Kwanini nyumba yako unaiita "kakibanda kangu"? Mungu hapendi kujishusha sana. Having too much humility is self destructive

Kuna siku nilikuwa kwenye ibada za Hawa manabii wa kizazi kipya,kwenye maombi nabii akawa akisema"Mungu baba, sisi ni Kama sisimizi,ni wadudu tu mbele zako"nikapoteza network nikakumbuka tuliambiwa tumeumbwa kwa mfano wa Mungu, Sasa kwa Nini hata tusiseme "Mimi ni pendo,Mimi ni nuru kwa kuwa nimeumbwa kwa mfano wako"nikawaza hata kujishushusha kuwe na kiasi,kujishushusha Sana mwishowe utakufuru.Moyo wenye shukrani humpendeza Mungu na Jamii yake.
Hakika friend. Upo sahihi. Tujifunze kushukuru katika kila hali.
 
Tatzo ni shiriki,wengi wana wahofia wachawi,wanaona wakisema huu mjengo wangu, wanahisi watarogwa kabisa wapotee wasifaidi Kukaa mjengoni,kwa hofu hyo wanasema kakibanda ili wabakie salama machoni pa wa wanafiki na wachawi.
 
Ukiona mtu anajishusha hivyo tofauti na uhalisia uliopo hapo ujue shida ni wewe mgeni,huaminiki,mzee wa kuzogoa,ndimi mbili na kadhalika.

Tena ukija kwangu sikwambii ni kakibanda bali ni kakijibanda alafu utajua mwenyewe.
 
Kuna mwamba alikuwa anajimwambafai sana amejenga nyumba ya nguvu siku amenipeleka kwake nilichoka sana banda fulani tu nahisi mchora ramani alikuwa kalewa na fundi alikuwa mzee wa miaka 80,finishing zero,nikabaki nashangaa tu!
Note;Acha watu wakusifie kwa ulichofanya sio wewe mwenyewe
 
Mungu hapendi kujishusha sana.
1. Unapoongelea Mungu ni bora ukatoa na nukuu wapi kasema hivo

2. Litazame pia kwa namna hii, Kichwa cha mtu hutoa tathmini kutokana ya kitu/hali kutegemea yale anayoyajua/aliyoyapanga. Mfano kama lengo/mpango wake ni kumiliki bonge la Mansion, mtu hyo hawez kujisifia kwa kuwa na cottage. Kwa namna jingine inawezekana msikilizaji ndo ukaona ni nyumba ya maana kwako ila kwake kutegemea na malengo yake akaona bado sana. Sio kujishusha mara zote, ni kukubaliana na hali alipo akitambua anapopaswa kufika
 
Ka Uzi kako kamejaa hekima ndo mana na Mm nimeweka ka post kangu
 
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa JamiiForums.

Sio kila siku tunapaswa kuandika, kusoma na kujadili makala zinazohusiana na masuala ya kizungu kama Cold War, jeshi na ujasusi wa KGB, CIA na Mossad. Leo ngoja tujadili kidogo masuala ya kimaisha katika jamii zetu hizi tunamoishi.

Ndugu zangu watanzania jifunzeni kujishusha lakini isiwe too much. Mungu hapendi mjishushe sana. Having too much humility is self destructive;

Unakuta mtu alikuwa anaishi katika nyumba ya kupanga vyumba viwili chumba na sebule, lakini kwa bahati nzuri akajinyima kisha kwa uwezo wa Mungu akajenga nyumba yake self-contained ya vyumba vitatu vya kulala.

Siku ama weeks kadhaa baada ya kuhamia unasema ngoja niende nikamtembelee ndugu, jamaa au rafiki yangu nifahamu anapokaa. Baada ya kufika na kusalimiana anakukaribisha ndani kisha anakwambia "karibu, haka ndio kakibanda kangu najifichamo na kafamilia kangu, si unajua tena ujenzi wa kimasikini"

Kwanini nyumba yako nzuri Mungu aliyokubariki uiite kakibanda? Au baadhi ya watu wanafikiri huko ndio kujishusha kwenyewe na ndio uungwana? Why don't you feel proud of what God blessed you with? Au haujui kuwa hata vinyonge havitaenda Mbinguni. Mtu amekuja kukutembelea mwambie kwa kujiamini kwamba, "hii ndio nyumba yangu. Nimeijenga mpaka stage hii ila Mungu akinijalia nitaimalizia taratibu tarabitu kwa maana pesa ngumu siku hizi"

Au unakutana na dada classmate wako wa secondary school na ulisikia aliolewa punde tu baada ya kumaliza shule. Unamuuliza "hongera Fatuma ninasikia uliolewa na fulani na umebarikiwa mtoto mmoja" utamsikia atakavyokujibu kwa kinyonge "kuolewa wapi kaka yangu, nipo tu ninasogeza naye maisha, si unajua tena mambo ya sogea tukae"

A thankful heart is one that is grateful and appreciative of who God is and the life He has given them despite the storms of life. I have learned that cultivating a thankful heart is a choice and it requires our intentional effort in achieving it.

Having too much humility is self destructive. Humility has to be practiced with care. Humility requires boundaries.

Watanzania msipende kujiweka kinyongenyonge na kujishusha saana. Jivunie kile ambacho Mungu amekubariki kwa wakati huo huku ukizidi kupambana ili usonge mbele zaidi.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Uzi mzuri sana,ila hapo mwisho ulipo andika USISAHAU:....ingependeza pale mwishoni baada ya neno IPASAYO ungemalizia na CHAGUA MAGUFULI...
 
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa JamiiForums.

Sio kila siku tunapaswa kuandika, kusoma na kujadili makala zinazohusiana na masuala ya kizungu kama Cold War, jeshi na ujasusi wa KGB, CIA na Mossad. Leo ngoja tujadili kidogo masuala ya kimaisha katika jamii zetu hizi tunamoishi.

Ndugu zangu watanzania jifunzeni kujishusha lakini isiwe too much. Mungu hapendi mjishushe sana. Having too much humility is self destructive;

Unakuta mtu alikuwa anaishi katika nyumba ya kupanga vyumba viwili chumba na sebule, lakini kwa bahati nzuri akajinyima kisha kwa uwezo wa Mungu akajenga nyumba yake self-contained ya vyumba vitatu vya kulala.

Siku ama weeks kadhaa baada ya kuhamia unasema ngoja niende nikamtembelee ndugu, jamaa au rafiki yangu nifahamu anapokaa. Baada ya kufika na kusalimiana anakukaribisha ndani kisha anakwambia "karibu, haka ndio kakibanda kangu najifichamo na kafamilia kangu, si unajua tena ujenzi wa kimasikini"

Kwanini nyumba yako nzuri Mungu aliyokubariki uiite kakibanda? Au baadhi ya watu wanafikiri huko ndio kujishusha kwenyewe na ndio uungwana? Why don't you feel proud of what God blessed you with? Au haujui kuwa hata vinyonge havitaenda Mbinguni. Mtu amekuja kukutembelea mwambie kwa kujiamini kwamba, "hii ndio nyumba yangu. Nimeijenga mpaka stage hii ila Mungu akinijalia nitaimalizia taratibu tarabitu kwa maana pesa ngumu siku hizi"

Au unakutana na dada classmate wako wa secondary school na ulisikia aliolewa punde tu baada ya kumaliza shule. Unamuuliza "hongera Fatuma ninasikia uliolewa na fulani na umebarikiwa mtoto mmoja" utamsikia atakavyokujibu kwa kinyonge "kuolewa wapi kaka yangu, nipo tu ninasogeza naye maisha, si unajua tena mambo ya sogea tukae"

A thankful heart is one that is grateful and appreciative of who God is and the life He has given them despite the storms of life. I have learned that cultivating a thankful heart is a choice and it requires our intentional effort in achieving it.

Having too much humility is self destructive. Humility has to be practiced with care. Humility requires boundaries.

Watanzania msipende kujiweka kinyongenyonge na kujishusha saana. Jivunie kile ambacho Mungu amekubariki kwa wakati huo huku ukizidi kupambana ili usonge mbele zaidi.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Hahahaha duh....this is an excellent piece...
 
Infantry soldier hongera. Unatupa nondo kwelikweli siku . Big up unatupa mada tofauti za kufikirisha na kuelimisha Ahsante kwa nguvu chanya unayotupa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom