Kwanini Nchi nyingi Duniani zinakataa matumizi ya Chanjo ya AstraZeneca?

Besta Mlagila

Senior Member
May 29, 2018
101
191
Tangu kuingia kwa Virusi vya Corona wataalamu wa Afya wamepambana kutafuta dawa na chanjo kukabiliana na gonjwa hili hatari bila mafanikio.

Hivi karibuni ziligundulika chanjo mbalimbali ikiwemo ASTRAZENECA ambayo ilipitishwa na Shirika la Afya Duniani kuanza kutumika kwa binadamu ili kupunguza na kuzuia vifo vilivyokuwa vikiendelea kutokea.

Katika siku za karibuni Nchi mbalimbali zimezuia matumizi ya CHANJO hiyo kwa madai kuwa ina madhara yanayoweza kupelekea kifo ambapo baadhi ya Nchi zimeripoti vifo vya watu vilivyojitokeza baada ya wao kupata CHANJO, japokuwa hawakuhusisha moja kwa moja vifo hivyo ni Chanjo ya AstraZeneca.

Kati ya Nchi zilizopiga marufuku matumizi ya CHANJO ya AstraZeneca ni Indonesia, Congo DRC, Norway, Denmark, Iceland, Bulgaria, Ireland, the Netherlands, France, Italy, Germany, Austria, Venezuela.

Sisi ambao bado Serikali yetu haijaamua kutumia CHANJO yoyote tunapaswa kujifunza nini?
 
Unajua nini Chanjo yeyote inachukua muda mpaka kudungurika na kuthibitisha kwamba ipo vizuri kwa matumizi ya binadamu ,sasa shida inawekanaje mtu agundua chanjo ndani ya miezi kadhaa na ikaanza kutumika kwa watu? Vita ya uchumi ni mbaya sana ndugu zanguni
 
Tangu kuingia kwa Virusi vya Corona wataalamu wa Afya wamepambana kutafuta dawa na chanjo kukabiliana na gonjwa hili hatari bila mafanikio.

Hivi karibuni ziligundulika chanjo mbalimbali ikiwemo ASTRAZENECA ambayo ilipitishwa na Shirika la Afya Duniani kuanza kutumika kwa binadamu ili kupunguza na kuzuia vifo vilivyokuwa vikiendelea kutokea.

Katika siku za karibuni Nchi mbalimbali zimezuia matumizi ya CHANJO hiyo kwa madai kuwa ina madhara yanayoweza kupelekea kifo ambapo baadhi ya Nchi zimeripoti vifo vya watu vilivyojitokeza baada ya wao kupata CHANJO, japokuwa hawakuhusisha moja kwa moja vifo hivyo ni Chanjo ya AstraZeneca.

Kati ya Nchi zilizopiga marufuku matumizi ya CHANJO ya AstraZeneca ni Indonesia, Congo DRC, Norway, Denmark, Iceland, Bulgaria, Ireland, the Netherlands, France, Italy, Germany, Austria, Venezuela.

Sisi ambao bado Serikali yetu haijaamua kutumia CHANJO yoyote tunapaswa kujifunza nini?

Suala ni kusitisha kwa kipindi fulani/ kwa muda.
Tunapaswa kujua kuwa dawa yoyote au chanjo inakuwa na tabia tofauti kwa kila mmoja wetu. Na kwa wakati mwingine kwa jamii tofauti.

Ukienda kwenye suala la ugunduzi wa dawa na upatikanaji wa dawa husika kwa jamii, kuna kitu kinaitwa POST MARKET SURVEILLANCE. Hii ni kwa dawa yoyote iliyoingizwa sokoni. Na mtu hutakiwa kulipoti chochote ambacho si cha kawaida ili mtengenezaji ajiridhishe kuwa tatizo husika linatokana na chanjo au dawa husika.

Pia, ukienda kwa chanjo husika kuna mambo mengi ya kujiuliza, kwani si chanjo ya kupima na kuchanja, ni mass vaccination hivyo basi ndio maana unaambiwa haijawa rahisi kusema tatizo linahusisha chanjo binafsi au la.

Kwani kuna watu tuna shida zetu hata kabla ya chanjo. Ingawa chanjo pia yaweza kuwa na shida.

Suala ni kusubiri majibu ya uchunguzi na kama kunahitajika adjustment kwa chochote.
 
Vita ya kiuchumi hivyo.

Screenshot_20210316-235607.jpg


Ukisikia vita vya kiuchumi huu ndio mfano halisi sasa.

Sio unasema tuna vita vya kiuchumi wakati hakuna anayeshindana na wewe, nyambafuu.
 
Back
Top Bottom