Kwanini Mukoko amendoka Young African, wakati bado aiipambania timu kwa hali na mali, huku mashabiki bado tunampenda?

Kurunzi

JF-Expert Member
Jul 31, 2009
9,277
9,912
Ukweli ni kwamba Mukoko ni mchezaji mgumu na anayejituma zaidi uwanjani. Tatizo ni kwamba umiliki wake wa mpira hauko vizuri. Mguso wake wa kwanza wa mpira sio mzuri kulinganisha na Aucho na Bangala. Mbaya zaidi ni kwamba Mauya ni mzuri zaidi katika umiliki wa mpira kuliko Mukoko. Tatizo la Mauya ni kwamba labda hajitumi sana uwanjani.

Kama ambavyo Mukoko na Mauya waliingia moja kwa moja katika kikosi cha kutokana na aina ya wachezaji waliowakuta basi ndivyo ambavyo Aucho na Bangala wameingia moja kwa moja katika kikosi cha kwanza kutokana na aina ya wachezaji waliowakuta.

Mauya amekuwa akicheza kutokana na kuwa mbele ya Mukoko kwa utulivu kwa mpira mguuni. Naambiwa kwamba kocha Nasreddine Nabi anamkubali zaidi. Hata hivyo bahati yake ya kuchezwa imechangiwa pia na uwezo wa Bangala kucheza nafasi nyingi tofauti, lakini pia majeraha ambayo yamekuwa yakiisumbua safu ya ulinzi ya Yanga.

Anapoumia beki yeyote wa kati wa Yanga, Bangala anarudi kucheza nyuma na kuwapisha Mauya na Aucho wacheze eneo la kiungo. Walipokosekana mabeki wote wa kulia wa Yanga, Djuma Shaban na Shomari Kibwana, basi Dickson Job amesogea kulia na Bangala amerudi kuwa mlinzi wa kati akicheza na Mwamunyeto.

Hata hivyo bado nafasi inakwenda kwa Mauya kucheza sambamba na Aucho. Na ni kweli kwamba Mauya ameitendea haki nafasi hiyo kwa kiasi kikubwa. Hii ina maana kwamba kwa sasa Mukoko anaangukia kuwa chaguo la nne katika orodha ya viungo wa chini achilia mbali Fei Toto anayejitanua peke yake pale mbele.

Tatizo kubwa zaidi kwa Mukoko limekuja baada ya Yanga kuamua kuongeza fundi mwingine katika eneo la kiungo. Salum Abubakar ‘Sure’ Boy ambaye naye ana utulivu mkubwa wa mpira mguuni kuliko Mukoko. Na hii inamaanisha kwamba Mukoko anakuwa chaguo la tano katika eneo la kiungo.

Haishangazi kuona watu wa Yanga wala hawashtuki kuona mkataba wa Mukoko umebakiza miezi mitano Yanga na hakuna anayejali. Umewahi kusikia mitandaoni watu wa Yanga wakiwa na hofu kwamba huenda Mukoko akaondoka klabuni kwao?

Umewahi kusoma mahala mashabiki wakisisitiza kwamba lazima waendelee kuwa na Mukoko? Umewahi kuona watu wa Yanga wakiwa na hofu kwamba huenda Mukoko ataenda Simba? wakati ule walikuwa na hofu wakati Simba walipoanzisha uvumi mitandaoni kwamba wanataka kuinasa saini yake.

Kumbe wakati ule ulikuwa wakati ule. Leo Yanga watakuw ana hofu zaidi ukiwaambia Simba wanamnyemelea Bangala au Aucho. Huu ndio ukweli. Hizi ndio alama za nyakati ambazo Mukoko analazimika kuzikubali. Kila kitabu na zama zake.

Naamini mwisho wa msimu huu Mukoko hatakuwa mchezaji wa Yanga. Lakini naamini pia kwamba endapo akisaini Simba au Azam bado mashabiki wa Yanga hawataulaumu uongozi wao ingawa ni kweli kwamba wanampenda mchezaji huyu. Ni kipenzi chao kikubwa.

Tatizo ni alama za nyakati. Sasa hivi Yanga inatembea yenyewe. Wachezaji upoteza umuhimu kikosini pindi wanapokuja wachezaji wengine muhimu zaidi. zipo nyakati ambazo Simba walikuwa wanamuona Shiza Kichuya kama staa mkubwa, lakini alipokuja Luis Miquissone wakajikuta wakitembea zaidi na kuachana na kina Kichuya.

Wakati mwingine huwa inatokea lakini kitu muhimu zaidi ni kuangalia maslahi ya timu. Ipo siku ambayo hata Aucho mwenyewe atapoteza umuhimu pindi atakapokuja mchezaji mkali zaidi yake. Labda kama hatakuja mkali zaidi yake ndipo ambapo ataendelea kuimbwa.

Karibu kwa Maoni
 
Maoni yangu ni kuwa ndugu mwandishi unapocopy habari kutoka chanzo kingine ni vyema kuwapa credit au kuwa acknowledge wahusika pia inasaidia👇👇



Kuhusu Mukoko kwenda TP MAZEMBE muache aende kwa kuwa ameona GREEN PASTURES zaidi na Yanga ilikuwepo kabla ya Mukoko, ipo wakati yeye akiwepo na hata akiondoka Yanga yetu itabakia vile vile ....cha msingi ni kumtakia kila la heri huko aendako ijapokuwa haitaondoa ukweli kuwa aliwahi kuwa moja kati ya wachezaji bora kuwahi kutokea kwa Yanga💪
 
Sawa ni kweli.

Lakini mukoko ni mchezaji anayekupa matokeo ya unachotafuta muda wowote ule yuko tayari kupambana alitusaidia Sana tulipokuwa wabovu.

Leo tumewapata kina aucho ambaye Lila Mwezi anaomba likizo kwenda kwao.

Hatukatai aucho ni mzuri Sana lakini ni heri pia kuwaacha wachezaji wanaoipenda team na wenye moyo muda wote.

Zawadi haaminiki leo atacheza kesho anaamka vibaya back pass kama zote.
 
Tafadhali ndugu mchambuzi; Yaani siku Simba wakisema wanamchukua Fiston MAYELE au Feisal mashabiki wa Yanga tutapata kifafa.

Btw mukoko wetu anatuuma tunampenda sana ila ila la kheir Jangwani ni nyumbani anakaribishwa anytime.
 
Ukweli ni kwamba Mukoko ni mchezaji mgumu na anayejituma zaidi uwanjani. Tatizo ni kwamba umiliki wake wa mpira hauko vizuri. Mguso wake wa kwanza wa mpira sio mzuri kulinganisha na Aucho na Bangala. Mbaya zaidi ni kwamba Mauya ni mzuri zaidi katika umiliki wa mpira kuliko Mukoko. Tatizo la Mauya ni kwamba labda hajitumi sana uwanjani.

Kama ambavyo Mukoko na Mauya waliingia moja kwa moja katika kikosi cha kutokana na aina ya wachezaji waliowakuta basi ndivyo ambavyo Aucho na Bangala wameingia moja kwa moja katika kikosi cha kwanza kutokana na aina ya wachezaji waliowakuta.

Mauya amekuwa akicheza kutokana na kuwa mbele ya Mukoko kwa utulivu kwa mpira mguuni. Naambiwa kwamba kocha Nasreddine Nabi anamkubali zaidi. Hata hivyo bahati yake ya kuchezwa imechangiwa pia na uwezo wa Bangala kucheza nafasi nyingi tofauti, lakini pia majeraha ambayo yamekuwa yakiisumbua safu ya ulinzi ya Yanga.

Anapoumia beki yeyote wa kati wa Yanga, Bangala anarudi kucheza nyuma na kuwapisha Mauya na Aucho wacheze eneo la kiungo. Walipokosekana mabeki wote wa kulia wa Yanga, Djuma Shaban na Shomari Kibwana, basi Dickson Job amesogea kulia na Bangala amerudi kuwa mlinzi wa kati akicheza na Mwamunyeto.

Hata hivyo bado nafasi inakwenda kwa Mauya kucheza sambamba na Aucho. Na ni kweli kwamba Mauya ameitendea haki nafasi hiyo kwa kiasi kikubwa. Hii ina maana kwamba kwa sasa Mukoko anaangukia kuwa chaguo la nne katika orodha ya viungo wa chini achilia mbali Fei Toto anayejitanua peke yake pale mbele.

Tatizo kubwa zaidi kwa Mukoko limekuja baada ya Yanga kuamua kuongeza fundi mwingine katika eneo la kiungo. Salum Abubakar ‘Sure’ Boy ambaye naye ana utulivu mkubwa wa mpira mguuni kuliko Mukoko. Na hii inamaanisha kwamba Mukoko anakuwa chaguo la tano katika eneo la kiungo.

Haishangazi kuona watu wa Yanga wala hawashtuki kuona mkataba wa Mukoko umebakiza miezi mitano Yanga na hakuna anayejali. Umewahi kusikia mitandaoni watu wa Yanga wakiwa na hofu kwamba huenda Mukoko akaondoka klabuni kwao?

Umewahi kusoma mahala mashabiki wakisisitiza kwamba lazima waendelee kuwa na Mukoko? Umewahi kuona watu wa Yanga wakiwa na hofu kwamba huenda Mukoko ataenda Simba? wakati ule walikuwa na hofu wakati Simba walipoanzisha uvumi mitandaoni kwamba wanataka kuinasa saini yake.

Kumbe wakati ule ulikuwa wakati ule. Leo Yanga watakuw ana hofu zaidi ukiwaambia Simba wanamnyemelea Bangala au Aucho. Huu ndio ukweli. Hizi ndio alama za nyakati ambazo Mukoko analazimika kuzikubali. Kila kitabu na zama zake.

Naamini mwisho wa msimu huu Mukoko hatakuwa mchezaji wa Yanga. Lakini naamini pia kwamba endapo akisaini Simba au Azam bado mashabiki wa Yanga hawataulaumu uongozi wao ingawa ni kweli kwamba wanampenda mchezaji huyu. Ni kipenzi chao kikubwa.

Tatizo ni alama za nyakati. Sasa hivi Yanga inatembea yenyewe. Wachezaji upoteza umuhimu kikosini pindi wanapokuja wachezaji wengine muhimu zaidi. zipo nyakati ambazo Simba walikuwa wanamuona Shiza Kichuya kama staa mkubwa, lakini alipokuja Luis Miquissone wakajikuta wakitembea zaidi na kuachana na kina Kichuya.

Wakati mwingine huwa inatokea lakini kitu muhimu zaidi ni kuangalia maslahi ya timu. Ipo siku ambayo hata Aucho mwenyewe atapoteza umuhimu pindi atakapokuja mchezaji mkali zaidi yake. Labda kama hatakuja mkali zaidi yake ndipo ambapo ataendelea kuimbwa.

Karibu kwa Maoni
Katika mfumo mukoko ameshindwa ku suit.

Ulitaka Mkataba wake uishe aende timu nyingine bure.?
 
Ukweli ni kwamba Mukoko ni mchezaji mgumu na anayejituma zaidi uwanjani. Tatizo ni kwamba umiliki wake wa mpira hauko vizuri. Mguso wake wa kwanza wa mpira sio mzuri kulinganisha na Aucho na Bangala. Mbaya zaidi ni kwamba Mauya ni mzuri zaidi katika umiliki wa mpira kuliko Mukoko. Tatizo la Mauya ni kwamba labda hajitumi sana uwanjani.

Kama ambavyo Mukoko na Mauya waliingia moja kwa moja katika kikosi cha kutokana na aina ya wachezaji waliowakuta basi ndivyo ambavyo Aucho na Bangala wameingia moja kwa moja katika kikosi cha kwanza kutokana na aina ya wachezaji waliowakuta.

Mauya amekuwa akicheza kutokana na kuwa mbele ya Mukoko kwa utulivu kwa mpira mguuni. Naambiwa kwamba kocha Nasreddine Nabi anamkubali zaidi. Hata hivyo bahati yake ya kuchezwa imechangiwa pia na uwezo wa Bangala kucheza nafasi nyingi tofauti, lakini pia majeraha ambayo yamekuwa yakiisumbua safu ya ulinzi ya Yanga.

Anapoumia beki yeyote wa kati wa Yanga, Bangala anarudi kucheza nyuma na kuwapisha Mauya na Aucho wacheze eneo la kiungo. Walipokosekana mabeki wote wa kulia wa Yanga, Djuma Shaban na Shomari Kibwana, basi Dickson Job amesogea kulia na Bangala amerudi kuwa mlinzi wa kati akicheza na Mwamunyeto.

Hata hivyo bado nafasi inakwenda kwa Mauya kucheza sambamba na Aucho. Na ni kweli kwamba Mauya ameitendea haki nafasi hiyo kwa kiasi kikubwa. Hii ina maana kwamba kwa sasa Mukoko anaangukia kuwa chaguo la nne katika orodha ya viungo wa chini achilia mbali Fei Toto anayejitanua peke yake pale mbele.

Tatizo kubwa zaidi kwa Mukoko limekuja baada ya Yanga kuamua kuongeza fundi mwingine katika eneo la kiungo. Salum Abubakar ‘Sure’ Boy ambaye naye ana utulivu mkubwa wa mpira mguuni kuliko Mukoko. Na hii inamaanisha kwamba Mukoko anakuwa chaguo la tano katika eneo la kiungo.

Haishangazi kuona watu wa Yanga wala hawashtuki kuona mkataba wa Mukoko umebakiza miezi mitano Yanga na hakuna anayejali. Umewahi kusikia mitandaoni watu wa Yanga wakiwa na hofu kwamba huenda Mukoko akaondoka klabuni kwao?

Umewahi kusoma mahala mashabiki wakisisitiza kwamba lazima waendelee kuwa na Mukoko? Umewahi kuona watu wa Yanga wakiwa na hofu kwamba huenda Mukoko ataenda Simba? wakati ule walikuwa na hofu wakati Simba walipoanzisha uvumi mitandaoni kwamba wanataka kuinasa saini yake.

Kumbe wakati ule ulikuwa wakati ule. Leo Yanga watakuw ana hofu zaidi ukiwaambia Simba wanamnyemelea Bangala au Aucho. Huu ndio ukweli. Hizi ndio alama za nyakati ambazo Mukoko analazimika kuzikubali. Kila kitabu na zama zake.

Naamini mwisho wa msimu huu Mukoko hatakuwa mchezaji wa Yanga. Lakini naamini pia kwamba endapo akisaini Simba au Azam bado mashabiki wa Yanga hawataulaumu uongozi wao ingawa ni kweli kwamba wanampenda mchezaji huyu. Ni kipenzi chao kikubwa.

Tatizo ni alama za nyakati. Sasa hivi Yanga inatembea yenyewe. Wachezaji upoteza umuhimu kikosini pindi wanapokuja wachezaji wengine muhimu zaidi. zipo nyakati ambazo Simba walikuwa wanamuona Shiza Kichuya kama staa mkubwa, lakini alipokuja Luis Miquissone wakajikuta wakitembea zaidi na kuachana na kina Kichuya.

Wakati mwingine huwa inatokea lakini kitu muhimu zaidi ni kuangalia maslahi ya timu. Ipo siku ambayo hata Aucho mwenyewe atapoteza umuhimu pindi atakapokuja mchezaji mkali zaidi yake. Labda kama hatakuja mkali zaidi yake ndipo ambapo ataendelea kuimbwa.

Karibu kwa Maoni
Chini ya Nabii tulitolewa mzunguko wa kwanza wa club bingwa Afrika, tumeshapoteza kombe la mapinduzi, sasa tunasubiria ligi. Kuondoka kwa Mkoko kuna nipa pichwa kuwa huenda mwalimu naye ni kimeo.Hoja itatolewa kuwa tunaongoza ligi, hata wakati tunamtegemea Sarpong kama mshambuliaji wetu muhimu tuliongoza ligi kwa muda mrefu. Kwa wachezaji ambao GSM kasajili, hata timu angepewa Meki Meksime, bado angeweza kuongoza ligi.
Nabi inabidi afanye jambo kuthibitisha ubora wake, nalo ni kuleta makombe.
 
Katika mfumo mukoko ameshindwa ku suit.

Ulitaka Mkataba wake uishe aende timu nyingine bure.?
Uko sahihi. Mukoko alifanya vizuri enzi za akina Kaze. Kiukweli alikuwa akikosekana, na timu inayumba!

Na hii ni baada ya enzi za Mwinyi Zahera kumtumia sana Fei Toto kama kiungo mkabaji! Ila baada ya kuja Mukoko, eneo la namba 6 lilipata mtu sahihi, na Fei Toto alipanda mbele.

Ila tangu aje Profesa Nabi, na usajili wa viungo wengine kama Aucho, Bangala, Sure Boy, na uwepo wa Fei Toto na Saido Ntibazonkiza! wamelifanya eneo la kiungo kuwa na viungo wengi!

Nadhani kwa mchezaji aina ya Mukoko Tonombe, isingekuwa busara kuendelea kuwa chaguo la pili. Hivyo kwenda timu kubwa kama TP Mazembe, ni jambo la heri kwake. Wananchi tunamtakia maisha mema kwenye klabu yake mpya. Na hakika tutammiss sana.
 
Chini ya Nabii tulitolewa mzunguko wa kwanza wa club bingwa Afrika, tumeshapoteza kombe la mapinduzi, sasa tunasubiria ligi. Kuondoka kwa Mkoko kuna nipa pichwa kuwa huenda mwalimu naye ni kimeo.Hoja itatolewa kuwa tunaongoza ligi, hata wakati tunamtegemea Sarpong kama mshambuliaji wetu muhimu tuliongoza ligi kwa muda mrefu. Kwa wachezaji ambao GSM kasajili, hata timu angepewa Meki Meksime, bado angeweza kuongoza ligi.
Nabi inabidi afanye jambo kuthibitisha ubora wake, nalo ni kuleta makombe.
Hao walio chukua kombe la mapinduzi wapo wapi?
 
Sawa ni kweli.

Lakini mukoko ni mchezaji anayekupa matokeo ya unachotafuta muda wowote ule yuko tayari kupambana alitusaidia Sana tulipokuwa wabovu.

Leo tumewapata kina aucho ambaye Lila Mwezi anaomba likizo kwenda kwao.

Hatukatai aucho ni mzuri Sana lakini ni heri pia kuwaacha wachezaji wanaoipenda team na wenye moyo muda wote.

Zawadi haaminiki leo atacheza kesho anaamka vibaya back pass kama zote.
Tulipokuwa wabovu. Kwa sasa timu ipo vizuri. Masharti ya Mukoko alidai yupo tayari kusaini lakini ahakikishiwe namba kikosi cha kwanza,
Kwa Nabi haiwezekani. Pia anatumia nguvu sana hivyo kujisababishia injuries na yellow cards. Risk kwa team. Namkumbuka sana Mukoko.
Kila laheri TP Mazembe.
 
Back
Top Bottom