Kwanini Police Traffic wakitoza fine kwa mobile printer, notification SMS isiende automatically kwa mmiliki wa gari??

Infantry Soldier

JF-Expert Member
Feb 18, 2012
15,893
16,317
ruggedjet4newsmall2for-routewith-receiptjpg.jpg

POLICE TRAFFIC WABORESHE CUSTOMER CARING KWA NAMNA HII.

Shikamooni wakubwa zangu wote.

Kitu ambacho police traffic wanapaswa kukumbushwa ni kuwa si wote wanaoendesha magari hapa Tanzania ni wamiliki wa magari hayo.

Wengine wameazima kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki zao. Wanatenda makosa ya barabarani lakini hawatoi taarifa kwa wamiliki halisi. Naomba police watusaidie kwa hili kama sehemu ya kuboresha huduma zao kwa jamii (hususan wamiliki wa vyombo vya usafiri)

Kama mtu akitoa pesa kutoka kwenye ATM ya bank anapata SMS notification wakati huo huo, kwanini Police Traffic wakitoza fine kwa ile machine yao (Mobile Ticket Printer) SMS notification isiende kwenye simu ya mmiliki wa chombo cha usafiri automatically muda ule ule??

Juzi jumapili nilienda kumtembelea classmate wangu Beautiful Nkosazana maeneo ya gongo la mboto dar es salaam. Wakati ananisindikiza mida ya saa kumi jioni tukiwa ndari ya gari yake ndogo maeneo ya airwing tulikutana na tuta dogo la plastic/rubber ambapo baada ya kulivuka mbele tukasimamishwa na police traffic wakiwa na turubai ndogo pembeni pamoja na camera system ambayo baada ya udadisi baada ya tukio nikagundua kumbe ile camera ilikuwa kwa ajili ya ku detect gari zilizotozwa fine kwa makosa ya barabarani lakini wamiliki hawakulipia fine hizo.

Baada ya mazungumzo na mvutano kama wa dakika 15 na yule askari, classmate akaja kugundua kuwa ile gari ilikuwa inadaiwa kiasi cha shillings 60,000 kwa makosa mawili ya barabarani yaliyofanywa na mdogo wake ambaye aliazima tu gari ya dada mwezi uliopita.

Sasa hapa nikawaza, endapo wakati traffic anatoa ile receipt ya kutoza fine kwa yule dogo, sms notification ingeweza kwenda kwa mmiliki wa gari automatically kusingekuwa na mvutano baina ya police na classmate wangu, pia itakuwa ni njia nzuri ya kuboresha uhusiano mwema baina ya police na wamiliki wa vyombo vya usafiri.

Kwa wataalamu wa ICT hii inawezekana??

Sipo sahihi muda wote. Haya ni mawazo yangu binafsi and I STAND TO BE CORRECTED.

OUR MOTTO
=======
KIJANA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USITUMIKE VIBAYA KUICHAFUA NCHI YAKO.

Espionage: Majasusi wa Mossad alivyoiba mkojo wa rais Hafez kwa kutumia CHOO CHA BANDIA - JamiiForums

Secretariat ya ajira, kwanini interview za kazi zisifanyike kwa kanda (Zones)? Kwanini wote tujazane Dar? - JamiiForums
 
Kwanini isiwezekane....
Hiyo ni Sawa na Ukienda ku draw hela kwenye atm .......Muda huo huo unapata Sms kwenye # yko kuwa kuna muhamala wa kutoa fedha umefanyika atm fulani na muda

Ova

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kihalali kabisa inatakiwa iwe hivyo, ila mifumo yetu tu ndio inavyo pelekwa, jiulize hata wakikukamata na kuandika kwenye liseni watakuuliza no ya simu lakini sms hakuji kwako kwanini?mikosa hilo ilipashwa kuja sms kwako.
 
Naomba nikusahihishee kidogo

Kuna kutoza faini kwa gari na kwa leseni

Wazo lako ni kwamba ikiandikiwa gari ndio mwenye gar apate taarifa ila kama ni kwa lesen bhas mwenye lesen apate taarifa

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu jamaa yangu aliovertake sehemu sio sahihi lakini gari ndio iliandikiwa kumbukumbu ya kudaiwa.

Sema hicho kitu alicho shauri muhusika kinawezekana tu.
Kwa sasa wanakuuliza tuandike namba gani ya simu?
Dereva akitaja yake basi SMS ya notification itaenda kwake, kama namba ya mwenye gari basi huyo ndio atapata SMS.
 
Kihalali kabisa inatakiwa iwe hivyo, ila mifumo yetu tu ndio inavyo pelekwa, jiulize hata wakikukamata na kuandika kwenye liseni watakuuliza no ya simu lakini sms hakuji kwako kwanini?mikosa hilo ilipashwa kuja sms kwako.
Yaani juzi kati wamekula 30,000 yangu nikawaza kama ni malipo halali ya serikali mbona uwazi mdogo sana. Unatoa lakini zinaishia kuliwa na wachache.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo tatizo sio polisi tatizo ni IT wa tanzania sio creativity hawaon oppotunity.... Kwa mfano wakileta app inayo kupa deni lako la barabara option ya kulipa moja kwa moja ambayo sio lazima uende NBC si wangekua matajir, TZ kuna magari magapi ICT wa hapa bongo wanazingua
 
Hapo tatizo sio polisi tatizo ni IT wa tanzania sio creativity hawaon oppotunity.... Kwa mfano wakileta app inayo kupa deni lako la barabara option ya kulipa moja kwa moja ambayo sio lazima uende NBC si wangekua matajir, TZ kuna magari magapi ICT wa hapa bongo wanazingua
System intergration baina ya servers za police na TRA haiwezekani?
 
Hapo tatizo sio polisi tatizo ni IT wa tanzania sio creativity hawaon oppotunity.... Kwa mfano wakileta app inayo kupa deni lako la barabara option ya kulipa moja kwa moja ambayo sio lazima uende NBC si wangekua matajir, TZ kuna magari magapi ICT wa hapa bongo wanazingua
Sio lazima kulipia kwa N B C, Mimi hulipa kwa Tigo Pesa na ninapata notification kutoka n b c. Kuwa nimelipia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
View attachment 856570
POLICE TRAFFIC WABORESHE CUSTOMER CARING KWA NAMNA HII.

Shikamooni wakubwa zangu wote.

Kitu ambacho police traffic wanapaswa kukumbushwa ni kuwa si wote wanaoendesha magari hapa Tanzania ni wamiliki wa magari hayo.

Wengine wameazima kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki zao. Wanatenda makosa ya barabarani lakini hawatoi taarifa kwa wamiliki halisi. Naomba police watusaidie kwa hili kama sehemu ya kuboresha huduma zao kwa jamii (hususan wamiliki wa vyombo vya usafiri)

Kama mtu akitoa pesa kutoka kwenye ATM ya bank anapata SMS notification wakati huo huo, kwanini Police Traffic wakitoza fine kwa ile machine yao (Mobile Ticket Printer) SMS notification isiende kwenye simu ya mmiliki wa chombo cha usafiri automatically muda ule ule??

Juzi jumapili nilienda kumtembelea classmate wangu Beautiful Nkosazana maeneo ya gongo la mboto dar es salaam. Wakati ananisindikiza mida ya saa kumi jioni tukiwa ndari ya gari yake ndogo maeneo ya airwing tulikutana na tuta dogo la plastic/rubber ambapo baada ya kulivuka mbele tukasimamishwa na police traffic wakiwa na turubai ndogo pembeni pamoja na camera system ambayo baada ya udadisi baada ya tukio nikagundua kumbe ile camera ilikuwa kwa ajili ya ku detect gari zilizotozwa fine kwa makosa ya barabarani lakini wamiliki hawakulipia fine hizo.

Baada ya mazungumzo na mvutano kama wa dakika 15 na yule askari, classmate akaja kugundua kuwa ile gari ilikuwa inadaiwa kiasi cha shillings 60,000 kwa makosa mawili ya barabarani yaliyofanywa na mdogo wake ambaye aliazima tu gari ya dada mwezi uliopita.

Sasa hapa nikawaza, endapo wakati traffic anatoa ile receipt ya kutoza fine kwa yule dogo, sms notification ingeweza kwenda kwa mmiliki wa gari automatically kusingekuwa na mvutano baina ya police na classmate wangu, pia itakuwa ni njia nzuri ya kuboresha uhusiano mwema baina ya police na wamiliki wa vyombo vya usafiri.

Kwa wataalamu wa ICT hii inawezekana??

Sipo sahihi muda wote. Haya ni mawazo yangu binafsi and I STAND TO BE CORRECTED.

OUR MOTTO
=======
KIJANA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USITUMIKE VIBAYA KUICHAFUA NCHI YAKO.

Espionage: Majasusi wa Mossad alivyoiba mkojo wa rais Hafez kwa kutumia CHOO CHA BANDIA - JamiiForums
Secretariat ya ajira, kwanini interview za kazi zisifanyike kwa kanda (Zones)? Kwanini wote tujazane Dar? - JamiiForums
Sitaki hata hiyo customer caring yao trafic, yani nifurahi nini sasa hapo kulimwa faini? maana kuna vitu vina boa sana, unakuta kuna makosa mtu unatakiwa kukumbushwa tu kama kosa la stika ya nenda kwa usalama nilikua sina juzi nimelimwa faini hata kama nilijisahau sasa kwanini asinakitie tu stika niende, kweli inaboa sana kisa utalipa ndani siku saba eti jipange utaipata tu yani it is disgusti kw kwel
 
Imekaa vzr kabisa! Utakuta mtu ana deni kubwa ambalo halijui akiambuwa mpaka anachanganyikiwa
 
Back
Top Bottom