza au nchi za dunia ya pili.
 
Back
Top Bottom