Kwanini napinga mchakato wa Katiba Mpya ulivyo sasa na kwanini wewe pia yakupasa uupinge

Kwa kweli Mwanakijiji umepembua vizuri sana na viashiria ulivyobainisha na dhahir shahir vitaleta mush'ker mwisho wa siku.

Nakupongeza sana kwa maono yako na kuhadharisha jamii ili usije kulaumika mwisho wa siku.
 
Kwanza M.M.M. bravo na asante kwa darasa. Ni haki na wajibu kuanza kulipia tuition fees sasa!

Sikuwahi kufikiria kwa ulinganifu tafsiri ya kiswahili na ile ya kiingereza ktk ibara ya 8 kama ulivyonyambulisha. Kwa vile tofauti ni kubwa namna hiyo (tuandishi na afsiri) mi nadhani lile suala la muda (katiba mpya kabla ya 2015) tusiliendekeze sana maana halitatupa tunachokihitaji.

Naungana nawe 110% kupinga kwa nguvu na hoja zote mchakato huu wa JK na CCM wa katiba mpya.
 
Mimi nakubaliana na wewe. Tumeundiwa Tume na Rais, huku SISI ndio wenye mamlaka kamili ya kuunda tume. Kwa nini tuendelee kudanganywa na kudanganyika juu ya hili? Nimejaribu kuwaelimisha wenzangu lakini hawanielewi, kwa kuwa wengi wao hawajawahi kuisoma katiba iliyopo HATA SIKU MOJA! Wanaona ni mambo ya siasa. Hii si siasa. Ni suala la kutunga sheria mama, itakayotawala mustakabali wote wa maisha yao. SIO SIASA!
 
Sasa mkitaka kuelewa hii "assault on popular sovereignty" angalia ni jinsi gani Rais na serikali imeamua kuwa wananchi wanapotaka kujiandikia katiba yao mambo gani wasiyajadili kabisa; mmejiuliza Rais na serikali imepata wapi madaraka ya kuwazuia wananchi kujadili mambo yote yanayohusiana na katiba? Hivi kama wananchi wanataka kuondokana Urais na kuwa na Mfalme kwanini wasiweze kufanya hivyo kupitia katiba mpya?
 
Wewe ni kipi ambacho Kikwete alifanya vibaya ukampinga?
Badala ya kuja na hoja, una-attack personalities.
Tuambie ni kwa nini wewe unaona ni bora kutengeneza katiba kwa kupitia tume badala ya baraza la katiba?



Tumbie basi wewe umechuja nini?
Mbona hamjibu hoja mnaishia kusema bravo tuu?



Wewe utaje kipi kizuri alichofanya Rais yeyote kabla ya Kikwete ambacho Kikwete hajakifanya zaidi. Nakwambia hutopata, mtabaki kutafuta vya kutafuta, ooh mara kofia, mara picha, hamna cha maana hata kimoja. Mnajua ndani ya roho zenu kuwa Kikwete ni Rais bora kwa Tanzania kuliko yeyote wa kabla yake.
 
Tangu mwanzo ninawasikitikia sana wote walio nje ya system huku wanaamini kuwa chini ya ccm watapata katiba bora kwa maslahi ya taifa hili. Ni nini ambacho kimewahi kufanywa na serikali hii kwa faida na maslahi ya wananchi wa kawaida wa taifa hili? Bahati mbaya sana tumekuwa taifa la 'bora liende'. Kiongozi mwenye akili timamu hawezi kukwambia 'toa maoni ila usigusie kabisa hili, lile, nk!!' Katiba gani ya taifa isiyogusia mambo yote muhimu yanayoligusa/liunda taifa husika?!
 
Sijui watu wetu wana matatizo gani!? Sote tulikuwa tunajua sheria iliyotungwa inatakataza watu kuzungumzia muungano au hata kutaka kuuvunja. Sasa watu wakashabikia lakini leo wanataka 'watu waruhusiwe kujadili Muungano". Hivi wakati inakatazwa kwanini hawakuchukua msimamo huo? Nilivyosema awali bado ni kweli - wale waliounga mkono na wenye kukubali mchakato huu hawana haki ya kulalamikia matokeo yake kwani matokeo yalikuwa dhahiri toka mwanzo.
 
Sijui watu wetu wana matatizo gani!? Sote tulikuwa tunajua sheria iliyotungwa inatakataza watu kuzungumzia muungano au hata kutaka kuuvunja. Sasa watu wakashabikia lakini leo wanataka 'watu waruhusiwe kujadili Muungano". Hivi wakati inakatazwa kwanini hawakuchukua msimamo huo? Nilivyosema awali bado ni kweli - wale waliounga mkono na wenye kukubali mchakato huu hawana haki ya kulalamikia matokeo yake kwani matokeo yalikuwa dhahiri toka mwanzo.

Ndio mzee hapa tz ndio huwa inatuletea matatizo.
 
Sijui watu wetu wana matatizo gani!? Sote tulikuwa tunajua sheria iliyotungwa inatakataza watu kuzungumzia muungano au hata kutaka kuuvunja. Sasa watu wakashabikia lakini leo wanataka 'watu waruhusiwe kujadili Muungano". Hivi wakati inakatazwa kwanini hawakuchukua msimamo huo? Nilivyosema awali bado ni kweli - wale waliounga mkono na wenye kukubali mchakato huu hawana haki ya kulalamikia matokeo yake kwani matokeo yalikuwa dhahiri toka mwanzo.

ujinga wa watu mkuu
 
kuna mambo ya awali ya yote ambayo Mzee Mwanakijiji umeyaacha na hapo ndipo mushkeli wote unakoanzia. Huwezi kutumia sheria za kawaida kuanzisha machakato wa kubadilisha katiba. Sheria za kawaida zahitaji simple majority ya wabunge kulingana na koram tu wakati marekebisho ya katiba huhitaji zaidi ya 2/3 ya wabunge wote bila ya kujali mahudhurio yao.

Kwa lugha nyingine sheria ambayo AG alikwenda nayo ya mchakato wa kurekebisha katiba inakiuka katiba...it is unconstitutional.period hakuna kifungu chochote kwenye katiba yetu ambacho kinaruhusu sheria za kawaida ktumika kunyambulisha katiba iliyopo bali sheria iliyopo ya kikatiba ni kupitia 2/3 ya Bunge lote.

Pili, utaratibu wa kukiuka katiba ni wa makusudi kwa sababu waliona iakuwa kupata idadi ya wabunge wa 2/3 kuweza kupitisha marekebisho ya kikatiba na kwa kufanya hivyo waliunda utaratibu wa ukwiukwaji wa katiba ili kulinda masilahi yao wenyewe.

Tatu, kutokana na mapungufu makubwa ya kikatiba ya sheria ya kurekebisha katiba basi tume aliyoiunda JK kusimamia mchakato wa kukusanya maoni ni batili, na hayo mabunge yote mawili ni batili bila ya kuangalia kama wanayo mamalka ya kikatiba ya kufanya hivyo. katika hukumu ya Mahakama Kuu ya Kenya dhidi ya mkutano wa Boma mahakama kuu ya Kenya ilitumia hoja hizo hizo kujibu ya kuwa mkutano wa Boma uliojumuisha wabunge, wanaharakati na warasimu ulikua batili kwa sababu wamiliki wa kenya ni raia na nafasi sawa hazikutolewa katika kuchagua tume na wananchi walipaswa washirikishwe....................hii kwa mahakama zetu ni hoja ambayo itatupwa kwa sababu kama huhoji uhalali wa sheria ya kurekebisha katiba kama imekiukakatiba utashindwa kuwashawishi kwa hoja ulizozibandika kule kwa sababu watesema demokrasia yetu ni ya kiuwakilishi tu.................kwa hiyo hao ni wawakilishi wa wananchi ingawaje hawakutumwa kwa minajili ya kurekebisha katiba..........
 
Last edited by a moderator:
Wewe utaje kipi kizuri alichofanya Rais yeyote kabla ya Kikwete ambacho Kikwete hajakifanya zaidi. Nakwambia hutopata, mtabaki kutafuta vya kutafuta, ooh mara kofia, mara picha, hamna cha maana hata kimoja. Mnajua ndani ya roho zenu kuwa Kikwete ni Rais bora kwa Tanzania kuliko yeyote wa kabla yake.

Ya kutoka usingizini ukataja ni kama haya;
1. Kudhibiti Mfumko wa bei
2. Kuchujuka kwa wapiga kura
3. Kuimarisha thamani ya Shilingi
4. Kushindwa kusimamia ilani ya chama chake
5. Hata chama kimemshinda!.
Sijakaa kuhorodhesha ni mengi mno.

Hatukutaka ashindwe kama wenzake walivyoshinwa ila aweze waliyoshindwa.
Watu tulikuwa na matumaini kuwa ataweza lakini wapi ndiyo maana kura zilishuka mno!.
Ajabu hata kutazamia hawezi!.

Ukitaka aliyoweza uliza utajiwe pia.
 
Mzee Mwanakijiji HONGERA nyingi umeishapewa! nami nongezea pia.
Nakuomba usife moyo kwa kubezwa na wanaopinga juhudi zako za kuelimisha jamii.!
 
Ya kutoka usingizini ukataja ni kama haya;
1. Kudhibiti Mfumko wa bei
2. Kuchujuka kwa wapiga kura
3. Kuimarisha thamani ya Shilingi
4. Kushindwa kusimamia ilani ya chama chake
5. Hata chama kimemshinda!.
Sijakaa kuhorodhesha ni mengi mno.

Hatukutaka ashindwe kama wenzake walivyoshinwa ila aweze waliyoshindwa.
Watu tulikuwa na matumaini kuwa ataweza lakini wapi ndiyo maana kura zilishuka mno!.
Ajabu hata kutazamia hawezi!.

Ukitaka aliyoweza uliza utajiwe pia.

1. Mfumko wa bei si tatizo kubwa sana, ni tatizo la dunia nzima kwa sasa, hujasikia Ethiopia na Ugiriki. Tatizo kukiwa na mfumko wa bei halafu ukashindwa kununua unachokihitaji.

2. Sijakuelewa, kwani wao magwanda (nguo) hata yachujuke?

3. Thamani ya Shillingi, ikiwa imeshuka, kwanini hutumii fursa hiyo kuuza mahindi yako nje ya Tanzania? au huna?

4. Ilani ya chama chake unaijuwa weyee? Chama kimemshinda?

5. wakati chama hicho hicho ndio wanaongoza nchi, au hilo hulijui? Utachekwa!
 
1. Mfumko wa bei si tatizo kubwa sana, ni tatizo la dunia nzima kwa sasa, hujasikia Ethiopia na Ugiriki. Tatizo kukiwa na mfumko wa bei halafu ukashindwa kununua unachokihitaji.

2. Sijakuelewa, kwani wao magwanda (nguo) hata yachujuke?

3. Thamani ya Shillingi, ikiwa imeshuka, kwanini hutumii fursa hiyo kuuza mahindi yako nje ya Tanzania? au huna?

4. Ilani ya chama chake unaijuwa weyee? Chama kimemshinda?

5. wakati chama hicho hicho ndio wanaongoza nchi, au hilo hulijui? Utachekwa!
Nahisi umeakisi ID yako
Umejitahidi hapo #1,
lakini hizi nchi ulizozitaja unajua ni kwanini zimefikia hapo mpaka ukazitaja kama ushahidi wa mfumko.
Kwingine umetumia jaziba refresh akili vizuri alafu ujaribu tena kwenye #2, #3, #4 na #5.
 
kuna mambo ya awali ya yote ambayo Mzee Mwanakijiji umeyaacha na hapo ndipo mushkeli wote unakoanzia. Huwezi kutumia sheria za kawaida kuanzisha machakato wa kubadilisha katiba. Sheria za kawaida zahitaji simple majority ya wabunge kulingana na koram tu wakati marekebisho ya katiba huhitaji zaidi ya 2/3 ya wabunge wote bila ya kujali mahudhurio yao.

Kwa lugha nyingine sheria ambayo AG alikwenda nayo ya mchakato wa kurekebisha katiba inakiuka katiba...it is unconstitutional.period hakuna kifungu chochote kwenye katiba yetu ambacho kinaruhusu sheria za kawaida ktumika kunyambulisha katiba iliyopo bali sheria iliyopo ya kikatiba ni kupitia 2/3 ya Bunge lote.

Pili, utaratibu wa kukiuka katiba ni wa makusudi kwa sababu waliona iakuwa kupata idadi ya wabunge wa 2/3 kuweza kupitisha marekebisho ya kikatiba na kwa kufanya hivyo waliunda utaratibu wa ukwiukwaji wa katiba ili kulinda masilahi yao wenyewe.

Tatu, kutokana na mapungufu makubwa ya kikatiba ya sheria ya kurekebisha katiba basi tume aliyoiunda JK kusimamia mchakato wa kukusanya maoni ni batili, na hayo mabunge yote mawili ni batili bila ya kuangalia kama wanayo mamalka ya kikatiba ya kufanya hivyo. katika hukumu ya Mahakama Kuu ya Kenya dhidi ya mkutano wa Boma mahakama kuu ya Kenya ilitumia hoja hizo hizo kujibu ya kuwa mkutano wa Boma uliojumuisha wabunge, wanaharakati na warasimu ulikua batili kwa sababu wamiliki wa kenya ni raia na nafasi sawa hazikutolewa katika kuchagua tume na wananchi walipaswa washirikishwe....................hii kwa mahakama zetu ni hoja ambayo itatupwa kwa sababu kama huhoji uhalali wa sheria ya kurekebisha katiba kama imekiukakatiba utashindwa kuwashawishi kwa hoja ulizozibandika kule kwa sababu watesema demokrasia yetu ni ya kiuwakilishi tu.................kwa hiyo hao ni wawakilishi wa wananchi ingawaje hawakutumwa kwa minajili ya kurekebisha katiba..........


Ruta, hayo yote unayoyasema nilishayasema huko nyuma. Ndio maana miye kwa dhamira yangu siamini kabisa kuwa mchakato huu una uhalali wowote na ninawabeza wale wote ambao wameukubali na kuukumbatia kwa vile "Rais kasema"!
 
Ruta, hayo yote unayoyasema nilishayasema huko nyuma. Ndio maana miye kwa dhamira yangu siamini kabisa kuwa mchakato huu una uhalali wowote na ninawabeza wale wote ambao wameukubali na kuukumbatia kwa vile "Rais kasema"!

Mzee Mwanakijiji nimekupata lakini haya unayoyasema sasa hivi ni masuala ya kisera na yako ndani ya uwezo wa nguvu wa vyama vya siasa Bungeni kwa maana ya ushawishi wao tu na mahakama hazina sauti juu ya hilo.........Ili kuwalazimisha kuachana na upuuzi wanaoendelea nao ni kuhoji uhalali wa sheria ya marekebisho ya katiba ndani ya katib ailiyopo. Utaratibu walioutumia ni unconstituional. Hakuna mahali katiba yetu imeruhusu hicho walichiokifanya na mahakama inayo mamlaka chini ya angalizo la hukumu ya majaji 7 wa court of appela katika kesi ya Mtikila versus the A.G ambyo walisema kama mageuzi ya katiba yanafanyika nje ya mchakato uliobainishwa na katiba mahakama yaweza kuombwa kuutengua.

haitoshi kusema hukubaliana na walichofanya kama huji na mikakati ya kurekebisha kwa maana ya mkakati upi wa kimahakama waweza kutengua haya madudu yao.............
 

haitoshi kusema hukubaliana na walichofanya kama huji na mikakati ya kurekebisha kwa maana ya mkakati upi wa kimahakama waweza kutengua haya madudu yao.............

Mojawapo ya vitu ambavyo huwa navikwepa sana ni kujaribu kuwawazia watu wengine; tayari tumeonesha tatizo wengine wafikirie nini cha kufanya
 
Mojawapo ya vitu ambavyo huwa navikwepa sana ni kujaribu kuwawazia watu wengine; tayari tumeonesha tatizo wengine wafikirie nini cha kufanya

Mzee Mwanakijiji I see where you are driving at....."not my cup of tea"....Are you not running away from our journalistic onus............to educate, inform and where relevant to entertain the society?
 
Last edited by a moderator:
Mzee Mwanakijiji I see where you are driving at....."not my cup of tea"....Are you not running away from our journalistic onus............to educate, inform and where relevant to entertain the society?

unajua mojawapo ya vitu vibaya sana ni kujaribu kuwaza kila kitu. Kuna tabia siku hizi utaiona sana ambapo utakuta watu wanasema "nyie mnaandika kukosoa tu andikeni basi na nini kifanyike". Kimsingi wanaosema hivi hawataki kufikiria nini kifanyike; wanataka watu waaambie tatizo, wawafikiria namna ya kulitatua na usipoangalia hata kupanga bajeti ya jinsi ya kulitatua.
 
unajua mojawapo ya vitu vibaya sana ni kujaribu kuwaza kila kitu. Kuna tabia siku hizi utaiona sana ambapo utakuta watu wanasema "nyie mnaandika kukosoa tu andikeni basi na nini kifanyike". Kimsingi wanaosema hivi hawataki kufikiria nini kifanyike; wanataka watu waaambie tatizo, wawafikiria namna ya kulitatua na usipoangalia hata kupanga bajeti ya jinsi ya kulitatua.
[MENTION]
Mzee Mwanakijiji[/MENTION] hawa watu wako sahihi kabisa kama siye tulio nje ys system tunaona mapungufu haitoshi kuyabainisha tu bila ya kuwapatia ufumbuzi maana wao watadai ya kuwa hawana jinsi. Hivyo ni jukumu letu tuwaonyeshe jinsi iliko na sababu za kwanini hawataki kunufaika nayo kama ni masilahi binafsi au upeo mdogo ndivyo vinawakwamisha basi tuwaumbue.................ukiwaamboa matatizo tu watasema hata wao wanayajua...........ila ninafurahi kwa,mba majibu yake kumbe awali ulikwisha kuwaambia...........tusichoke kuyarudia tena na tena hadi waelimike kuwa kama wao ni mazezeta wajue siyo wote...........
 
Back
Top Bottom