Kwanini Tanzania ina kazi ya kuzuia bidhaa zisivuke mipaka yake?

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,301
12,600
Tanzania inatumia gharama kubwa kuzuia karafuu, mahindi, kahawa, ng'ombe, madini na bidhaa nyingine zisivushwe nje ya mipaka yake na wakulima, wafugaji na wachimbaji wadogo Wa madini kwa lengo la kutafuta soko na bei nzuri za bidhaa zao.

Kwanini tusitafute kwanini watu wanataka kuvusha bidhaa zao nje ya nchi?
 
Mkuu unaonaje ukiwekeza kwenye kilimo cha nyanya?
Mahindi, mbaazi na karafuu n.k mazao ambayo soko lake linategemea upepo wa kisiasa !

Kilimo cha nyanya mtu atake asitake soko ni uhakika.
 
Nail
Mkuu unaonaje ukiwekeza kwenye kilimo cha nyanya?
Mahindi, mbaazi na karafuu n.k mazao ambayo soko lake linategemea upepo wa kisiasa !

Kilimo cha nyanya mtu atake asitake soko ni uhakika.[/QUOTE
Nilishalimaga nyanya hali yangu ikawa mbaya. Iko siku wakulima pia watasusa kulima mahindi kwakuwa hayarudishi gharama za mkulima, na hapo ndio taifa litakumbwa na njaa.

Siasa zinazopunguza mfumko Wa bei kwa kumlalia mkulima zitashindwa tu sio mrefu.
 
Tanzania inatumia gharama kubwa kuzuia karafuu, mahindi, kahawa, ng'ombe, madini na bidhaa nyingine zisivushwe nje ya mipaka yake na wakulima, wafugaji na wachimbaji wadogo Wa madini kwa lengo la kutafuta soko na bei nzuri za bidhaa zao.

Kwanini tusitafute kwanini watu wanataka kuvusha bidhaa zao nje ya nchi?
Ndio nchi pekee ambayo inafurahia Raia wake kuwa masikini
 
Mkuu unaonaje ukiwekeza kwenye kilimo cha nyanya?
Mahindi, mbaazi na karafuu n.k mazao ambayo soko lake linategemea upepo wa kisiasa !

Kilimo cha nyanya mtu atake asitake soko ni uhakika.
Unajua chochote kuhusu Nyanya au unaandika tu
Ni zao lipi lingine Duniani linaloweza kumpa mtu hasara kama nyanya ?
 
Mkuu unaonaje ukiwekeza kwenye kilimo cha nyanya?
Mahindi, mbaazi na karafuu n.k mazao ambayo soko lake linategemea upepo wa kisiasa !

Kilimo cha nyanya mtu atake asitake soko ni uhakika.

Mkuu kuna wakati tulilima nyanya wengi kwa wingi zikakosa soko, kuna msimu tena wakulima walilima mbaazi zikakosa soko, mahindi pia siku hizi hayana soko bila shaka muda sio mwingi wataacha kulima mahindi kibiashara.

Hizi siasa za kumaliza mfumko Wa bei kwa kuwatia hasara wakulima karibu zitafikia tamati. Njaa italikumba taifa very soon kama mahindi yataendelea kukosa bei nchini.
 
sababu kubwa ni uhaba wa vyakula au mazao yalozalishwa hizo sababu nyingine ni ndogo tuuu na ndo maana ukiangalia vinavyozuiwa zaidi ni mazao ya chakula
 
Mkuu unaonaje ukiwekeza kwenye kilimo cha nyanya?
Mahindi, mbaazi na karafuu n.k mazao ambayo soko lake linategemea upepo wa kisiasa !

Kilimo cha nyanya mtu atake asitake soko ni uhakika.
Mkuu nyanya soko lake halipo kama unavyodhani. Zikiadimika sokoni, ni zimeadimika kweli. Ila zikishajaa sasa ..inakuwa kituko. Mfano juzi kati iv kreti ya nyanya ilifika hadi 65,000 ..ila leo sasa kreti 8000.

Huu ndo ubaya wa nyanya sokoni.
 
Back
Top Bottom