Kwanini Serikali inawabagua walimu wenye shahada kwenye ajira?

msovero

JF-Expert Member
Jun 30, 2019
839
1,472
Kuna kitu hakipo sawa kwenye ajira za walimu.

Kwenye kila kibali cha ajira kinachotoka idadi ya walimu wenye shahada wapatao fursa ya kuajiriwa serikalini huwa ni ndogo sana kulinganisha na walimu wa ngazi zingine za kielimu kama vile cheti na diploma.

Kielelezo kizuri ni ajira zilizotoka juzi ukizichunguza kwa makini utakubaliana na hiki ninachokisema.

Kwani katika hizo ajira, wenye shahada walioajiriwa hawafiki hata robo ya waajiriwa wote(wapo chini ya 1500 kati ya 8000).

Tukumbuke asilimia kubwa ya walimu hawa wamesomeshwa na serikali hivyo wanadaiwa na bodi ya mikopo(HESLB). Lakini cha kushangaza serikali ni kama inatoa kipaumbele kidogo kwa wao kuajiriwa.

Je, ni kipi hasa kinafanya walimu hao waajiriwe kwa uchache kuliko walimu wengine?

Je, watalipaje madeni yao ya mikopo kama serikali itaendelea kuwaacha mitaani?
 
Mbona jibu simple kabisa hapo, kwani hujui mwenye degree atatakiwa kulipwa mshahara mkubwa zaid ya mwenye cheti na diploma?
mshahara wa wenye degree watano, utakwenda kwa wenye cheti na diploma 50.

Ni hayo tu, maendeleo hayana chama
Umepotosha mkuu,tofauti ya mshahara kwa Mwalimu Wa diploma na degree ni almost 190,000 kwa uwiano Wa daraja C na D sasa hio ya walimu watano Wa degree kiajili walimu 50 Wa diploma na Cheti inatoka wapi?

Maana hata Mwalimu Wa degree mmoja kwa mshahara wake hawezi kuajiri walimu wawili,maana mwalimu Wa Cheti anaanza na daraja B amabalo linamshahara Wa 400,000+ ,wakati mwalimu Wa degree ananza na mshahara usiozidi 720,000
 
Kuna kitu hakipo sawa kwenye ajira za walimu.

Kwenye kila kibali cha ajira kinachotoka idadi ya walimu wenye shahada wapatao fursa ya kuajiriwa serikalini huwa ni ndogo sana kulinganisha na walimu wa ngazi zingine za kielimu kama vile cheti na diploma.

Kielelezo kizuri ni ajira zilizotoka juzi ukizichunguza kwa makini utakubaliana na hiki ninachokisema. Kwani katika hizo ajira, wenye shahada walioajiriwa hawafiki hata robo ya waajiriwa wote(wapo chini ya 1500 kati ya 8000).

Tukumbuke asilimia kubwa ya walimu hawa wamesomeshwa na serikali hivyo wanadaiwa na bodi ya mikopo(HESLB). Lakini cha kushangaza serikali ni kama inatoa kipaumbele kidogo kwa wao kuajiriwa.

Je, ni kipi hasa kinafanya walimu hao waajiriwe kwa uchache kuliko walimu wengine?

Je, watalipaje madeni yao ya mikopo kama serikali itaendelea kuwaacha mitaani?
Ni sababu ya kutaka kujificha ktk takwimu, kwa malengo ya kuonyesha serikali imetoa ajira nyingi ktk sekta ya elimu na wala si shahuku ya kutaka kutoa elimu bora.

Sent from my Nokia 2.1 using JamiiForums mobile app
 
Umepotosha mkuu,tofauti ya mshahara kwa Mwalimu Wa diploma na degree ni almost 190,000 kwa uwiano Wa daraja C na D sasa hio ya walimu watano Wa degree kiajili walimu 50 Wa diploma na Cheti inatoka wapi?

Maana hata Mwalimu Wa degree mmoja kwa mshahara wake hawezi kuajiri walimu wawili,maana mwalimu Wa Cheti anaanza na daraja B amabalo linamshahara Wa 400,000+ ,wakati mwalimu Wa degree ananza na mshahara usiozidi 720,000
Uko sahihi mkuu
 
Si mlikuwa mnajifanya mnafaulu Sana ma-A A na ma B mkachaguliwa directly mkasome bachelor huko ....
Sie ambao maksi zetu tia mchuzi tulianzia level ndogo saivi tumekula shavu....

Msipende kujifanya mna akili Sana ,mkafaulu Sana mkatuona Sisi vilaza haya vipi na madigirii yenu. "mjiajiri" hakuna namna.


Use Ur brain...
 
Jibu lako ni hili hapa.

Walimu hao wenye degree ni wachache ukilinganisha na wenye certificate na ndio maana katika kuajiri utaona wao wachache kwa idadi ila kwenye ratio ni sawasawa tu...

Watu wanabwabwaja tu.
Hiyo ilikuwa zamani mkuu...
Kwa sasa wenye degree wapo wengi sana wanaweza kuwapita hata wenye diploma. Mf. Chuo kimoja tu cha Dar (udsm) kinazalisha zaidi ya walimu 2000 kwa mwaka lakini kati ya hao wanaopata fursa za ajira ni chini ya walimu 500 Wengine zaidi ya 1500 wanaachwa. Kwa muktadha kama huo huwezi kusema ratio iko sawa sawa ikiwa idadi ya waajiriwa ni ndogo mara dufu ya idadi ya wanaoachwa...
 
Hiyo ilikuwa zamani mkuu...
Kwa sasa wenye degree wapo wengi sana wanaweza kuwapita hata wenye diploma. Mf. Chuo kimoja tu cha Dar (udsm) kinazalisha zaidi ya walimu 2000 kwa mwaka lakini kati ya hao wanaopata fursa za ajira ni chini ya walimu 500 Wengine zaidi ya 1500 wanaachwa. Kwa muktadha kama huo huwezi kusema ratio iko sawa sawa ikiwa idadi ya waajiriwa ni ndogo mara dufu ya idadi ya wanaoachwa...
Kuna vyuo vya kati 35 vinavyotoa cheti na diploma nchi nzima.
Makadirio ya wahitimu kwa chuo kimoja ni >500 kwa mwaka...
Piga 500 x 35 = 17500 ...hayo ni makadirio ya chini,
Kwahiyo idadi ya walimu wa cheti na diploma wanaohitimu kwa mwaka ni kubwa kuliko degree,
 
Umepotosha mkuu,tofauti ya mshahara kwa Mwalimu Wa diploma na degree ni almost 190,000 kwa uwiano Wa daraja C na D sasa hio ya walimu watano Wa degree kiajili walimu 50 Wa diploma na Cheti inatoka wapi?

Maana hata Mwalimu Wa degree mmoja kwa mshahara wake hawezi kuajiri walimu wawili,maana mwalimu Wa Cheti anaanza na daraja B amabalo linamshahara Wa 400,000+ ,wakati mwalimu Wa degree ananza na mshahara usiozidi 720,000

Mshahara wa mwalimu wa degree unazidi kiasi ulichokitaja.
 
Si mlikuwa mnajifanya mnafaulu Sana ma-A A na ma B mkachaguliwa directly mkasome bachelor huko ....
Sie ambao maksi zetu tia mchuzi tulianzia level ndogo saivi tumekula shavu....
Msipende kujifanya mna akili Sana ,mkafaulu Sana mkatuona Sisi vilaza haya vipi na madigirii yenu ...."mjiajiri" hakuna namna.








Use Ur brain...
Unajua maana ya Brain?
 
Back
Top Bottom