ni ngumu
JF-Expert Member
- Sep 25, 2016
- 4,293
- 7,154
Kama mwanamke inanikera kuona wanawake wanatumiwa na kudhihakiwa juu wakati wahusika wengine wapo huru kuzidi kuvuruga.Hivi umeshaona hata uzi mmoja umeandikwa akidhihakiwa mwanaume kwasababu ni single father?Zaidi ya uzi kila kukicha akitukanwa single mother wakati mwanaume anahusika na hasemwi!!Sasa nimtetee kwa lipi wakati dhambi zote anapewa single mother?
Mwanaume hawezi kupata dhihaka yeyote sababu sio victim....
Eleweni kitu kimojA baba zenu hawakuwa wajinga kuwalinda nyie zaidi kuliko watoto wa kiume..
Jamii haikufanya ujinga kumlinda mwanamke kuliko mwanaume..
Ifike mahali mkubali ngono zembe na za kipuuzi puuzi ni risk sana kwa mwanamke kuliko mwanaume.Huu ukweli muukubali...
Ukiniletea hoja ya mwanaume mmoja anazAlisha wanwake 5 na kuwatelekeza.Mimi nitakwambia ni sawa tu kwenye akili yake sababu hamna chochote kinachobadilika kwenye mwili wake au maisha yake.Upuuzi wake madhara yake hayaonekani kwa mda huo,m.Sasa wewe upuuzi wako wa kushika mimba bila ndoa tena na kisharobaro ili upate watoto wazuri,madhara yake je?Nayo yamejifichA au...
Mwanaume mmoja wanawake 10 na wewe unajikuta mfuasi wa haki sawa.Unakuwa nao wanaume watatu huna habari.Safi sana mwanaume anakuangalia anakuchora tu unavyojibu msg kiwiziwizi anakuchunia tu sasa ulivyompuuzi unashika mimba ukitarajia kuna mwanaume ataikubali thubutuuuuu..Hapo ndo utaelewa vzr mchezo ulikuwa unacheza ni wakipuuzi..
Be smart ukiamua kuingia kwenye mapenzi tena be smart kweli kweli maana mchezo unaoingia kucheza ni mgumu kwako kuliko unavyodhani.Utakula ngumi za uso za kutosha ujikute umezeeka wakati wanawake wenzako wapo busy ku enjoy maisha..