Kwanini Rais Magufuli (Mwenyekiti wa SADC) hakwenda kwenye msiba Mugabe?

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,484
51,059
Raisi Magufuli ni mwenyekiti wa SADC, kwa muktadha huo ni kiongozi mkubwa katika ukanda huu wa kusini mwa Afrika.

Leo nchi ya Zimbabwe imepata msiba wa kufiwa na muasisi wa Taifa huru la Zimbabwe, Je ni kitu gani kimemfanya raisi Magufuli ambaye ni mwenhekiti wa SADC asiende kwenye msiba wa mpigania uhuru huyo?

Majuzi rais mstaafu mzee Mwinyi alitueleza kuwa wakati yeye akiingia madarakani nchi yetu ilikuwa na uhaba mkubwa mno wa fedha za kigeni na hali ilikuwa mbaya sana lakini serikali ya Mugabe ilitusaidia sana kwenye wakati huo wa shida. Je si ingekuwa vizuri raisi wetu japo kukumbuka uhusiano huu mzuri kwa kushiriki msiba wa kiongozi huyu mpigania uhuru?

Wakati wa kifo cha baba wa Taifa, Mugabe alikuja msibani kulia nasi na kutupa pole Watanzania, kwa nini sisi raisi wetu hajaenda kwenye msiba huu mzito?

Wakati wa uongozi wa Mugabe kama rais wa AU, alishiriki kikamilifu katika kuutambulisha mchango wa Tanzania kwenye harakati za Ukombozi wa Afrika, ni yeye aliyeendesha kampeni ya kuuita ukumbi mmoja wa mikutano wa AU kwa jina la Nyerere. Hii ni baada ya kizazi hiki kuanza kusahau mchango wa mwalimu katika liberation.

Je kwa nini raisi Magufuli Personally kwa niaba ya Watanzania hajaenda kuhani msiba?

Tunajua yupo makamu wa raisi, lakini Makamu wa Raisi siyo Raisi. Na hata nchi nyingine zenye maraisi nazo zina makamo wa raisi pia, lakini je kwa nini wameenda maraisi wenyewe na siyo makamu wao?.
 
Huyu jamaa hanaga historia nzuri ya kuhudhuria misibani... Hachelewi kuliamsha dude!!
 
Nini maana ya makamu wa raisi?kwani lazima kwenda ? Tumuacheni jembe apige kazi bhana
 
Rais wetu yuko busy na mambo ya kujenga nchi, kule ameenda muwakilishi ndugu Samia ambaye ni makamo sidhani kama kuna ubaya wa yeye kuwa huko. Si msiba tu, ingekuwa ni uhidhinishaji wa mikataba ya kimaitaifa sawa!
 
Rais wetu yuko busy na mambo ya kujenga nchi, kule ameenda muwakilishi ndugu Samia ambaye ni makamo sidhani kama kuna ubaya wa yeye kuwa huko. Si msiba tu, ingekuwa ni uhidhinishaji wa mikataba ya kimaitaifa sawa!

Je maraisi wote waliowahi kuhudhuria misiba yetu kama wa baba wa Taifa walikuwa hawana kazi ya kufanya katika nchi zao?
Au ni Magufuli peke yake anayachapa kazi wengine woote wanapoteza muda tu?
 
Je maraisi wote waliowahi kuhudhuria misiba yetu kama wa baba wa Taifa walikuwa hawana kazi ya kufanya katika nchi zao?
Au ni Magufuli peke yake anayachapa kazi wengine woote wanapoteza muda tu?
Kuna hiyo kitu yaitwa internal motive mkuu, Magufuli is not the one who is taking care of our colleagues issues, hapa ndani tuna mambo makubwa yanatuhangaisha kuliko kuzingatia hizo diplomatic relation
 
acha wafu wazike wafu wao, yule nanii aliyetafutiwa na BASHITE moja ya masharti ni kutokwenda msibani
 
Huyu Rais anatuharibia sana Mahusiano yetu na majirani, tuliyoyajenga kwa gharama kubwa. kwani sissi Tanzania ni kisiwa? ni kawaida kuhani misiba, hata kama hajazikwa kupitapita kwa marais wenzako wanakuona ona, utani kidogo, inatosha, au ataona aibu kuongea. ujue marais vijana wanapenda sana utani,fikiria out going Congo presdent Kabila, alivoanza kumtania jiwe pale AU Adis ababa....
''Mr prezdaa how are you today ma-men i-jiwe?''
Dei say, you wanna buy jel fighters meeen! wid you? hapo jiwe akili yote ilikufa ganzi, hana hamu ya kwenda kujichanganya na Ma-Rais vitoto mpaka leo. kipaji hicho hana, zaidi ya kukemea kemea tu kwa kiswahili.
siku hiyo hasira ziliishia kwa wandishi wa habari hee!

asione aibu hata mimi nilikuwa kama yeye sijui kitu lakini niliona jhapana lazima nijue lugh ya adui yetu, aije niteta akaniangamiza mbele yake.
aende tu hapo Buguruni English tuition nyuma ya Lozana Bar bei rahisi tu kama pesa inamuuma.
 
Huyu Rais anatuharibia sana Mahusiano yetu na majirani, tuliyoyajenga kwa gharama kubwa. kwani sissi Tanzania ni kisiwa? ni kawaida kuhani misiba, hata kama hajazikwa kupitapita kwa marais wenzako wanakuona ona, utani kidogo, inatosha, au ataona aibu kuongea. ujue marais vijana wanapenda sana utani,fikiria out going Congo presdent Kabila, alivoanza kumtania jiwe pale AU Adis ababa....
''Mr prezdaa how are you today ma-men i-jiwe?''
Dei say, you wanna buy jel fighters meeen! wid you? hapo jiwe akili yote ilikufa ganzi, hana hamu ya kwenda kujichanganya na Ma-Rais vitoto mpaka leo. kipaji hicho hana, zaidi ya kukemea kemea tu kwa kiswahili.
siku hiyo hasira ziliishia kwa wandishi wa habari hee!

asione aibu hata mimi nilikuwa kama yeye sijui kitu lakini niliona jhapana lazima nijue lugh ya adui yetu, aije niteta akaniangamiza mbele yake.
aende tu hapo Buguruni English tuition nyuma ya Lozana Bar bei rahisi tu kama pesa inamuuma.
masharti ya ma GAMBOSH toka SIMIYU
 
Raisi Magufuli ni mwenyekiti wa SADC, kwa muktadha huo ni kiongozi mkubwa katika ukanda huu wa kusini mwa Afrika.

Leo nchi ya Zimbabwe imepata msiba wa kufiwa na muasisi wa Taifa huru la Zimbabwe, Je ni kitu gani kimemfanya raisi Magufuli ambaye ni mwenhekiti wa SADC asiende kwenye msiba wa mpigania uhuru huyo?

Majuzi rais mstaafu mzee Mwinyi alitueleza kuwa wakati yeye akiingia madarakani nchi yetu ilikuwa na uhaba mkubwa mno wa fedha za kigeni na hali ilikuwa mbaya sana lakini serikali ya Mugabe ilitusaidia sana kwenye wakati huo wa shida. Je si ingekuwa vizuri raisi wetu japo kukumbuka uhusiano huu mzuri kwa kushiriki msiba wa kiongozi huyu mpigania uhuru?

Wakati wa kifo cha baba wa Taifa, Mugabe alikuja msibani kulia nasi na kutupa pole Watanzania, kwa nini sisi raisi wetu hajaenda kwenye msiba huu mzito?

Wakati wa uongozi wa Mugabe kama rais wa AU, alishiriki kikamilifu katika kuutambulisha mchango wa Tanzania kwenye harakati za Ukombozi wa Afrika, ni yeye aliyeendesha kampeni ya kuuita ukumbi mmoja wa mikutano wa AU kwa jina la Nyerere. Hii ni baada ya kizazi hiki kuanza kusahau mchango wa mwalimu katika liberation.

Je kwa nini raisi Magufuli Personally kwa niaba ya Watanzania hajaenda kuhani msiba?

Tunajua yupo makamu wa raisi, lakini Makamu wa Raisi siyo Raisi. Na hata nchi nyingine zenye maraisi nazo zina makamo wa raisi pia, lakini je kwa nini wameenda maraisi wenyewe na siyo makamu wao?.
Pekenyua tujue maana baada ya kuwa m/kit wa sadc praise team waliandaa azimio la kumpongeza sasa leo hajaenda
 
Raisi Magufuli ni mwenyekiti wa SADC, kwa muktadha huo ni kiongozi mkubwa katika ukanda huu wa kusini mwa Afrika.

Leo nchi ya Zimbabwe imepata msiba wa kufiwa na muasisi wa Taifa huru la Zimbabwe, Je ni kitu gani kimemfanya raisi Magufuli ambaye ni mwenhekiti wa SADC asiende kwenye msiba wa mpigania uhuru huyo?

Majuzi rais mstaafu mzee Mwinyi alitueleza kuwa wakati yeye akiingia madarakani nchi yetu ilikuwa na uhaba mkubwa mno wa fedha za kigeni na hali ilikuwa mbaya sana lakini serikali ya Mugabe ilitusaidia sana kwenye wakati huo wa shida. Je si ingekuwa vizuri raisi wetu japo kukumbuka uhusiano huu mzuri kwa kushiriki msiba wa kiongozi huyu mpigania uhuru?

Wakati wa kifo cha baba wa Taifa, Mugabe alikuja msibani kulia nasi na kutupa pole Watanzania, kwa nini sisi raisi wetu hajaenda kwenye msiba huu mzito?

Wakati wa uongozi wa Mugabe kama rais wa AU, alishiriki kikamilifu katika kuutambulisha mchango wa Tanzania kwenye harakati za Ukombozi wa Afrika, ni yeye aliyeendesha kampeni ya kuuita ukumbi mmoja wa mikutano wa AU kwa jina la Nyerere. Hii ni baada ya kizazi hiki kuanza kusahau mchango wa mwalimu katika liberation.

Je kwa nini raisi Magufuli Personally kwa niaba ya Watanzania hajaenda kuhani msiba?

Tunajua yupo makamu wa raisi, lakini Makamu wa Raisi siyo Raisi. Na hata nchi nyingine zenye maraisi nazo zina makamo wa raisi pia, lakini je kwa nini wameenda maraisi wenyewe na siyo makamu wao?.
Sijui umekula maharagwe ya wapi wewe?
 
Back
Top Bottom