Kwanini ni ngumu kuamua kutokuwa na mtoto Afrika?

Joel360

JF-Expert Member
Sep 21, 2013
981
631
Why can't we(Africans) set apart woman and motherhood.

Africa kama wewe ni mwanamke basi ni kama vile hujakamilika bila kuzaa.

Karibia kila mwanamke Africa anataka azae.

Kwa muda mrefu sana nimekuwa nikitafuta mwanamke ambaye yeye hana mpango wa kuzaa wala kuwa na mtoto. Si jambo la ajabu katika nchi za nje ya Africa, nchi za wenzetu kuna idadi kubwa sana ya wanawake ambao wao wamefanya maamuzi ya kutokuwa na watoto na hakuna mtazamo wowote usiofaa ambao wamepokea kutoka kwa watu wengine. Kwanini ? Kwa sababu nchi za wenzetu kuwa mwanamke hakumaanishi kwamba lazima uwe mama.

Sina tatizo lolote na suala la uzazi na nawapenda sana watoto. Ila hili suala linapaswa kuwa maamuzi ya mtu na si sheria au kanuni kama ilivyo Africa.

Baadhi ya watu kuchagua kutozaa hakumaanishi binadamu wataisha. Kumbuka kuna watu wengi ambao wanapenda kuzaa. Kwahiyo watu wachache wakiamua kutozaa wala haiwezi kuwa tatizo.

Lakini kuzaa ni sehemu ya tamaduni ya Muafrica. Trust me, hata hapa kuna watu watakuja kunikashifu na kuhisi nna matatizo ya uzazi. Yaani kama vile hili suala la ndoa bila watoto ni mwiko Africa. Ukitaka kuoa mwanamke ambae hana mpango wa kuzaa basi utasubiri sana,

Niulize mimi, nimeanza kutafuta huyo mwanamke muda mrefu sana na nahisi kabisa kama hayupo. Nakutana na wanawake wagumba ambao nao wananiogopa KABISA eti wanahisi nimepewa masharti na mganga wa kishirikina nisiwe na mtoto au wanaogopa labda ntawatoa kafara, khaaa! Mimi na ushirikina ni ardhi na anga, viko mbali sana na havitakutana.

Yaani ukitaka ndoa bila watoto Africa basi utaishia kufunga ndoa na mwanamke mwenye umri mkubwa ambae ame-hit menopause au mwanamke mgumba ambae hatoacha kunywa mitishamba ili apate mtoto.

Kwa mwanamke wa Africa hili suala haliingii KABISA akilini eti awe amechagua kutokuwa na mtoto kama MIMI au watu katika nchi zilizoendelea ambao wanachagua.

Swali muhimu: Kwanini ni ngumu kuamua kutokuwa na mtoto Afrika? Labda nipate mawazo yenu pia.

Swali la msingi ni: Why can't we (Africans) set apart woman and motherhood.
 
Jibu ni Rahisi tu, Africa tuna Utamaduni wetu ambao kwa Kiasi Kikubwa ndo hivyo kama ulivyosema kuwa na Mtoto

na Si sahihi Kutulinganisha na Wazungu au hayo mataifa mengine kama ambavyo umepigia mfano, Ila Sio ishu hayo ni mawazo yako ni si kosa kuwa hivyo Ulivyo amua ila pia nikushauri,

Unaweza kuendelea kutafuta mwanamke wa aina hiyo unayotaka au Ikibidi uende huko ambako kutozaa ni sehemu ya Tamaduni zao nadhani utafanikisha lengo lako Mkuu
 
Jibu ni Rahisi tu, Africa tuna Utamaduni wetu ambao kwa Kiasi Kikubwa ndo hivyo kama ulivyosema kuwa na Mtoto

na Si sahihi Kutulinganisha na Wazungu au hayo mataifa mengine kama ambavyo umepigia mfano, Ila Sio ishu hayo ni mawazo yako ni si kosa kuwa hivyo Ulivyo amua ila pia nikushauri, Unaweza kuendelea kutafuta mwanamke wa aina hiyo unayotaka au Ikibidi uende huko ambako kutozaa ni sehemu ya Tamaduni zao nadhani utafanikisha lengo lako Mkuu

Sent from my SM-C9000 using JamiiForums mobile app
Kwa kweli naendelea kutafuta ila kuhusu kwenda, hahaha itakuwa jambo la ajabu kidogo. Eti niendee abroad kwa sababu ya kutafuta mwanamke tu.

Ila Asante sana kwa ushauri wako.
 
Kama mnaona alafu hamtaki watoto then kwanini muoane?
Si muishi tu kama girlfriend na boyfriend ambapo main goal itakuwa ni sex then at the end everbody dies alone which sounds nonsense to me.
Naturally marriage is all about family and by family I meant having kids.
 
Why can't we(Africans) set apart woman and motherhood.

1.Africa kama wewe ni mwanamke basi ni kama vile hujakamilika bila kuzaa.

2.Kwa sababu nchi za wenzetu kuwa mwanamke hakumaanishi kwamba lazima uwe mama.

3.Ila hili suala linapaswa kuwa maamuzi ya mtu na si sheria au kanuni kama ilivyo Africa.


4.Lakini kuzaa ni sehemu ya tamaduni ya Muafrica.


Swali la msingi ni: Why can't we(Africans) set apart woman and motherhood.

mbna umejijibu hapo mwenyewe kwenye mada yako hizo QUOTE nne zinakupa jibu la maswari yko
so sioni jambo la wewe kulalama ikiwa mada yako ina majibu tayali ambayo umeyajibu wewe mwenyewe

1. africa kama wewe ni mwanamke basi ni kama vile hujakamilika bila kuzaa.
"ndio nature tuliyoipokea toka mababu na mabibi zetu"

2.Kwa sababu nchi za wenzetu kuwa mwanamke hakumaanishi kwamba lazima uwe mama.
"ndio nature waliyoipokea toka kwa mababu na mabibi zao so fanya mpango uhamie CANADA"

3.Ila hili suala linapaswa kuwa maamuzi ya mtu na si sheria au kanuni kama ilivyo Africa.
"nitajie nchi moja tu AFRCA ambapo ni sheria au ipo kanuni ndogondigo kuwa ukiolewa au ukiwa na mahusiano lazima uzae"

4.Lakini kuzaa ni sehemu ya tamaduni ya Muafrica.
"Sasa hilo ndio jibu ukishakuwa muafrica ni muafrca huwezi kuwa mzungu na laazima ufate tamaduni za mwafrca ama uhamue ULAYA

na mm nakwambia kuzaa ni nature ya mwanadamu iwe kidini au kisayansi na kuna article kabisa za kisayansi zinazousiana na magonjwa ya tumbo ya kinamama
zinaelezea hujitibu yenyewe pindi mwanamke akishabeba ujauzito
yaan kwa LUGHA nyepesi mwanamke hurekebisha viungo vyake vya mwili hata kiakili akishabeaba Ujauzito na kuzaa ndio hupevuka kabisa kuwa imala
Angalia masingle mother wanavyopambana na maisha

na hata upande wa kufurahia Sex wanawake walozaa ndio rahisi zaidi kufika organism na kufurahia sex kuliko wasio zaa
na ndo mana mwanamke akishazaa kuchedwa ni rahisi 7bu ile rah halisi ss ndio huipata so hutamani sex mara kwa mara

kuthibitisha hilo waangalie wadada maarufu tanzania mpk duniani ambao hawajazaa huw wanavurugwa sana na mifumo yao ya mwili na akili inakuwa Aiipo sawa

sasa mwanamke gani mwenye fulsa ya kuzaa aache kuzaa aangaike na wewe
 
Kama mnaona alafu hamtaki watoto then kwanini muoane?
Si muishi tu kama girlfriend na boyfriend ambapo main goal itakuwa ni sex then at the end everbody dies alone which sounds nonsense to me.
Naturally marriage is all about family and by family I meant having kids.
Mkuu una point kama nukta
 
Kama mnaona alafu hamtaki watoto then kwanini muoane?
Si muishi tu kama girlfriend na boyfriend ambapo main goal itakuwa ni sex then at the end everbody dies alone which sounds nonsense to me.
Naturally marriage is all about family and by family I meant having kids.

😀 😀 😀 😀 correct
 
Ninyi ndio mnafanya maadili yanazidi kumomonyoka kwa kuiga hadi visivyofaa.

Kila jamii dunia ina mila na desturi zake, na uwezi lazimisha zifanane kisa tu unataka jamii yako iwe sawa na jamii nyingine unayo itaka wewe.

Kwa Africa dhumuni kubwa la ndoa ni kuanzisha familia, familia ambayo itabeba jina lako, itaendeleza utamaduni wako, itakuwakilisha pindi utakapo kuwa haupo hai na sio vingnevyo. Kwaiyo tambua dhamira ya tamaduni flan kabla ya kuifananisha na tamaduni za jamii zingne.
 
Ulichosahau ata huko unakosema sio lazima mwanamke kuzaa pia kuna child adoption na surrogate mother maana yake wanataman kuwa na watoto ila wanaogopa/hawapend kubeba ujauzito
 
Athari za( kuamua )kutokuzaa ni nyingi na zina madhara makubwa sana ukilinganisha na kuzaa. Tafsiri sahihi ya kuoa/kuolewa ni nini hasa zaidi ya kuwa na familia?
 
Kama mnaona alafu hamtaki watoto then kwanini muoane?
Si muishi tu kama girlfriend na boyfriend ambapo main goal itakuwa ni sex then at the end everbody dies alone which sounds nonsense to me.
Naturally marriage is all about family and by family I meant having kids.
Mkuu,

Kwa hivyo watu wasio na uwezo wa kupata watoto kibaiolojia wasioe na kuolewa?
 
Mkuu,

Kwa hivyo watu wasio na uwezo wa kupata watoto kibaiolojia wasioe na kuolewa?
Hapana sijamaanisha hivyo, hiyo ni only applicable kwa wenye uwezo wa kupata watoto.
Watu wasio na uwezo wa kupata watoto haimaanishi hawataki watoto, wanataka kupata watoto but there's no other way around.
 
mbna umejijibu hapo mwenyewe kwenye mada yako hizo QUOTE nne zinakupa jibu la maswari yko
so sioni jambo la wewe kulalama ikiwa mada yako ina majibu tayali ambayo umeyajibu wewe mwenyewe

1. africa kama wewe ni mwanamke basi ni kama vile hujakamilika bila kuzaa.
"ndio nature tuliyoipokea toka mababu na mabibi zetu"

2.Kwa sababu nchi za wenzetu kuwa mwanamke hakumaanishi kwamba lazima uwe mama.
"ndio nature waliyoipokea toka kwa mababu na mabibi zao so fanya mpango uhamie CANADA"

3.Ila hili suala linapaswa kuwa maamuzi ya mtu na si sheria au kanuni kama ilivyo Africa.
"nitajie nchi moja tu AFRCA ambapo ni sheria au ipo kanuni ndogondigo kuwa ukiolewa au ukiwa na mahusiano lazima uzae"

4.Lakini kuzaa ni sehemu ya tamaduni ya Muafrica.
"Sasa hilo ndio jibu ukishakuwa muafrica ni muafrca huwezi kuwa mzungu na laazima ufate tamaduni za mwafrca ama uhamue ULAYA

na mm nakwambia kuzaa ni nature ya mwanadamu iwe kidini au kisayansi na kuna article kabisa za kisayansi zinazousiana na magonjwa ya tumbo ya kinamama
zinaelezea hujitibu yenyewe pindi mwanamke akishabeba ujauzito
yaan kwa LUGHA nyepesi mwanamke hurekebisha viungo vyake vya mwili hata kiakili akishabeaba Ujauzito na kuzaa ndio hupevuka kabisa kuwa imala
Angalia masingle mother wanavyopambana na maisha

na hata upande wa kufurahia Sex wanawake walozaa ndio rahisi zaidi kufika organism na kufurahia sex kuliko wasio zaa
na ndo mana mwanamke akishazaa kuchedwa ni rahisi 7bu ile rah halisi ss ndio huipata so hutamani sex mara kwa mara

kuthibitisha hilo waangalie wadada maarufu tanzania mpk duniani ambao hawajazaa huw wanavurugwa sana na mifumo yao ya mwili na akili inakuwa Aiipo sawa

sasa mwanamke gani mwenye fulsa ya kuzaa aache kuzaa aangaike na wewe
Umemaliza kila kitu
 
Ulichosahau ata huko unakosema sio lazima mwanamke kuzaa pia kuna child adoption na surrogate mother maana yake wanataman kuwa na watoto ila wanaogopa/hawapend kubeba ujauzito
Yeye mwenyewe tu baba yake angekuwa na hizo akili kama za kwake, je angekuwapo hapa kutype upuuuzi wake huu.

Mambo mengine ni shida ya kukaa mbali na nyumba za ibada tu.
 
Africa Ni nature broo ..usiangaike kutafuta majibu naona unajuta sna kuzaliwa anyway cjui pepo gani chafu amekuingia na ataki kabsa kukuachia ukaongeze dunia. Huku huna shida zozote ni chuki za kuwachukia malaika

Naamuru kwa jinaaaa la yesu na kwa damu yake. Toka achia kjna huyu mnayemshikiliaa asioe Wal kutaka watoto. Toka achia ...
Nb nende kimara korogwe muone mchungji mastai akuongoze kwa sala ukirudi apA utatoa ushuhuda na jinsi watot wanavyoketa raha
 
Hapana sijamaanisha hivyo, hiyo ni only applicable kwa wenye uwezo wa kupata watoto.
Watu wasio na uwezo wa kupata watoto haimaanishi hawataki watoto, wanataka kupata watoto but there's no other way around.
Kama umuhimu wa kuoa/ kuolewa ni kupata mtoto mtu, ukiwa huna nia ya kupata mtoto hakuna umuhimu wa kuoa/kuolewa, wasioweza kupata mtoto kibaiolojia kwa nini waoe au kuolewa?
 
Kama mnaona alafu hamtaki watoto then kwanini muoane?
Si muishi tu kama girlfriend na boyfriend ambapo main goal itakuwa ni sex then at the end everbody dies alone which sounds nonsense to me.
Naturally marriage is all about family and by family I meant having kids.
muue
 
Yeye mwenyewe tu baba yake angekuwa na hizo akili kama za kwake, je angekuwapo hapa kutype upuuuzi wake huu.

Mambo mengine ni shida ya kukaa mbali na nyumba za ibada tu.
Kuna mda tunataman mambo ya kijinga pasipo kujua madhara yake kama tungefanyiwa ss ingekuweje
 
Kwa kweli naendelea kutafuta ila kuhusu kwenda, hahaha itakuwa jambo la ajabu kidogo. Eti niendee abroad kwa sababu ya kutafuta mwanamke tu.

Ila Asante sana kwa ushauri wako.
Weye nae sema tu domo zege tu! huna lolote ! hao wa nje si wanakuja kutalii? kibao! wapo tele hapo Arusha? mikumi, nk Ma tx-kibao huko mikoani? waalimu, Manurse wa nje wanakuja kujitolea huko kwenu mbwinde ! mama janeti huyo hapo yupo hataki mtoto!
 
Back
Top Bottom