Sakasaka Mao
JF-Expert Member
- Sep 29, 2016
- 10,142
- 12,188
Kwani asingelijenga alipojenga na kwake asijenge ama akafanya mambo yake mengine, wewe ungelijuaje?Hivi Maraisi wa Africa wana shauriwa kweli? Museveni Raisi wa uganda kafungua shule zuri ya kisasa Mkoani Geita wilaya ya Chato elio jengwa kwa gharama za serikali ya uganda kwa pesa ya walipa kodi ya waganda, wakati Tz aliko jenga hiyo shule ina afuenu katika miundombinu ya shule kuliko Uganda.
Nini lengo la Museveni kunyima waganda shule nzuri na kuja kuijenga Tz?
Museveni analenga nini kupata kutoka Tz?
Hizi ndo hari ya baathi ya shule za sarikali kule nchini uganda
Hivi kutoa msaada hadi uwe umejitosheleza kwako na kujieneza kabisa?
Hata nchi zilizoendelea, wanapomwaga misaada kwetu, huwa kwao hawana jambo ambalo hawajalitekeleza linalohitaji pesa?
Ninachowashangaa hasa hulka ya waTz kwa sasa sijui ni nini kimetupata!
Inamaana unapoenda kwa mfano kununua shati, halafu akatokea mtu mwingine kuanza kuthamanisha hiyo hela uliyoitumia kununulia shati kwa mifuko ya sementi na kukwambia: "wee mjinga unanunuaje shati badala ya mifuko ya sementi", hivi utamuelewaje huyo mtu kuingilia mipango yako na utashi wako?
Zikijengwa barabara, mnasema zingelijengwa shule, zikinunuliwa ndege, mnasema ingelijengwa hospitali, yaani hakuna jema kwenu!
Ujue kila kitu kina manufaa yake kwa wakati wake.
Na ni bora kuwa na kitu chochote kinachoonekana kuliko pesa zilizotengeneza hicho kuishia mifukoni na kuliwa na mafisadi, ambapo wewe kama raia hauna udole wa kulazimisha jambo lolote serikalini ilifanye na likatekelezwa kama unavyotaka.
Sisi kila tunachokiona kinafanywa na serikali chenye muelekeo wa maendeleo huwa tunasema: "ahsante" kwa kushukuru.
Sent using Jamii Forums mobile app