Kwanini Tanzania inahujumu undugu Afrika ya Mashariki?

Mbona unateseka kunijibu mimi, nimeleta bandiko la gazeti wacha kunijadili, jadili kilichoandikwa kwenye gazeti, mimi siye mwandishi wala sio mwandishi wa habari.
Jifunze kutumia muda wako vizuri.
Kwa hiyo haya ni mawazo ya wakenya wengi dhidi ya watanzania
 
Turkana Ni kenya ila nahisi pale ndo jehanam na fukara namba moja duniani anaishi pale.

Teh teh teh, wenyewe huwa wanapakana kuwa si Kenya. Mfano ukisema njaa Turkana kenya. Watabisha mpaka asubuhi ingine ije. Watasema njaa ipo turkana, lakini siyo Kenya. Wenyewe kitu chochote nje ya Nairobi siyo Kenya. Nairobi pekee wanaikubali kuwa ndiyo kenya.
 
Ebu tutolee uchafu huu hapa. Kwanza kiswahili kilichoandikwa ni kibovu. Mpangilio wa muundo, maudhui na muktadha ni mbovu kupindukia. Pia herufi za maneno zimekosewa. Mfano, badala la kuandika suala anaandika swala.

Inaonekana muandishi hata historia Afrika Mashariki haijui... eti KIKWETE aliamua kujitoa jumuiya ya Afrika Mashariki na kujiunga na nchi za Kusini mwa Afrika. Huyu mpumbavu hajui kuwa sisi ni founding members wa SADC. Kama ilivyo kwa EAC kuwa founding members, ndivyo ilivyo kwa SADC. Hatujajiunga na SADC kama Rwanda walivyojiunga EAC. Mpumbavu tu ndiye atakayefuatilia maandishi yaliyokosa mashiko na ueledi kama gazeti hili.

Lingine ni kuwa no matter WHAT sisi tutamuenzi Nyerere daima, kwa kuwa hakutuuza au kuiuza NCHI YETU kwa wanyonyaji kama baba YENU Kenyatta alivyofanya. Amewatupa kwenye utumwa. Mnalia lia lkn hakuna la kufanya.
Rudi kwa kucheka ahahaha tihihihi
 
Wakenya wanateseka nini maana taifa pekee duniani linalowanyima usingizi ni Tanzania
 
Sio Wakenya wote. Usituseme wote katika kauli moja. Mimi kwa mfano nawapenda wasichana waT.z
Ni kweli si wote, ila takribani humaanisha kukaribia wote na sijamaanisha kwamba watu wabusara hawapo ila sampuli za mtoa mada wako wengi na nayaona sana hayo mawazi yao mara kupitia mitandaoni
 

Sambamba na sakata ya ‘Brexit’ ya Uingereza kujitenga jumuiya ya Ulaya ‘European Union’ (EU) yamkini Tanzania inajitia katika mwiba huo wanaojichoma waingereza.

Tukitathmini kwa kina mwenendo wa Tanzania katika swala zima la uwiano, umoja na maendeleo ya watu wa kanda hii ya Afrika Mashariki tunaona imekuwa kikwazo kikubwa kwa lengo hili nyeti.


Cha kushangaza ni kwamba mmoja wa waanzilishi wa jumuiya hii ni baba wa taifa hili yaani Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Zaidi ya yote makao makuu ya jumuiya ya Afrika mashariki yalianzishwa mjini Arusha kule kule Tanzania na kudumu hadi leo. Akiwa na baba wa taifa la Kenya marehemu Mzee Jomo Kenyatta sambamba na Rais Milton Obote walianzisha umoja huu wa kanda.


Hatahivyo ndoto ya muungano thabiti wa Afrika mashariki umetatizwa na majirani wabongo kaka blaza kwa sababu tutakazobainisha hapa.


SEE ALSO :Dar revokes licences of forex bureaus

Kizungumkuti ni kwa Tanzania kuwa na woga na Kenya kwa kuona kuwa watamezwa kiuchumi na jirani alopiga hatua


kubwa za uchumi na siasa. Kimsingi ni wivu wa kuona maendeleo ya Kenya unaowazuzua watanzania.Tatizo hili lilianzishwa na Nyerere mwenyewe aloshindwa kuinuwa taifa lake kiuchumi alivyofanya Jomo.


Kivipi?


Nyerere alisoma na kupata elimu ya juu ya chuo kikuu maarufu kule Scotland cha Edinbourgh katika masomo ya siasa na uchumi. Sasa badala ya kutilia mkazo elimu na kuanzisha msingi kwa wananchi wake alipiga


mbiyu ya kuendeleza Kiswahili kwa umoja wa nchi.


SEE ALSO :Ex-CEO of Bank M charged with fraud, money laundering

Changamoto ya maendeleo


Je, itawezekana vipi kuboresha watu wasio na elimu hususan kiuchumi? Ni kweli Kiswahili kimeondosha ukabila na


kuleta mshikamano wa mtanzania lakini bado wamesalia ujingani katika karne hii ya teknolojia.


Nyerere wa kabila la kizanaki kutoka kijiji cha Butiama kule Bukoba, alisomeshwa na wamishonari kidini na kielimu.Mbona hakutaka watanzania wasome kama yeye? Kunapofuka moshi kuna moto. Nyerere alihofu watanzania


wakisoma wataerevuka na kutisha uongozi wake.Alitaka wawe wajinga ili awatawale na kuwazuzuwa Nyerere alifaulu kwani watanzania mpaka leo wanamuenzi.


SEE ALSO :An escape that shouldn't cost you much

Twakumbuka nyimbo fulani ya kale kule bongo inayojumuisha mapenzi mazito ya wabongo kwa Nyerere. Mistari ni hii:-


“Ndugu Juliasi Kambarage Nyerere si kwamba yeye tu….ni kiongozi halisi…bali pia ni mwalimu.. alo na kipaji cha ukarimu…. Na hakuna asiye mfahamu…anayeshirikiana nasi katika shidana raha...”


Kimsingi Nyerere aliwateka akili watanzania kifikra akitumia masomo ya kifalsafa na siasaalosoma kule Edinbourgh.


Nyerere mjanja alianzisha siasa za ujamaa na kujitegemea na kuwarundika watanzania katika ufukara wa ukulima wa


kikale. Aliogopa kukuza wasomi bali alitaka wajinga kuwaongoza. Aghalabu alizinduwa azimio la Arusha kama sheria kuu ya kikatiba.Akifuata siasa za kidikteta na za kiimla za Mao Tse Tung wa China, Nyerere alisuta ubepari kabisa asijuwe kuna nukta fulani nyeti katika mfumo huu ambao Kenya walifata.


SEE ALSO :Traders say quality of Tanzanian tea improves

Malumbano


Nyerere katika kilele cha uhasama na Kenya alitaja Kenya kuwa jamii ya mtu kula mtu mwenzake. Akimjibu Kenyatta kwa kuiita Tanzania nchi ya mtu asiyekula chochote! Nyerere mwenywe alikiri mwishoni mwa awamu yake kuwa ujamaa haukuleta ufanisi kama kwanza alofikiria.Alijidanganya kuwa Tanzania ingekua ama Uchina asijuwe uchanga wa taifa lake ukilinganisha na China pevu.


Matokeo yake watanzania walifukarika wakawa madutu na washamba wakiwa ndani ya nchi tajiri ya raslimali sufufu lakini bila ya wasomi na watalamu wakugunduwa na kukuza. Huku Nyerere akilemaza watanzania Jomo Kenyatta aliendeleza elimu kwa wakenya akisisitiza matumizi ya kiingereza kama lugha ya kimataifa na kiuchumi.


Kenya ilpiga hatuwa huku vijana wakisoma kwa bidii wakati watanzania wakipepeta kiswahili kule katika vijiji vya ujamaa na kujitegemea.


Nyerere aliboresha udikteta wa chama kimoja cha TANU kisha cha mapinduzi (CCM) ikifata mfumo wa Uchina.


Wakiwa bila ilimu ya fikra watanzania walimuabudu Mwalimu aliyekuwa akiwachekesha kwa hotuba zake za mahanjam na uchali zilojaa inadi, sitiazai na hekaya za Abunuasi. Kenya ilipiga hatua kubwa kiuchumi na


Nyerere alifahamu hili na hata kuitambuwa Kenya kama nyota ya jaha na hata kujisahau na kuitaja katika hotuba zake.


Mfano dhahiri ni pale vijana wengi wa Tanzania walivyotaka kwenda nje ya nchi kule Ulaya na Marekani kwa masomo na makazi kama wenzao wakenya walivyosaidiwa na serikali yao. Nyerere alipochoka na kerohili aliwaambia watanzania hao hivi (nukuu):-


Ulaya iliyo Afrika


‘Uraya (ulaya) yanini? na uraya iko hapa hapa jirani (Nairobi)!.. nendeni hapa uraya !’alisema huku kama kawaida


yake akishangiliwa kwa nderemo na vifijo naye akihitimisha kwa kicheko chake kirefu cha gugumizi’ hee..hee..heee!’


Nyerere ambaye alibarikiwa kwa kuzungumza kwa haraka kama cherehani ya stima aliheshimiwa kupita kiasi na jibulake kwa swali lolote lilichukuliwa ukweli mtupu na hakuna wakupinga kwani baba kasema!


Viongozi wa chama tawala cha CCM kama Ngumbare Mwiro, Rashid Kawawa na kina Abeid Jumbe walishikilia sera za mwalimu kikamilifu na kuzitekeleza. Marais waliofuata kama Benjamin Mkapa, Ali Hassan Mwinyi, Jakaya Mrisho Kikwete na kwa kiasi fulani wa sasa John Pombe Magufuli walifata sera za Mwalimu. Aghalabu mfano wa m’buyu mkongwe ilikuwa kazi kung’owa kabisa mizizi ya ujamaa alozika Nyerere katika ardhi ya Tanzania.


Twaweza kusema Kikwete ambaye alikuwa kiongozi kijana wakati wa Nyerere alifuzu sera na hata tabia za babu yake huyo.


Alipokuwa Rais Kikwete alitawala kama Nyerere na kuzidi kulemaza Tanzania hususan kiuchumi


kwani ufisadi ulizidi kukithiri huku yeye akichekacheka tu! Kikwete alipenda sana kusafirinje ya nchi kwa kigezo cha kusoma mambo ya nchi ziloendelea.


Kuna wakati alitembelea Uhispania na kwende katika uwanja wa timu maarufu ya soka Barcelona kule Camp Nou. Aliporudi Tanzania aliisifu uwanja huo wa mpira ulivyopendeza eti ni mzuri!


Ni wakati wa Kikwete Tanzania ilipojitenga kwa muda na jumuiya ya Afrika mashariki na kujiunga na umoja wa kusini


mwa Afrika yaani SADEC.



Eti tuseme ulaya iliyoko africa, siku hizi Ulaya ni Dar ndugu yangu, mambo yame change, hahaaa hah
tapatalk_1557249123521.jpeg
IMG_20190503_012004_084.jpeg
 
Nahisi mtoa uzi haijui Tz kwanza eti anasema the late mwal.nyerere alitokea Butiama eti ipo bukoba "" huo ni UJINGA wa mkenya kujifanya anajua kumbe hajui geographia ya TZ .... Secondly , ukisema JK alijaribu kujitoa EAC ni ujinga sanaaa iv umesahau ile kitu UK aliifuel kwa ajili ya kuisideline TZ ile mliita Collision of willingness , huu ujinga mliitaka kuzitekanchi za maziwa makuu karibu na na kenya punde mlipo saini kupewa mkopo na bank ya exima china , na JK alikuja kenya na akahutubia ktk bunge la kenya na akasema hakuna kiongozi wa Tz ambaye atadiriki kuitoa Tz ndani ya jumuiya .... For God sake mpango wenu uli fail mchana kweupe wale mliojidanganya kuwateka akili wamewakimbia kweupeeee nchi kama Burundi ikikataa upuuzi wenumchana kweupe kujenga miundombinu kwa ajii ya kuunganisha nchi na nchi sio jambo

Ata wa kenya wenyewe baadhi mnahofu na EAC mfano mzuri Juzi M7 alivyokuja Kenya mlikubaliana Ug alete mayai na asali lkn days later baadhinya wakenya wqka mind kuhusu soko lao la mayai na asali zinazozalishwa ndan ya kenya
 
Naona tunarudi kule kule....

Ugomvi usio na maana!

Kenya kiuchumi mpo mbele,Tanzania tuko nyuma,sasa sijui kwanini kila siku tunagombana about this fact?

Heri tuwe tunajadiliana mbinu mbalimbali za kuendelea.....

Walao mbinu za kuipita Kenya!

Tukana this,tukana that,does not mean anything whatsoever!
 
Bro, umespend muda mwingi sana kucrash our Father of the Nation and our ideologies . And who told you if we fully integrate into EAC will solve our issues?

Let us be clear to you and whoever thinks like you, Tanzania is a sovereign state and the obligation is to Tanzanians first.......... hatuko tayari kuwa pushed, hii EA Federation tunaenda nayo pole pole bwana, let us prepare our children, our systems kwanza.

We are the most resourseful and mouth-watering nation in the block, our economic strides are potent na tutaingia siku tukiwa tayari not otherwise. Msitusukume sukume kwani what agenda have you got behind doors?

And kwa taarifa yako hakuna EAC bila Tanzania, afterall nakushangaa my bother, progress ipo vizuri ndo mana integration is moving in stages, yes sisi tuko bullish and slow kwan tunawahi wapi na hii EAC kuopen our borders kirahisi while we have our own issues to harmonize.

Usilazimishe haraka hii ndoa, acha tupendane kwanza them tutaoa tu. Learn to treat your fellow country men with honor and respect kwanza then ndo uwaze ya TZ. Hatuko tayari kuwa joined with you until you are civilized.
 
Famous quote by Julius NYERERE.
Ulaya iliyopo Africa.
Kama unataka kwenda ulaya, nenda Kenya.
Utakumbukwa kwa hili. Endelea kupumzika kwa amani
 
Back
Top Bottom