Kwanini siwezi kuaccess sehemu ya dini?

Sokomoko

JF-Expert Member
Mar 29, 2008
1,915
127
Mods na wapendwa wanaJF,

Nimekuwa kwa muda mrefu najaribu kufungua sehemu ya dini ili kuweza kuweka post zitakazotuelimisha na kuwa karibu na Mungu lakini inasema kuwa ni kwa "members only" mimi ni member lakini inaonyesha kama nimefungingwa kuingia sehemu hiyo naomba niulize je tatizo hili ni langu peke yangu au kwa members wote?

Ahsanteni
 
Huko si kwa wote mkuu, mpaka kwa maombi rasmi.

Peleka ombi lako
 
Inawezekana umri wako bado, Seriously waombe mods kwa pm watakujibu ila wewe ukienda si utatusumbua huko?
 
Inawezekana umri wako bado, Seriously waombe mods kwa pm watakujibu ila wewe ukienda si utatusumbua huko?

Usikhofu mkuu nitaelimisha na sio kukashifu dini ya mtu. Mimi ni mwislamu na dini yangu inakataza kumlazimisha asiekuwa muislamu kuamini dini ya kiislamu ila kwa hiyari yake na jinsi atakavyopambanua aya na hadith. Madhumuni ya dini ni kuleta usawa kwa watu watu wote wawe sawa na sio kutoleana maneno makali na kashfa zisizo na msingi na hiyo ni dhambi kubwa sana kwa Mungu.
 
Mods na wapendwa wanaJF,

Nimekuwa kwa muda mrefu najaribu kufungua sehemu ya dini ili kuweza kuweka post zitakazotuelimisha na kuwa karibu na Mungu lakini inasema kuwa ni kwa "members only" mimi ni member lakini inaonyesha kama nimefungingwa kuingia sehemu hiyo naomba niulize je tatizo hili ni langu peke yangu au kwa members wote?

Ahsanteni
Ndugu yangu kwa kusema kweli hawa Mods kwa kitendo chao cha kulificha jukwaa la dini hawajatenda haki hata kidogo... Ili jukwaa lilitakiwa kuwa wazi na kila mwanachama wa JF alipaswa kuwa na access nalo na ikiwezekana hata wasio wanachama walipaswa waweze kusoma kile kilichomo mule... Lakini kwa sababu zao ambazo wenyewe wanaziona ni za msingi wameamua kulificha mpaka uombe ruhsa kwao, kitu ambacho mimi binafsi siafikiani nacho.

Anyway wewe wasiliana nao Mods ili wakupe access.
 
ndugu yangu kwa kusema kweli hawa mods kwa kitendo chao cha kulificha jukwaa la dini hawajatenda haki hata kidogo... Ili jukwaa lilitakiwa kuwa wazi na kila mwanachama wa jf alipaswa kuwa na access nalo na ikiwezekana hata wasio wanachama walipaswa waweze kusoma kile kilichomo mule... Lakini kwa sababu zao ambazo wenyewe wanaziona ni za msingi wameamua kulificha mpaka uombe ruhsa kwao, kitu ambacho mimi binafsi siafikiani nacho.

Anyway wewe wasiliana nao mods ili wakupe access.

unayoyasema ni ya kweli na inakera sana nadhani hiyo sehemu ya dini ipo kwa ajili ya kuelimishana zaidi na sio kupakana matope. Kuzuia ndiko kumefanya mtu akizungumza kitu kuhusu dini ya mwenzie watu wanaanza kukashifiana maana hakuna jukwaa la dini na matokeo yake watu wanakula ban......
 
Wasiliana na X-paster,Max na wengineo wengi mabingwa wa jukwaa la Dini/ Imani watakupa maelekezo namna ya kuaccess.
 
Back
Top Bottom