Kwanini Mungu hakurekebisha kilichosababisha shetani akaasi kabla ya kumuumba binadamu?

Huyu ni muhuni mvuta bangi kwa muonekano tu wamaandishi unaweza kujua tabia yake cjui kama anawajal hata wazazi wake
Kujali wazazi hili nalo unahitaji ufundishwe kweli !! halafu umejuaje mimi mvuta bangi ? kijana jikite kwenye mambo ya msingi
 
Huyu mpagani yupo kwa kubishan wala c kujifunza sasa ni sawa unapoteza muda tu mtu ukimwambia yule aliekua juu kunguru yeye akiamua kusema yule mbuzi hata umwabiaje hatoelewa ndo kashaamua kusema mbuzi sasa hapo ni sawa na kubishana sio kujadiliana
Najua huna uwezo wa kujibu maswali yale.

Ulipoambiwa Mola ameumba dhambi kama unatumia akili vizuri hukupaswa tena kuuliza au kutaka kujua chanzo cha dhambi,haoa umefanya matumizi mabaya ya akili.

Kuwepo kwa dhambi ni jambo moja nakuitenda dhambi ni jambo lingine. Kwa maana hiyo ndio maana ule mfano wa Morogoro uliukimbia.
 
Huyu mpagani yupo kwa kubishan wala c kujifunza sasa ni sawa unapoteza muda tu mtu ukimwambia yule aliekua juu kunguru yeye akiamua kusema yule mbuzi hata umwabiaje hatoelewa ndo kashaamua kusema mbuzi sasa hapo ni sawa na kubishana sio kujadiliana
Mbona unalialia humu kama hauna cha kuandika kaa pembeni upate elimu mbadala
 
1. Hoja yako ya maombi ni dhaifu sana , kwasababu kabla ujafikiria kuomba huyo Mungu wako alishajua , yaani unapita mule mule kwenye mipango yake, tena kama kukubali au kukataa maombi pia alishajua kitambo , unachofanya ww ni kujitekenya na kucheka mwenyewe
Naona unaendelea kuonyesha ufinyu wako wa kufikiri.
.Mungu anajua kila kitu mpaka namna gani hizo nyenzo zinatumika sasa wewe unaona nyenzo ni jambo kubwa , wakati majibu na matumizi ya nyenzo zile Mungu wako anajua ata kabla ujazitumia huyu vip ahahahhahaahaahaa
Ndio maana nikasema hivi kujua kwake hayo hakukuzuii weww kutenda mambo yako,ndio maana unatenda unavyotaka na unatumia akili na unatumia hisia.

Naona maswali yangu unayakwepa. Unapo ambiwa jambo fulani baya usilifanye ltakudhuru wewe ukalifanya,hapo unakuwa umefanyiwa au umefanya kwa mapenzi yako au umeshinikizwa ?

Nakupa teba mfano mwingine sababu unakwepa maswali yangu. Mfano una mtoto na unamjua kabisa huyu mtoto tabia yake,mfano ukimpa hela huwa anaenda kufanya nini,ukampa hela kisha akafanya kile unachokijua,hapo utasemaje ? Yaani ukasema hivi "Fulani nikimpa hela tu huwa najua lazima atanunua pipi tu". Je hapa huyu mtoto anakuwa amelazimishwa au ametumia uhuru wake na hali ya kuwa hilo weww unalijua ? Ndio maana narudi kule kule ya kuwa kujua kwake wewe hakukuzuii kufanya jambo.

Naendelea ......
 
Huyu mpagani yupo kwa kubishan wala c kujifunza sasa ni sawa unapoteza muda tu mtu ukimwambia yule aliekua juu kunguru yeye akiamua kusema yule mbuzi hata umwabiaje hatoelewa ndo kashaamua kusema mbuzi sasa hapo ni sawa na kubishana sio kujadiliana
Uko sahihi kabisa hawa huwa hawaumizi kichwa na ni hodari wa kukuwepa maswali.

Yaani wanabisha tu.
 
Ok wanatheolojia wanasema.

Baada ya shetan kuovu.. Hakutupwa siku iyoiyo.

Bali alipewa nafasi kadhaaa wa kadhaa kujisahihisha.

Shetan mpaka akawa anafuatwa na washaur wakimsihi kabisaa atubu wapiiiiiiiu.

Shetan akaachiwa siku kadhaa ajitathimin nakutubu wapiiiu




Njia pekee ikawa ni kumtoa eneo la watakatifu.


Unajua Mungu ni Mfalme, wa haki na huruma nareehema.

Kwa namana ulivyoandika tu inadhihirisha kuwa ni mafundisho ya viongozi wa dini tena kwa watoto ya kulazimisha shetani aonekane ana hatia

Si unajua vitoto vya siku hizi vinajiongeza kwaiyo lazima wavipange mapema
 
Naona unaendelea kuonyesha ufinyu wako wa kufikiri.

Ndio maana nikasema hivi kujua kwake hayo hakukuzuii weww kutenda mambo yako,ndio maana unatenda unavyotaka na unatumia akili na unatumia hisia.

Naona maswali yangu unayakwepa. Unapo ambiwa jambo fulani baya usilifanye ltakudhuru wewe ukalifanya,hapo unakuwa umefanyiwa au umefanya kwa mapenzi yako au umeshinikizwa ?

Nakupa teba mfano mwingine sababu unakwepa maswali yangu. Mfano una mtoto na unamjua kabisa huyu mtoto tabia yake,mfano ukimpa hela huwa anaenda kufanya nini,ukampa hela kisha akafanya kile unachokijua,hapo utasemaje ? Yaani ukasema hivi "Fulani nikimpa hela tu huwa najua lazima atanunua pipi tu". Je hapa huyu mtoto anakuwa amelazimishwa au ametumia uhuru wake na hali ya kuwa hilo weww unalijua ? Ndio maana narudi kule kule ya kuwa kujua kwake wewe hakukuzuii kufanya jambo.

Naendelea ......
Mifano unayotoa inachekesha sana mimi kama baba naweza kujua jambo lakini lisitokee( hakuna ajabu ), tofauti na Mungu wako analolijua ndio linalotokea , bahati nzuri anayajua mambo kabla ata ayajafanyika na ata yakifanyika yatatoa majibu sawa na kile alichokuwa anajua kuwa kitafanyika. huu ndio uhuru wa bendera wewe endelea kurukaruka tu
 
Uko sahihi kabisa hawa huwa hawaumizi kichwa na ni hodari wa kukuwepa maswali.

Yaani wanabisha tu.
Acheni kujifariji vijana ,hakuna jambo wewe Zuri utalifanya Mungu wako akulijua kabla , yote anayajua kabla ayajatokea na baada ya kutokea , wewe ni bendera fuata upepo
 
Acheni kujifariji vijana ,hakuna jambo wewe Zuri utalifanya Mungu wako akulijua kabla , yote anayajua kabla ayajatokea na baada ya kutokea , wewe ni bendera fuata upepo
Hili liko wazi na hakuna aliye kataa na kujua kwake hakunizuii mimi nisifanye ninacho taka na hili mpaka kwako na mfano wako.
 
Hili liko wazi na hakuna aliye kataa na kujua kwake hakunizuii mimi nisifanye ninacho taka na hili mpaka kwako na mfano wako.
Unachokifanya kilishajulikana na Mungu wako kabla ujakifanya , na bahati nzuri huwezi kubadilisha , hii ndio maana ya kujitekenya na kucheka mwenyewe
 
Mifano unayotoa inachekesha sana mimi kama baba naweza kujua jambo lakini lisitokee( hakuna ajabu ),
Safi kabisa na hapa ndipo unapo ona ukamilifu wa Mola kwamba yeye hakosei,na vipi likatokea hilo jambo utasemaje ? Kwamba ulimlazimisha au utasema huo ni uhuru wa bendera kama unavyouita ?
tofauti na Mungu wako analolijua ndio linalotokea ,
Ndio maana nasema ya kuwa kujua kwake kwako hakukuzuii wewe kutofanya unalotaka,huelewi wapi ?

Ungekuwa unajibu maswali yangu lazima ungeona ujinga wako uko wapi.

Tuendelee ...
 
Back
Top Bottom