Brooklyn
JF-Expert Member
- Mar 17, 2009
- 1,459
- 284
Wadau hebu tushauriane kuhusu masuala ya rangi za nyumba na sababu zipi zinafanya rangi ziwe zinabanduka tena ndani ya muda mfupi tu. Je ni mafundi wetu hawajui namna ya kuandaa kuta kabla ya kupaka rangi au ni ubora wa rangi zetu? Karibu kila nyumba ninazotembea hapa Dar zimeathiriwa na tatizo hili. Unaweza kukuta nyumba ni nzuri sana lakini ukiitizama kwa makini unaona baadhi ya maeneo rangi imeanza kubanduka. Maeneo sugu yanayoathiriwa sana na tatizo hili ni kama vile kuta za jikoni, bafuni, kwenye slubs n.k. Je wadau mafundi wetu wanakosea wapi? Ili kuepuka tatizo hili tufanyeje?