Kwanini Nakupenda

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
Katika dunia hii iliyojaa watu wengi na vitu vingi kama hivi , nimeamini na nitaendelea kuamini kwamba wewe ndio mkweli kwa sababu tumekuwa wote kwa kipindi hichi kirufu siwezi kusema kwa muda gani .

Lakini niseme tu kuwa na wewe nime ENJOY , nimekuwa na matumaini , kila saa ninakuwa na muwasho wa kuongea na wewe au kuwa karibu na wewe saa zote sema tu majukumu yanatulazimu tuwe mbali wakati mwingine .

Pamoja na yote haya sijui kama umeshawahi kujiuliza kwanini nakupenda , hata wewe hujawahi kuniuliza kwanini nakupenda , kwa hakika swali hili ni gumu sana ukiniuliza ni swali ambali halina jibu moja linamajibu mengi tena yanamaelezo mengi tu .

Kuna wakati Fulani nilipata matatizo nilikuwa sehemu Fulani , siku yangu ilikuwa imeishiwa charge , sikuwa na namba nyingine kichwani zaidi ya yako nilikupigia simu kukutaarifu kuhusu suala lile .

Bila ajizi ukaja pale eneo la tukio tukaongea kisha nikakuachia simu yangu uende nayo kwako usiku ule uliona sms nyingi sana kutoka kwa watu mbali mbali iliyokutisha zaidi ni ile iliyokuwa inataka mchango wa harusi .

Huku hangaika na hawa watu wengine waliokuwa wanasumbua katika ile simu badala yake uliweka malengo katika kushugulikia matatizo yaliyotokea katika maisha yetu yangu mimi na wewe .

Watu wengi wamejaribu kuingilia mahusiano yetu kwa njia mbali mbali haswa kwa wenyewe kutumia mitandao ya internet kuandika habari chafu kuhusu wewe kwa kutumia jina langu , yote haya umeona na umewatambua .
Natambua kwa hakika wewe ni mrembo , unavutia mimi napenda kusema wewe ni MY SWEETEST THING kwangu hakuna kitu kizuri kama wewe hata sijajaribu hata siku moja wala sintojaribu kukufananisha na mwingine au kitu chochote kile .

Kwangu umekuwa ni nuru inayongaa kila siku , umekuwa ni perfume bora kuliko zote isiyoisha utamu wa harufu yake wakati wa joto, baridi hata mwili unavyojaa jasho , umekuwa ni taa inayoniongoza katika mema na mazuri wakati wote wa maisha yetu .
 
aisee hebu na nyie wadau someni kidogo hapa nimeitoa huko 2008
 
ndetichia hata mi nimeshangaa ila ni 2008 ilikuwa nahic hata member walikuwa wachache
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom