Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,506
- 217,767
Taarifa kutoka Morogoro zinadokeza kwamba Mbunge wa Chadema Mh Devota Minja amekamatwa na jeshi la polisi kwa Amri haramu ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro , kwa kosa la kufuata muongozo wa kuzuia Corona wa shirika la Afya la dunia ( WHO ) na kugawa Barakoa bora kabisa za viwango vya N 95 kwa Wakazi wa Morogoro ili kuwakinga na maambukizi ya virusi hivyo hatari .
Taarifa zaidi zinaeleza kwamba Mh Mbunge ametakiwa kusalimisha Baracoa zake kwa RC huyo ili ofisi ya RC izigawe kwa wananchi , sasa sisi wafuatiliaji wabishi tumejiuliza kisa cha RC kung'angania barakoa za Mh Mbunge ili azigawe yeye , kwanini Ofisi ya Mkoa isitafute barakoa zake na kuzigawa badala ya kutaka kuchukulia kiki kwenye barakoa za mbunge wa Chadema ?
Bali kinachofahamika ni kwamba Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kabla ya kuteuliwa kuwa RC alikuwa Mwenyekiti wa ccm mkoa wa Arusha .