Kwanini Prince Bagenda na Buberwa Kaiza wanaonesha kumchukia Rais Magufuli japo walikuwa wapiga debe wake mwaka 2015

chiembe

JF-Expert Member
May 16, 2015
11,943
20,496
Hawa watu walikuwa wapiga debe wakubwa wa JPM 2015, waliandika makala za kumsifu na kumjenga kisiasa.

Lakini naona siku za karibuni wameanza kuonyesha upinzani mkubwa sana kwa Rais wetu mpendwa.

Buberwa Kaiza katika kurasa zake za mitandao ya kijamii, anafanya ukosoaji mkubwa japo anajaribu kujifichaficha

Prince Bagenda yeye alifikia kutunga kitabu,japo kabla hajakiachia, vyombo vyetu pendwa vya usalama vikampa angalizo

Je, watu hawa wana uroho wa madaraka walidhani kwa kuandika vipeperushi tu wangepata uteuzi? Watanzania tumekuwaje? Kila kitu ukifanya mpaka upate kitu?

Viva JPM
#matege
 
Watu walikuwa hawajamuelewa hapo mwanzoni ,walikuwa wanadanganywa kwamba ni mchapa kazi kwasababu amekariri idadi ya samaki, ng'ombe, mbuzi, kuku na kilometer za barabara.

Katika kipindi chake cha uwaziri alipiga dili nyingi sana za kukupunguza upana wa barabara na kupiga cha juu ,kanunua meli bovu kwa 8B .

Ni mtu wa visasi sana ,alitaka kubomoa jengo la lowassa la tanesco kwa kisirani tu kumkomoa lowassa na alipoingia akaanza nalo amelibomoa lakini barabara yake na daraja wala haijafika hata kama jengo lisingebomolewa,alimfunga Lema wa Northern Engineering kisa tu alitoa mpunga kwenye kampeni ya Ukawa.

Hawakujua Hawakujua...
 
Hawa watu walikuwa wapiga debe wakubwa wa JPM 2015, waliandika makala za kumsifu na kumjenga kisiasa.

Lakini naona siku za karibuni wameanza kuonyesha upinzani mkubwa sana kwa Rais wetu mpendwa.

Buberwa Kaiza katika kurasa zake za mitandao ya kijamii, anafanya ukosoaji mkubwa japo anajaribu kujifichaficha


Prince Bagenda yeye alifikia kutunga kitabu,japo kabla hajakiachia, vyombo vyetu pendwa vya usalama vikampa angalizo

Je watu hawa wana uroho wa madaraka walidhani kwa kuandika vipeperushi tu wangepata uteuzi? Watanzania tumekuwaje? Kila kitu ukifanya mpaka upate kitu?

Viva JPM
#matege
Kwa alivyomnyanyasa Erick Kabendera hadi mama yake akafariki. Hata mimi tu nimemchukia Magufuli na mimi sio mhaya . Sasa kwa wahaya ndo itakuwaje???
 
Watu walikuwa hawajamuelewa hapo mwanzoni ,walikuwa wanadanganywa kwamba ni mchapa kazi kwasababu amekariri idadi ya samaki,ng'ombe,mbuzi ,kuku na kilometer za barabara .

Katika kipindi chake cha uwaziri alipiga dili nyingi sana za kukupunguza upana wa barabara na kupiga cha juu ,kanunua meli bovu kwa 8B .

Ni mtu wa visasi sana ,alitaka kubomoa jengo la lowassa la tanesco kwa kisirani tu kumkomoa lowassa na alipoingia akaanza nalo amelibomoa lakini barabara yake na daraja wala haijafika hata kama jengo lisingebomolewa,alimfunga Lema wa Northern Engineering kisa tu alitoa mpunga kwenye kampeni ya Ukawa.

Hawakujua Hawakujua.........


Kwa levo yako hutakiwi kabisa kuongea hear say kama hiyo ya jengo la Lowasa la TANESCO..
Uzushi mtupu
 
Sidhani kama wanamchukia, lkn kwa kuwa umejiaminisha kuwa kutofautiana kimawazo na kimtazamo ni chuki, basi utachoka kuandika nyuzi maana watu kibao, hawaridhishwi na kinachoendelea nchini.

Na ukumbuke kutoridhishwa na jambo/Mambo fulani dhidi ya mtu si chuki!
 
Back
Top Bottom