Kwanini sitaupigia kura Mlima Kilimanjaro, Hifadhi ya Serengeti wala Hifadhi ya Ngorongoro

CHASHA FARMING

JF-Expert Member
Jun 4, 2011
7,789
8,914

Wakuu mimi sitapiga kura kwa ajili ya Kutafuta Kivutio cha Tanzania Kitakacho Ingia Kwenye Maaajabu saba ya Bara La Africa kwa sababu zifuatazo,

1. Hifadhi za Taifa na Vivutio vingine havijawahi kunufaisha Watanzania

2. Watakao Nufaika na Hizo Kura ni Viongozi wa Ngazi za Juu pamoja na Wazungu, Ndo maana wazungu wako mbele sana kwenye kuhamasisha,

3. Hii kampeni ni neema kwa Wazungu na si Watanzania, sisi tutabakia kwenda kuomba vibalua tu kwao

4. Hoteli zote zilizo Jengwa kwenye Hifadhi za Serengeti na Ngorongoro zinamilikiwa wa wageni kwa asilimia 100, hakuna mzawa mmoja mwenye hoteli huko hata Camp tu,

5. Hifadhi za Serengeti, Ngorongoro na Zinginezo wanawathamini sana Watalii wa Kizungu na si Watanzania, watalii wa kitanzania huwa hawapewi umuhimu wowote ule katika hizo hifadhi, na Kuna Kipindi Hifadhi ya Ngorongori iliwahi kujenga Vyoo kwa ajili ya Wazungu na vingine kwa ajili ya Watu weusi/wabongo,

Na hadi leo hii Abilia wabongo wanaosafiri kwa Mabasi kwenda Musoma huwa wakifika Geti la Ngorongo hawaruhusiwi kutumia vyoo vya wageni bali kuna vya kwao viko Geti No 1 ukiwa unatokea Karatu kuingia Hifadhini

- Wakuu Sekta ya Utalii hapa Tanzania Inaongozwa na Wazungu Kutoka Ulaya, Marekani, South Africa na Wahindi, na watanzania ni wachache sana kwenye hii secta na wengi ni wafanya kazi tu na si wamiliki wa Makampuni ya utalii,

-Mlima Kilimanjaro- Huu Mlima wanao nufaika nao ni Makampuni ya Kitalii ya Wazungu yenye Makao makuu yao Mjini Arusha na Moshi, na asilimia zaidi ya 98 ya Makampuni ya Kitalii kanda ya Kasikazini yanamilikiwa na wazungu na ni asilimia kama 2 tu ndo inayo milikiwa na Wabongo na hata hivyo kampuni za wabongo ni Ndogo sana Kiuwezo ikilinganisha na Za wazungu

Makampuni mengi ya Kitalii yana Offisi huko kwao Ulaya na Marekani na Booking zote na Payment hufanyika huko huko Ulaya na Marekani huku wageni huja kupanda Mlima tu na mara nyingi na pesa za kununulia Vinyago na kuwapa Tips Madreva wanao waendesha, sasa je TRA inawezaje kukagua mapato ya hawa watu wakati acaunt ziko Ulaya na Marekani? na Malipo yanafanyika hukohuko Ulaya?

JE HAPO ANAYE NUFAIKA NI NANI?

2. HIFADHI YA SERENGETI
Hii nayo ni Hifadhi ya Taifa kwa Jina tu ila kimatendo wanao iongoza ni Wazungu kutoka Ulaya wa
Frankfurt Zoological society, hawa ndo wana usemi wa mwisho kuhusu hizi hifadhi na si Serengeti pekee bali hata Ngorongoro, wakiongea hakuna wakupinga kitu na Maranyingi wamekuwa wanakuja na Policy za kuwakandamizaWatanzania na kuwaona wanyama ndo wana haki pekee na si watanzania

3. Ngorongoro- hii nayo ni jina tu kwamba ni Hifadhi ya Taifa ila kimatendo hii hifadhi ni kama Limited Company,

Kwa kifupi wanaonufaika na Hifadhi na Vivutio vingine ni Wazungu na Watanzania Wachache wanao Torosha Wanyama kwenda Nje ya Nchi, Wananchi wengine tumebakia Mashabiki wa kuhamasishwa kupiga kura tu,

Ni iliaumu sana Serikali kwa kuto kuwezesha Watanzania wazawa Kumiliki Makampuni na Badala yake Makampuni yanamilikiwa na Wazungu, na wazawa wamebakia kuwa Vibarua
 
ni kweli kabisa makampuni yote ya Utalii arusha yanamilikiwa na wazungu na watanzania tumebakia kuwa madreva tu na wabeba mizigo ya wazungu
 
siku hitaji kuisoma makala yako yote naunga mkono hoja huu utakuwa ni ujinga mkubwa kura za nini? hata usipokuwa ajabu kuna ajabu gani? na ukiwa ajabu kuna maajabu gani tutatayo yaona kama sio kupoteza wakati tu ni vile hatuna cha kukifanya
 
Na mimi sipigiiiiiii.
Hivi ajabu siku hizi mpaka lipigiwe kura?
 
mura chacha, umesema vema na umejitahidi kutooa vizuri sababu zako ingawa nyingine ni za kijumla zaidi.
 
mura chacha, umesema vema na umejitahidi kutooa vizuri sababu zako ingawa nyingine ni za kijumla zaidi.

Mkuu za kiujuma ni zipi hizo? Mimi nilicho jaribu kueleza ndo ninacho kifahamu, Hifadhi za Tiafa zilisha uzwa ila kimawazo bado ni hifadhi zetu lakini kwa Matendo zainawenyewe wanao faidika na hizo hifadhi
 
Kuvipigia kura ivyo vivutio ni sawa na kulipa kodi Tz while beneficially wakubwa wa iyo kodi ni wakubwa
Nikipataga mwanya wa kutolipa kodi huwa silipi bse ndo posho v8 za wakubwa ndo naifadhili safari za jk nalipa wauaji wa watz ie polisi
 
Mkuu nakuunga mkono asilimia mia moja. Nimeangalia maeneo mengi ambapo rasilimali zimegundulika. Badala ya kuwa faraja kwa jamii inayozunguka eneo hilo sasa imekuwa ni adha. Kitendo cha Mlima kilimanjaro kwa mfano ukitangazwa ni ajabu la saba la dunia, kwa uzoefu wa hapa Tanzania, wananchi wanaoishi kuzunguka mlima watahamishwa kwa nguvu kupisha wawekezaji na bila fidia. Angalia watu wanaoishi maeneo yenye madini na mbuga jinsi wanavyofanyiwa. SIUNGI MKONO MAENEO HAYA KUPANDISHWA HADHI.
 

Maji yanayo miminika kutoka milima Kilimanjaro kupitia mito kadhaa sasa hakuna tena, mito mingi imekauka. Kisa cha kukauka mito hii na mifereji ni wazungu wanaoitwa wawekezaji katika mashamba makubwa ya kahawa, hutumia maji hayo kumwagilia mashamba ya kahawa.

Katika mito ile, uoto asili umepotea.......mito na mifereji iliokuwa inatiririsha maji hakuna tena......wanyama kama kima waliokuwa wanaishi juu ya miti kando ya mito wanapotea......kima hao huingia majumbani kwa watu kutafuta chakula matokeo yake wengi huishia kuuwawa.

Kibanga Msese
 
Mkuu za kiujuma ni zipi hizo? Mimi nilicho jaribu kueleza ndo ninacho kifahamu, Hifadhi za Tiafa zilisha uzwa ila kimawazo bado ni hifadhi zetu lakini kwa Matendo zainawenyewe wanao faidika na hizo hifadhi

ila mtihani wa vyoo tulifeli vibaya sana !
 

Maji yanayo miminika kutoka milima Kilimanjaro kupitia mito kadhaa sasa hakuna tena, mito mingi imekauka. Kisa cha kukauka mito hii na mifereji ni wazungu wanaoitwa wawekezaji katika mashamba makubwa ya kahawa, hutumia maji hayo kumwagilia mashamba ya kahawa.

Katika mito ile, uoto asili umepotea.......mito na mifereji iliokuwa inatiririsha maji hakuna tena......wanyama kama kima waliokuwa wanaishi juu ya miti kando ya mito wanapotea......kima hao huingia majumbani kwa watu kutafuta chakula matokeo yake wengi huishia kuuwawa.

Kibanga Msese

Mkuu ni kweli kabisa, Na hakuna hata Mtanzania wa Chini atakaye nufaika na haya maajabu, Wazungu ndo watakao nufaika, na ndo maana wako mstari wa mbele kwenye kuhamasisha.
 

Wakuu mimi sitapiga kura kwa ajili ya Kutafuta Kivutio cha Tanzania Kitakacho Ingia Kwenye Maaajabu saba ya Bara La Africa kwa sababu zifuatazo,

1. Hifadhi za Taifa na Vivutio vingine havijawahi kunufaisha Watanzania

2. Watakao Nufaika na Hizo Kura ni Viongozi wa Ngazi za Juu pamoja na Wazungu, Ndo maana wazungu wako mbele sana kwenye kuhamasisha,

3. Hii kampeni ni neema kwa Wazungu na si Watanzania, sisi tutabakia kwenda kuomba vibalua tu kwao

4. Hoteli zote zilizo Jengwa kwenye Hifadhi za Serengeti na Ngorongoro zinamilikiwa wa wageni kwa asilimia 100, hakuna mzawa mmoja mwenye hoteli huko hata Camp tu,

5. Hifadhi za Serengeti, Ngorongoro na Zinginezo wanawathamini sana Watalii wa Kizungu na si Watanzania, watalii wa kitanzania huwa hawapewi umuhimu wowote ule katika hizo hifadhi, na Kuna Kipindi Hifadhi ya Ngorongori iliwahi kujenga Vyoo kwa ajili ya Wazungu na vingine kwa ajili ya Watu weusi/wabongo,

Na hadi leo hii Abilia wabongo wanaosafiri kwa Mabasi kwenda Musoma huwa wakifika Geti la Ngorongo hawaruhusiwi kutumia vyoo vya wageni bali kuna vya kwao viko Geti No 1 ukiwa unatokea Karatu kuingia Hifadhini

- Wakuu Sekta ya Utalii hapa Tanzania Inaongozwa na Wazungu Kutoka Ulaya, Marekani, South Africa na Wahindi, na watanzania ni wachache sana kwenye hii secta na wengi ni wafanya kazi tu na si wamiliki wa Makampuni ya utalii,

-Mlima Kilimanjaro- Huu Mlima wanao nufaika nao ni Makampuni ya Kitalii ya Wazungu yenye Makao makuu yao Mjini Arusha na Moshi, na asilimia zaidi ya 98 ya Makampuni ya Kitalii kanda ya Kasikazini yanamilikiwa na wazungu na ni asilimia kama 2 tu ndo inayo milikiwa na Wabongo na hata hivyo kampuni za wabongo ni Ndogo sana Kiuwezo ikilinganisha na Za wazungu

Makampuni mengi ya Kitalii yana Offisi huko kwao Ulaya na Marekani na Booking zote na Payment hufanyika huko huko Ulaya na Marekani huku wageni huja kupanda Mlima tu na mara nyingi na pesa za kununulia Vinyago na kuwapa Tips Madreva wanao waendesha, sasa je TRA inawezaje kukagua mapato ya hawa watu wakati acaunt ziko Ulaya na Marekani? na Malipo yanafanyika hukohuko Ulaya?

JE HAPO ANAYE NUFAIKA NI NANI?

2. HIFADHI YA SERENGETI
Hii nayo ni Hifadhi ya Taifa kwa Jina tu ila kimatendo wanao iongoza ni Wazungu kutoka Ulaya wa
Frankfurt Zoological society, hawa ndo wana usemi wa mwisho kuhusu hizi hifadhi na si Serengeti pekee bali hata Ngorongoro, wakiongea hakuna wakupinga kitu na Maranyingi wamekuwa wanakuja na Policy za kuwakandamizaWatanzania na kuwaona wanyama ndo wana haki pekee na si watanzania

3. Ngorongoro- hii nayo ni jina tu kwamba ni Hifadhi ya Taifa ila kimatendo hii hifadhi ni kama Limited Company,

Kwa kifupi wanaonufaika na Hifadhi na Vivutio vingine ni Wazungu na Watanzania Wachache wanao Torosha Wanyama kwenda Nje ya Nchi, Wananchi wengine tumebakia Mashabiki wa kuhamasishwa kupiga kura tu,

Ni iliaumu sana Serikali kwa kuto kuwezesha Watanzania wazawa Kumiliki Makampuni na Badala yake Makampuni yanamilikiwa na Wazungu, na wazawa wamebakia kuwa Vibarua

Mkuu hoja yako na wote walioiunga mkono ya kutokuupigia kura haina mashiko hata kidogo maana inaonyesha dhahiri umefikiria hatua moja mbele, naamini ungetulia kidogo na kufikiri miaka hata mitano mbele basi ungekuwa wakwanza kuupigia na kushawishi wengine waupigie kura pia....................kwani unadhani CCM watatawala milele?

Timiza wajibu wako kama mzalendo wa nchi hii maana kesho na keshokutwa wajibu wako utawasidia CUF au CDM au TLP au yeyote atakaye shika dola kuja kufaidi na matunda ya uzalendo wako
 
Mkuu ni kweli kabisa, Na hakuna hata Mtanzania wa Chini atakaye nufaika na haya maajabu, Wazungu ndo watakao nufaika, na ndo maana wako mstari wa mbele kwenye kuhamasisha.
Badilisha I'd yako kwanza,unanilazimisha nikuchukie japo umeongea p point.
 
Kitu cha ajabu ni cha ajabu tu hakina sababu ya kupigiwa kura.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
kwani tukivunja nao mkataba na ikaanzishwa taasisi ya hifadhi tanzania hatuwezi kutoka kama nchi?
 
Nashangaa dunia inatafuta vivutio vya kuingiza kwenye maajabu ya ulimwengu ilihali sisi wote Watanzania inatakiwa tuwekwe bila kupigiwa kura kwenye maajabu saba ya bara la Africa hata ya dunia tumeshakwishaqualify
 
Back
Top Bottom