Kwanini Nokia isirudie zamani?

Ryzen

JF-Expert Member
Dec 6, 2012
7,305
8,655
Hivi wadau ni Mimi tu au?

Ni mimi tu ninayeona Simu za Zamani za Nokia kama Nokia2700, Xpress Music, E71 N.k zilikuwa Bora kabisa kuliko za sasa?

Je, Nokia hawawezi kuzalisha tena hizo Simu?

nokia-c5.jpg
images%20(11).jpg
images%20(10).jpg
 
Nok
Nokia ni Analog.Sasa hivi tupo 4G
Hahaaaa..
Tupo 5G mzee,
Nokia hizo 4G zenu za miaka hii alitoa miaka 12 iliyopita kwa lumia 900.

Hapa sizungumzii microsoft wala HMD Global watenegenezaji wa Nokia jina,
Hapa nazungumzia Nokia Mwenyewe.
 
Hivi wadau ni Mimi tu au?
Ni mimi tu ninayeona Simu za Zamani za Nokia kama Nokia2700, Xpress Music, E71 N.k zilikuwa Bora kabisa kuliko za sasa?

Je Nokia hawawezi kuzalisha tena hizo Simu?

View attachment 1490945View attachment 1490946View attachment 1490947
mkuu toka 2010 Nokia waliajiri CEO wa kwanza wa kigeni akazipiga chini hizo simu, na software husika ikauzwa kampuni fulani ireland sasa hivi imefungiwa haitumiki, watu walilalamika sana wakataka ifanywe open source na kampuni nyingi zilikuwa interested ila hakuna aliefanikiwa, kifupi ilikuwa ni scandal kubwa sana na mpaka leo huyo CEO hapendwi sana na wapenzi wa Nokia.

sasa hivi zipo simu kama hizo za Nokia ila hazitengenezwi na Nokia wenyewe bali kampuni Inaitwa HMD, japo muonekano ni kama wa Nokia ila ufanyaji kazi ni tofauti, unatumia os ya kaios ambayo ipo slow, haina mambo mengi na mvuto kama symbian.

nokia wenyewe sasa hivi wapo zaidi kwenye Networking mambo ya 5g, magari yanayojiendesha yenyewe, kulicence technology etc

japan wana feature phone za Aina hio ambazo zina muonekano mzuri na pengine software nzuri pia, ila upatikanaji wake ni mgumu sana
Infobar xv
6.jpg


unaweza ziangalia zaidi hapa
Kyoex - Shop Buy our selection of Japanese Keitai Slide Phones
Kyoex - Shop Buy our selection of Japanese Keitai Flip Phones
 
Nokia ya sasa inamilikiwa na mtu mwingine sio yule wa zamani ndio maana ata product zao sio kali kama zile za mwanzoni.
 
Back
Top Bottom