Kwanini spika anaijibia serikali..??

MtazamoWangu

JF-Expert Member
Apr 25, 2009
313
7
Waungwana leo kwenye kipindi cha maswali kwa PM bungeni sikufurahishwa na kitendo cha Spika kila wakati kuingilia kati maswali ya wabunge kwa PM, suala la wizi wa nyaraka ZNZ na chanzo cha kujiuzuru Jumbe na suala la mahakama ya kazi na ahadi za CCM, siulizi majibu yake ambayo mara zote hayana tija, bali nauliza:
1. Je kati ya spika na waziri mkuu (PM) nani anayeisemea serikali??
2. anaposimama PM bungeni nini nafasi ya spika???
3. Je spika ni muongeaji wa chama, CCM, bungeni??? ana haki ya kukitetea chama chake??
4. Spika anapojibu swali aliloulizwa waziri mkuu, anafanya vile kwa nafasi gani?? je majibu yake ndio msimamo wa serikali??

hili limekuwa linatokea sana sio kwa PM tu bali hata kwa mawaziri wengine, mimi naona Spika aiche serikali ijibu yale wananchi wanayowatuma wabunge wao wakaulize wajibu wenyewe, watupe tu majibu ya "hovyohovyo" ili tujue hiyo ndio serikali yetu.
bado najifunza kanuni za bunge ili tukapambane vizuri lakini pia swala la Spika kuzuia waziri asijibu swali la mbunge ni kukandamiza haki ya kujieleza, na kazi za bunge...serikali lazima iulizwe na itoe maelezo ya kutosha kwa wananchi wake.

kama serikali haitaki kujibu au hawana majibu wanaweza wakatoa maelezo yakujitosheleza sio Spika kutumia nafasi yako kuwazima wabunge kuwakilisha hoja za wanaowawakilisha....
 
inategeana na swali lenyewe na kanuni zinasemaje. hata mimi nilisikiliza leo asubuhi lakini sidhani kama alaumiwe spika, hata wale wabunge hawakuwa na maswali mazuli. mengi utaona yanarudiwa, (mf. kuhuzu malipo ya wapemba, limerudiwa) au swali lenye jibu linaloeleweka (mf. nchi ina dini gani? spika alimwambia aangalie kwenye katiba) nk mimi nafikiri Spika yupo sahihi ili wabunge waweze kuuliza maswali yenye mantiki kuliko kupoteza muda na story za kusikiasikia
 
Waungwana leo kwenye kipindi cha maswali kwa PM bungeni sikufurahishwa na kitendo cha Spika kila wakati kuingilia kati maswali ya wabunge kwa PM, suala la wizi wa nyaraka ZNZ na chanzo cha kujiuzuru Jumbe na suala la mahakama ya kazi na ahadi za CCM, siulizi majibu yake ambayo mara zote hayana tija, bali nauliza:
1. Je kati ya spika na waziri mkuu (PM) nani anayeisemea serikali??
2. anaposimama PM bungeni nini nafasi ya spika???
3. Je spika ni muongeaji wa chama, CCM, bungeni??? ana haki ya kukitetea chama chake??
4. Spika anapojibu swali aliloulizwa waziri mkuu, anafanya vile kwa nafasi gani?? je majibu yake ndio msimamo wa serikali??

hili limekuwa linatokea sana sio kwa PM tu bali hata kwa mawaziri wengine, mimi naona Spika aiche serikali ijibu yale wananchi wanayowatuma wabunge wao wakaulize wajibu wenyewe, watupe tu majibu ya "hovyohovyo" ili tujue hiyo ndio serikali yetu.
bado najifunza kanuni za bunge ili tukapambane vizuri lakini pia swala la Spika kuzuia waziri asijibu swali la mbunge ni kukandamiza haki ya kujieleza, na kazi za bunge...serikali lazima iulizwe na itoe maelezo ya kutosha kwa wananchi wake.

kama serikali haitaki kujibu au hawana majibu wanaweza wakatoa maelezo yakujitosheleza sio Spika kutumia nafasi yako kuwazima wabunge kuwakilisha hoja za wanaowawakilisha....

Huyo ndiye Supika Six AKA mzee wa supidi AKA mzee wa misifa ... sidhani kama anajua mipaka ya kazi yake
 
Ni jukumu la spika kusimamia mijadala bungeni kama mbunge anauliza swali siivyo ndivyo au mahala sio pake spika humuelimisha kufanya hivyo si kuijibia serkali ni wajibu wake
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom