Habari wadau!
Mdogo wangu alitangaza kutaka kuoa, kwa kuwa ni jambo la heri tukapeleka barua na taratibu za mahali zikafua!
Tumechumbia mtoto Wa kirangi mzuri sana!
Mahali wametutajia ng'ombe saba, tukakubali wala hatukulia lia kupunguziwe.
Wakatupa thamani moja ya ng'ombe kwa laki nne.
Kwa kuwa tulienda Dodoma, ili kuepuka usumbufu tulibeba kwa tahadhali million 5.
Ikawa baada ya kutamkiwa mahali yetu tukaingia kwenye hazina yetu tukatoa milioni mbili na laki nane cash! (2,800,000/=) na kuwalipa!
Nashangaa wakakataa katakata kupokea ikawa marumbano makubwa!
Na kikubwa walicholalamikia wale wakwe eti ni kwanini hatujaomba kupunguziwa mahali?
Kingine ni vile utaratibu wa kulipa, kwanini tunalipa yooote?
Walihoji kuwa kwani hatujui kwamba mahali huwa hailipwi yoote?
Walisisitiza kwamba makabila yote Tanzania huwa ni marufuku kutoa mahali yote sasa sisi kwanini tunalipa yoote?
Baada ya msuguano kwa hasira nikachukua Pesa ya mahali waoaji tukakubaliana kwamba tuahirishe tutakuja siku nyingine!
Swali, Kuna kosa gani mahali kulipwa yote?
Mdogo wangu alitangaza kutaka kuoa, kwa kuwa ni jambo la heri tukapeleka barua na taratibu za mahali zikafua!
Tumechumbia mtoto Wa kirangi mzuri sana!
Mahali wametutajia ng'ombe saba, tukakubali wala hatukulia lia kupunguziwe.
Wakatupa thamani moja ya ng'ombe kwa laki nne.
Kwa kuwa tulienda Dodoma, ili kuepuka usumbufu tulibeba kwa tahadhali million 5.
Ikawa baada ya kutamkiwa mahali yetu tukaingia kwenye hazina yetu tukatoa milioni mbili na laki nane cash! (2,800,000/=) na kuwalipa!
Nashangaa wakakataa katakata kupokea ikawa marumbano makubwa!
Na kikubwa walicholalamikia wale wakwe eti ni kwanini hatujaomba kupunguziwa mahali?
Kingine ni vile utaratibu wa kulipa, kwanini tunalipa yooote?
Walihoji kuwa kwani hatujui kwamba mahali huwa hailipwi yoote?
Walisisitiza kwamba makabila yote Tanzania huwa ni marufuku kutoa mahali yote sasa sisi kwanini tunalipa yoote?
Baada ya msuguano kwa hasira nikachukua Pesa ya mahali waoaji tukakubaliana kwamba tuahirishe tutakuja siku nyingine!
Swali, Kuna kosa gani mahali kulipwa yote?