Kwanini Tanzania haijavunja Uhusiano na Gadaffi?

mzee mwanakijiji mi sioni sababu za kufanya hivyo sisi kama tanzania, mwalimu alikuwa anapima nani anaonewa ndo anasasimama kwa upande unaoonewa, ndo maana alisimama upande wapalestina dhidi ya islaeli pia akaitambua BIAFRA KAMA NCHI katika ule mgogoro wa nigeria, sasa kwa upande wa libya kwa mtu mwenye akili zake hawezi kuwaunga mkono waasi sababu wale wanatumiwa na nchi za maghalibi kuleta uasi libya. kama basi kila anayeitwa dikteta na nchi za magharibi ni wa kumkataa basi angemkataa kamanda fidel castro. mi naona ni sahihi kwa tanzania kuwa na msimamo wake bila kuangalia nani yuko wapi, hao senegal na liberia wanafanya hivyo kwa maslahi yao binafsi, je unataka na sisi tuwatambue waasi kulinda maslahi yetu pasipokujali ukweli uko wapi?
 
suala la Libya linatugawa kati ya wale tunaomwona ni dikteta na wale wanaomuona ni hero yaani ndg zetu Waslam kisa kawajengea misikiti na alikuwa ana-finance daily running ya Islamic institutions! Hizo ndivyo siasa zetu zilivyokuwa cheap kiasi cha haki ya wana-Libya wanaopigania Uhuru kuwa compromised kisa kujengewa nyumba za ibada na serikali ya dhalimu huyu wa wananchi wa Libya
geza ulole dikteta ni mtu wa aina gani na kwa tafsiri ya nani? ni nini kilichokufanya umuone dikteta? je udikteta wake ulileta faida au hasara kwa watu wake? je wewe mwenye nchi yenye demokrasia hiyo demokrasia imekusaidia nini? ndugu jaribu kupima kwa vipimo vyako na wala si vipimo vya nchi za magharibi. kumbuka marekani walimuolodhesha NELSON MANDELA KAMA GAIDI HATARI WA KIMATAIFA JE ULIAMINI NA HILI?
 
mzee mwanakijiji mi sioni sababu za kufanya hivyo sisi kama tanzania, mwalimu alikuwa anapima nani anaonewa ndo anasasimama kwa upande unaoonewa, ndo maana alisimama upande wapalestina dhidi ya islaeli pia akaitambua BIAFRA KAMA NCHI katika ule mgogoro wa nigeria, sasa kwa upande wa libya kwa mtu mwenye akili zake hawezi kuwaunga mkono waasi sababu wale wanatumiwa na nchi za maghalibi kuleta uasi libya. kama basi kila anayeitwa dikteta na nchi za magharibi ni wa kumkataa basi angemkataa kamanda fidel castro. mi naona ni sahihi kwa tanzania kuwa na msimamo wake bila kuangalia nani yuko wapi, hao senegal na liberia wanafanya hivyo kwa maslahi yao binafsi, je unataka na sisi tuwatambue waasi kulinda maslahi yetu pasipokujali ukweli uko wapi?

Ielweke kuwa north Africa and arab spring is a regional uprising and not an islolated case.
Kwanini wa Libya tuwaite waasi na wale wa Tunisia, Egypt, Bahrain, Iran, Syria, Qatar, Saudia Arabia, Yemen, Morocco, Algeria n.k tuwaite wakombozi au wapigania haki n.k.!!!

Kama 'waasi' walibya wametumwa na nchi za magharibi je wale wa Egypt, Tunisia na kwingineko wametumwa na nani? Hivi si kweli kuwa Egypt ya Hosni Mobarak ilikuwa na manufaa kwa magharibi kuliko ilivyo hivi sasa? kwanini western countries zitume watu kumuondoa 'mtu wao'., kama dhana ya kutumwa itakuwa sahihi!!

Ni vema unapokuwa na info ukajaribu kufanya analysis na ku connect dots otherwise unaweza kuji contradict. Suala la Libya liangaliwe kwa upana wake na sio hisia au fungamano kwasababu ya.

Niendelee kuonyesha misimamo ya nchi yetu katika mambo kadhaa siku za nyuma.
Msimamo wa Tz kuhusu Sudan, ni kuunga mkono waasi na kujitenga kwa kusini.
Msimamo wa Tz kuhusu kongo ni kukamatwa Laurent Nkunda na kuiunga mkono serikali ya Kabila.
Msimamo wa Tz kuhusu Zimbabwe ni kuiunga mkono serikali ya Jongwe hata kama inaua watu na kuchakachua demokrasi.
Msimamo wa Tz kuhusu Somalia ni kuunga mkono serikali ya mpito.

Msimamo wa Tz kuhusu Libya ni nini?
 
Wakati wa Nyerere Tanzania haikuwa na utata katika masuala ya siasa za Kimataifa; tulitambua POLISARIO na PLO kama vyama vilivyokuwa vinawakilisha maslahi ya watu wa Western Sahara na Palestina. Hatukuona shida kutambua na kutoa ushirikiano kwa vyama vya ANC na vingine vya haarakati za ukombozi wa Kusini mwa Afrika. Tulitambua dhana ya utu wa mtu na kukataa kuhusiana na tawala dhalimu. Ndio sababu ya kuwa tayari kujitoa Commonwealth kama RSA ingeruhusiwa kuingizwa ndani.

Wakati huo Tanzania ilikuwa kiongozi katika masuala ya haki za watu na kukataa ukandamizaji wa watawala dhidi ya watu wao. Watanzania wenyewe walitembea kifua mbali kwani kuitwa Mtanzania ilikuwa inaendana kabisa na kuwa "mpigania haki za wanyonge". Ukisema "Tanzania" ulikuwa unazungumzia sauti ya Afrika katika masuala ya Kimataifa. Hakutukuwa na ukaribu sana na nchi za Kimagharibi kiasi cha kushindwa kuwambia ukweli. (kesho inshallah, nitawawekea barua ya Nyerere kwa JFK kuhusu Angola/Mozambique na RSA).

Leo hii Tanzania hii ya Mwalimu imekatwa mkia na haina tena uwezo wa kusimama na kunyoshea kidole mtu yeyote. Haiwezi kuwanyoshea kidole Wamarekani wala Waingereza (Nyerere alivunja hata uhusiano na Waingereza! huku akimtimua Padre mmoja kutoka nchini!). Tanzania hii ya sasa haina uwezo hata wa kujenga hoja ya kimaadili dhidi ya tawala dhalimu. Matokeo yake ni kuwa Tanzania ndugu zangu sasa inafuata. Ndugu zangu, Tanzania inafuata nchi za Senegal, Liberia, Qatar, n.k linapokuja suala la Libya.

Tanzania ambayo ilikuwa na sauti ya kukataa viongozi wake wamepewa misaada ya magari kiasi kwamba hawawezi tena kuzungumza na wanabakia kumung'unya maneno. Maskini Tanzania hii. Najiuliza mpaka nani atambue Baraza la Mpito la Waasi kule Libya ndio Tanzania ifuate? Kwanini nchi kama Liberia, Botswana na Senegal zimeweza kuvunja mahusiano na Gaddafi lakini nchi kongwe kama Tanzania imeshindwa hata kuonesha kuwatambua uwepo wao?

Yawezekana kweli viongozi wetu wamekuwa so compromised kiasi kwamba wema umekuwa uovu na uovu umekuwa wema? Ni kweli Taifa letu limenunuliwa hadi sauti yake - ukiondolewa kununuliwa kwa wanyama na raslimali zake? Kwanini sauti za Upinzani nchini zinashindwa kupiga kelele kutaka serikali ivunje uhusiano na serikali ya LIbya? Rais wa Senegal ambaye alikuwa ni mpinzani kwa muda mrefu alielewa hili na hakuonesha utata tena yeye alienda kutangazia msimamo wake ndani ya Libya yenyewe (kule Benghazi), kina Kikwete wanashindwa nini? Wanaogopa nini? Tanzania haina tena ile moral standing ya kukemea udhalimu?

Mmm Mwanakijiji umeongea sana,lakini inaelekea hujui kinachoendelea katika nchi za kiarabu.Kwanza nikuambie kwamba Gadafi is better than most African dictators.Ameboresha maisha ya watu wake sana.Kosa la Gadafi ni kuwa na mafuta,na kuwazuia Wamarekani na vibaraka wao wa Ulaya kutumia mafuta hayo kama wanavyotaka katika adhma yao ya kufanikisha the NWO(New World Order).Harakati zote zinazoendelea katika nchi za Kiarabu zinalenga katika kujaribu kuondoa regimes zote ambazo kwa njia moja au nyingine ni kikwazo au zinaweza kuwa kikwazo katika kujenga mfumo mpya wa dunia(NWO).Sasa nikupe ya mwaka,Iran sio kikwazo,ni mshirika.Fanya homework utagundua hilo.Kwa mandondocha Wamarekani/Wazungu wa Ulaya ni maadui kabisa wa Iran.Kwa kumalizia naunga mkono kwaTanzania kutounga mkono au kutotambua ile Council ya mpito iliyoundwa na Wamarekani, ni vibaraka tu hao!
 
Waasi wa libya ni wahuni tu wale. Ghadafi for Libya. Mapunduzi ya waasi wa libya ni ya kihuni wakisaidiana na North Atlantic Terrorism Organization (NATO)
 
Ielweke kuwa north Africa and arab spring is a regional uprising and not an islolated case.
Kwanini wa Libya tuwaite waasi na wale wa Tunisia, Egypt, Bahrain, Iran, Syria, Qatar, Saudia Arabia, Yemen, Morocco, Algeria n.k tuwaite wakombozi au wapigania haki n.k.!!!

Kama 'waasi' walibya wametumwa na nchi za magharibi je wale wa Egypt, Tunisia na kwingineko wametumwa na nani? Hivi si kweli kuwa Egypt ya Hosni Mobarak ilikuwa na manufaa kwa magharibi kuliko ilivyo hivi sasa? kwanini western countries zitume watu kumuondoa 'mtu wao'., kama dhana ya kutumwa itakuwa sahihi!!

Ni vema unapokuwa na info ukajaribu kufanya analysis na ku connect dots otherwise unaweza kuji contradict. Suala la Libya liangaliwe kwa upana wake na sio hisia au fungamano kwasababu ya.

Niendelee kuonyesha misimamo ya nchi yetu katika mambo kadhaa siku za nyuma.
Msimamo wa Tz kuhusu Sudan, ni kuunga mkono waasi na kujitenga kwa kusini.
Msimamo wa Tz kuhusu kongo ni kukamatwa Laurent Nkunda na kuiunga mkono serikali ya Kabila.
Msimamo wa Tz kuhusu Zimbabwe ni kuiunga mkono serikali ya Jongwe hata kama inaua watu na kuchakachua demokrasi.
Msimamo wa Tz kuhusu Somalia ni kuunga mkono serikali ya mpito.

Nini msimamo wa Tz kuhusu Libya ni nini?

Tofauti kubwa ya Libya na hizi other Arab uprising ni kwamba hawa "waasi" wa libya wamekua wakitumia heavy weaponry, walienda
wakateka kambi ya jeshi Bengazi na kupora heavy weapons.

Huwezi kuwafananisha hawa "waasi" na wale wa Egypt ambao kimsingi walikusanyika Tahrir square na kuparalyse the whole nation for weeks,
sanasana kulikuwa na rabsha ndogondogo za hapa na pale.

Hata Tunisia, baada ya waandamanaji wale wa mwanzo kuuawa na serikali ikaamua kuwafukuza kazi Minister wa interior, pressure za
waandamanaji ambao by far walikua more "peacefull" but with a lot of passion on their country ndio walipofanikiwa kumkimbiza Ben Ali.

If its about dictatorship, mbona kibaraka mkuu wa U.S mfalme wa Saudi Arabia, hanyooshewi kidole wakati huko kuna sheria kali mpaka wanawake hawaruhusiwi kuendesha magari? na Baraza la mawaziri lote lipo connected by blood na rulling royal family.

Libya its all about oil reserves? Tena usiingize kabisa historia ya Balkans na Kosovo war on this, maana tunaweza tukaanzisha a new topic on that
alone. Hao AU uliosema wangetatua tatizo la Ivory Coast lakini wakaonekana kufail, kilitokea nini mpaka mfaransa akaamua kuintervene
unilaterally? Why isit kwenye suala la Libya alikimbilia NATO na UN security Council?... Think with your head dude.

What about issue ya Bengazi kuwa na historical beef na utawala wa Gadhafi? Maana kama ni uprising ya kitaifa basi ndo iwe Bengazi tu mwezi karibu wa nne huu?
 
Safi sana wachangiaji kwa kusimamia haki, kama kuna usalama wa Taifa humu wanapima upepo kuona Watanzania wana msimamo gani kuhusu ishu ya Libya, ni bora wakamfikishia mkuu habari kwamba Watanzania hawataki kabisa kuungana na Wauaji wa Nato, wanaotaka kuiba mafuta ya Libya, watanzania tunataka Sovereignity ya Libya iheshimiwe, tunaamini demokrasia hailetwi na mabomu ya Nato, na tunaamini kwamba kinachoendelea Libya siyo kuwalinda raia, bali ni kutafuta "regime change" ili kusimika vibaraka watakao wahakikishia uvunaji wa mafuta ya libya kwa bei bwererebwerere, kinyume hata na azimio lenyewe la UNSC namba 1973. Watanzania tunalaani mauji ya raia wasio na hatia, na tunaitaka serikali yetu iwe makini kwa sababu hawa jamaa hawachelewi ku"stimulate" uasi katika mataifa mengine ya Afrika ili wapate "pretext" ya kuzivamia nchi hizo kwa kisingizio cha humanitarian intervention. Tunataka Serikali yetu, either kwa dhahiri au kwa siri ipinge mkakati wa devide and rule unaochezwa na Hillary Clinton, na tunataka sewrikali yetu ikiwezekana impe kanali Ghadafi msaada wa siri wa kijeshi ili kulinda uhuru wa Africa!, Ghadafi alitusaidia Watanzania wakati wa Mafuriko ya kule Kilosa na akaahidi kuwajengea waathirika wa mafuriko yale nyumba 200, sasa ni saa yetu kukumbuka fadhila ya watu wa Libya ambao leo wamegawanywa na Nato katika makundi ya "Walibya wanaofaa kulindwa(wale wa Benghazi), na Walibya wanaofaa kushambuliwa(wale wa Tripoli).

Cheki hii mada ya Ghadafi na Mafuriko ya Kilosa hapa Jf.
https://www.jamiiforums.com/tanzani...osa-imekuwa-ahadi-ya-ccm-uchaguzi-2010-a.html
 
Hawa maraisi wetu Mkapa na Kikwete ni maraisi wanaojali maisha ya wananchi wao kuliko kingine. Ndio maana wako kimya na mambo ya kuingilia matatizo ya nchi za watu kuliko kwanza kutatua matatizo yako. Hawa ndio maraisi wapendao wananchi wao. Kumvimbia mmarekani na mwingireza , siku zote aumiaye ni mwananchi na sio raisi aliye madarakani. Kwa nini yeyey nyerere hakuthubutu kuvunja uhusiano wa kibalozi na Lyibya mwaka 1978? Si Lyibya ilitushambulia kwa kupitia mgongo wa Iddi Amini? Kwa nini yeye nyerere hakuvunja uhusiano wa kibalozi na Iran, wakati Iran ilipotaka kutufanya vibaraka wake? U Pamoja na kugunduliwa kwa zo la jute huko pakistan, lakini unajua kwa nini Zao la mkonge halimfaidii mlala hoi hapa tanzania?Kuporomoka kwa zao la mkonge na kuuwa bidhaa zote za mkonge hapa nchi kumechangiwa sana na kelele za kutukana mabepari. Ivory Cost inaongoza duniani kwa kusambaza cocoa, angalia Huphet Bhon alivyo ulinda mtaji na ona jinsi Ivorian wanavyotesa.Ukijifanya wewe ni kidodomo cha kutukana mataifa tajiri, wao hukukomoa katika uchumi wako na mwisho wa siku aumiaye ni mwananchi kwa kujikuta. Nawasifu sana maraisi wetu hawa kwa kutojiingiza katika migogoro ya watu na hivyo wao wamekalia kujenga maisha bora ya mtanzania.
 
mi naona ni sahihi kwa tanzania kuwa na msimamo wake bila kuangalia nani yuko wapi, hao senegal na liberia wanafanya hivyo kwa maslahi yao binafsi, je unataka na sisi tuwatambue waasi kulinda maslahi yetu pasipokujali ukweli uko wapi?

Msimamo huo wa Tanzania kuhusu Libya ni upi huo ? Hilo ndilo swali la msingi. Kwa nini tunaogopa kutoa tamko rasmi kama nchi au tunasubiri tuone Walibya wangapi wanaangamia ili tuwaunge mkono washindi. Gadafi kapora madaraka mwaka 1969 (miaka zadi ya arobaini iliyopita) na sawa na hapa kwetu ameweza kudumu madarakani kwa kutumia dola kuzima upinzani. Kama Walibya wanampenda kwa mema aliyowafanyia, kwa nini anaogopa kuachia madaraka hadi amwandae Mwanaye kumrithi ? Kwa kuwa sote yaonekana tunaogelea kwenye dimbwi lile lile aliko Gadafi, kwa nini tunakosa ujasiri wa kumuunga mkono wazi wazi na kuwalaani hao waasi wasio na shukrani - si aliwatoa mbali kama CCM ilivyotutoa mbali ?

Ukweli ni kuwa tunatambua udhaifu wetu na kama Gadafi serikali yetu inatumia mbinu zile zile za kifashisti za kuzima upinzani ili iweze kubaki madarakani. Tunashuhudia polisi wetu wakitumiwa kuwaua raia wasio na hatia mradi CCM inabaki madarakani na hii inatokea kwa sababu CCM inajua fika madhambi yake dhidi ya Watanzania. Kuna wakati tulikuwa masikini lakini tuliheshimika lakini hivi sasa pamoja na umasikini wa kutisha tumepoteza hata hiyo heshima tuliyokuwa nayo kwani magamba ndio yamekuwa vazi letu la kitaifa. Tutamwambiaje jirani yetu avae huku wenyewe tunatembea tukiwa watupu magamba mwili mzima na hatuoni hata haya kujivunia hali hiyo.

Usiku tunawafungulia geti wezi waje watuibie mifugo yetu halafu mchana, bila aibu wala soni, hao tunafunga safari bakuli mkononi kwenda kuomba mboga kwa wezi hao hao. Wanapojitokeza wazalendo kulinda na kutetea tusiendelee kuibiwa, tunawafungulia mbwa wawararue na kuwachanachana. Kesho yake wezi wale wale wanarudi na kutusifia kwa jinsi tunavyojitahidi kudumisha amani na utulivu na sisi kama mazezeta tunashangilia na kujipongeza huku matumbo yakikoroma kwa njaa. Kila baada ya miaka mitano kwa vigelegele tunawasindikiza watawala (si viongozi) hadi meza kuu na kuwaacha wakijichana na sisi tukirudi kwenye umasikini wetu ! Wako wengine huamua kubaki chini ya meza wakinenepa kwa makombo wanayotupiwa !
 
Wakuu zangu,
Nimekuwa nikisoma huu mjadala kwa muda na hakika nimegundua kwamba Udini haupo kwa viongozi bali wao ni reflection yetu sisi wenyewe.. Sisi ni wadini kupita hata maelezo yaani inatisha!..

Labda niseme tu kwamba Swala la foreign policy zetu ni swala ambalo bado lipo ktk mfumo wa kutofunganama na upande wowote isipokuwa sisi tunatazama pia maslahi yanchi yetu. haijalishi kama ntunampenda Gadhaffi au hatumpendi isipokuwa tunatazama haki ya na Usawa..

Hivyo hatuwezi kuchukua ule msemo wa adui ya rafiki ni adui yako isipokuwa adui wa Tanzania na mkiukaji haki za kibinadamu ndiye tunaweza vunja mahusiano naye ikiwa hakuna ushawishi wa kuvuruga amani iliyopo..

Labda niwakumbushe tu kwamba Libya palikuwa hakuna matatizo, siku zote wakiwa wamefungiwa na nchi za Magharibi tulikuwa na mahusiano nao wakati haki hizo zikivunjwa au zikiwepo na haikutokea hata siku moja Mtanzania kudai tuvunje mahusiano na Libya wakati nchi za magharibi wamevunja. Na hata waliporudisha mahusiano sisi hatukuhusika wala kuchukua upande wowote zaidi ya kuendelea kuamini kwamba Gadhaffi alikuwa kiongozi wa Libya na tulimpa heshima zote kama mwanzo..

sasa nirudi ktk swala lenyewe, Gadhaffi hakuanza vita isipokuwa wananchi wenyewe ndio walioanzisha vita ya kumwondoa Gadhafii madarakani. na iliwezekana tu baada ya Gadhaffi mwenyewe kufanya makosa ya kukubali mkataba na UK kuwarudisha kampuni ya mafuta Shell nchini mwake kwa makubaliano ambayo bado yalikuwa na Utata ingawa wananchi wengi wa Marekani na Uk hawakuelewa sababu ya UK kukubaliana na Gadhaff..

Walipoingia nchini, UK kwa kushirikiana na Ufaransa wakaeneza sumu na sababu ilikuwa ndigo tu yaani Gadhaff katawala miaka 40 ni dikteta na hakuna Demokrasia, swala hili hata jana tu ktk economic forum walijaribu sana kuwashawishi Qatar ili waanzishe vurugu against mtawala wao kwa madai kama hayo na kama kuna mtu alitazama mahojiano hayo aliona jinsi wananchi wa Qatar walivyopinga mtawamo wa western country ktk Utawala kwani wananchi wake wanapata kila kitu na huwezi kulinganisha na nchi yeyote ya magharibi. Na walifikia kuhoji nini maana ya kuongoza nchi ikiwa neno kutawala litapewa tafsiri mbaya ili mradi tu kukamilisha demokrasia hata kama haipo. Ebu tuwaulize hao western Countries mbona Mugabe alikuwa zaidi ya Gadhaff lakini hawakuingia? maanake sioni tofauti baina yao tena naweza kusema Mugabe alikuwa na bado ni mshenzi kwa kila kitu? WHY!

Kwa hiyo, tanzania lazima tuwe wakweli wa nafsi zetu wenyewe. Binafsi sioni sababu ya Tanzania kuonyesha msimamo wake ikiwa hatukubaliani na lolote linalofanyika aidha iwe Gadhaff au mashambulizi ya kumwondoa ambayo pia yanakiuka sheria za Umoja wa Mataifa (kuvamia nchi) ili kumwondoa kiongozi wake.

Hakuna mmoja wetu anayelaani kitendo cha NATO kupiga mabomu Libya ili kumwondoa Gadhaffi ingawani kinyume cha kanuni za kimataifa na haiwezekani kabisa makosa mawili yakahalalisha sisi tuunge mkono mojawapo.

Makoisa yote anayolaumiwa Gadaffi yanafanyika Kongo, Syria, Yemen, India, Pakistan lakini wamefanya kipi zaidi ya kuwekeza zaidi ktk nchi hizo. Tazama Iraq, Afghanstan na hata Misri ambako huyu Mubarak alikuwa tajiri kuliko hata BillGates lakini hawakusema lolote hadi kaondolewa madarakani..Mnafikiri Marekani hawakujua kwamba Mubarak ni tajiri kuliko Bill Gates? walijua na wanawajua wengi sana hasa nchi za kiarabu ambao ni matajiri kuliko hata Mubarak lakini maadam wana interest zao huko hawatafanya lolote.

Hivyo basi Tanzania tunaweza kutokubaliana na Gadaff kutawala Libya kwa muda wote ule lakini pia hatukubaliani na maamuzi yaliyochukuliwa kumwondoa madarakani. Na to say the truth, vita wameianzisha hawa wapiganaji baada ya kuvamia maghala ya silaha na kuanza kupigana vita kuelekea Tripoli, hii huwezi kuisikia ktk meadi yeyote isipokuwa tu pale gadhaff alipojibu mapigo ndio ushenzi wake ukazungumzwa...

Sasa tujiulize hivi kweli tukitaka kumwondoa JK iwe kwa sababu yeote ile legit na tukaingia msituni iwe kwa sababu yeyote ile legit lakini tukachukua silaha na kupambana na askari wetu, ina maana wao wanatakiwa kufanya nini?

I mean kesho wananchi wachukue silaha kupambana na utawala wa JK mnataka askari wetu watupe silaha na kujiunga na upande wa wananchi hata kama wao wamekiuka misingi ya kutafuta haki yao.. jamani haiwezekani hata siku moja wananchi wakachukua sheria mkononi ktk nchi huru, isipokuwa wanaweza kuandamana kama walivyofanya mwanzoni kule Bengazi na askari wengi walijiunga nao ktk maandamano lakini siku walipochukua silaha na kuanza safari ya Libya pale ndipo walipotangaza vita wenyewe dhidi ya serikali yao.. Sasa wanalalamika kipi ikiwa wameamua kufa ili kuikomboa nchi yao basi na iwe hivyo lakini msitake sisi Watanzania kuanza kuchagua upande hata kama hatukubaliani na upande wowote.
 
Mi nafikiri wewe ndo wa kulaumiwa sio Tanzania, wewe mwenyewe umesema wale ni" waasi wa libya" na huo ndio ukweli, sasa ni vipi tz na heshima zake zote hizi ilizonazo iwatambue waasi? hilo haliwezekani ndugu yangu. Wale ni waasi wa libya, na nchi zote zilizowatambua ni nchi ambazo zimefuata karoti kujipendekeza kwa marekani na nchi za magharibi, hamna lolote zaidi ya hapo. Hatuwezi kuwatambua waasi, kwa kuwa kwa kufanya hivyo ni kukaribisha uasi nchini kwetu, ile ni njia haramu na ni vibaraka tu hawana lolote wale.

Hapo kwenye nyekundu....!Dah!Hivi bado tuna heshima?!
 
Wenye akili wanasema "ni afadhali mtu anayefanya maamuzi mabaya kuliko yule asiyefanya maamuzi kabisa". Kweli katika hili uongozi wetu umeonyesha kuwa sisi ni ndumilakuwili wa ajabu kabisa. Nadhani kama nchi ilipaswa itoe msimamo wake, kama upande wa Waasi au wa Gadaffi. Kwa upande wangu naona hawa waasi ni vibaraka tu wa mataifa ya wakubwa. Naona kuna hatua ya maksudi katika kuhakikisha kuwa huyu bwana mkubwa anaondolewa madarakani. Kwani yeye kosa lake kubwa ni nini hasa? Taarifa zilizopo zinaonyesha kuwa Libya ni moja ya nchi za kiafrika zenye maisha mazuri sana. Ghadaffi amejitahidi sana kuibadilisha nchi hiyo na kuwaletea maendeleo wananchi wake. Amekuwa mstari wa mbele kabisa katika kutetea maslahi ya waafrika dhidi ya mataifa yanayotaka kunyonya utajiri wao. Na hiyo ndo dhambi yake kubwa kabisa. Sasa katika yote hayo ilibidi nchi yetu itoe msimamo wake kuhusiana na hili. Kama ni upande wa Ghadaffi basi waseme au upande wa waasi. Hatutakiwi kubaki vuguvugu hata siku moja. Huu ni unafiki uliozidi kiwango.
Ukiangalia hoja zinazotolewa hapa bila shaka bara hili lina sababu zote za kuwa bara lenye migogoro na maafa. Watu hawajui chanzo cha migogoro ni ukosefu wa demokrasi inayoweka serikali kwa ridhaa ya wananchi na si nguvu za silaha. Gadafi mtu niliyemsikia enzi zote za maisha yangu kuwa mtu katili eti leo tunataka kujidanganya kuwa ni kiongozi mzuri wa bara hili. Eti hana kosa. Eti kwa kuvimbisha shingo dhidi ya wazungu hata kama anaua na kukandamiza walibya eti anafaa make anatupa kichwa kidogo waafrika. Viongozi bora wa Afrika ni Mugabe, Ghadafi na Museveni kwa kuwa wametuambia wachawi wetu ni wazungu. Mimi nasema watawala kama Ghadafi na wengine hawafai. Afrika tunataka viongozi si watawala. Eti maisha Libya ni mazuri sana kiasi kwamba kumwondoa Ghadafi ni kuaribia Afrika. Maisha ya Libya sikatai ni bora kuliko nchi nyingi za kiafrika lakini watu wa Libya wataka maisha zaidi ya hayo wanayopewa na Ghaafi. Jamani binadamu hataishi kwa mkate tu. Uhuru ni kitu muhimu sana. Kama tunasema maisha ya Libya ni mazuri basi tuwaite wazungu waje watutawale tuwe na maisha mazuri ila hatuna uhuru. Kila mpenda uhuru anafurahia vuguvugu la nchi za kiarabu mnafikiri Ghadafi yeye hakustahili kuwepo kwenye hilo kundi? Wananchi wa Libya hawakutaka nchi za magharibi ziingilie ila hawakuwa na ujanja baada ya Ghadafi kuwatangazia maafa makubwa wanaompinga. Waliowaita nchi za magharibi kuwasaidia ni wananchi wa Libya mnaounga utawala wa Gadafi ndio mna uchungu na Libya kuliko wenyeji?Afrika tuna tatizo hili kuwa hatuthamini maisha na hivo yeyote anayechezea maisha ya watu kama Gadafi tunamwona ni mtu wa kawaida tu. Wazungu wataendelea kututawala tu tukiendelea na upuuzi huu wa kupuuza mauaji ya watu kwa kiburi cha uafrika. Tanzania wanashindwa kuachana na Gadafi manake serikali haina moral authority hiyo. Wameoza kama Gadafi.
 
Sina la kusema zaidi!

gaddafi_pix.jpg
angalia waafrika tunavyouza utu kwa vitu kama majengo! Ina maana hayo majengo ni bora zaidi ya maamuzi ya wana Libya? ya kutaka uhuru wa kuchagua na demokrasia?
 
Msimminye JK kwenye hili kihivyo,hata mwalimu alitumia mwavuli wa "Kutofungamana na upande wowote" pale ilipokuja kwenye issue tata kama hizi.JF is fair and balanced.
Maoni yangu binafsi toka awali ni kwamba Gaddafi will prevail.Kinyume cha hapo Libya haitakuwepo.
 
Wakati wa Nyerere Tanzania haikuwa na utata katika masuala ya siasa za Kimataifa; tulitambua POLISARIO na PLO kama vyama vilivyokuwa vinawakilisha maslahi ya watu wa Western Sahara na Palestina. Hatukuona shida kutambua na kutoa ushirikiano kwa vyama vya ANC na vingine vya haarakati za ukombozi wa Kusini mwa Afrika. Tulitambua dhana ya utu wa mtu na kukataa kuhusiana na tawala dhalimu. Ndio sababu ya kuwa tayari kujitoa Commonwealth kama RSA ingeruhusiwa kuingizwa ndani. Wakati huo Tanzania ilikuwa kiongozi katika masuala ya haki za watu na kukataa ukandamizaji wa watawala dhidi ya watu wao. Watanzania wenyewe walitembea kifua mbali kwani kuitwa Mtanzania ilikuwa inaendana kabisa na kuwa "mpigania haki za wanyonge". Ukisema "Tanzania" ulikuwa unazungumzia sauti ya Afrika katika masuala ya Kimataifa. Hakutukuwa na ukaribu sana na nchi za Kimagharibi kiasi cha kushindwa kuwambia ukweli. (kesho inshallah, nitawawekea barua ya Nyerere kwa JFK kuhusu Angola/Mozambique na RSA). Leo hii Tanzania hii ya Mwalimu imekatwa mkia na haina tena uwezo wa kusimama na kunyoshea kidole mtu yeyote. Haiwezi kuwanyoshea kidole Wamarekani wala Waingereza (Nyerere alivunja hata uhusiano na Waingereza! huku akimtimua Padre mmoja kutoka nchini!). Tanzania hii ya sasa haina uwezo hata wa kujenga hoja ya kimaadili dhidi ya tawala dhalimu. Matokeo yake ni kuwa Tanzania ndugu zangu sasa inafuata. Ndugu zangu, Tanzania inafuata nchi za Senegal, Liberia, Qatar, n.k linapokuja suala la Libya.Tanzania ambayo ilikuwa na sauti ya kukataa viongozi wake wamepewa misaada ya magari kiasi kwamba hawawezi tena kuzungumza na wanabakia kumung'unya maneno. Maskini Tanzania hii. Najiuliza mpaka nani atambue Baraza la Mpito la Waasi kule Libya ndio Tanzania ifuate? Kwanini nchi kama Liberia, Botswana na Senegal zimeweza kuvunja mahusiano na Gaddafi lakini nchi kongwe kama Tanzania imeshindwa hata kuonesha kuwatambua uwepo wao? Yawezekana kweli viongozi wetu wamekuwa so compromised kiasi kwamba wema umekuwa uovu na uovu umekuwa wema? Ni kweli Taifa letu limenunuliwa hadi sauti yake - ukiondolewa kununuliwa kwa wanyama na raslimali zake? Kwanini sauti za Upinzani nchini zinashindwa kupiga kelele kutaka serikali ivunje uhusiano na serikali ya LIbya? Rais wa Senegal ambaye alikuwa ni mpinzani kwa muda mrefu alielewa hili na hakuonesha utata tena yeye alienda kutangazia msimamo wake ndani ya Libya yenyewe (kule Benghazi), kina Kikwete wanashindwa nini? Wanaogopa nini? Tanzania haina tena ile moral standing ya kukemea udhalimu?
kweli we chizi, niliona thread yako inaenda kulia gafla naiona ipo kushoto. We umevamia tu haya mambo, wote waliowatambua waasi ndio vibaraka wa nchi za magharibi na nia yao ni nchi zingine zifuate mkumbo wa kuwatambua waasi bila kujua reason behind ili ghadafi aonekane hakubaliki na viongozi wenzie wa africa na waweze kumtoa madarakani kurahisi.
 
Mkandara, huu ni upotoshaji. Wakati mwingine tujaribu kuwa wakweli!
Ebu tuwekee matatizo waliyokuwa nayo halafu tulinganishe na haya waliyonayo sasa plus wanayoendelea kuwa nayo.Halafu u conclude kama ile mission ya "kuwa protect civilian" bado ni relevant ama la.
 
Ebu tuwekee matatizo waliyokuwa nayo halafu tulinganishe na haya waliyonayo sasa plus wanayoendelea kuwa nayo.Halafu u conclude kama ile mission ya "kuwa protect civilian" bado ni relevant ama la.
Yaani unataka niamini kwamba "Libya palikuwa hakuna matatizo"?
 
Wakati wa Nyerere Tanzania haikuwa na utata katika masuala ya siasa za Kimataifa; tulitambua POLISARIO na PLO kama vyama vilivyokuwa vinawakilisha maslahi ya watu wa Western Sahara na Palestina. Hatukuona shida kutambua na kutoa ushirikiano kwa vyama vya ANC na vingine vya haarakati za ukombozi wa Kusini mwa Afrika. Tulitambua dhana ya utu wa mtu na kukataa kuhusiana na tawala dhalimu. Ndio sababu ya kuwa tayari kujitoa Commonwealth kama RSA ingeruhusiwa kuingizwa ndani.

Wakati huo Tanzania ilikuwa kiongozi katika masuala ya haki za watu na kukataa ukandamizaji wa watawala dhidi ya watu wao. Watanzania wenyewe walitembea kifua mbali kwani kuitwa Mtanzania ilikuwa inaendana kabisa na kuwa "mpigania haki za wanyonge". Ukisema "Tanzania" ulikuwa unazungumzia sauti ya Afrika katika masuala ya Kimataifa. Hakutukuwa na ukaribu sana na nchi za Kimagharibi kiasi cha kushindwa kuwambia ukweli. (kesho inshallah, nitawawekea barua ya Nyerere kwa JFK kuhusu Angola/Mozambique na RSA).

Leo hii Tanzania hii ya Mwalimu imekatwa mkia na haina tena uwezo wa kusimama na kunyoshea kidole mtu yeyote. Haiwezi kuwanyoshea kidole Wamarekani wala Waingereza (Nyerere alivunja hata uhusiano na Waingereza! huku akimtimua Padre mmoja kutoka nchini!). Tanzania hii ya sasa haina uwezo hata wa kujenga hoja ya kimaadili dhidi ya tawala dhalimu. Matokeo yake ni kuwa Tanzania ndugu zangu sasa inafuata. Ndugu zangu, Tanzania inafuata nchi za Senegal, Liberia, Qatar, n.k linapokuja suala la Libya.

Tanzania ambayo ilikuwa na sauti ya kukataa viongozi wake wamepewa misaada ya magari kiasi kwamba hawawezi tena kuzungumza na wanabakia kumung'unya maneno. Maskini Tanzania hii. Najiuliza mpaka nani atambue Baraza la Mpito la Waasi kule Libya ndio Tanzania ifuate? Kwanini nchi kama Liberia, Botswana na Senegal zimeweza kuvunja mahusiano na Gaddafi lakini nchi kongwe kama Tanzania imeshindwa hata kuonesha kuwatambua uwepo wao?

Yawezekana kweli viongozi wetu wamekuwa so compromised kiasi kwamba wema umekuwa uovu na uovu umekuwa wema? Ni kweli Taifa letu limenunuliwa hadi sauti yake - ukiondolewa kununuliwa kwa wanyama na raslimali zake? Kwanini sauti za Upinzani nchini zinashindwa kupiga kelele kutaka serikali ivunje uhusiano na serikali ya LIbya? Rais wa Senegal ambaye alikuwa ni mpinzani kwa muda mrefu alielewa hili na hakuonesha utata tena yeye alienda kutangazia msimamo wake ndani ya Libya yenyewe (kule Benghazi), kina Kikwete wanashindwa nini? Wanaogopa nini? Tanzania haina tena ile moral standing ya kukemea udhalimu?

Hivi tafsiri ya uovu kwa nini inafinywa sana? Ni kwa maslahi ya nani? Unataka kuniambia kwamba hao wanaopigana na Gaddafi ambao kimsingi ni wahaini wanatakiwa watambuliwe kwa sababu tu serikali za magharibi zinawatambua? Mimi sidhani kwamba walibya wale wana haki ya kuendesha uasi na kuiondoa serikali iliyoko madarakani kwa njia haramu wanastahili kupaziwa sauti za kuwaunga mkono. Ni vizuri pia ikaangaliwa kwamba wakti wa Nyerere mwelekeo wa siasa zetu ulikuwa ni tofauti na leo na ndiyo maana harakati uliznukuu wewe zilikuwa ni zile za ukombozi kutoka katika mifumo ya kikoloni. Hapa unatutaka tuunge mkono vitendo vya kihaini eti tu ili tuonekane tuna moral standing. That is wrong and I respectfully beg to differ with you. Mimi naamini kwamba kinachoendelea sasa Libya ni mob justice dhidi ya Gaddafi lakini kwa vile ina baraka za wakubwa wenye bifu na dhamira mbaya na Gaddafi ndiyo leo yuko ICC na familia yake inaendelea kuangamizwa!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom