Polisi huvalishwa na sisi wananchi, wanaishi kwenye nyumba zinazogharamiwa na sisi wananchi, wanasafirishwa kwa magari yanayogharamiwa na sisi wananchi. Hata buti na soksi zao ni sisi wananchi ndio tunaogharamia.
Matarajio ya wananchi ilikuwa ni kuona hawa wanaogharamiwa karibia kila kitu na wananchi, wanafanya kazi ya kuwalinda wananchi na mali zao kwa uadilifu mkubwa. Bahati mbaya, ni kinyume kabisa.
Yaani pesa ya mwananchi, polisi wanatumia katika harakati ovu, harakati za kubambikizia watu kesi (na hili hata Rais alilikemea) na wakati fulani kufanya matukio ambayo kwa tafsiri halisi ni utekaji.
Wananchi tulitangaziwa kuna ushahidi mzito dhidi ya Mbowe na wenzake kuhusika kwenye njama za kufanya ugaidi. Tukaambiwa kuna mashahidi na vielelezo. Tukawa na shauku kubwa ya kusikia na kuona.
Wananchi tulitarajia kuona vielelezo kama vile mabomu ambayo yangetumika kulipulia vituo vya mafuta, labda na mashine kama vile chainsew za kuangushia miti kuziba barabara, na pengine hata bunduki au zana ambazo zingetumika kuua viongozi.
Maajabu ya karne, kila shahidi anasimama mbele ya mahakama kupiga stories namna alivyosafiri kufika Moshi na kwenda Dar, alivyokula njiani, alivyobadilisha gari, alivyoingiza majina ya watu kwenye register book ya polisi! Mtu wa Tigo, tulitatajia angeleta mawasiliano ya siri ya hao magaidi waliyokuwa wanafanya katika maandalizi ya kufanya ugaidi. Cha ajabu analeta story ya kutuma muamala wa shilingi laki 5! Ujinga mkubwa! Kutuma laki 5 ndiyo ugaidi? Basi Watanzania wote ni magaidi. Maana hakuna ambaye hajawahi kutuma fedha.
Shahidi anaelezea kuwa walikuwa wanasajili namba za simu. Kusajili namba za simu ndiyo ugaidi? Kama ni ugaidi, basi sisi sote ni magaidi. Na siro, na Kingai na waendesha mashtaka wote, pamoja na jaji basi ni magaidi. Maana sote kwa wakati fulani tumesajili laini za simu.
Mpaka leo, hakuna hata mmoja aliyetoa kielelezo cha ugaidi wala maelezo yanayothibitisha ugaidi kupangwa au kutendeka.
Mahakama badala ya kusikiliza kesi halisia, inapoteza muda kusikiliza stories za akina Kingai na wenzake. Mawakili wa Serikali badala ya kufanya kazi wanazostahili kufanya, wamekuwa wachombezaji wa mashahidi ambao kwa ufahamu wa kawaida, ni dhahiri ni mashahidi wa kutengenezwa, na hawana chochote cha maana cha kuoambia mahakama. Nadala ya kuleta vielelzo vya maana, wanaleta makaratasi waliyoyaandika wenyewe, na kuwalazimisha wqtuhumiwa kusaini. Ni ujinga wa hali ya juu.
Pesa yetu inateketea bila sababu kwa vile tu polisi hawana uchungu na pesa yetu. Tunawavalisha, tunawasafirisha, tunawalisha na kuwatibu ili wawalinde raia na mali zao, na siyo hii michezo isiyo na vichwa wala miguu. Inasikitisha sana. Taifa hili hatutakuja kupiga hatua kwa sababu pesa yetu kidogo inayopatikana, tunaitumia kwa mambo ya hovyo, tukiacha mambo ya msingi.
Wananchi tupaze sauti kuwataka polisi wafanye kazi wanazostahili kifanya, au la Jeshi la polisi liundwe upya, na hawa polisi wachafuzi wafukuzwe.
Matarajio ya wananchi ilikuwa ni kuona hawa wanaogharamiwa karibia kila kitu na wananchi, wanafanya kazi ya kuwalinda wananchi na mali zao kwa uadilifu mkubwa. Bahati mbaya, ni kinyume kabisa.
Yaani pesa ya mwananchi, polisi wanatumia katika harakati ovu, harakati za kubambikizia watu kesi (na hili hata Rais alilikemea) na wakati fulani kufanya matukio ambayo kwa tafsiri halisi ni utekaji.
Wananchi tulitangaziwa kuna ushahidi mzito dhidi ya Mbowe na wenzake kuhusika kwenye njama za kufanya ugaidi. Tukaambiwa kuna mashahidi na vielelezo. Tukawa na shauku kubwa ya kusikia na kuona.
Wananchi tulitarajia kuona vielelezo kama vile mabomu ambayo yangetumika kulipulia vituo vya mafuta, labda na mashine kama vile chainsew za kuangushia miti kuziba barabara, na pengine hata bunduki au zana ambazo zingetumika kuua viongozi.
Maajabu ya karne, kila shahidi anasimama mbele ya mahakama kupiga stories namna alivyosafiri kufika Moshi na kwenda Dar, alivyokula njiani, alivyobadilisha gari, alivyoingiza majina ya watu kwenye register book ya polisi! Mtu wa Tigo, tulitatajia angeleta mawasiliano ya siri ya hao magaidi waliyokuwa wanafanya katika maandalizi ya kufanya ugaidi. Cha ajabu analeta story ya kutuma muamala wa shilingi laki 5! Ujinga mkubwa! Kutuma laki 5 ndiyo ugaidi? Basi Watanzania wote ni magaidi. Maana hakuna ambaye hajawahi kutuma fedha.
Shahidi anaelezea kuwa walikuwa wanasajili namba za simu. Kusajili namba za simu ndiyo ugaidi? Kama ni ugaidi, basi sisi sote ni magaidi. Na siro, na Kingai na waendesha mashtaka wote, pamoja na jaji basi ni magaidi. Maana sote kwa wakati fulani tumesajili laini za simu.
Mpaka leo, hakuna hata mmoja aliyetoa kielelezo cha ugaidi wala maelezo yanayothibitisha ugaidi kupangwa au kutendeka.
Mahakama badala ya kusikiliza kesi halisia, inapoteza muda kusikiliza stories za akina Kingai na wenzake. Mawakili wa Serikali badala ya kufanya kazi wanazostahili kufanya, wamekuwa wachombezaji wa mashahidi ambao kwa ufahamu wa kawaida, ni dhahiri ni mashahidi wa kutengenezwa, na hawana chochote cha maana cha kuoambia mahakama. Nadala ya kuleta vielelzo vya maana, wanaleta makaratasi waliyoyaandika wenyewe, na kuwalazimisha wqtuhumiwa kusaini. Ni ujinga wa hali ya juu.
Pesa yetu inateketea bila sababu kwa vile tu polisi hawana uchungu na pesa yetu. Tunawavalisha, tunawasafirisha, tunawalisha na kuwatibu ili wawalinde raia na mali zao, na siyo hii michezo isiyo na vichwa wala miguu. Inasikitisha sana. Taifa hili hatutakuja kupiga hatua kwa sababu pesa yetu kidogo inayopatikana, tunaitumia kwa mambo ya hovyo, tukiacha mambo ya msingi.
Wananchi tupaze sauti kuwataka polisi wafanye kazi wanazostahili kifanya, au la Jeshi la polisi liundwe upya, na hawa polisi wachafuzi wafukuzwe.