Kwanini sherehe za muungano huwa hazifanyiki Zanzibar?

"SHEREHE ZA MUUNGANO MWAKA 2011"

Mvua yasitisha sherehe za Muungano
April 26, 2011

MVUA kubwa iliyoanza ghafla jana ilisitisha sherehe za maadhimisho yamiaka 47 ya muungano waTanganyikanaZanzibarkatika uwanja wa Amaan mjiniZanzibar.Sherehe hizo zilizoanza majira ya saa 3;00 asubuhi ziliingia dosari hiyo huku tayari mgeni rasmi Rais Jakaya Kikwete akiwa ameshakagua gwaride na kujumuika na viongozi wenzake katika jukwaa kuu.
Viongozi wengine waliokuwepo katika sherehe hizo ni pamoja na Rais wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar, Dk Ally Mohammed Shein, Makamu wake wa kwanza Seif Sharrif Hamad na makamamu wake wa pili Balozi Seid Idd.
Wengine waliokuwepo ni pamoja naMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dk Gharib Bilal, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Anna Makinda, Spika wa Baraza la Wawakilishi Pandu Ameir Kificho, Mkuu wa majeshi ya Ulinzi Davis Mwamunyange, Mkuu wa jeshi la Polisi Said Mwema, Rais mstaafu wa awamu ya pili Ally Hassan Mwinyi, Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa na Rais mstaafu wa awamuya sita wa SMZ Dk Salim Amour.
Vilevile walikuwepo viongozi wa vyama vya siasakamavile mwenyekiti wa Chama cha Wananchi, CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, Katibvu mkuu mstaafu wa CCM Philip Mangula, Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi James Mbatia na wanadiplomasia wanaoziwakisha nchi zao nchini.
Rais Kikwete aliingia uwanjani hapo majira ya saa nne asubuhi akiwa kwenye gari la wazi na kuwapungua mamia ya wananchi waliokuwepo uwanjani hapo na baadaye kukagua gwaride.
Baada ya hapo gwaride lilipita mbele ya jukwaa kuu kwa mwendo wa kasi na mwendo wa pole.
Ulipowadia wakati wa halaiki iliyoshirikisha wanafunzi 500, ndipo mvua ilianza kunyesha na baadaye kuivuruga kabisa sherehe hiyo.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo kipindi kilichokuwa kikifuata ni ngoma za asilia. Lakini mvua ilipozidi washereheshaji walitangaza kukatisha sherehe hiyo na viongozi wakaanza kuondoka.
Kauli mbiu ya sherehe hiyo ilikuwa ni "Miaka 47, tuwaenzi waasisi wetu, Tudumishe muungano, matunda ya miaka 47 ya mapinduzi na miaka 50 ya Uhuru, amani, utulivuna maendeleo ni matokeo ya muungano wetu, zilionekana kudorora hasa kutokana na mahudhurio hafifu ya wananchi. Sehemu mbalimbali za uwanja huo zilionekana kuwa wazi huku wafuasi wa CCM waliokuwa wamevaa sare nao wakiwa wachache.
Hata hivyo sherehe hizo zilionekana kudorora hasa kutokana na mahudhurio hafifu ya wananchi. Licha ya wanafunzi waliokuwa wamevaa sare nyeupe na wale waliovaa sawa na rangi za bendera ya Taifa na wafuasi wa CCM. Maeneomengine ya uwanja huo yalikuwa wazi.
Taarifa zaidi zinasema kuwa Serikaliilituma mabasi zaidi ya 20 vijijini ili kukusanya watu kwaajili ya kuhudhuria sherehe hizo, lakini hawakufika.
Hali hiyo imejitokeza huku kukiwa na manung'uniko mengi kutoka kwawananchi visiwani humo wakitaka muungano huo ufanyiwe tathimini upya.
Wakati huo huo, Umoja wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Zanzibar umetoa tamko kuhusu hali ya muungano.
Huku wakitoa ushahidi wa tume kadhaa zilizoundwa ili kutafuta maoni ya wananchi kama vile Tume ya Jaji Nyalali na ile ya Jaji Kisanga, jumuiya hizo zimesema kuwa muungano kati yaTanganyikanaZanzibarumekosa kukubalika ba Wazanzibari tangu siku yake ya kwanza hadi leo.
Huku wakikilaumu CCM kwa kuhodhimuungano, wamesema kuwa nguvu zaZanzibarkatika kama mshirika mmoja kamili wa muungano huo hazipio kwa kuongezewa mambo yamuungano nay ale yasiyo ya muungano yamekuwa yakiilemeaZanzibar.
"Kwa karibu miaka yote 47 muungano huu umekuwa ni miliki ya chama kimoja cha siasa cha CCM, ukitoa miaka michache ya 1964-1977".
Jumuiya hizo zimetaka kuwepo kwa majadiliano ya muungano ambapo wametaka pia nafasi ya Rais waZanzibarkatika muunganokamamakamu wa kwanza wa Rais.
"Mjadala wowote wa muungano ule urudishe nafasi ya rais waZanzibarkatika muungano na sio ilivyovyo hivi sasa ambapo Rais waZanzibarya maana wala amri yoyote ile katika muungano" imesema taarifa hiyo.
bi-samia.jpg

CHANZO: ZNZ KWETU

Ahsante kwa taarifa mkuu.Hata hivyo,bado hakuna uwiano na inaonekana zilifanyika kwa bahati mbaya tu!
 
Na pia juwa ofisi zote za muungano makao makuu yako bara z'bar ni mkoa tu sawa na shinyanga
 
Jamani hili ni swali ambalo mimi binafsi huwa najiuliza! Miaka karibu yote sherehe za Muungano huwa zinafanyikia uwanja wa Taifa jijini Dar-es-salaam kama sikosei ila kama nimekosea mwenye ukweli wa jambo hili atujuze.

Hii nayo inaweza kuwa ni kero mojawapo ya Muungano?
Sikutegemea swali jepesi kama hili litaulizwa na mtu mkongwe hapa great thinkers, mwaka jana sherehe hizi zilifanyika uwanja wa amani znz, lakini hakuna hata mtu aliyeuliza,sherehe hizi hufanyika kwa kupokezana kila mwaka bara na vizsiwani.
 
Sikutegemea swali jepesi kama hili litaulizwa na mtu mkongwe hapa great thinkers, mwaka jana sherehe hizi zilifanyika uwanja wa amani znz, lakini hakuna hata mtu aliyeuliza,sherehe hizi hufanyika kwa kupokezana kila mwaka bara na vizsiwani.

"sio kweli hata kidogo, sherehe hizi hazifanyiki kwa kupokezana, ni mara chache sana zimewahi fanyika huku zanzibar. hiyo mwaka JUZI na sio jana zilipofanyika huku hazikuwa na mvuto hata kidogo. ni ukweli usiopingika wengi wetu huku zanzibar hatuutaki huu muungano FEKI. ni kutawaliwa kwa nguvu tu kwa nchi yetu na tanganyika iliyojivisha jina la tanzania .... kama kweli tunataka muungano basi tuwe na muungano wa mashirikiano tu na si huu mfumo tulionao sasa"
 
Wakuu habari ya asubuhi; leo nimekuja na hoja kwamba ni kwanini mara nyingi sana sherehe za muungano hufanyikia tanzania bara tena kila mara dar na si kokote kule,huku znz waki bakia mdomo wazi sherehe kwao ni ndoto,je inatoa picha gani kwa wa znz?
 
Kama sio kwa nini? Mimi binafsi tangu jizaliwe mika zaidi 35 iliyopita sijawahi kusikia sherehe hizi zikifanyika zanzibar. I stand to be corrected!
 
Hili swali hata mimi niliwahi uliza hapa jukwaani.Sidhani kama utapata jibu la kuridhisha.
 
nasubiri majibu, na je siku ikija kufanyika zanzibar nani atapigiwa mizinga na kukagua gwaride?
 
Zifanyike Zanzibar kwani udongo ulichanganyiwa wapi?udongo ulichanganywa Tanganyika,so lazima zifanyike Tanganyika!
 
Hutakaa uelimike kwake wewe muungano ni kuazimisha zanzibar vinginevyo siyo muungano kweli kunawatu na viatu.
 
Zifanyike Zanzibar kwani udongo ulichanganyiwa wapi?udongo ulichanganywa Tanganyika,so lazima zifanyike Tanganyika!
Duh! uasanii mpaka Magogoni sijui upande wa pili wa wa usanii huu kisiwani panaitwaje,But God forbid kwa ujinga huu wa maccm kwa kudhani yanalinda muungano?Itakuwa balaa.Eeeh mungu shusha neema zako hawa interahamwe wajitambue.Hivi mtu mpuuzi kama mwalimu wa kwaya (Komba) na takakataka mwingine anayeitwa abdalla bulembo majura(hata jina lake nimeandika kwa lower case kwa jinsi alivyo lower case upstairs)wanaweza kusimama mbele yetru wananchi na kutamka uharo kama ule bungeni?Aaaaaarrggghhhhh! It's very much Flabbergasting,mmmxxxuuuu shenzi type kwa wajumbe wote waliobaki ktk genge la MABAMBA!
 
In spare time,different people have different hobbies.Some people may choose to go on a date with their lovers with beautiful hairdressing and fashionable clothes.To improve personal image,more and more people choose to wear synthetic wigs for women even including men.And to my surprise,there are mens long wigs for sale in the market.
 
Back
Top Bottom