Daimler
JF-Expert Member
- Sep 11, 2018
- 556
- 973
Wadau amani iwe kwenu.
Kwa wanaume ambao tunafanya shughuli za hapa na pale za kujipatia kipato, tumezoea kuwa na hela muda wote mfukoni. Hata hivyo, inapotokea siku umekosa kabisa fedha mfukoni na hauna njia ya haraka ya kuipata, njaa itaanza kukuuma hata mida ya saa 1 asubuhi.
Cha ajabu ni kuwa, hata ukifanikiwa kunywa chai muda wa saa 4 asubuhi, walahi hautatoboa saa 6 kwani njaa kali itakukamata balaa. Halafu mbaya, muda wa kwenda kunywa chai ama chakula cha mchana ukikaribia, unakosa kabisa amani na kushindwa kufanya kazi vyema.
Cha kushangaza ni kuwa, siku hela ikikutembelea, unaweza usiwe umekula chochote kuanzia asubuhi hadi jioni lakini still hauta-feel njaa kabisa.
Wadau sijui kama hali hii inanipata mimi tu ama inatupata wote.