Kwanini Serikali ya Kikwete imedhamiria kututaabisha, kututesa na kutukomoa?

TAMKO

JF-Expert Member
Oct 11, 2011
1,090
762
Tumeikosea nini maskini sisi wananchi, kwanini serikali hii itutendee hivi kikatili kila siku afadhali ya jana. kama lipo tulilo kukoseeni mtusamehe jamani lakini sio hivi. nchi yetu wenyewe lakini twaiona chungu kweli kweli.

BIASHARA mtaji utafute kwa jasho mwenyewe, ufungue ujasiriamali wako kisha sikilizia hiyo kero utayoipata mpaka upate leseni. ukiitenga bishara faster wameshawahi kudai makato ya kodi na ushuru ushenzi mtupu. mnavuna msipopataabikia.

wakulima wanasota kulima mazao yao, mtu anafungasha kiroba chake atoke porini aje mjini akiuze apate hela lau ya sukari anapambana na mlolongo wa mijitu njiani inakaba ipewe ushuru wa mazao, hata ndizi nne tano wanakukaba. mbaya zaidi huna pa kushtaki. Kiongozi yeyote utayemshatakia atakupatia kero kubwa zaidi.

kwenye usalama ndio Hovyo kabisa. Polisi mwenye uzalendo kumpata ni kama almasi. hata ikitokea akawepo ni tone la maji masafi kwenye bahari, system nzima imeoza. ukimwona polisi mwenye bidii ukampongeza kosa kubwa sana umemchongea kwa misukule mabosi wake watamtupia porini msimwone tena, polisi mzalendo ni adui wa kutisha sana ndani ya jeshi letu. naamini ipo CV maalum ya kumpa askari cheo kikubwa. nadhani lazima aprove ukatili wake na roho mbaya yake kabla ya kuwa mkuu wa kituo au kamishna. Siamini na tena sitaki kuamini kwamba Polisi wameshindwa kuligundua, kulisaka na kulitokomeza kundi la vijana hatari "mbwamwitu" ambao hufanya matukio makubwa na mabaya ya uharifu. miaka na miaka nasikia habari za kundi hilo. ni kundi la wavulana wadogo kabisa ambao sipati picha wakikua watakuwa na matunda gani ndani ya taifa letu.

kama kweli Intellijensia ya Polisi na serikali wameshindwa kulidhibiti kundi hili basi usalama wa nchi hii uko mashakani sana. Vijana hawa ambao interest yao ni fedha akitokea mjinga mmoa mwenye fedha akawafadhili ni rahisi kuwatoa kwenye mtazamo wa uchumi na kuwadumbukiza kwenye mtazamo wa kisiasa ambao madhara yake hayata pimika. sote tunajua dogodogo army ilianza kama kundi la vibaka kama hili.

polisi wa leo hawakamati wahalifu kabisa. ile tabia ya nyakati zile ukamwona polisi anatimua mhalifu na kumtia nguvuni haipo tena. kila mtaaa kuna vijana wanajipulizia mabange tu tena waziwazi na polisi wanawachekea tu. KIKWETE kwani nani kakulazimisha kuwa mkuu wa nchi?? Kushindwa uongozi ni kitendo cha uzalendo ACHA..! JIUZULU sio aibu..! NI USHUJAA.Uongozi ni Kipaji labda mwenyezi Mungu hakukupatia kipaji hicho babangu acha tu waachie wengine ni Ushujaa sio aibu.

unajichanganya mwenyewe unaichanganya na nchi basi mambo yote holela holela. Uliona wapi on earth mtu anaunda tume yeye mwenyewe, Tume imfanyie kazi yake yeye ya kukusanya maoni ya Kuunda katiba, kisha Tume inamletea majibu husika, anawapongeza na kuwasifia kwa kazi nzuri, anaikubali ripoti na kuilabel kwamba ni ripoti yake halali kwa kuisaini. anaipeleka pahala watu waijadili ripoti yake mwenyewe. kisha kwenye maneno ya utangulizi akiongea na wanamjadala anaanza kwa kuiponda ripoti yake mwenyewe. means anajiponda mwenyewe mbele ya kadamnasi hii kama sio zaidi ya kiroja ni nini. ?? kama from point Pai uliona ripoti sio unawamegea waziwazi kwamba HIKI-SICHO FULL STOP. . ni kama mfano wa baba mwenye nyumba, anaham ya kula jogoo, basi anawaita watoto wake anawaonyesha moja ya jogoo wakalikamate. wanapiga mbio na kwa jasho wanamkamatia mzee alichotaka. kisha mzeee anamwendea mchinjaji anamsihi amchinjie jogoo wake akamle. lakini wakati anamkabidhi mchinjaji anamponda sana jogoo, "kwanza jogoo mwenyewe hovyo, aliwahi kuugua kifaduro, jogoo huyu kwanza ana dengue, hata ukimchinja simli" Mchinjaji lazima abaki ameduwaa, huyu mzee vipi, kuku alete mwenyewe na kumponda amponde yeye huyo huyo tena..!!

Simtakii Mkuu wa nchi ashuke barabarani kuwakamata trafic wanaokamua madereva kila siku, simtakii raisi ashuke azikemee serikali za mitaa kwa kuwakaba raia kwa ushuru usio na tija, simtakii rais akawasake Mbwamwitu awaangamize no.. wajibu wake mkuu ni kuisimamia na kuitekeleza katiba aliyonayo mkononi mwake. kama tatizo ni mbwamwitu ng'oa wakuu wa polisi au wakuu wa kanda maalum weka wengine wameshindwa kazi ndio wajibu wako, rungu unalo mbona umeliweka uvunguni miaka karibia tisa sasa?. Raisi angekuwa na meno, akaisimamia katiba kikamilifu kiongozi mmoja angemwajibisha mwenzake na mwenzake na ufanisi wa kazi lazima ungetokea. asilimia kubwa ya wanawake wanaokwenda ofisi zenye mabosi wanaume ukianzia mawaziri lazima waombwe "ngono" . sikatai mwanamke kutongozwa lakini pale ngono inapoombwa kukiwa na hitaji kwa raia ni ubakaji na hongo ya nguvu. lakini unadhani ni kwanini Kiongozi anajiachia na kutumia ofisi kwa mambo yake binafsi ni kwa sababu ya UUngu-mtu aliojipachikia. anaamini hayupo wa kumwadabisha. hata kama yupo hana meno ya kung'ata ni mbwa koko tu. hata ukienda kumshataki kwa bosi wake bosi wake nae ndo zaidi yake. kama katiba ingetekelezeka hakuna ambaye angeichezea nchi, mpaka unakuta zanzibar wanampokonya Madaraka raisi naye anaangalia tu anachekelea hapo kuna mkuu wa nchi tena?.

ni kama mwanaume mwenye wake wawili, siku moja anakuja mwanaume na kumwambia kuanzia leo huyu bibi mdogo nachukua mimi, na wewe unachekelea tu.. hauwezi kuitwa mwanaume tena. jinsia ni ya kiume lakini matendo.. mm.

naandika haya kwa machungu sana kwa sababu ni wajibu wako.kama wananchi wa kiwalani leo wanateswka na mbwamwitu hao, kesho kkoo keshokutwa dar yote na kisha mikoani tarajia hata usalama wa makazi yako utakuwa hatarini. ukiwa kiongozi unajivunia ulinzi ila utashangaa kesho utapoacha uongozi ulinzi utayeyuka. hata kama utakuwa nao sio kivilee,.. unapewa askari koko wawili watatu ambao wakistuliwa mbio kisha utaona machungu ya mbwamwitu au wahalifu. sio vizuri kujivuna, ukiwa juu jua kesho utakuwa chini, kama usipokiondoa kinyesi leo utakuja chini utakikuta wewe na watoto wako na jamii yote. ukibisha rudia somo la historia. Ingawa kuna mazuri umeyafanya tunayaona, umetengeneza barabara kwa kweli hapo dole.. ingawa watu wanasema ni kazi ya magufuli lakini magufuli ni nani si waziri wako!! hapo dole, cha pili Umefanikiwa kumleta Obama Tanzania. heko. ingawa mie mwananchi wa kawaida sijaona matunda ya ziara yake. kingine kizuri umevunja rekodi ya kutembelea nchi nyingi zaidi kuliko rais Yeyote Tanzania. heko. na kingine una utu aisee, kutembelea wagonjwa, misiba na sherehe umevunja rekodi. kuna wakati niliwahi kupropose tuwe na maraisi wawili. rais mwenye meno ambaye ni mtendaji na mkuu wa nchi pamoja na ceremonial president.

Ok hata kama ni kweli kwamba CCM hiyo 2015 itaondoka madarakani, but kwa Muda uliobaki embu jaribu kuonyesha kwamba nchi hii ina Raisi. fanya liwalo na liwe, safisha nchi at least tukiwa wazee sana tuseme yule ceremonial president ukingoni mwa uongozi wake alipata meno, akaisafisha nchi..
 
Ni kutokuwa na mawazo ya nini alitakiwa kuifanyia Tanzania,alikuwa na nia ya kuitengeneza CV ionekane aliwahi kuwa RAIS.Pole zetu.
 
Naona umeandika kwa uchungu sana mpendwa. Hivi vipengele vya uwajibikaji wa polisi na viongozi maofisini vinanifanya naumia, pia mifano ya Tume ya katiba na Rais, pale naona mifano imesadifu. Sahihi kabisa.

Ila kwa ujumla umemlaumu sana Rais kwa "kutowajibika". Hilo nadhani siyo sahihi sana. Kosa kubwa siyo lake kwa kutowajibika. Kosa kubwa ni la wananchi kumchagua wakati walijua siyo muwajibikaji.

Nilikuwepo wakati anateuliwa kugombea. Nikawaambia "yule mwenzetu ni msanii tu, hatatupeleka kokote". Wakaniambia "ni mjeshi yule, wajeshi wako vizuri"! Basi siyo neno wakampa miaka mitano. Akavurunda, wote wakaona. Ikaja ile ngwe ya kuchaguana tena. Nikapiga kelele mpaka wakaniambia watanishughulikia! Lakini nikawaambia waache ushabiki kwani hata kama wanapikiwa ubwabwa, watakula jioni moja tu ila ubwabwa huo wataulipia kwa miaka mitano ya mauzauza na mafinyufinyu mchanganyiko. Bado wakampa tena! Sasa mlitaka afanye nini? Amefanya what he always does!

Kimsingi tujilaumu sisi kama Watanzania kwani tuna mamlaka ya kumpa au kutompa mtu dhamana ya kutuongoza. Ni kwa nini tukampa yeye? Ni wazi tunajua kabisa kuwa serikali ikiwa dhaifu nchi inakuwaje, lakini ni kwa nini tumewapa mamlaka hayo? Mbaya zaidi tunafanya nini kuhakikisha makosa hayarudii?

Najua imekuuma sana, hata mimi inaniuma. Na najua kuna wengine ambao inawauma zaidi, wale walioishia selo kwa kubambikiwa kesi na polisi, wale walioishia kubakwa na viongozi kama Kapuya, kwa kuwa wana shida, na huenda hata shida zao hazijatatuliwa. Wale waliofiwa na wapendwa wao theatre kwa sababu ya umeme kukatika wakati kodi wanalipa, hata na wale ambao wameishia kuwa mafukara wa kutupwa kwa sababu serikali haiwasaidii pembejeo, na hata wanapojitahidi masoko ni shida,wanalanguliwa, na wakijitahidi kujitwisha kichwani mazao yao wanakabiliana na system za majambazi wa kodi na ushuru!

Ila kulalamika pekee haisaidii. Hawa wataendelea kufanya hivyo. na tukiwapa nafasi tena wataendelea kurudia na uenda wakabuni mabaya zaidi! Nadhani ni wakati wa kuchukua hatua. Anza kwa kuwaelimisha wote unaowakuta kuhusu nguvu ya kura zao. Waambie wasirudie makosa tena. Waambie waache ushabiki wa kijinga kwani wanaoathirika mwishoni siyo wale wanaowashabikia ila ni wao!

Wasisitize kujisajili kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Wahimize kujitokeza kupiga kura muda ukifika. Waambie kura zao ni za maana katika kuleta mabadiliko nchini. Najua watakwambia zinaibiwa, lakini hiyo siyo sababu ya kufanya ushindi wa majambazi uwe rahisi. Halafu waambie na wao wakawaambie wenzao hivyo! Hapo utakuwa umesaidia sana kulipiga vita tatizo.
 
Tumeikosea nini maskini sisi wananchi, kwanini serikali hii itutendee hivi kikatili kila siku afadhali ya jana. kama lipo tulilo kukoseeni mtusamehe jamani lakini sio hivi. nchi yetu wenyewe lakini twaiona chungu kweli kweli.

BIASHARA mtaji utafute kwa jasho mwenyewe, ufungue ujasiriamali wako kisha sikilizia hiyo kero utayoipata mpaka upate leseni. ukiitenga bishara faster wameshawahi kudai makato ya kodi na ushuru ushenzi mtupu. mnavuna msipopataabikia.

wakulima wanasota kulima mazao yao, mtu anafungasha kiroba chake atoke porini aje mjini akiuze apate hela lau ya sukari anapambana na mlolongo wa mijitu njiani inakaba ipewe ushuru wa mazao, hata ndizi nne tano wanakukaba. mbaya zaidi huna pa kushtaki. Kiongozi yeyote utayemshatakia atakupatia kero kubwa zaidi.

kwenye usalama ndio Hovyo kabisa. Polisi mwenye uzalendo kumpata ni kama almasi. hata ikitokea akawepo ni tone la maji masafi kwenye bahari, system nzima imeoza. ukimwona polisi mwenye bidii ukampongeza kosa kubwa sana umemchongea kwa misukule mabosi wake watamtupia porini msimwone tena, polisi mzalendo ni adui wa kutisha sana ndani ya jeshi letu. naamini ipo CV maalum ya kumpa askari cheo kikubwa. nadhani lazima aprove ukatili wake na roho mbaya yake kabla ya kuwa mkuu wa kituo au kamishna. Siamini na tena sitaki kuamini kwamba Polisi wameshindwa kuligundua, kulisaka na kulitokomeza kundi la vijana hatari "mbwamwitu" ambao hufanya matukio makubwa na mabaya ya uharifu. miaka na miaka nasikia habari za kundi hilo. ni kundi la wavulana wadogo kabisa ambao sipati picha wakikua watakuwa na matunda gani ndani ya taifa letu.

kama kweli Intellijensia ya Polisi na serikali wameshindwa kulidhibiti kundi hili basi usalama wa nchi hii uko mashakani sana. Vijana hawa ambao interest yao ni fedha akitokea mjinga mmoa mwenye fedha akawafadhili ni rahisi kuwatoa kwenye mtazamo wa uchumi na kuwadumbukiza kwenye mtazamo wa kisiasa ambao madhara yake hayata pimika. sote tunajua dogodogo army ilianza kama kundi la vibaka kama hili.

polisi wa leo hawakamati wahalifu kabisa. ile tabia ya nyakati zile ukamwona polisi anatimua mhalifu na kumtia nguvuni haipo tena. kila mtaaa kuna vijana wanajipulizia mabange tu tena waziwazi na polisi wanawachekea tu. KIKWETE kwani nani kakulazimisha kuwa mkuu wa nchi?? Kushindwa uongozi ni kitendo cha uzalendo ACHA..! JIUZULU sio aibu..! NI USHUJAA.Uongozi ni Kipaji labda mwenyezi Mungu hakukupatia kipaji hicho babangu acha tu waachie wengine ni Ushujaa sio aibu.

unajichanganya mwenyewe unaichanganya na nchi basi mambo yote holela holela. Uliona wapi on earth mtu anaunda tume yeye mwenyewe, Tume imfanyie kazi yake yeye ya kukusanya maoni ya Kuunda katiba, kisha Tume inamletea majibu husika, anawapongeza na kuwasifia kwa kazi nzuri, anaikubali ripoti na kuilabel kwamba ni ripoti yake halali kwa kuisaini. anaipeleka pahala watu waijadili ripoti yake mwenyewe. kisha kwenye maneno ya utangulizi akiongea na wanamjadala anaanza kwa kuiponda ripoti yake mwenyewe. means anajiponda mwenyewe mbele ya kadamnasi hii kama sio zaidi ya kiroja ni nini. ?? kama from point Pai uliona ripoti sio unawamegea waziwazi kwamba HIKI-SICHO FULL STOP. . ni kama mfano wa baba mwenye nyumba, anaham ya kula jogoo, basi anawaita watoto wake anawaonyesha moja ya jogoo wakalikamate. wanapiga mbio na kwa jasho wanamkamatia mzee alichotaka. kisha mzeee anamwendea mchinjaji anamsihi amchinjie jogoo wake akamle. lakini wakati anamkabidhi mchinjaji anamponda sana jogoo, "kwanza jogoo mwenyewe hovyo, aliwahi kuugua kifaduro, jogoo huyu kwanza ana dengue, hata ukimchinja simli" Mchinjaji lazima abaki ameduwaa, huyu mzee vipi, kuku alete mwenyewe na kumponda amponde yeye huyo huyo tena..!!

Simtakii Mkuu wa nchi ashuke barabarani kuwakamata trafic wanaokamua madereva kila siku, simtakii raisi ashuke azikemee serikali za mitaa kwa kuwakaba raia kwa ushuru usio na tija, simtakii rais akawasake Mbwamwitu awaangamize no.. wajibu wake mkuu ni kuisimamia na kuitekeleza katiba aliyonayo mkononi mwake. kama tatizo ni mbwamwitu ng'oa wakuu wa polisi au wakuu wa kanda maalum weka wengine wameshindwa kazi ndio wajibu wako, rungu unalo mbona umeliweka uvunguni miaka karibia tisa sasa?. Raisi angekuwa na meno, akaisimamia katiba kikamilifu kiongozi mmoja angemwajibisha mwenzake na mwenzake na ufanisi wa kazi lazima ungetokea. asilimia kubwa ya wanawake wanaokwenda ofisi zenye mabosi wanaume ukianzia mawaziri lazima waombwe "ngono" . sikatai mwanamke kutongozwa lakini pale ngono inapoombwa kukiwa na hitaji kwa raia ni ubakaji na hongo ya nguvu. lakini unadhani ni kwanini Kiongozi anajiachia na kutumia ofisi kwa mambo yake binafsi ni kwa sababu ya UUngu-mtu aliojipachikia. anaamini hayupo wa kumwadabisha. hata kama yupo hana meno ya kung'ata ni mbwa koko tu. hata ukienda kumshataki kwa bosi wake bosi wake nae ndo zaidi yake. kama katiba ingetekelezeka hakuna ambaye angeichezea nchi, mpaka unakuta zanzibar wanampokonya Madaraka raisi naye anaangalia tu anachekelea hapo kuna mkuu wa nchi tena?.

ni kama mwanaume mwenye wake wawili, siku moja anakuja mwanaume na kumwambia kuanzia leo huyu bibi mdogo nachukua mimi, na wewe unachekelea tu.. hauwezi kuitwa mwanaume tena. jinsia ni ya kiume lakini matendo.. mm.

naandika haya kwa machungu sana kwa sababu ni wajibu wako.kama wananchi wa kiwalani leo wanateswka na mbwamwitu hao, kesho kkoo keshokutwa dar yote na kisha mikoani tarajia hata usalama wa makazi yako utakuwa hatarini. ukiwa kiongozi unajivunia ulinzi ila utashangaa kesho utapoacha uongozi ulinzi utayeyuka. hata kama utakuwa nao sio kivilee,.. unapewa askari koko wawili watatu ambao wakistuliwa mbio kisha utaona machungu ya mbwamwitu au wahalifu. sio vizuri kujivuna, ukiwa juu jua kesho utakuwa chini, kama usipokiondoa kinyesi leo utakuja chini utakikuta wewe na watoto wako na jamii yote. ukibisha rudia somo la historia. Ingawa kuna mazuri umeyafanya tunayaona, umetengeneza barabara kwa kweli hapo dole.. ingawa watu wanasema ni kazi ya magufuli lakini magufuli ni nani si waziri wako!! hapo dole, cha pili Umefanikiwa kumleta Obama Tanzania. heko. ingawa mie mwananchi wa kawaida sijaona matunda ya ziara yake. kingine kizuri umevunja rekodi ya kutembelea nchi nyingi zaidi kuliko rais Yeyote Tanzania. heko. na kingine una utu aisee, kutembelea wagonjwa, misiba na sherehe umevunja rekodi. kuna wakati niliwahi kupropose tuwe na maraisi wawili. rais mwenye meno ambaye ni mtendaji na mkuu wa nchi pamoja na ceremonial president.

Ok hata kama ni kweli kwamba CCM hiyo 2015 itaondoka madarakani, but kwa Muda uliobaki embu jaribu kuonyesha kwamba nchi hii ina Raisi. fanya liwalo na liwe, safisha nchi at least tukiwa wazee sana tuseme yule ceremonial president ukingoni mwa uongozi wake alipata meno, akaisafisha nchi..
Unajitesa peke yako, ujinga wako ndiyo unaokutesa, uzembe wako ndiyo unaokutesa, Upumba pumba wako ndiyo unakutesa. ACHA kutegemea kuletewa au Serikali kudhani itakuletea sukari na chunvi nyumbani kwako wala kudhani serikali itakufulia nguo zako, utasubiri hadi utanuka. UKAWA wanapiga posho ktk mikutano yao wewe ovyoooooooo.
 
Tumeikosea nini maskini sisi wananchi, kwanini serikali hii itutendee hivi kikatili kila siku afadhali ya jana. kama lipo tulilo kukoseeni mtusamehe jamani lakini sio hivi. nchi yetu wenyewe lakini twaiona chungu kweli kweli.

BIASHARA mtaji utafute kwa jasho mwenyewe, ufungue ujasiriamali wako kisha sikilizia hiyo kero utayoipata mpaka upate leseni. ukiitenga bishara faster wameshawahi kudai makato ya kodi na ushuru ushenzi mtupu. mnavuna msipopataabikia.

wakulima wanasota kulima mazao yao, mtu anafungasha kiroba chake atoke porini aje mjini akiuze apate hela lau ya sukari anapambana na mlolongo wa mijitu njiani inakaba ipewe ushuru wa mazao, hata ndizi nne tano wanakukaba. mbaya zaidi huna pa kushtaki. Kiongozi yeyote utayemshatakia atakupatia kero kubwa zaidi.

kwenye usalama ndio Hovyo kabisa. Polisi mwenye uzalendo kumpata ni kama almasi. hata ikitokea akawepo ni tone la maji masafi kwenye bahari, system nzima imeoza. ukimwona polisi mwenye bidii ukampongeza kosa kubwa sana umemchongea kwa misukule mabosi wake watamtupia porini msimwone tena, polisi mzalendo ni adui wa kutisha sana ndani ya jeshi letu. naamini ipo CV maalum ya kumpa askari cheo kikubwa. nadhani lazima aprove ukatili wake na roho mbaya yake kabla ya kuwa mkuu wa kituo au kamishna. Siamini na tena sitaki kuamini kwamba Polisi wameshindwa kuligundua, kulisaka na kulitokomeza kundi la vijana hatari "mbwamwitu" ambao hufanya matukio makubwa na mabaya ya uharifu. miaka na miaka nasikia habari za kundi hilo. ni kundi la wavulana wadogo kabisa ambao sipati picha wakikua watakuwa na matunda gani ndani ya taifa letu.

kama kweli Intellijensia ya Polisi na serikali wameshindwa kulidhibiti kundi hili basi usalama wa nchi hii uko mashakani sana. Vijana hawa ambao interest yao ni fedha akitokea mjinga mmoa mwenye fedha akawafadhili ni rahisi kuwatoa kwenye mtazamo wa uchumi na kuwadumbukiza kwenye mtazamo wa kisiasa ambao madhara yake hayata pimika. sote tunajua dogodogo army ilianza kama kundi la vibaka kama hili.

polisi wa leo hawakamati wahalifu kabisa. ile tabia ya nyakati zile ukamwona polisi anatimua mhalifu na kumtia nguvuni haipo tena. kila mtaaa kuna vijana wanajipulizia mabange tu tena waziwazi na polisi wanawachekea tu. KIKWETE kwani nani kakulazimisha kuwa mkuu wa nchi?? Kushindwa uongozi ni kitendo cha uzalendo ACHA..! JIUZULU sio aibu..! NI USHUJAA.Uongozi ni Kipaji labda mwenyezi Mungu hakukupatia kipaji hicho babangu acha tu waachie wengine ni Ushujaa sio aibu.

unajichanganya mwenyewe unaichanganya na nchi basi mambo yote holela holela. Uliona wapi on earth mtu anaunda tume yeye mwenyewe, Tume imfanyie kazi yake yeye ya kukusanya maoni ya Kuunda katiba, kisha Tume inamletea majibu husika, anawapongeza na kuwasifia kwa kazi nzuri, anaikubali ripoti na kuilabel kwamba ni ripoti yake halali kwa kuisaini. anaipeleka pahala watu waijadili ripoti yake mwenyewe. kisha kwenye maneno ya utangulizi akiongea na wanamjadala anaanza kwa kuiponda ripoti yake mwenyewe. means anajiponda mwenyewe mbele ya kadamnasi hii kama sio zaidi ya kiroja ni nini. ?? kama from point Pai uliona ripoti sio unawamegea waziwazi kwamba HIKI-SICHO FULL STOP. . ni kama mfano wa baba mwenye nyumba, anaham ya kula jogoo, basi anawaita watoto wake anawaonyesha moja ya jogoo wakalikamate. wanapiga mbio na kwa jasho wanamkamatia mzee alichotaka. kisha mzeee anamwendea mchinjaji anamsihi amchinjie jogoo wake akamle. lakini wakati anamkabidhi mchinjaji anamponda sana jogoo, "kwanza jogoo mwenyewe hovyo, aliwahi kuugua kifaduro, jogoo huyu kwanza ana dengue, hata ukimchinja simli" Mchinjaji lazima abaki ameduwaa, huyu mzee vipi, kuku alete mwenyewe na kumponda amponde yeye huyo huyo tena..!!

Simtakii Mkuu wa nchi ashuke barabarani kuwakamata trafic wanaokamua madereva kila siku, simtakii raisi ashuke azikemee serikali za mitaa kwa kuwakaba raia kwa ushuru usio na tija, simtakii rais akawasake Mbwamwitu awaangamize no.. wajibu wake mkuu ni kuisimamia na kuitekeleza katiba aliyonayo mkononi mwake. kama tatizo ni mbwamwitu ng'oa wakuu wa polisi au wakuu wa kanda maalum weka wengine wameshindwa kazi ndio wajibu wako, rungu unalo mbona umeliweka uvunguni miaka karibia tisa sasa?. Raisi angekuwa na meno, akaisimamia katiba kikamilifu kiongozi mmoja angemwajibisha mwenzake na mwenzake na ufanisi wa kazi lazima ungetokea. asilimia kubwa ya wanawake wanaokwenda ofisi zenye mabosi wanaume ukianzia mawaziri lazima waombwe "ngono" . sikatai mwanamke kutongozwa lakini pale ngono inapoombwa kukiwa na hitaji kwa raia ni ubakaji na hongo ya nguvu. lakini unadhani ni kwanini Kiongozi anajiachia na kutumia ofisi kwa mambo yake binafsi ni kwa sababu ya UUngu-mtu aliojipachikia. anaamini hayupo wa kumwadabisha. hata kama yupo hana meno ya kung'ata ni mbwa koko tu. hata ukienda kumshataki kwa bosi wake bosi wake nae ndo zaidi yake. kama katiba ingetekelezeka hakuna ambaye angeichezea nchi, mpaka unakuta zanzibar wanampokonya Madaraka raisi naye anaangalia tu anachekelea hapo kuna mkuu wa nchi tena?.

ni kama mwanaume mwenye wake wawili, siku moja anakuja mwanaume na kumwambia kuanzia leo huyu bibi mdogo nachukua mimi, na wewe unachekelea tu.. hauwezi kuitwa mwanaume tena. jinsia ni ya kiume lakini matendo.. mm.

naandika haya kwa machungu sana kwa sababu ni wajibu wako.kama wananchi wa kiwalani leo wanateswka na mbwamwitu hao, kesho kkoo keshokutwa dar yote na kisha mikoani tarajia hata usalama wa makazi yako utakuwa hatarini. ukiwa kiongozi unajivunia ulinzi ila utashangaa kesho utapoacha uongozi ulinzi utayeyuka. hata kama utakuwa nao sio kivilee,.. unapewa askari koko wawili watatu ambao wakistuliwa mbio kisha utaona machungu ya mbwamwitu au wahalifu. sio vizuri kujivuna, ukiwa juu jua kesho utakuwa chini, kama usipokiondoa kinyesi leo utakuja chini utakikuta wewe na watoto wako na jamii yote. ukibisha rudia somo la historia. Ingawa kuna mazuri umeyafanya tunayaona, umetengeneza barabara kwa kweli hapo dole.. ingawa watu wanasema ni kazi ya magufuli lakini magufuli ni nani si waziri wako!! hapo dole, cha pili Umefanikiwa kumleta Obama Tanzania. heko. ingawa mie mwananchi wa kawaida sijaona matunda ya ziara yake. kingine kizuri umevunja rekodi ya kutembelea nchi nyingi zaidi kuliko rais Yeyote Tanzania. heko. na kingine una utu aisee, kutembelea wagonjwa, misiba na sherehe umevunja rekodi. kuna wakati niliwahi kupropose tuwe na maraisi wawili. rais mwenye meno ambaye ni mtendaji na mkuu wa nchi pamoja na ceremonial president.

Ok hata kama ni kweli kwamba CCM hiyo 2015 itaondoka madarakani, but kwa Muda uliobaki embu jaribu kuonyesha kwamba nchi hii ina Raisi. fanya liwalo na liwe, safisha nchi at least tukiwa wazee sana tuseme yule ceremonial president ukingoni mwa uongozi wake alipata meno, akaisafisha nchi..


Kamwe, mwiko, haiwezekani na hawezi kuweza kufanya unavyofikiria. Kwanza hayo mawazo yako kamwe hatokaa yamfikie kwasababu counduits zake zote zinasema maneno ambayo yeye na chama chake wanataka kuyasikia. Your play wont be played forever on his ears!!!! Ni sisi wenyewe tuamke, tuwafundishe wenzetu wenye upeo mdogo na tuwauhishe wale wenye upeo mkubwa ambao wamepotezwa na mahitaji ya matumbo yao -- hapo tutaikomboa nchi hii.
 
Hufanyi kazi, upo tu kijiweni, tangu asbh hadi jioni, umevaa tu kata k unataka good life, kweli?
 
Unajitesa peke yako, ujinga wako ndiyo unaokutesa, uzembe wako ndiyo unaokutesa, Upumba pumba wako ndiyo unakutesa. ACHA kutegemea kuletewa au Serikali kudhani itakuletea sukari na chunvi nyumbani kwako wala kudhani serikali itakufulia nguo zako, utasubiri hadi utanuka. UKAWA wanapiga posho ktk mikutano yao wewe ovyoooooooo.

NI Kweli kabisa mkuu serikali haiwezi kuleta hivyo vitu ulivyovitaja, ila serikali inaweza kutengeneza unafuu wa upatikanaji wa hivyo vitu, mfano serikali ndio inaweza kudhibiti mfumuko wa bei, serikali ndio yenye uwezo wakutoa maji mto ruvu mpaka tandale kwa mtogole na sisi tukayapata kwa bei nafuu,,,, serikali ndio inaweza kufanya bei ya sabuni kuwa ndogo kwa kudhibiti wazalishaji, serikali ndio yenye uwezo wa kupunguza mfumuko wa bei ya vyakula na sisi wananchi tukapata hicho chakula kwa urahisi....serikali ndio yenye uwezo wakuleta umeme na gas ya kuaminika ili sisi tuipate kirahisi, au wewe mwenzetu unawezw kuufuata umeme kidatu na ukatandaza nguzo mpaka kwako tandika au mbagala kibondemaji??

hayo machache niliyoyataja ndio majukumu ya serikali kwa kuwa sisi ni wazalishaji na walipa kodi..
 
Toka huyu rais aingie madarakani hakuna alichofanya zaidi ya kusafiri tu na kutembeza bakuli.

Haya maendeleo tulio nayo hata asingekuwepo rais tungefikia tu tena yangezidi nina uhakika.

Nayakumbuka yale maneno ya John Mnyika bungeni kuhusu uzembe wa serikali ya CCM, mwanzoni nilishtuka nikaona amezidi mipaka ila sasa ninaona ni sawa tu tena ni zaidi ya pale.
 
Hufanyi kazi, upo tu kijiweni, tangu asbh hadi jioni, umevaa tu kata k unataka good life, kweli?

hivi wewe hizo kazi unazosema zikowapi?? watu wana degree, masters mpaka phd kazi hamna tuko nao mtaa, akinafulani haooo bungeni, au hujaona juzi wale walemavu walivyokuwa wakilalamika baada ya kujiajili bila support ya mtu halafu wamefanyiziwa, na danadana kama kawa baada ya kuomba maeneo,,
hebu tuambiee wewe hiyo kazi unayofanya kama umejiajili au ndo walewale, baba mdogo sijui shangazi...yaani kamlete.
usifikili mambo yako rahisi hivyo, hebu amka siku moja jifanye kama huna kazi wala mchongo wowote ndio unaanza harafu ingia mtaani utafute 1000-4000 mpaka jioni uone kama rahisi hiyo unavyosema,, acha kudharau watu kana kwamba hawajishughulishi vile ila wewe ndo pekee unafanya kazi,,, mbona hao walimu wanaofanya kazi wana miezi3 no salary, mbona hao wanaofanya kazi wanalalamikia PAYE, na gharama kubwa za maisha serikali sikivu iko kimya,,,, unajua gharama ya kuishi ya mtu asiye au aliye na familia kwa siku???
gharama ya chini ya chakula ni 10000/day - 10000 * 30 = 300000, bado matibabu, hujavaa, usafiri nk.
haya niambie kima cha chini cha mshahara ni sh ngapi? kina lingana na hizo gharama??

aiseeeeeeee,, anakofanyia kazi sio sehemu rasmi, anatakiwa aende karume anakuta vibanda vyote akinafulani wameshanunua, ameamua kuuza nguo mtaani mnamfukuza mnasema uchafu, haya ameamua kupiga debe daladala - mwendokasi hayo,, dah ameua mtaji amenunua bodaboda marufuku town, tigo nao wamemgeuza mtaji, basi yupo kijiweni tu anauza bangi mumkamate mumpeleke keko mchezo uishe.... wengine wameamua kwenda kulima pembejeo hamna, tumeamua kuwa wachimbaji wadogo-ooooh eneo kapewa mwekezaji,, na sisi tufanyeje sasa mnatuambia tufanye kazi, ipi sasa...
 
Mkuu,

Mtazamo wangu ni kwamba uongozi wa nchi ni taswira (reflection) ya jamii. Mara nyingi tunalalamika kuhusu uongozi mbovu lakini tunasahau ya kuwa hao viongozi ni sisi wenyewe tuliowaweka, na tunaoendelea kuwaweka madarakani. Wakati viongozi wa vyama vya upinzani wamefanya kazi kubwa sana ya kutoa elimu ya umma kuwatoa wananchi kwenye usingizi waliolala kwa miaka mingi ili wajielewe ya kuwa wao (wananchi) ndiyo wenye uwezo wa kuleta mabadiliko, bado kuna watu wachache wanaonufaika na hali hii ambao wameendelea kuwabeza na kuendelea kuwapulizia dawa ya usingizi mamilioni ya wananchi, walale, wasifurukute na serikali ya ccm iendelee kuwepo madarakani. Wako tayari mpaka kutumia vitisho mbalimbali tena hadharani mfano jeshi litachukua nchi, tutaingia msituni, nchi itakuwa ya kidini n.k. Matokeo yake wananchi waliolala usingizi wa pono, wamebakia kudanganywa na kuendelea kuwarudisha watu wale wale madarakani. Sasa nchi imekuwa ya ukoo wa panya, kuanzia baba, mama na watoto. Siyo siri ya kuwa wakati wa uchaguzi wa Mbunge wa jimbo la Chalinze baba na mama wametumia nafasi zao kumpigia debe kijana wao, kwa kutumia mali za serikali kwenye kampeni ya chama, kwa kuwa tu mgombea ubunge ni mtoto wa Rais. Siyo siri ya kuwa mgombea uchaguzi wa jimbo la Kalenga aliwekwa ili kuhakikisha ya kuwa ccm inashinda bila kuthibitisha ya kuwa mgombea mwenyewe hata si raia wa Tanzania. Hii ni mifano michache tu, lakini ukweli ni kwamba watu hao hao wa Chalinze na Kalenga wamewarudisha wagombea wa ccm kwenye nafasi za ubunge pamoja na kwamba ni wazi wangepata wabunge bora zaidi na wenye uchungu zaidi na wananchi wao kwa kuchagua wagombea wa vyama vya upinzani. Wananchi wamelala, na wanaongezewa dawa ya usingizi. Na wameridhika na hiyo hali wala hawaulizi maswali kama haya tunayouliza wewe na mimi.

Mpaka hapo jamii itakapobadili mtazamo wake, wananchi watakapozinduka kutoka usingizini na kugundua ya kuwa ukiona manyoya ujue keshaliwa, hakutakuwa na mabadiliko ya kweli. La kufanya sasa ni wewe na mimi kuendelea kutoa elimu ya umma, elimu ya utaifa, ili sisi tulioona mwanga tuwaonyeshe mwanga na wale walioko bado usingizini.

Kazi bado ni ngumu, lakini kitaeleweka!
 
Acha kulalamika,mjini kuna mbwana wengi,kama maisha yamekushinda tafuta bwana.uzembe wako mwenyewe halafu unalaumu serekali.
 
Nasema kama MTAENDEKEZA UZEMBE, huku kutwa mkicheza vigodoro, hamwezi pata maisha mazuri kamwe! Tuchapeni kazi vijana.
 
Naona umeandika kwa uchungu sana mpendwa. Hivi vipengele vya uwajibikaji wa polisi na viongozi maofisini vinanifanya naumia, pia mifano ya Tume ya katiba na Rais, pale naona mifano imesadifu. Sahihi kabisa.

Ila kwa ujumla umemlaumu sana Rais kwa "kutowajibika". Hilo nadhani siyo sahihi sana. Kosa kubwa siyo lake kwa kutowajibika. Kosa kubwa ni la wananchi kumchagua wakati walijua siyo muwajibikaji.

Nilikuwepo wakati anateuliwa kugombea. Nikawaambia "yule mwenzetu ni msanii tu, hatatupeleka kokote". Wakaniambia "ni mjeshi yule, wajeshi wako vizuri"! Basi siyo neno wakampa miaka mitano. Akavurunda, wote wakaona. Ikaja ile ngwe ya kuchaguana tena. Nikapiga kelele mpaka wakaniambia watanishughulikia! Lakini nikawaambia waache ushabiki kwani hata kama wanapikiwa ubwabwa, watakula jioni moja tu ila ubwabwa huo wataulipia kwa miaka mitano ya mauzauza na mafinyufinyu mchanganyiko. Bado wakampa tena! Sasa mlitaka afanye nini? Amefanya what he always does!

Kimsingi tujilaumu sisi kama Watanzania kwani tuna mamlaka ya kumpa au kutompa mtu dhamana ya kutuongoza. Ni kwa nini tukampa yeye? Ni wazi tunajua kabisa kuwa serikali ikiwa dhaifu nchi inakuwaje, lakini ni kwa nini tumewapa mamlaka hayo? Mbaya zaidi tunafanya nini kuhakikisha makosa hayarudii?

Najua imekuuma sana, hata mimi inaniuma. Na najua kuna wengine ambao inawauma zaidi, wale walioishia selo kwa kubambikiwa kesi na polisi, wale walioishia kubakwa na viongozi kama Kapuya, kwa kuwa wana shida, na huenda hata shida zao hazijatatuliwa. Wale waliofiwa na wapendwa wao theatre kwa sababu ya umeme kukatika wakati kodi wanalipa, hata na wale ambao wameishia kuwa mafukara wa kutupwa kwa sababu serikali haiwasaidii pembejeo, na hata wanapojitahidi masoko ni shida,wanalanguliwa, na wakijitahidi kujitwisha kichwani mazao yao wanakabiliana na system za majambazi wa kodi na ushuru!

Ila kulalamika pekee haisaidii. Hawa wataendelea kufanya hivyo. na tukiwapa nafasi tena wataendelea kurudia na uenda wakabuni mabaya zaidi! Nadhani ni wakati wa kuchukua hatua. Anza kwa kuwaelimisha wote unaowakuta kuhusu nguvu ya kura zao. Waambie wasirudie makosa tena. Waambie waache ushabiki wa kijinga kwani wanaoathirika mwishoni siyo wale wanaowashabikia ila ni wao!

Wasisitize kujisajili kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Wahimize kujitokeza kupiga kura muda ukifika. Waambie kura zao ni za maana katika kuleta mabadiliko nchini. Najua watakwambia zinaibiwa, lakini hiyo siyo sababu ya kufanya ushindi wa majambazi uwe rahisi. Halafu waambie na wao wakawaambie wenzao hivyo! Hapo utakuwa umesaidia sana kulipiga vita tatizo.

sure
ingawa hakuna ajwa ya miaka. kumpa dereva mbovu aendeshe gari lako kwa miaka kumi ni muda mwingi sana. jambo hili tulitazame upya, hakunaga spea ya miaka ikipita imepita.
 
Nasema kama MTAENDEKEZA UZEMBE, huku kutwa mkicheza vigodoro, hamwezi pata maisha mazuri kamwe! Tuchapeni kazi vijana.

walioshiba wana matusi nyie.. wamejisahau sana. ukisha kalia kiti cha madaraka huku kwetu Afrika na kaukichaa flan kanakuandama na ulevi wa kiaina. unajiapiza wewe uko salama pande zote, mtu akilalamika tatizo anaitwa mjinga, mzembe, hohehahe, mpuuzi flan, maisha ni mzunguko frend, si uko juu, hapa chini unadhani panamngojea nani utatua tu tena soon kama huamini mwone Joyce Banda huko Malawi, uchizi umempata baada ya kuhisi anang'oka madarakani. anakurupuka kukaba demokrasia kwa kusitisha zoezi la kuhesabu kura, too late. anataka apewe 90 days, ajipange kuondoka manake alikuwa hata kisaikolojia hajajiandaa kuachia nchi, ndio maaana kale ka msemo cheo ni dhamana CCM wameshakazika kwenye kaburi lisiloonekana, watashangaa.!!
 
na bado mwendo ni huo huo......tena ngoja uchaguzi 2015 tushinde tena hamna rangi mtaacha kuona
 
sure
ingawa hakuna ajwa ya miaka. kumpa dereva mbovu aendeshe gari lako kwa miaka kumi ni muda mwingi sana. jambo hili tulitazame upya, hakunaga spea ya miaka ikipita imepita.

Sure.
Nadhani tuanzie hapa, sasa, mimi na wewe. We go out there, tell everybody ajiandikishe kupiga kura, na akapige kura. Tuwaambie waache ubwege wa kuuza vitambulisho vya kupigia kura. Na waache kuchagua mabwege!

What do you say?
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom