Kwanini Serikali mnapandisha madaraja watumishi kwa upendeleo?

Trust None

JF-Expert Member
Feb 12, 2018
1,260
4,415
Ni wazi kuwa katika mchakato wa kupanda madaraja watumishi ajira mpya 2012, walipanda lakini wakanyang'anywa mwaka 2016.

Wengine (wa 2012) wakapanda mwaka 2017 na wengine 2018 na wameendelea na mishahara mipya mpaka leo. Kwanini walipandisha baadhi ya halmashauri?

Waraka mpya wa kupandisha madaraja kuanzia mei mos 2019 naona unatekelezwa tofauti katika halmashauri tofauti. Wengine wanapandisha wa 2012 tu, wengine 2012 na 2013, wengine 2012, 2013 na 2014. Katika ufatiliaji wanadai kuwa walipokea maagizo ya kufanya wanayoyafanya. Kwanini watoe waraka baadae watoe maagizo kimyakimya?

HOJA:
-Je, hayo maagizo wamepewa baahi ya halmashauri tu?
-Kwanini wanapandisha tofauti tofauti kama maagizo yapo sawa?
-Ni uzembe wa maafisa utumishi?
-Kama mishahara inalipwa na hazina, bajeti za halmashauri zinahusikaje?

NB: Uchunguzi unaendelea mpaka mishahara itoke tuone kama wanapanda kwa maneno au matendo.
 
Nasikia walipanda wa kinondoni kipindi cha utakatishaji wa ubunge wa mtulia.
 
Ni wazi kuwa katika mchakato wa kupanda madaraja watumishi ajira mpya 2012, walipanda lakini wakanyang'anywa mwaka 2016.

Wengine (wa 2012) wakapanda mwaka 2017 na wengine 2018 na wameendelea na mishahara mipya mpaka leo. Kwanini walipandisha baadhi ya halmashauri?

Waraka mpya wa kupandisha madaraja kuanzia mei mos 2019 naona unatekelezwa tofauti katika halmashauri tofauti. Wengine wanapandisha wa 2012 tu, wengine 2012 na 2013, wengine 2012, 2013 na 2014. Katika ufatiliaji wanadai kuwa walipokea maagizo ya kufanya wanayoyafanya. Kwanini watoe waraka baadae watoe maagizo kimyakimya?

HOJA:
-Je, hayo maagizo wamepewa baahi ya halmashauri tu?
-Kwanini wanapandisha tofauti tofauti kama maagizo yapo sawa?
-Ni uzembe wa maafisa utumishi?
-Kama mishahara inalipwa na hazina, bajeti za halmashauri zinahusikaje?

NB: Uchunguzi unaendelea mpaka mishahara itoke tuone kama wanapanda kwa maneno au matendo.

Fanyeni kazi acheni malalamiko , tunajenga uchumi kwanza.
 
Ni wazi kuwa katika mchakato wa kupanda madaraja watumishi ajira mpya 2012, walipanda lakini wakanyang'anywa mwaka 2016.

Wengine (wa 2012) wakapanda mwaka 2017 na wengine 2018 na wameendelea na mishahara mipya mpaka leo. Kwanini walipandisha baadhi ya halmashauri?

Waraka mpya wa kupandisha madaraja kuanzia mei mos 2019 naona unatekelezwa tofauti katika halmashauri tofauti. Wengine wanapandisha wa 2012 tu, wengine 2012 na 2013, wengine 2012, 2013 na 2014. Katika ufatiliaji wanadai kuwa walipokea maagizo ya kufanya wanayoyafanya. Kwanini watoe waraka baadae watoe maagizo kimyakimya?

HOJA:
-Je, hayo maagizo wamepewa baahi ya halmashauri tu?
-Kwanini wanapandisha tofauti tofauti kama maagizo yapo sawa?
-Ni uzembe wa maafisa utumishi?
-Kama mishahara inalipwa na hazina, bajeti za halmashauri zinahusikaje?

NB: Uchunguzi unaendelea mpaka mishahara itoke tuone kama wanapanda kwa maneno au matendo.
60% Wanaopandishwa katika miaka hiyo 2012,2013 wengi wanatia Rushwa,

Rushwa zimetawala maofisin hasa idara zinazohusika na orodha ya upandishaji madaraja
 
Utumishi bado hajapatikan mtu sahihi ...kuna baadhi ya kero za wafanyakazi ni rahisi lakini wanashindwa kuzikabili
 
Kigoma Ujiji hali ni hiyo hiyo 2011 wachache hawakupanda 2012+ hao wote No kupanda madaraja kweli hali ni tete aisee kazi imekua utumwa na si msaada kwa utumishi
 
Nchi moja,mmeajiriwa au mlipanda cheo mwaka mmoja nyuma ila kuja kupata cheo kingine mnatofautiana,na hapo mtu huna kosa lolote la kiutumishi,it's not fair
Utumishi mjipange...
 
Uzembe wa halmashauri.
Mwaka huu wapo ambao washapanda. Lkn halmashauri nyingine bado kama ya g
 
Nchi moja,mmeajiriwa au mlipanda cheo mwaka mmoja nyuma ila kuja kupata cheo kingine mnatofautiana,na hapo mtu huna kosa lolote la kiutumishi,it's not fair
Utumishi mjipange...
Hawapo fair kabisa intake ya 2012 Geita walipanda 2016. Kigoma/Ujiji wote intake hiyo hawajapanda na baadhi wamesoma pamoja utegemee kuna jipya hapo Serikali yetu haina fair kabisa ktk hili
 
Uzembe wa halmashauri.
Mwaka huu wapo ambao washapanda. Lkn halmashauri nyingine bado kama ya geita
 
Kimsingi maagizo yanayotolewa hadharani au kwenye nyaraka ni tofauti na kinachofanyika maofisini.
 
Acha kulalamika vigezo vipo hapa. Soma hiyoo!
IMG-20190511-WA0002.jpeg
IMG-20190511-WA0000.jpeg
IMG-20190511-WA0001.jpeg
IMG-20190511-WA0003.jpeg
 
mwenzenu nilikaa miaka 12 bila kupanda daraja nikaamua kupiga chini kibarua nikaanza maisha mengine nje ya safina ya utumishi kiukweli nilipata changamoto ya kutoungwa mkono na mtu yeyote kuanzia kwenye familia yangu hadi ukoo lakini Mola hamtupi mja wake leo wana enjoy na watoto wanasoma shule bora, makazi bora na biashara inaendelea nilishasahau maisha ya kitumwa ya kupeleka mbuzi au hela ndo upande daraja na miaka mitatu ijayo kama mambo yatenda kama yanavyokwenda basi nitakuwa na mtaji sawasawa pension ambayo ningeipewa miaka 24 ijayo.
 
Back
Top Bottom