Kwanini Mwl. Nyerere alipigiwa kura licha ya kuwa mgombea pekee lakini leo mgombea akibaki pekee anatangazwa kapita bila kupingwa?

Lord OSAGYEFO

JF-Expert Member
Feb 19, 2021
3,086
4,881
Wadau nawakumbusha tu wakati wa Awamu ya 1

Hayati baba wa taifa Mwl. Nyerere licha ya kuwa ni mgombea pekee hakuwa na mpinzani hakuwahi kutangazwa kuwa kapita bila kupingwa badala yake wananchi walimpigia kura na kuhesabiwa kisha matokeo kutangazwa.

Lakini leo tume ya uchaguzi mgombea akibaki pekee yake badala ya wananchi kumpigiwa kura Tume ya Uchaguzi inatangaza kuwa mgombea amepita bila kupingwa kitu ambacho sio sahihi kwani wapiga kura hawajapewa haki yao ya kikatiba ya kuchagua hakika ni utaratibu mbovu sana.

Mgombea akibaki pekee yake apigiwe kura ndio ziamue asitangazwe kuwa kapita bila kupingwa
20211024_122213.jpg
 
Labda sheria zinatofautiana. Ukizingatia sheria (katiba) siyo msahafu inafanyiwa amendments kila wakati
 
Yesu anapingwa Muhammad anapingwa Ila ccm mgombea wake hapingwi halafu hamtaki kubadili katiba.
 
Katiba ndio inasema hivyo mkuu
Ukituonesha hiyo ibara kwenye hii katiba utakuwa umetusaidia wengi ktk kujua hili jambo na tuweze juwa kuwa lini lilibadirishwa kutoka kuwa kupigiwa kura kwa mgombea mmoja enzi za JKN na mpaka kugeuzwa kuwa kupita bila kupingwa
 
Back
Top Bottom