Kwanini Rais anadhani kukusanya Hela ndio kukuza Uchumi?

tapatalk_jpeg_1544296142852.jpeg
 
Swali lako la msingi sana. Binafsi sina jibu, ila niruhusu niongeze na mimi maswali nisiokua na majibu nayo pia.

***Kuna faida gani serikali kua na hela nyingi wakati raia wana dhiki/shida. Wanafunga biashara kwa kupigwa NGWALA na TRA kwenye kodi na kusababisha ajira kua ngumu???

*** Kuna haja gani nchi kua na ndege nyingi na miradi ya flyover, wakati raia (wasiokua hata na ndoto ya kuja kuzipanda hizo ndege) hata hela ya kula milo miwili ni kitendawili kisichokua na jibu???

*** Kuna haja gani kupoteza MAMILIONI kwaajili ya kununulia VX wabunge na kuwalipa mshahara MILLIONI 99.5 na posho ya kujikimi MILLIONI 24.8 kwa mwaka, wabunge wenyewe wasiokua na umuhimu/faida yoyote kutetea raia/wafanyakazi/wafanyabiashara???

*** Kuna haja gani raia kuchagua viongozi kwa nia ya kuishi maisha ya kujikwamua na umasikini na kuishi kwa amani, ila wanajikuta wakiishi na HOFU juu ya kesho yao???
 
Anadhani hela ndiyo msingi wa maendeleo amesahau busara ya Mwl. Nyerere kuwa pesa sio msingi wa maendeleo
 
Back
Top Bottom