Kwanini NSSF hawanipi mafao yangu yote baada ya kuacha ajira?

manwest1

JF-Expert Member
Apr 25, 2014
225
134
Nilikuwa katika ajira kwa muda wa miezi 17. Katika muda huo wote nilikuwa nachangia mfuko wa NSSF kwa mujibu wa sheria. Mwezi wa tatu mwaka huu tulipunguzwa kazi kutokana na Covid 19.

Nilijaza fomu za NSSF ili niweze kupata hela yangu iliyopo huko nianze biashara. Niliambiwa kwakuwa nimefanya kazi miezi 17 nitaanza kwakulipwa asilimia 50 (50%) ya hela iliyopo NSSF. Nililipwa hiyo asilimia 50.

TATIZO ni kwamba kila nikifuatilia kiasi kilichobaki nakipataje naambiwa HICHO SITAWEZA KUKIPATA MPAKA UTARATIBU MPYA UTAKAPO TOLEWA. Nilienda ofisi nyingine nikaambiwa SIWEZI KULIPWA HICHO KILICHOBAKIA.

Fikiria ni asilimia 50 yaani nusu unalipwa nusu hulipwi. Naambiwa hata wale waliovuka miezi 18 katika ajira, baada ya kulipwa hizo asilimia 30 kwa miezi 6. Hulipwi tena kiasi kilichobaki. Huu ni utaratibu gani jamani. Si uonevu huu. Naomba wajuzi wa haya mambo wanisaidie.

Nifanye nini?
 
Yani umefanya kazi Mwaka Mmoja na Miezi mitano tu

Ushafungua Uzi wa unataka Mafao yako

Mbona una Masihara Sana Mkuu Watu wamefany kazi miaka na Miaka Na wanazungushwa mpaka leo Wewe juzi tuu unalalamika hivyo

Hawawezi kukupa kaka Msema kweli Mpenzi wa Mungu
 
Yani umefanya kazi Mwaka Mmoja na Miezi mitano tu

Ushafungua Uzi wa unataka Mafao yqko

Mbona una Masihara Sana Mkuu Watu wamefany kazi miaka na Miaka Na wanazungushwa mpaka leo Wewe juzi tuu unalalamika hivyo

Hawawezi kukupa kaka Msema kweli Mpenzi wa Mungu
Mshahara unaolipwa ndio unao matter. Unaweza fanya kazi miaka mia ila usinifikie mimi kwa jumla ya hela uliyopata. Ni basi tu si busara kutaja mshahara wangu hapa au nafasi niliyokuwa nafanya kazi. In short mimi si mtumwa wa ajira hivyo natumika kuwaelekeza watu experience yangu katika kazi ( Kama expat) nikitoka hapo nasepa na biashara zangu ambazo ndio nguzo yangu kubwa. Ila this time nimeshangaa kukutana na haya. Nia ya kuandika haya ni kuwatahadharisha na kuwafungua macho watu kama wewe ambao mtatoka mmezeeka halafu mfe na presha huku.
 
Hii mifuko ya pensheni inakuwaga migumu sana kutoa mipunga ya watu sijui inakuwa shida ipo wapi

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Yes na hii inakatisha tamaa sana kuingia humo. Binafsi nafanya biashara ya hela nyingi na natamani sana nijiunge lile fao la hiari ila ninapotazama wanavyobadilika badilika naona ni bora niwe na saving yangu binafsi tu kwenye bank kama fixed deposit basi.
 
Hii mada inanihusu sana na nna hasira sana na hawa CCM kwa kitendo wanachofanyia watanzania wanaopoteza kazi.

Laana zote ziende kwa Rais na wabunge wa CCM ambao ndio hupitisha mambo yote mabaya ya kuwanyonya watanzania hasa waliokosa kazi.

October 28 hayupo mwanaukoo wangu au rafiki yangu ataipigia kura CCM.
 
Kumbe wanatoa 30 ,%kwa miezi sita
Yes kama umechangia kwa zaidi ya miezi 17 wanakupa 30% ya kiwango cha mshahara wa mwisho uliokuwa unalipwa kila mwezi kwa miezi sita na baada ya hapo ndio maumivu huanza maana hawaeleweki the rest watakupa lini.
 
Hii mada inanihusu sana na nna hasira sana na hawa nguruwe ccm kwa kitendo wanachofanyia watz wanaopoteza kazi......

Laana zote ziende kwa rais na wabunge wa ccm ambao ndio hupitisha mambo yote mabaya ya kuwanyonya watz hasa waliokosa kazi.....

October 28 hayupo mwanaukoo wangu au rafiki yangu ataipigia kura ccm
Pole sana mkuu ila usikasirike sana ukaharibu afya yako.
 
Unapewa kwa mkupuo au kila mwezi wanaingiza kwa miezi 6?
Yes kama umechangia kwa zaidi ya miezi 17 wanakupa 30% ya kiwango cha mshahara wa mwisho uliokuwa unalipwa kila mwezi kwa miezi sita na baada ya hapo ndio maumivu huanza maana hawaeleweki the rest watakupa lini.
 
Hatari sana nilidhani 50,%ya michango yako kumbe 30%ya mshahara . Sasa ada za shule utatoa 30%au. Hebu nikumbushe fomula ya kuona salio
 
Back
Top Bottom