Kurunzi
JF-Expert Member
- Jul 31, 2009
- 9,277
- 9,912
Ukweli ni kwamba Mukoko ni mchezaji mgumu na anayejituma zaidi uwanjani. Tatizo ni kwamba umiliki wake wa mpira hauko vizuri. Mguso wake wa kwanza wa mpira sio mzuri kulinganisha na Aucho na Bangala. Mbaya zaidi ni kwamba Mauya ni mzuri zaidi katika umiliki wa mpira kuliko Mukoko. Tatizo la Mauya ni kwamba labda hajitumi sana uwanjani.
Kama ambavyo Mukoko na Mauya waliingia moja kwa moja katika kikosi cha kutokana na aina ya wachezaji waliowakuta basi ndivyo ambavyo Aucho na Bangala wameingia moja kwa moja katika kikosi cha kwanza kutokana na aina ya wachezaji waliowakuta.
Mauya amekuwa akicheza kutokana na kuwa mbele ya Mukoko kwa utulivu kwa mpira mguuni. Naambiwa kwamba kocha Nasreddine Nabi anamkubali zaidi. Hata hivyo bahati yake ya kuchezwa imechangiwa pia na uwezo wa Bangala kucheza nafasi nyingi tofauti, lakini pia majeraha ambayo yamekuwa yakiisumbua safu ya ulinzi ya Yanga.
Anapoumia beki yeyote wa kati wa Yanga, Bangala anarudi kucheza nyuma na kuwapisha Mauya na Aucho wacheze eneo la kiungo. Walipokosekana mabeki wote wa kulia wa Yanga, Djuma Shaban na Shomari Kibwana, basi Dickson Job amesogea kulia na Bangala amerudi kuwa mlinzi wa kati akicheza na Mwamunyeto.
Hata hivyo bado nafasi inakwenda kwa Mauya kucheza sambamba na Aucho. Na ni kweli kwamba Mauya ameitendea haki nafasi hiyo kwa kiasi kikubwa. Hii ina maana kwamba kwa sasa Mukoko anaangukia kuwa chaguo la nne katika orodha ya viungo wa chini achilia mbali Fei Toto anayejitanua peke yake pale mbele.
Tatizo kubwa zaidi kwa Mukoko limekuja baada ya Yanga kuamua kuongeza fundi mwingine katika eneo la kiungo. Salum Abubakar ‘Sure’ Boy ambaye naye ana utulivu mkubwa wa mpira mguuni kuliko Mukoko. Na hii inamaanisha kwamba Mukoko anakuwa chaguo la tano katika eneo la kiungo.
Haishangazi kuona watu wa Yanga wala hawashtuki kuona mkataba wa Mukoko umebakiza miezi mitano Yanga na hakuna anayejali. Umewahi kusikia mitandaoni watu wa Yanga wakiwa na hofu kwamba huenda Mukoko akaondoka klabuni kwao?
Umewahi kusoma mahala mashabiki wakisisitiza kwamba lazima waendelee kuwa na Mukoko? Umewahi kuona watu wa Yanga wakiwa na hofu kwamba huenda Mukoko ataenda Simba? wakati ule walikuwa na hofu wakati Simba walipoanzisha uvumi mitandaoni kwamba wanataka kuinasa saini yake.
Kumbe wakati ule ulikuwa wakati ule. Leo Yanga watakuw ana hofu zaidi ukiwaambia Simba wanamnyemelea Bangala au Aucho. Huu ndio ukweli. Hizi ndio alama za nyakati ambazo Mukoko analazimika kuzikubali. Kila kitabu na zama zake.
Naamini mwisho wa msimu huu Mukoko hatakuwa mchezaji wa Yanga. Lakini naamini pia kwamba endapo akisaini Simba au Azam bado mashabiki wa Yanga hawataulaumu uongozi wao ingawa ni kweli kwamba wanampenda mchezaji huyu. Ni kipenzi chao kikubwa.
Tatizo ni alama za nyakati. Sasa hivi Yanga inatembea yenyewe. Wachezaji upoteza umuhimu kikosini pindi wanapokuja wachezaji wengine muhimu zaidi. zipo nyakati ambazo Simba walikuwa wanamuona Shiza Kichuya kama staa mkubwa, lakini alipokuja Luis Miquissone wakajikuta wakitembea zaidi na kuachana na kina Kichuya.
Wakati mwingine huwa inatokea lakini kitu muhimu zaidi ni kuangalia maslahi ya timu. Ipo siku ambayo hata Aucho mwenyewe atapoteza umuhimu pindi atakapokuja mchezaji mkali zaidi yake. Labda kama hatakuja mkali zaidi yake ndipo ambapo ataendelea kuimbwa.
Karibu kwa Maoni
Kama ambavyo Mukoko na Mauya waliingia moja kwa moja katika kikosi cha kutokana na aina ya wachezaji waliowakuta basi ndivyo ambavyo Aucho na Bangala wameingia moja kwa moja katika kikosi cha kwanza kutokana na aina ya wachezaji waliowakuta.
Mauya amekuwa akicheza kutokana na kuwa mbele ya Mukoko kwa utulivu kwa mpira mguuni. Naambiwa kwamba kocha Nasreddine Nabi anamkubali zaidi. Hata hivyo bahati yake ya kuchezwa imechangiwa pia na uwezo wa Bangala kucheza nafasi nyingi tofauti, lakini pia majeraha ambayo yamekuwa yakiisumbua safu ya ulinzi ya Yanga.
Anapoumia beki yeyote wa kati wa Yanga, Bangala anarudi kucheza nyuma na kuwapisha Mauya na Aucho wacheze eneo la kiungo. Walipokosekana mabeki wote wa kulia wa Yanga, Djuma Shaban na Shomari Kibwana, basi Dickson Job amesogea kulia na Bangala amerudi kuwa mlinzi wa kati akicheza na Mwamunyeto.
Hata hivyo bado nafasi inakwenda kwa Mauya kucheza sambamba na Aucho. Na ni kweli kwamba Mauya ameitendea haki nafasi hiyo kwa kiasi kikubwa. Hii ina maana kwamba kwa sasa Mukoko anaangukia kuwa chaguo la nne katika orodha ya viungo wa chini achilia mbali Fei Toto anayejitanua peke yake pale mbele.
Tatizo kubwa zaidi kwa Mukoko limekuja baada ya Yanga kuamua kuongeza fundi mwingine katika eneo la kiungo. Salum Abubakar ‘Sure’ Boy ambaye naye ana utulivu mkubwa wa mpira mguuni kuliko Mukoko. Na hii inamaanisha kwamba Mukoko anakuwa chaguo la tano katika eneo la kiungo.
Haishangazi kuona watu wa Yanga wala hawashtuki kuona mkataba wa Mukoko umebakiza miezi mitano Yanga na hakuna anayejali. Umewahi kusikia mitandaoni watu wa Yanga wakiwa na hofu kwamba huenda Mukoko akaondoka klabuni kwao?
Umewahi kusoma mahala mashabiki wakisisitiza kwamba lazima waendelee kuwa na Mukoko? Umewahi kuona watu wa Yanga wakiwa na hofu kwamba huenda Mukoko ataenda Simba? wakati ule walikuwa na hofu wakati Simba walipoanzisha uvumi mitandaoni kwamba wanataka kuinasa saini yake.
Kumbe wakati ule ulikuwa wakati ule. Leo Yanga watakuw ana hofu zaidi ukiwaambia Simba wanamnyemelea Bangala au Aucho. Huu ndio ukweli. Hizi ndio alama za nyakati ambazo Mukoko analazimika kuzikubali. Kila kitabu na zama zake.
Naamini mwisho wa msimu huu Mukoko hatakuwa mchezaji wa Yanga. Lakini naamini pia kwamba endapo akisaini Simba au Azam bado mashabiki wa Yanga hawataulaumu uongozi wao ingawa ni kweli kwamba wanampenda mchezaji huyu. Ni kipenzi chao kikubwa.
Tatizo ni alama za nyakati. Sasa hivi Yanga inatembea yenyewe. Wachezaji upoteza umuhimu kikosini pindi wanapokuja wachezaji wengine muhimu zaidi. zipo nyakati ambazo Simba walikuwa wanamuona Shiza Kichuya kama staa mkubwa, lakini alipokuja Luis Miquissone wakajikuta wakitembea zaidi na kuachana na kina Kichuya.
Wakati mwingine huwa inatokea lakini kitu muhimu zaidi ni kuangalia maslahi ya timu. Ipo siku ambayo hata Aucho mwenyewe atapoteza umuhimu pindi atakapokuja mchezaji mkali zaidi yake. Labda kama hatakuja mkali zaidi yake ndipo ambapo ataendelea kuimbwa.
Karibu kwa Maoni