ISRAEL JR
JF-Expert Member
- Feb 1, 2013
- 1,439
- 630
CHADEMA KWISHAAAAAmani iwe nanyi wana JF,
Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA ) kijenotyipia ( ki-mtazamo wa ndani ) kimeshakufa kibudu ila kifenotyipia ( ki-mtazamo wa nje ) bado kinaishi hali hii ilishawahi kuvikumba vyama vya National Convention for Constitutional Reform ( NCCR -Mageuzi ) baada ya Uchaguzi mkuu wa mwaka 1995 na baadae Chama cha Civic United Front ( CUF ) baada ya Uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 mpaka naandika makala hii kamwe si NCCR -Mageuzi wala CUF iliyowahi kuinuka baada ya kufa kijenotyipia,
===
Chadema mara baada ya kubadili malengo yake kutoka kuwa chama cha kusimamia masilahi ya wananchi mpaka Chama cha kutafutia nafuu ya maisha kwa viongozi wake wa juu ndio ulikuwa mwanzo wa mwisho wa Chama hiki kikongwe nchini chenye zaidi ya miaka thelathini ( 30 ) sasa,
===
Vyama vyote hivi tangu NCCR -Mageuzi,CUF na sasa Chadema sababu ya vifo vyao ni ileile ya mgawanyo usio sawia wa keki za Chama wala sio ccm-tanzania kama wanavyowaaminisha wananchi na Ushahidi mkubwa ni huu vyama vyote vitatu pamoja na kupata mabilioni ya Shilingi toka kwenye ruzuku na michango mbalimbali ya wanachama na wahisani bado havijawahi kuwa na mali zao zisizohamishika ( mfano, ofisi za kisasa za Chama ) kuonesha kuwa maisha ya vyama hivyo si ya muda mrefu ( temporary Polical Parties )
===
Unapoona Halima Mdee na wenzake 18 wanakimbilia keki ya Chama kwa mbio kali kumzidi Freeman Mbowe au John Heche ni ushahidi mwingine kuwa Chadema ilishaondoka kuwa chama aminiwa kwa masilahi ya Watanzania mpaka Chama cha kucheza kidali Poo kwenye fursa na pesa,
===
Zoezi la " Chadema Digital " limewadhihirishia pasina kuacha shaka Viongozi na Wanachama kuwa Chama chao kimeshakufa rasmi reffence is made to Shinyanga -Kahama and Msalala wanachama waliosajiliwa kidijitali kwa majimbo yote mawili hawakufikia wanachama miambili ( 200 ), Watanzania ni watu makini sana kuliko Chadema mnavyofikiria,
===
....Nisiwachoshe nitaendelea kidogo kidogo mpaka Part 10...... ila kwa hatua ya Sasa wanaotaka siasa au nafasi za kisiasa kama Ubunge|Udiwani au Uenyekit wa vijiji,mitaa na vitongoji waende CCM-Tanzania ndio chama kinachoweza kulea vipaji na vipawa vya mwanasiasa yeyote awaye,
View attachment 2003106