Kwanini Mwl. Nyerere anapendwa sana hapa Nyumbani?

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,786
Sijawahi kuelewa mpaka leo hii ni kwa nini Kiongozi wa kwanza wa Taifa hili Mlm.Nyerere anapendwa sana hapa kwetu, wkt kiukweli Nyerere anapaswa achukiwe sana siajabu klk Viongozi wote waliopita kama tulikuwa tunatafuta sababu ya kuchukuia Viongozi wetu kama baadhi yetu tufanyavyo leo hii, Nyerere alifanya social experiment Tanzania!

Kwa wasiofahamu maana ya social experiment ni kama vile kutengeneza dawa mpya ambayo hauna uhakika nayo kama inafaa kutumiwa na binadamu hivyo unaamua kuijaribu kwa baadhi ya binadamu na ukiona inafaa basi unaitumia ukiona haifai unaitupa!
Na hicho ndicho Mlm.Nyerere na utawala wake ulichofanya Tanzania, lkn cha ajabu Mtanzania kwa Mlm.Nyerere humwambii kitu ni kama vile unamuongelea Mungu!

Na cha ajabu zaidi labda kuliko vyote kuna watu wanaoichukia CCM kuliko kitu chochote Dunia hii lkn wanampenda Mlm.Nyerere na kumuondoa kwenye lawama zote wanazoipa CCM, tena wanakwenda mbali na kumuita kwamba alikuwa Mwana demokrasia, kwamba Utawala wake ulikuwa wa kidemokrasia, hivyo nashindwa kuelewa mtu anawezaje kuitenganisha CCM na Mlm.Nyerere? Unawezaje kutenganisha Umaskini na kudumaa kwa uchumi wa Tanzania na Mlm.Nyerere? Unawezaje kumlaumu, Mwinyi, Kikwete, au Mkapa na kumuacha Mlm.Nyerere?

Watu wanaongelea kila siku matatizo ya Zanziba na Muungano wetu lkn Mlm.Nyerere wanamtoa kwenye equation na kulaumu wengine, hili linawezekana vipi?
Watu wanalalamikia khs Elimu ya Tanzania kuwa Duni na wanalaumu Maraisi wote lkn Mlm.Nyerere wanamtoa kwenye lawama, hili linawezekana vipi wkt Mlm.Nyerere ameongoza TZ kwa miaka 24 na ndani ya hiyo miaka kwa mfano hapa Dar hakujenga Shule hata moja ukiacha zile alizotaifisha ktk Taasisi za kidini, watu wengi wamesoma Shule kwa shifti wiki hii asubuhi ijayo mchana, tena Wanafunzi walikuwa wanakaa chini hakuna madawati, lkn lawama wanapewa maraisi waliofuata, kwa nini?

Binafsi mpaka leo sielewi ni kwa nini Mlm.Nyerere hata anapendwa hapa Tanzania, hata nikianza kungalia sifa zote anazopewa na ukianza kuichambua moja baada ya nyingine utakuta wala siyo yeye anayestahili hiyo sifa!
Tukianza na Kiswahili, wengi wanafikiri TZ tunaongea Kiswahili shauri ya Nyerere, siyo kweli, Nyerere amezaliwa amekikuta Kiswahili kinatumiwa TZ nzima, ukija kwenye umoja wa Kitaifa, TZ ilikuwa moja kabla hata Nyerere hajazaliwa na ameikuta moja, tofauti tu TZ iliitwa majina tofauti vipindi mbali mbali lkn haijawahi kuwa na mtengano wala vita vya wenyewe kwa wenyewe kabla, sasa sielewi kwa nini umoja wa Taifa hili anapewa sifa yeye!

Binafsi kama kuna jambo Mlm.Nyerere alifanikiwa kama vile Wakoloni Waingereza ni brain washing, au kupumbaza watu kiakili, watu wamepumbazwa, na ndiyo maana hapa TZ hakuna anayeweza kumlaumu Mzungu kwa lolote, Mzungu anapendwa na kuabudiwa kama Mungu na haijalishi Mzungu atafanya nini atatetewa tu, Mzungu mmoja akivamiwa na majambazi hata Bunge litasimama na kuanza kujadilia kama hoja ya dharura, Mzungu hata akipiga Mwafrika risasi tutamteteta na kumlaumu Mwafrika mwenzetu aliyepigwa risasi na Mzungu kwamba ni kosa lake, hiyo ndiyo maana ya brain washing ...
 
Hahahaha ninawaambia watu every day watanzania no sawa na MTU aliyejikwaa na kudondokea ktika matope na kuanza kulaum matope yalomchafua n sio kisiki alichojikwalia
 
Watu wanamtazama kiongozi wao na wanaona anafanana nao kimavazi na katika ile hali ya kutokuwa na makuu.

Kwao inakuwa rahisi kuamini katika nia njema hata kama labda katika uhalisia wa mambo kufanikiwa kwa hiyo nia kunaweza kuchukua hata miaka 50 ijayo.

JKN aliaminika katika mtazamo huo wa kujishusha, angeweza kushirikiana na wazungu wengi mabepari na angeweza kufanikisha uchimbaji wa madini mengi tangu enzi hizo na angekuwa mmoja wa wamiliki wa machimbo. Hakufanya hivyo.

Mobutu aliamua kuiibia Zaire lakini waliomzika kule Morocco hawafiki watu 20. JKN hakuwa fisadi na watu walikimbia na msafara uliobeba mwili wake kuanzia airport mpaka msasani. Uaminifu ulikuwa sababu tosha ya kukubalika kwa walio wengi.
 
Sijawahi kuelewa mpaka leo hii ni kwa nini Kiongozi wa kwanza wa Taifa hili Mlm.Nyerere anapendwa sana hapa kwetu, wkt kiukweli Nyerere anapaswa achukiwe sana siajabu klk Viongozi wote waliopita, Nyerere alifanya social experiment Tanzania!

Kwa wasiofahamu maana ya social experiment ni kama vile kutengeneza dawa mpya ambayo hauna uhakika nayo kama inafaa kutumiwa na binadamu hivyo unaamua kuijaribu kwa baadhi ya binadamu na ukiona inafaa basi unaitumia ukiona haifai unaitupa!
Na hicho ndicho Mlm.Nyerere na utawala wake ulichofanya Tanzania, lkn cha ajabu Mtanzania kwa Mlm.Nyerere humwambii kitu ni kama vile unamuongelea Mungu!

Na cha ajabu zaidi labda kuliko vyote kuna watu wanaoichukia CCM kuliko kitu chochote Dunia hii lkn wanampenda Mlm.Nyerere na kumuondoa kwenye lawama zote wanazoipa CCM, tena wanakwenda mbali na kumuita kwamba alikuwa Mwana demokrasia, kwamba Utawala wake ulikuwa wa kidemokrasia, hivyo nashindwa kuelewa mtu anawezaje kuitenganisha CCM na Mlm.Nyerere? Unawezaje kutenganisha Umaskini na kudumaa kwa uchumi wa Tanzania na Mlm.Nyerere? Unawezaje kumlaumu, Mwinyi, Kikwete, au Mkapa na kumuacha Mlm.Nyerere?

Watu wanaongelea kila siku matatizo ya Zanziba na Muungano wetu lkn Mlm.Nyerere wanamtoa kwenye equation na kulaumu wengine, hili linawezekana vipi?
Watu wanalalamikia khs Elimu ya Tanzania kuwa Duni na wanalaumu Maraisi wote lkn Mlm.Nyerere wanamtoa kwenye lawama, hili linawezekana vipi wkt Mlm.Nyerere ameongoza TZ kwa miaka 24 na ndani ya hiyo miaka kwa mfano hapa Dar hakujenga Shule hata moja ukiacha zile alizotaifisha ktk Taasisi za kidini, watu wengi wamesoma Shule kwa shifti wiki hii asubuhi ijayo mchana, tena Wanafunzi walikuwa wanakaa chini hakuna madawati, lkn lawama wanapewa maraisi waliofuata, kwa nini?

Binafsi mpaka leo sielewi ni kwa nini Mlm.Nyerere hata anapendwa hapa Tanzania, hata nikianza kungalia sifa zote anazopewa na ukianza kuichambua moja baada ya nyingine utakuta wala siyo yeye anayestahili hiyo sifa!
Tukianza na Kiswahili, wengi wanafikiri TZ tunaongea Kiswahili shauri ya Nyerere, siyo kweli, Nyerere amezaliwa amekikuta Kiswahili kinatumiwa TZ nzima, ukija kwenye umoja wa Kitaifa, TZ ilikuwa moja kabla hata Nyerere hajazaliwa na ameikuta moja, tofauti tu TZ iliitwa majina tofauti vipindi mbali mbali lkn haijawahi kuwa na mtengano wala vita vya wenyewe kwa wenyewe kabla, sasa sielewi kwa nini umoja wa Taifa hili anapewa sifa yeye!

Binafsi kama kuna jambo Mlm.Nyerere alifanikiwa kama vile Wakoloni Waingereza ni brain washing, au kupumbaza watu kiakili, watu wamepumbazwa, na ndiyo maana hapa TZ hakuna anayeweza kumlaumu Mzungu kwa lolote, Mzungu anapendwa na kuabudiwa kama Mungu na haijalishi Mzungu atafanya nini atatetewa tu, Mzungu mmoja akivamiwa na majambazi hata Bunge litasimama na kuanza kujadilia kama hoja ya dharura, Mzungu hata akipiga Mwafrika risasi tutamteteta na kumlumu Mwafrika mwenzetu aliyepigwa risasi na Mzungu kwamba ni kosa lake, hiyo ndiyo maana ya brain washing ...
Ni kweli kabisa. Huwezi tenganisha CCM na Nyerere au Muungano wenye kero na Nyerere. Watu wanasahau kuwa Nyerere aliifanya nchi hii kuwa ya chama kimoja chenye hatamu ya kila kitu, hali ambayo JPM anataka irejee. Kuna umuhimu gani wa uongozi wa CCM kuendelea kutoa maelekezo kwa watendaji wa serikali wakati hii nchi si tena ya chama kimoja chenye hatamu juu ya serikali. Wajibu wa chama cha siasa ni kuandaa uongozi kuchukua nchi kwenye uchaguzi, baada ya uchaguzi ni wajibu wa uongozi wa serikali kutumikia wananchi kikatiba bila kuingiliwa na sera za chama cha siasa.
 
Huyu mwalimu au alikuwa na kitu ya kutaftia riziki ndo maana anapendwa?maana hata Leo hii mfano mfuga ka dog alafu kaite lile jina la mwalimu,ugomvi unaanza kwa majirani kabla haujafika kwa mwenyekiti wa mtama.lakn kale ka dog ukikaita majina mengne ya viongozi sawa.
 
hata matatizo makubwa ya hii nchi yalisababishwa na utawala wa mwalimu mfano vita ya Uganda,vita ukombozi msumbiji na Afrika kusini n.k..!!!lakini mwalimu hakuwa mnafiki alithubutu kusema wazi na alisimamia alichokisema hakutumia sana mabavu kutawala japo alikuwa mbabe lakini alitumia kipawa cha uongozi kuitawala Tanzania,alithubutu kupunguza mpaka mshahara wake ili kuwa saidia wananchi wake aliifahamu vyema dunia na mahitaji ya dunia kwa wakati huo.!!
 
Mwache Baba wa taifa apumzike kwa amani, Nyerere alikuwa na nia nzuri sana na nchi hii ila viongozi waliofuata ndo wametufikisha hapa kwa ulafi wao.
 
Huyu alikuwa wa ajabu.

Atakumbukwa milele na milele japokuwa alikuwa na mapungufu!!
 
Kweli Ccm inaelekea kufa. Sasa kujiponya mnamgeuzia kibao Nyerere matatizo yenu ya sasa?
Nyerere aliooanza kutawala alikuwa na wakati mgumu kujenga misingi, kusomesha wataalamu wake na kuonyesha njia.
Waliofuata ndio badala ya kuendekeza wao wakaiba na kuharibu kila kitu.
Wizi, uzembe,ufisadi, na madudu yote ya ccm ya sasa msiyahusishe na Mwl. Haya ni yenu wenyewe na ubazazi wenu.
 
Kweli Ccm inaelekea kufa. Sasa kujiponya mnamgeuzia kibao Nyerere matatizo yenu ya sasa?
Nyerere aliooanza kutawala alikuwa na wakati mgumu kujenga misingi, kusomesha wataalamu wake na kuonyesha njia.
Waliofuata ndio badala ya kuendekeza wao wakaiba na kuharibu kila kitu.
Wizi, uzembe,ufisadi, na madudu yote ya ccm ya sasa msiyahusishe na Mwl. Haya ni yenu wenyewe na ubazazi wenu.
Hayo hayo madudu wa CCM mkayapokea kwa mikono miwili. Akili zenu za upigaji zikafunika kabisa upeo wenu wa kuelewa mahitaji ya taifa tena kwenye mwaka wa uchaguzi.
Mkabadilishia gia angani wakati hakukuwa na umuhimu wa kufanya mlichofanya. Yule yule ambaye mwalimu JKN alisema hafai kupewa nchi, mkaona anawafaa na hapo ndipo mlipofulia vibaya mno.
Mwalimu JKN aliposema tuwakwepe kama ukoma wale wote wanaotumia kila wanachoweza kukitumia kwa ajili ya kwenda Ikulu alikuwa anaongea kinabii, ilikuwa mwaka 1995 lakini yeye alikuwa anauzungumzia uchaguzi wa 2015.
 
Ukiangalia kwa makini, watu duniani wanawapenda sana wanasiasa wenye swaga, na wanaojiamini sana. Hata km mwanasiasa huyo hafanyii watu maendeleo lakini anapendwa tu kwa swaga zake mfn Dr slaa anapendwa kwa swaga zake. Nyerere yeye aliitumia uaminifu wake km alivolelewa, swaga na elimu yake vizuri. Bahati nzuri kipindi hiko afrika ilikuwa na giza hivo alitumia mwanya huo vizuri. Waliomfahamu vizuri nyerere wanajitutumua tu kumpenda lakini hakuna anaempenda. Watu wa hali ya chini ndo waliompenda sana. Kuna wanasiasa hawawezi sana kuongea lakini ni wachapa kazi lakini hapendwi hata km anatimiza ahadi zote.
 
Hayo hayo madudu wa CCM mkayapokea kwa mikono miwili. Akili zenu za upigaji zikafunika kabisa upeo wenu wa kuelewa mahitaji ya taifa tena kwenye mwaka wa uchaguzi.
Mkabadilishia gia angani wakati hakukuwa na umuhimu wa kufanya mlichofanya. Yule yule ambaye mwalimu JKN alisema hafai kupewa nchi, mkaona anawafaa na hapo ndipo mlipofulia vibaya mno.
Mwalimu JKN aliposema tuwakwepe kama ukoma wale wote wanaotumia kila wanachoweza kukitumia kwa ajili ya kwenda Ikulu alikuwa anaongea kinabii, ilikuwa mwaka 1995 lakini yeye alikuwa anauzungumzia uchaguzi wa 2015.
Mmejazwa ujinga mpaka umekolea mioyoni mpaka kwenye bandama. Unaweza kuweka hapa huo ushihidi wa Mwl kutamka hamtaki fulani? Na mbona ccm yote ilikuwa inamtaka Lowassa isipokuwa JK tuu? Ushahidi ni nani aliyekuwa mpaka kaimbwa kwenye NEC (wakiwemo hao kina Majaliwa) kuwa wanaimani naye?
CCM ya Mwl haikuwa ya rushwa kama hii msimsingizie mzee wa watu.
Mada hii inazungumzia ccm na Nyerere, hayo ya chama kingine kumsimamisha mtu sio utetezi
 
Mmejazwa ujinga mpaka umekolea mioyoni mpaka kwenye bandama. Unaweza kuweka hapa huo ushihidi wa Mwl kutamka hamtaki fulani? Na mbona ccm yote ilikuwa inamtaka Lowassa isipokuwa JK tuu? Ushahidi ni nani aliyekuwa mpaka kaimbwa kwenye NEC (wakiwemo hao kina Majaliwa) kuwa wanaimani naye?
CCM ya Mwl haikuwa ya rushwa kama hii msimsingizie mzee wa watu.
Mada hii inazungumzia ccm na Nyerere, hayo ya chama kingine kumsimamisha mtu sio utetezi
CCM ilimtaka mgombea huyo baada ya miaka mingi ya yeye kutengeneza network ambayo JPM anaivunjilia mbali bila huruma kwa sasa.

CCM ya JKN haikuwa na rushwa lakini hiyo haitunyimi uhalali wa kuongelea juhudi zake katika kukiokoa chama tangu akiwa hai, dhidi ya watu waliokuwa kinyume na jinsi alivyokilea chama.

Watu ambao walifikia hatua ya kumkosea heshima kwa kumwambia eti aende sehemu ile ile aliyomchafua mwanasiasa mmoja ili akamsafishe kisiasa.

Huwezi kumzungumzia Nyerere na CCM aliyoihangaikia bila ya kuzizungumzia juhudi zake katika kukitetea chama dhidi ya upigaji na wapigaji.
 
Sijawahi kuelewa mpaka leo hii ni kwa nini Kiongozi wa kwanza wa Taifa hili Mlm.Nyerere anapendwa sana hapa kwetu, wkt kiukweli Nyerere anapaswa achukiwe sana siajabu klk Viongozi wote waliopita kama tulikuwa tunatafuta sababu ya kuchukuia Viongozi wetu kama baadhi yetu tufanyavyo leo hii, Nyerere alifanya social experiment Tanzania!

Kwa wasiofahamu maana ya social experiment ni kama vile kutengeneza dawa mpya ambayo hauna uhakika nayo kama inafaa kutumiwa na binadamu hivyo unaamua kuijaribu kwa baadhi ya binadamu na ukiona inafaa basi unaitumia ukiona haifai unaitupa!
Na hicho ndicho Mlm.Nyerere na utawala wake ulichofanya Tanzania, lkn cha ajabu Mtanzania kwa Mlm.Nyerere humwambii kitu ni kama vile unamuongelea Mungu!

Na cha ajabu zaidi labda kuliko vyote kuna watu wanaoichukia CCM kuliko kitu chochote Dunia hii lkn wanampenda Mlm.Nyerere na kumuondoa kwenye lawama zote wanazoipa CCM, tena wanakwenda mbali na kumuita kwamba alikuwa Mwana demokrasia, kwamba Utawala wake ulikuwa wa kidemokrasia, hivyo nashindwa kuelewa mtu anawezaje kuitenganisha CCM na Mlm.Nyerere? Unawezaje kutenganisha Umaskini na kudumaa kwa uchumi wa Tanzania na Mlm.Nyerere? Unawezaje kumlaumu, Mwinyi, Kikwete, au Mkapa na kumuacha Mlm.Nyerere?

Watu wanaongelea kila siku matatizo ya Zanziba na Muungano wetu lkn Mlm.Nyerere wanamtoa kwenye equation na kulaumu wengine, hili linawezekana vipi?
Watu wanalalamikia khs Elimu ya Tanzania kuwa Duni na wanalaumu Maraisi wote lkn Mlm.Nyerere wanamtoa kwenye lawama, hili linawezekana vipi wkt Mlm.Nyerere ameongoza TZ kwa miaka 24 na ndani ya hiyo miaka kwa mfano hapa Dar hakujenga Shule hata moja ukiacha zile alizotaifisha ktk Taasisi za kidini, watu wengi wamesoma Shule kwa shifti wiki hii asubuhi ijayo mchana, tena Wanafunzi walikuwa wanakaa chini hakuna madawati, lkn lawama wanapewa maraisi waliofuata, kwa nini?

Binafsi mpaka leo sielewi ni kwa nini Mlm.Nyerere hata anapendwa hapa Tanzania, hata nikianza kungalia sifa zote anazopewa na ukianza kuichambua moja baada ya nyingine utakuta wala siyo yeye anayestahili hiyo sifa!
Tukianza na Kiswahili, wengi wanafikiri TZ tunaongea Kiswahili shauri ya Nyerere, siyo kweli, Nyerere amezaliwa amekikuta Kiswahili kinatumiwa TZ nzima, ukija kwenye umoja wa Kitaifa, TZ ilikuwa moja kabla hata Nyerere hajazaliwa na ameikuta moja, tofauti tu TZ iliitwa majina tofauti vipindi mbali mbali lkn haijawahi kuwa na mtengano wala vita vya wenyewe kwa wenyewe kabla, sasa sielewi kwa nini umoja wa Taifa hili anapewa sifa yeye!

Binafsi kama kuna jambo Mlm.Nyerere alifanikiwa kama vile Wakoloni Waingereza ni brain washing, au kupumbaza watu kiakili, watu wamepumbazwa, na ndiyo maana hapa TZ hakuna anayeweza kumlaumu Mzungu kwa lolote, Mzungu anapendwa na kuabudiwa kama Mungu na haijalishi Mzungu atafanya nini atatetewa tu, Mzungu mmoja akivamiwa na majambazi hata Bunge litasimama na kuanza kujadilia kama hoja ya dharura, Mzungu hata akipiga Mwafrika risasi tutamteteta na kumlumu Mwafrika mwenzetu aliyepigwa risasi na Mzungu kwamba ni kosa lake, hiyo ndiyo maana ya brain washing ...
How old are you? Let me know then i will respond to your verbal tirade against Nyerere.
 
Hao wengi umetumia vipimo gani kuwatambua? binafsi simkubali / kumsujudu huyo Nyerere .
 
Hivi watanzania tutamlaumu Nyerere mpaka lini? Wamepita marais wangapi hapa kwa nini wasirekebishe makosa ya mwalimu JKN? Je sisi watanzania tumejipangaje kurekebisha makosa. Utakuta kuna watu hapa kila siku kusifia Bwana Yule pamoja na ubabe anaoonesha. Kama tunataka mabadiliko kitu gani kinatushinda? Tunachagua hovyo hovyo, tukiongozwa hovyo hovyo tusilalamike hovyo hovyo.
 
Nadhani ungewaweka na viongozi wengine wa zama za nyerere tuone walichofanyia nchi ili kuzipa uhalali hoja zako au utwambie ww umeleta athari gani chanya kwa taifa! Vinginevyo jkn alikosea lkn makosa yake hayafiki hayafiki hata robo yako!
 
Back
Top Bottom