Kwanini mwaka 2015 Dr. Slaa aliwatukana CCM wenyewe wakashangilia?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
17,871
33,236
Wakati akitoka CHADEMA na kuuungana na CCM dhidi ya UKAWA, Dr. Wilbrod Slaa alisema maneno haya yaliyokuja kushabikiwa sana na wana CCM.
Ukitoa kinyesi chooni na kukipeleka Chumbani maana yake hata chumba chako ni CHOO na kitakuwa kinanuka zaidi kuliko choo cha kawaida. Dr. Wilbrod Slaa
Dr. Slaa alikifananisha kitendo cha CHADEMA kumpokea Edward Lowassa toka CCM kama sawa na kutoa kinyesi chooni na kukiweka chumbani. Kwa mfano wake huo, hapo alimaanisha kuwa Kinyesi alikuwa ni Lowassa na choo ni CCM.

Ukifikiria kwa makini utaona ni rahisi kukisafisha chumba kilichowekwa kinyesi na kuwa kisafi tena, kuliko kukibadilisha choo kuwa chumba cha kawaida. Kwa nini CCM waliona sawa tu chama chao wakati ule kufananishwa na choo?

Choo ni sehemu kunakotupwa kinyesi na ili kiwe choo ni lazima kila mara kinyesi kipya kiingie. Lakini kinyesi hakigeuki kuwa kipya baada ya kutolewa chooni, badala yake hukauka, harufu mbaya hupotea na hatimaye huweza kutumiwa kama mbolea

Ni kwa nini Dr. Slaa wakati ule aliiona CCM kama ni choo na CHADEMA kama ni chumba safi kilichochafuliwa na kinyesi kilichotoka kwenye choo? Slaa aliamini kwamba Lowassa ni "fisadi" aliyelelewa na chama chenye mfumo wa kifisadi. Lakini ni kwa nini CCM walizifurahia kauli hizo za Slaa?

Slaa alisema kuwa CCM "imejaa" watu waoga, CCM hawana ujasiri na wana CCM walishangilia sana. Leo CCM wakiitwa waoga kwa nini wanakuwa mbogo? Kwenye kila ufisadi wanatajwa watu wa CCM lakini kwa kuwa chama chenyewe kimejaa watu waoga hawana ujasiri wa kuchukua hatua dhidi ya mafisadi hao.

Leo nikiangalia miaka miwili nyuma najiuliza ni kwa nini CCM wakati ule waliona sawa tu chama chao kufananishwa na choo leo washangae wahalifu wa ufisadi wanaotajwa kwenye kila tume inayoundwa na wao wenyewe, kutoka kwenye chama chao!?

Ni kwa nini CCM walishangilia Dr.Slaa kukifananisha chama chao na choo?
 
Wakati akitoka CHADEMA na kuuungana na CCM dhidi ya UKAWA, Dr. Wilbrod Slaa alisema maneno haya yaliyokuja kushabikiwa sana na wana CCM.
Dr. Slaa alikifananisha kitendo cha CHADEMA kumpokea Edward Lowassa toka CCM kama sawa na kutoa kinyesi chooni na kukiweka chumbani. Kwa mfano wake huo, hapo alimaanisha kuwa Kinyesi alikuwa ni Lowassa na choo ni CCM.

Ukifikiria kwa makini utaona ni rahisi kukisafisha chumba kilichowekwa kinyesi na kuwa kisafi tena, kuliko kukibadilisha choo kuwa chumba cha kawaida. Kwa nini CCM waliona sawa tu chama chao wakati ule kufananishwa na choo?

Choo ni sehemu kunakotupwa kinyesi na ili kiwe choo ni lazima kila mara kinyesi kipya kiingie. Lakini kinyesi hakigeuki kuwa kipya baada ya kutolewa chooni, badala yake hukauka, harufu mbaya hupotea na hatimaye huweza kutumiwa kama mbolea

Ni kwa nini Dr. Slaa wakati ule aliiona CCM kama ni choo na CHADEMA kama ni chumba safi kilichochafuliwa na kinyesi kilichotoka kwenye choo? Slaa aliamini kwamba Lowassa ni "fisadi" aliyelelewa na chama chenye mfumo wa kifisadi. Lakini ni kwa nini CCM walizifurahia kauli hizo za Slaa?

Slaa alisema kuwa CCM "imejaa" watu waoga, CCM hawana ujasiri na wana CCM walishangilia sana. Leo CCM wakiitwa waoga kwa nini wanakuwa mbogo? Kwenye kila ufisadi wanatajwa watu wa CCM lakini kwa kuwa chama chenyewe kimejaa watu waoga hawana ujasiri wa kuchukua hatua dhidi ya mafisadi hao.

Leo nikiangalia miaka miwili nyuma najiuliza ni kwa nini CCM wakati ule waliona sawa tu chama chao kufananishwa na choo leo washangae wahalifu wa ufisadi wanaotajwa kwenye kila tume inayoundwa na wao wenyewe, kutoka kwenye chama chao!?

Ni kwa nini CCM walishangilia Dr.Slaa kukifananisha chama chao na choo?
Niwe wa kwanza kureply....hata mimi sjui kwanini walifurahia kufananishwa na choo
 
Leo nimeelewa ni kwa nini walikaa kimya. Kila wakati kipya huja na hiyo ndiyo kazi ya choo!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom