Keynez
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 2,397
- 3,884
Kuna biashara kubwa inafanyika kati ya nchi hizi mbili na hasa toka kipindi cha Urais wa Kikwete tumekuwa kwenye msukumo wa kuwakutanisha wafanyabiashara wa Tanzania na Marekani. Mfano ni hivi majuzi tu kuna kundi la wafanyabiashara wa Marekani walifanya mkutano na wafanyabiashara na mamlaka mbalimbali mjini Dar es Salaam.
Cha kushangaza mpaka leo hakuna Income Tax Treaty kati ya Tanzania na Marekani.
Kwa mtazamo wangu, hili jambo linaweza kuwa na faida kubwa sana kwetu. Kwa mfano, hii itawalazimu Watanzania waishio Marekani ambao bado hawajaukana Utanzania kulazimika kudeclare kipato chao kila mwaka kwa TRA na pia kulipa kodi ndani ya Tanzania kila mwaka. Tunaweza kuamua labda hii hela iende katika mfuko maalumu kwa ajili ya kazi fulani mfano elimu ya juu au ya msingi.
Hata Wamarekani wanaoishi nje ya Marekani wanalazimika kila mwaka wajaze fomu kusema wameingiza kiasi gani na wanalipa kodi huko Marekani hata kama wameishi mwaka mzima nje ya nchi yao.
Kuna masuala ya malipo ya royalty mfano kwenye shughuli kama za sanaa. Itakuwa rahisi sana kwa wasanii wa Tanzania kufaidika na kazi zao zinapotumika nchini Marekani. Sasa hivi sijui ni utaratibu gani unatumika kwenye suala kama hili. Badala ya kila siku kuja na sheria za kubana watu, embu mara moja moja tuje na sheria za kumfaidisha Mtanzania.
Pia itasaidia kujua takwimu sahihi zinazowahusu Watanzania walioko huko Marekani kitu ambacho kwa sasa hatuna. Tumekuwa tunafanya makongamano mbalimbali ya Diaspora kila mwaka tukiongelea fursa za uwekezaji na jinsi gani tunaweza kuwatumia Watanzania walioko nje kwa fursa za kiuchumi zilizoko Tanzania.
Takwimu ni zaidi ya kujua tu kuna watanzania wangapi walioko nje ya nchi. Inabidi kujua kipato chao, kazi wanazofanya, elimu yao, nk. Hatuwezi kuja na sera sahihi bila kuwa na takwimu sahihi.
Kwa haraka haraka hizo ni faida za kuwa na hiyo Income Tax Treaty lakini kuna faida nyingi zaidi zilizo direct na indirect ya kuwa na hii kitu.
Cha kushangaza mpaka leo hakuna Income Tax Treaty kati ya Tanzania na Marekani.
Kwa mtazamo wangu, hili jambo linaweza kuwa na faida kubwa sana kwetu. Kwa mfano, hii itawalazimu Watanzania waishio Marekani ambao bado hawajaukana Utanzania kulazimika kudeclare kipato chao kila mwaka kwa TRA na pia kulipa kodi ndani ya Tanzania kila mwaka. Tunaweza kuamua labda hii hela iende katika mfuko maalumu kwa ajili ya kazi fulani mfano elimu ya juu au ya msingi.
Hata Wamarekani wanaoishi nje ya Marekani wanalazimika kila mwaka wajaze fomu kusema wameingiza kiasi gani na wanalipa kodi huko Marekani hata kama wameishi mwaka mzima nje ya nchi yao.
Kuna masuala ya malipo ya royalty mfano kwenye shughuli kama za sanaa. Itakuwa rahisi sana kwa wasanii wa Tanzania kufaidika na kazi zao zinapotumika nchini Marekani. Sasa hivi sijui ni utaratibu gani unatumika kwenye suala kama hili. Badala ya kila siku kuja na sheria za kubana watu, embu mara moja moja tuje na sheria za kumfaidisha Mtanzania.
Pia itasaidia kujua takwimu sahihi zinazowahusu Watanzania walioko huko Marekani kitu ambacho kwa sasa hatuna. Tumekuwa tunafanya makongamano mbalimbali ya Diaspora kila mwaka tukiongelea fursa za uwekezaji na jinsi gani tunaweza kuwatumia Watanzania walioko nje kwa fursa za kiuchumi zilizoko Tanzania.
Takwimu ni zaidi ya kujua tu kuna watanzania wangapi walioko nje ya nchi. Inabidi kujua kipato chao, kazi wanazofanya, elimu yao, nk. Hatuwezi kuja na sera sahihi bila kuwa na takwimu sahihi.
Kwa haraka haraka hizo ni faida za kuwa na hiyo Income Tax Treaty lakini kuna faida nyingi zaidi zilizo direct na indirect ya kuwa na hii kitu.