Kwanini Rais Samia amesema hataki mabango, Je hii ndiyo demokrasia?

The lost

JF-Expert Member
Jul 3, 2017
2,695
8,208
Kuna maneno yanayosemekana yametamkwa na mkuu wa nchi ya kwamba yeye hataki kuona wananchi wamebeba mabango. Swali langu ni kwanini hataki wananchi wafikishe ujumbe kwa njia ya mabango?

Je wote wataweza kumuuliza maswali na kupata dukuduku na kero zao?

Mabango ni haki ya wananchi kueleza kero zao na kama kweli hataki basi tutakuwa tumepata pigo kubwa na huenda uongozi wake ukawa wenye matokea hasi haswa ukizingatia sisi wananchi tunahitaji UHURU na haki ya KUSIKILIZWA.
 
Mimi nilimsikiliza na nikamuelewa. Alisema hataki kuona mabango akifanya ziara wilayani au mikoani kwa sababu kero za wananchi wa mkoa au wilaya husika zinatakiwa zishugulikiwe na wanaosimamia jukumu hilo kwa niyaba yake ambao ni Mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa.

Hivyo aliyasema hayo ili kuwahamasisha watendaji husika kusimamia ktk kutatua kero za wananchi, kwani kuibuka kwa mabango ya kero za wananchi kunaashiria wahusika hawajitumi ipasavyo ktk kusimamia lero zao.
 
Alichoongea ni sahihi katika jamii zetu ambapo shida zinatokea kuna wasaidizi kama watendaji mitaa/vijiji, wa kata, mkurugenzi, mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa hawa watu lazima wakae na watu wao kusikiliza na kutatua kero za wananchi sio mpaka Raisi aje hii nchi ni kubwa sana kusema MH. Raisi ataenda kusikiliza shida kote ni kazi ndio maana anateuwa wasadizi ambao ni wakurugenzi, wakuu wa Wilaya, makatibu tawala, wakuu wa mikoa na wengine hao kazi ni kusimamia na kutekeleza sera za maendeleo na kusikiliza shida za wananchi na kwenye yale mabango kuna kero na shida za wananchi sasa hao wateule wanafanya nini, huyo wa Mwanza hayo mabango anayotaka wananchi waje nayo hayana pongezi yana masikitiko kwanini asiwatembelee wananchi akatatue shida zao.
 
Kuna maneno yanayosemekana yametamkwa na mkuu wa nchi ya kwamba yeye hataki kuona wananchi wamebeba mabango. Swali langu ni kwanini hataki wananchi wafikishe ujumbe kwa njia ya mabango?

Je wote wataweza kumuuliza maswali na kupata dukuduku na kero zao?

Mabango ni haki ya wananchi kueleza kero zao na kama kweli hataki basi tutakuwa tumepata pigo kubwa na huenda uongozi wake ukawa wenye matokea hasi haswa ukizingatia sisi wananchi tunahitaji UHURU na haki ya KUSIKILIZWA.
Maana ni kuwa kero zitatuliwe zisiwe za kubebewa mabango,kwani hiyo ni ishara ya kutoridishwa na mambo,au kutokusikilizwa kwa shida za wa husika.
 
Mimi nilimsikiliza na nikamuelewa. Alisema hataki kuona mabango akifanya ziara wilayani au mikoani kwa sababu kero za wananchi wa mkoa au wilaya husika zinatakiwa zishugulikiwe na wanaosimamia jukumu hilo kwa niyaba yake ambao ni Mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa.

Hivyo aliyasema hayo ili kuwahamasisha watendaji husika kusimamia ktk kutatua kero za wananchi, kwani kuibuka kwa mabango ya kero za wananchi kunaashiria wahusika hawajitumi ipasavyo ktk kusimamia lero zao.
Uko sahihi sana Mkuu
 
Kuna maneno yanayosemekana yametamkwa na mkuu wa nchi ya kwamba yeye hataki kuona wananchi wamebeba mabango. Swali langu ni kwanini hataki wananchi wafikishe ujumbe kwa njia ya mabango?

Je wote wataweza kumuuliza maswali na kupata dukuduku na kero zao?

Mabango ni haki ya wananchi kueleza kero zao na kama kweli hataki basi tutakuwa tumepata pigo kubwa na huenda uongozi wake ukawa wenye matokea hasi haswa ukizingatia sisi wananchi tunahitaji UHURU na haki ya KUSIKILIZWA.

You picked on her out of context.
 
Mimi nilimsikiliza na nikamuelewa. Alisema hataki kuona mabango akifanya ziara wilayani au mikoani kwa sababu kero za wananchi wa mkoa au wilaya husika zinatakiwa zishugulikiwe na wanaosimamia jukumu hilo kwa niyaba yake ambao ni Mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa.

Hivyo aliyasema hayo ili kuwahamasisha watendaji husika kusimamia ktk kutatua kero za wananchi, kwani kuibuka kwa mabango ya kero za wananchi kunaashiria wahusika hawajitumi ipasavyo ktk kusimamia lero zao.
Rais inabidi awe muangalifu sana katika kauli zake ili zisitafsiriwe vibaya.

Mathalani, kauli hii inaweza kutafsiriwa kama anaminya uhuru wa wananchi kujieleza.

Ingefaa kama angefafanua kuwa wananchi wana haki ya kikatiba kueleza matatizo yao kwenye mabango, ila, anachotaka ni kuona watendaji wanatatua matatizo kabla hayajafika kwenye mabango.
 
Rais inabidi awe muangalifu sana katika kauli zake ili zisitafsiriwe vibaya.

Mathalani, kauli hii inaweza kutafsiriwa kama anaminya uhuru wa wananchi kujieleza.

Ingefaa kama angefafanua kuwa wananchi wana haki ya kikatiba kueleza mstatizo yao kwenye mabango, ila, anachotaka ni kuona watendaji wanatatua matatizo kabla hayajafika kwenye mabango.
Rejea ile hotuba yake..., mbona hilo lipo wazi??
 
Mimi nilimsikiliza na nikamuelewa. Alisema hataki kuona mabango akifanya ziara wilayani au mikoani kwa sababu kero za wananchi wa mkoa au wilaya husika zinatakiwa zishugulikiwe na wanaosimamia jukumu hilo kwa niyaba yake ambao ni Mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa.

Hivyo aliyasema hayo ili kuwahamasisha watendaji husika kusimamia ktk kutatua kero za wananchi, kwani kuibuka kwa mabango ya kero za wananchi kunaashiria wahusika hawajitumi ipasavyo ktk kusimamia lero zao.
Well said my friend!!!

Lakini kama Chalamila katumbuliwa kwa maneno ya kuwaambia wananchi wabebe mabango sijui kama Mh. Rais kachukua maamuzi hayo kutokana na sababu hiyo, lazima kutakuwa na kitu kingine alichokifanya Chalamila

Kwanini nasema hivyo, ni kutokana na sababu zifuatazao;

1. Kuandika mabango inamsaidia Mh. Rais kufahamu matatizo ya wananchi yanayowasumbua.

2. Baada ya kuyasoma mabango itamsaidia Mh. Rais kuchukua maamuzi, ikiwa baadhi ya kero ziko ndani ya uwezo wa RC basi atawajibishwa

3. Kuyasoma mabango na utendaji wa RC ni vitu viwili tofauti

4. Uataratibu wa kumuandikia mabango mkuu wa nchi ni kitu cha kawaida kwa nchi zoote zenye kufuata demokrasia

Ndio maana nasema sidhani kama Mh. Rais kamuondoa Chalamila kwa kuwaambia wananchi waandike mabango, lazima kuna sababu ingine ambayo sisi hatuijui.

Asante.
 
Kuna maneno yanayosemekana yametamkwa na mkuu wa nchi ya kwamba yeye hataki kuona wananchi wamebeba mabango. Swali langu ni kwanini hataki wananchi wafikishe ujumbe kwa njia ya mabango?

Je wote wataweza kumuuliza maswali na kupata dukuduku na kero zao?

Mabango ni haki ya wananchi kueleza kero zao na kama kweli hataki basi tutakuwa tumepata pigo kubwa na huenda uongozi wake ukawa wenye matokea hasi haswa ukizingatia sisi wananchi tunahitaji UHURU na haki ya KUSIKILIZWA.
Umemsikia wapi akiongea? Au na wewe unakuja kuanzisha thread kwa maneno ya kusikia kutoka kwenye vijiwe?
 
Kuna maneno yanayosemekana yametamkwa na mkuu wa nchi ya kwamba yeye hataki kuona wananchi wamebeba mabango. Swali langu ni kwanini hataki wananchi wafikishe ujumbe kwa njia ya mabango?

Je wote wataweza kumuuliza maswali na kupata dukuduku na kero zao?

Mabango ni haki ya wananchi kueleza kero zao na kama kweli hataki basi tutakuwa tumepata pigo kubwa na huenda uongozi wake ukawa wenye matokea hasi haswa ukizingatia sisi wananchi tunahitaji UHURU na haki ya KUSIKILIZWA.
 
Mimi nilimsikiliza na nikamuelewa. Alisema hataki kuona mabango akifanya ziara wilayani au mikoani kwa sababu kero za wananchi wa mkoa au wilaya husika zinatakiwa zishugulikiwe na wanaosimamia jukumu hilo kwa niyaba yake ambao ni Mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa.

Hivyo aliyasema hayo ili kuwahamasisha watendaji husika kusimamia ktk kutatua kero za wananchi, kwani kuibuka kwa mabango ya kero za wananchi kunaashiria wahusika hawajitumi ipasavyo ktk kusimamia lero zao.
Bravo.
Yaani sitapoteza muda kujibu
Ushamjibu

mods fungeni thread.
 
Ingefaa kama angefafanua kuwa wananchi wana haki ya kikatiba kueleza matatizo yao kwenye mabango, ila, anachotaka ni kuona watendaji wanatatua matatizo kabla hayajafika kwenye mabango.
In all fairness, hivyo ndivyo alivyosema na pia ndivyo nilivyomuelewa mimi.
 
In all fairness, hivyo ndivyo alivyosema na pia ndivyo nilivyomuelewa mimi.
Sasa hawa wanaoanzisha thread misleading ni kwa ajili ya tongotongo za kawaida za wabongo wasiojua kusoma na kusikiliza au wapo katika kazi maalum?

Naona pattern, siku hizi kabla ya kujadili ripoti za alichosema rais, inafaa kuuuliza video au audio. Mara ya pili wiki hii naona habari ya rais inapotoshwa.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Raisi alisisitiza kabisa wasizuie wananchi kuandika mabango lakini wahakikishe hizo kero wanazitatua kabla hazijafika kwake, Na akiona bango labda liwe swala la kitaifa,sasa kuna watu wasiopenda kuelewa wamegeuza kauli yake.
 
Raisi alisisitiza kabisa wasizuie wananchi kuandika mabango lakini wahakikishe hizo kero wanazitatua kabla hazijafika kwake, Na akiona bango labda liwe swala la kitaifa,sasa kuna watu wasiopenda kuelewa wamegeuza kauli yake.
Ahsante mkuu.

Nafikiri kuna umuhimu wa kuanzisha megathread ya kauli za rais, kuzirekodi zote kwa video, kuziweka pamoja, na kuzi update kila mpya zinapotoka.

Kwa kupitia thread hii, watu waweze kuhakiki nini kilisemwa kabla ya kujadili ripoti potofu za nini kilisemwa.
 
Kuna maneno yanayosemekana yametamkwa na mkuu wa nchi ya kwamba yeye hataki kuona wananchi wamebeba mabango. Swali langu ni kwanini hataki wananchi wafikishe ujumbe kwa njia ya mabango?

Je wote wataweza kumuuliza maswali na kupata dukuduku na kero zao?

Mabango ni haki ya wananchi kueleza kero zao na kama kweli hataki basi tutakuwa tumepata pigo kubwa na huenda uongozi wake ukawa wenye matokea hasi haswa ukizingatia sisi wananchi tunahitaji UHURU na haki ya KUSIKILIZWA.
... Rais alituma ujumbe kwa wateule wake kwamba wananchi wakibeba mabango maana yake wateule/mteule anayehusika ameshindwa kutekeleza wajibu wake wa kuwaondolea wananchi kero zao hadi kufikia hatua ya kubeba mabango!

Hivyo hataki kuyaona means wateule wakatekeleze ipasavyo majukumu yao kero za wananchi ziishe mabango yasionekane! Hakumaanisha kwamba amezuia mabango au demokrasia kama unavyotaka kupotosha. Umeelewa?
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom