Kwanini Salum Mwalim hafai kuwa mbunge Kinondoni?

wandamba

JF-Expert Member
Apr 29, 2014
510
839
Salum Mwalimu ni mmoja wapo wa wagombea Ubunge jimbo la Kinondoni kwenye uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika Februari 17, 2018.

Ni ukweli ulio dhahiri Salum Mwalim sio chaguo letu wakazi wa jimbo la Kinondoni kutokana na sababu zifuatazo:-

1. Hana Ilani ya uchaguzi

Hii ni sababu inayomfanya Salum Mwalimu kutokufaa kuwa Mbunge jimbo la Kinondoni. Chama kilichoshinda na kushika dola kuanzia 2015 hadi 2020 ni CCM ambacho ilani yake ndio inaongoza Serikali.

Leo Salum Mwalimu anapoomba ridhaa ya kuwa Mbunge ataleta maendeleo kwa ilani ipi? Kwanini wana Kinondoni wamchague Mtu asiye na ilani, asiyeweza kuwaletea maendeleo?

2. Hana pesa za kutekeleza ahadi zake

Salum hakubaliani na ilani ya CCM ambayo ndio inaongoza dola, ndio yenye Serikali inayomiliki pesa zote hapa nchini. Anayowahaidi wana Kinondoni atatekeleza kwa ilani ipi? Salum atapata wapi pesa za kutoa huduma za kijamii? Atatoa wapi pesa za kujenga miundombinu? Atatoa wapi mabilioni ya kuwapa mikopo vijana na kina Mama endapo hakubaliani na ilani ya CCM? Kama hayawezi yote hayo, atawezaje kuwaletea maendeleo wana Kinondoni?

3. Chama chake hakina mahusiano mema na Serikali

Kwa nyakati zote Chadema wamekuwa hawana mahusiano mema na Serikali ndio maana kutwa wanaitukana Serikali majukwaani, mitandaoni na mikutanoni. Wanaitukana Serikali ambayo ndio ina ilani, inamiliki pesa zote, inayopanga namna ya kupeleka maendeleo.

Salum anautaka Ubunge wakati anajua fika chama chake hakina mahusiano mema na Serikali inayotekeleza ilani ya uchaguzi. Atawezaje kuwaletea maendeleo wana Kinondoni?

4. Hana uzoefu
Salum anaomba kura aende Bungeni kwenda kujifunza namna ya kufanya kazi. Hana uzoefu wowote ule, anahitaji muda wa kujifunza na si kipindi hiki ambacho wana Kinondoni wanahitaji kiongozi mwenye uzoefu, wanahitaji maendeleo.

Narudia tena kusema Salum Mwalim hafai kuwa Mbunge wa Kinondoni.

Mussa Seif,
Bodaboda Kinondoni.
 
wandamba Hoja hazina mashiko kwa sababu

1. Kutokuwep maelewan ya chama kwa cham haihusian na kuleta maendeleo

2. Anayetoa pes za maendeleo ya jimbo siyo cham hiy ni mipango ya serikal
 
Pole sana naona umeandika uhalo mtupu. Uliponiacha hoi eti Boda2 Kinondoni nyambafu.
 
Hivi mpaka tunafikia kiwango hiki cha umasikini wa kutisha, elimu duni, maradhi ya kupindukia na rushwa iliyokithiri (mpaka akaja mtumbua majipu) ni kwa sababu hatukuwa na ilani za uchaguzi!??

Mradi tumeshajijua kuwa sisi ni wajinga basi tusiendeleze ujinga huo, sema tu umeandika kwa simu lakini ingelikuwa wino na karatasi ungepata hasara zaidi ya muda uliotumia kuandika huu upuuzi.
 
Salum Mwalim ni mmoja wapo wa wagombea Ubunge jimbo la Kinondoni kwenye uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika Februari 17, 2018.

Ni ukweli ulio dhahiri Salum Mwalim sio chaguo letu wakazi wa jimbo la Kinondoni kutokana na sababu zifuatazo:-

1. *Hana Ilani ya uchaguzi*

Hii ni sababu inayomfanya Salum Mwalim kutokufaa kuwa Mbunge jimbo la Kinondoni. Chama kilichoshinda na kushika dola kuanzia 2015 hadi 2020 ni CCM ambacho ilani yake ndio inaongoza Serikali.

Leo Salum Mwalim anapoomba ridhaa ya kuwa Mbunge ataleta maendeleo kwa ilani ipi? Kwanini wana Kinondoni wamchague Mtu asiye na ilani, asiyeweza kuwaletea maendeleo?

2. *Hana pesa za kutekeleza ahadi zake*

Salum hakubaliani na ilani ya CCM ambayo ndio inaongoza dola, ndio yenye Serikali inayomiliki pesa zote hapa nchini. Anayowahaidi wana Kinondoni atatekeleza kwa ilani ipi? Salum atapata wapi pesa za kutoa huduma za kijamii? Atatoa wapi pesa za kujenga miundombinu? Atatoa wapi mabilioni ya kuwapa mikopo vijana na kina Mama endapo hakubaliani na ilani ya CCM? Kama hayawezi yote hayo, atawezaje kuwaletea maendeleo wana Kinondoni?

3. *Chama chake hakina mahusiano mema na Serikali*

Kwa nyakati zote Chadema wamekuwa hawana mahusiano mema na Serikali ndio maana kutwa wanaitukana Serikali majukwaani, mitandaoni na mikutanoni. Wanaitukana Serikali ambayo ndio ina ilani, inamiliki pesa zote, inayopanga namna ya kupeleka maendeleo.

Salum anautaka Ubunge wakati anajua fika chama chake hakina mahusiano mema na Serikali inayotekeleza ilani ya uchaguzi. Atawezaje kuwaletea maendeleo wana Kinondoni?

4. *Hana uzoefu*
Salum anaomba kura aende Bungeni kwenda kujifunza namna ya kufanya kazi. Hana uzoefu wowote ule, anahitaji muda wa kujifunza na si kipindi hiki ambacho wana Kinondoni wanahitaji kiongozi mwenye uzoefu, wanahitaji maendeleo.

Narudia tena kusema Salum Mwalim hafai kuwa Mbunge wa Kinondoni.

Mussa Seif,
Bodaboda Kinondoni.
Wewe ndio unaona hafai lakini sisi tuliowengii tunaona anafaa na sifa anazooo ila kwasababu wee ni type ya Mtulia mnayempenda mwanaume mwenzenu mnaona hafai
 
Mbona unarukaruka kama maharage yanayoiva? au maji ya shingo.!? inaonekana mgombea wako siku za mwishoni hizi hajazi hata sebule!
 
Kwenye #3 naweza kukubaliana na Wewe kwa 100% ila huko Kwingine kote sikubaliani na Wewe hata ndani ya Wabunge wa CCM haya ' madhaifu ' yapo isipokuwa tu yanafunikwa kwa ' nguvu ' ya Chama ' dola ' na Chama ' tawala '.

USHAURI

Siku nyingine unapokuwa unafanya ' thorough analysis ' basi jitahidi mno uwe ' neutral ' hasa katika upangiliaji wako wa hoja. Kuna tatizo nimeliona hapo na ndiyo maana nimeona nikukumbushe kidogo hili.
 
Kweli kabisa,mwalimu hafai kuwa mbunge,bali shangazi yako pamoja na msukule ndiyo wanaofaa.
 
Salum Mwalimu ni mmoja wapo wa wagombea Ubunge jimbo la Kinondoni kwenye uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika Februari 17, 2018.

Ni ukweli ulio dhahiri Salum Mwalim sio chaguo letu wakazi wa jimbo la Kinondoni kutokana na sababu zifuatazo:-

1. Hana Ilani ya uchaguzi

Hii ni sababu inayomfanya Salum Mwalimu kutokufaa kuwa Mbunge jimbo la Kinondoni. Chama kilichoshinda na kushika dola kuanzia 2015 hadi 2020 ni CCM ambacho ilani yake ndio inaongoza Serikali.

Leo Salum Mwalimu anapoomba ridhaa ya kuwa Mbunge ataleta maendeleo kwa ilani ipi? Kwanini wana Kinondoni wamchague Mtu asiye na ilani, asiyeweza kuwaletea maendeleo?

2. Hana pesa za kutekeleza ahadi zake

Salum hakubaliani na ilani ya CCM ambayo ndio inaongoza dola, ndio yenye Serikali inayomiliki pesa zote hapa nchini. Anayowahaidi wana Kinondoni atatekeleza kwa ilani ipi? Salum atapata wapi pesa za kutoa huduma za kijamii? Atatoa wapi pesa za kujenga miundombinu? Atatoa wapi mabilioni ya kuwapa mikopo vijana na kina Mama endapo hakubaliani na ilani ya CCM? Kama hayawezi yote hayo, atawezaje kuwaletea maendeleo wana Kinondoni?

3. Chama chake hakina mahusiano mema na Serikali

Kwa nyakati zote Chadema wamekuwa hawana mahusiano mema na Serikali ndio maana kutwa wanaitukana Serikali majukwaani, mitandaoni na mikutanoni. Wanaitukana Serikali ambayo ndio ina ilani, inamiliki pesa zote, inayopanga namna ya kupeleka maendeleo.

Salum anautaka Ubunge wakati anajua fika chama chake hakina mahusiano mema na Serikali inayotekeleza ilani ya uchaguzi. Atawezaje kuwaletea maendeleo wana Kinondoni?

4. Hana uzoefu
Salum anaomba kura aende Bungeni kwenda kujifunza namna ya kufanya kazi. Hana uzoefu wowote ule, anahitaji muda wa kujifunza na si kipindi hiki ambacho wana Kinondoni wanahitaji kiongozi mwenye uzoefu, wanahitaji maendeleo.

Narudia tena kusema Salum Mwalim hafai kuwa Mbunge wa Kinondoni.

Mussa Seif,
Bodaboda Kinondoni.
Yawezekana hata babako hakustahili kuwa babako shauriana na mama yako
Kama unavyoshauri wana kinondoni juu ya salim mwalimu.
 
Mh Rais alikua na uzoefu gani wa kuongoza nchi kabla hajachukua madaraka?
Uongozi ni hekima, busara, upeo wa kupambanua mambo na mahusiano mazuri na unaowaongoza.
Salum mwalimu anawafaa wana kinondoni kuliko yule anaedai anampenda magu balaa
Pia Bunge ndilo linapitisha budget ya nchi. Kwa hiyo basi miradi ya maendeleo kama maji, barabara, elimu etc sio hisani. Tatizo tumeendekeza chuki, uchama na upendeleo ndio maana tunabaguana hata kwenye mambo ya msingi yanayogusa jamii ya watanzania.
Hii mbegu inayopandikizwa na watawala itakuja kuliangamiza hili taifa.
 
Back
Top Bottom