Kwanini mlikataa Kikwete kuitwa dhaifu?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,260
33,857
Kama Rais John Magufuli anasifiwa kwa kuchukua maamuzi ambayo watangulizi wake walishindwa kuchukua na pia anasifiwa kwa kufanya yale ambayo watangulizi wake walishindwa kufanya. NI kwa nini basi kina John Mnyika walipokuwa wanasema Kikwete ni dhaifu kwa kushindwa kuchukua hatua kwa uharibifu uliofanywa na Mtangulizi wake Mkapa walishutumiwa?

Kwa haya yanayofanywa na Magufuli kama vile kufukuza wafanyakazi hewa, kutaka kubadili mikataba ya madini, kufuta safari za nje, na mengine mengi si dalili kwamba mtangulizi wake alilea mambo yasiyofaa kwa nchi yetu? Wale waliokuwa wanamtetea Kikwete kwamba si dhaifu leo hii bado wanamtetea angalau kwa maneno tu? CCM ina watu wasio na msimamo kabisa!

Si kwamba kuwa Kikwete hana mambo mema alipokuwa Rais. Kwa mfano aliachilia watu wafanye walichoona kinafaa mradi hawavunji sheria, aliendesha siasa za uchangamano, alijenga haiba ya ushirika kitaifa na kimataifa. Bila shaka kwa haya wapo pia wanaomkumbuka!!
 
Mkuu unafki unaimaliza sana nchi yetu kipindi wanatoka povu wapinzani kuwa kikwete ni dhaifu na uongozi umemshinda ikapelekea hadi mnyika kutimuliwa bungeni watu walitukejeli sana ooh sijui tukaitwa wadini, tukaitwa tuna wivu sijui tunataka juisi za ikulu na mengine yenye dhihaka sasa cha kushangaza leo hii kila mwana ccm anasema AWAMU IMEBADILIKA SERIKALI SIO DHAIFU TENA!!! Sasa tuwaeleweje wamabadilila badilika kma vinyonga

Nilitegemea ndugai atamuomba msamaha mnyika kwa kumtimua bungeni kumbe alikuwa ametoa unabii ambao leo nchi nzima wameugundua.... nachojua hta awamu ijayo wanaccm hawa hawa wanaomsifia magufuli watasema AWAMU YA SITA IMELETA MABADILIKO SIO YA KIDIKTETA TENA!!!!

Doublestandards zinashangaza nchii hii
 
Vyama vyetu hivi na hasa CCM imewajengea hofu viongozi na hasa wabunge ya kutokukosoa chama na hasa kiongozi mkuu wa nchi. Hii imewafanya kuwa watumwa wa fikra huru, hawawezi kwenda kinyume na maoni na sera za chama hata kama zinaingamiza taifa.

Wanapoitana kwenye vikao vya chama, hulazimika kutanguliza maslahi ya chama na si wananchi. Humfanya kiongozi mkuu wa nchi mungumtu asiyekosolewa hata kama anaitumbukiza nchi shimoni e.g. Mswaada wa sheria ya mafuta na Gas waliolazimishwa kupitisha usiku wa manane, mradi Kikwete atoke madarakani huku akiwa ameisaini. Hata baada ya wapinzani wao ku protest na kutoka bungeni hakuna aliyejali.

Napendekeza mihimili yetu mitatu iwe na vyombo vya juu ili kuvidhibiti kutenda kwa uwajibikaji na kizalendo badala ya kuamua na kupitisha mambo kisiasa zaidi na kukumbatia udhaifu wa kiongozi.
 
Kama Rais John Magufuli anasifiwa kwa kuchukua maamuzi ambayo watangulizi wake walishindwa kuchukua na pia anasifiwa kwa kufanya yale ambayo watangulizi wake walishindwa kufanya. NI kwa nini basi kina John Mnyika walipokuwa wanasema Kikwete ni dhaifu kwa kushindwa kuchukua hatua kwa uharibifu uliofanywa na Mtangulizi wake Mkapa walishutumiwa?

Kwa haya yanayofanywa na Magufuli kama vile kufukuza wafanyakazi hewa, kutaka kubadili mikataba ya madini, kufuta safari za nje, na mengine mengi si dalili kwamba mtangulizi wake alilea mambo yasiyofaa kwa nchi yetu? Wale waliokuwa wanamtetea Kikwete kwamba si dhaifu leo hii bado wanamtetea angalau kwa maneno tu? CCM ina watu wasio na msimamo kabisa!

Si kwamba kuwa Kikwete hana mambo mema alipokuwa Rais. Kwa mfano aliachilia watu wafanye walichoona kinafaa mradi hawavunji sheria, aliendesha siasa za uchangamano, alijenga haiba ya ushirika kitaifa na kimataifa. Bila shaka kwa haya wapo pia wanaomkumbuka!!


Siyo CCM tu hata wengi ya wananchi wasio na vyama hawajitambui. We need uprising ya nguvu kushikisha adabu hawa viongozi wapuuzi waliotuibia.
 
Kama Rais John Magufuli anasifiwa kwa kuchukua maamuzi ambayo watangulizi wake walishindwa kuchukua na pia anasifiwa kwa kufanya yale ambayo watangulizi wake walishindwa kufanya. NI kwa nini basi kina John Mnyika walipokuwa wanasema Kikwete ni dhaifu kwa kushindwa kuchukua hatua kwa uharibifu uliofanywa na Mtangulizi wake Mkapa walishutumiwa?

Kwa haya yanayofanywa na Magufuli kama vile kufukuza wafanyakazi hewa, kutaka kubadili mikataba ya madini, kufuta safari za nje, na mengine mengi si dalili kwamba mtangulizi wake alilea mambo yasiyofaa kwa nchi yetu? Wale waliokuwa wanamtetea Kikwete kwamba si dhaifu leo hii bado wanamtetea angalau kwa maneno tu? CCM ina watu wasio na msimamo kabisa!

Si kwamba kuwa Kikwete hana mambo mema alipokuwa Rais. Kwa mfano aliachilia watu wafanye walichoona kinafaa mradi hawavunji sheria, aliendesha siasa za uchangamano, alijenga haiba ya ushirika kitaifa na kimataifa. Bila shaka kwa haya wapo pia wanaomkumbuka!!

Jambo la ajabu alipongia bungeni hivi karibuni JK alishangiliwa na kuambiwa "we miss you"
Hata wapinzani wanamkumbuka Mr dhaifu!.Usihofu kwa yote haya, hii ndo miujiza ya siasa
 
Siyo CCM tu hata wengi ya wananchi wasio na vyama hawajitambui. We need uprising ya nguvu kushikisha adabu hawa viongozi wapuuzi waliotuibia.
Lakini wapinzani waseme nini wakati wao wapo wachache? Kila mwaka ni watanzania husikika wakisema wapinzani hawajakomaa kushika nchi, cha ajabu hao waliokomaa ndiyo hao kila siku wanatutengeneza uoza unaolenda harufu ya uvundo wa ufisadi kwenye jamii yetu. Inawezekana CCM imekomaa kwenye kufanya ufisadi na vitisho kiasi kwamba wananchi wanaiogopa?
 
Kama Rais John Magufuli anasifiwa kwa kuchukua maamuzi ambayo watangulizi wake walishindwa kuchukua na pia anasifiwa kwa kufanya yale ambayo watangulizi wake walishindwa kufanya. NI kwa nini basi kina John Mnyika walipokuwa wanasema Kikwete ni dhaifu kwa kushindwa kuchukua hatua kwa uharibifu uliofanywa na Mtangulizi wake Mkapa walishutumiwa?

Kwa haya yanayofanywa na Magufuli kama vile kufukuza wafanyakazi hewa, kutaka kubadili mikataba ya madini, kufuta safari za nje, na mengine mengi si dalili kwamba mtangulizi wake alilea mambo yasiyofaa kwa nchi yetu? Wale waliokuwa wanamtetea Kikwete kwamba si dhaifu leo hii bado wanamtetea angalau kwa maneno tu? CCM ina watu wasio na msimamo kabisa!

Si kwamba kuwa Kikwete hana mambo mema alipokuwa Rais. Kwa mfano aliachilia watu wafanye walichoona kinafaa mradi hawavunji sheria, aliendesha siasa za uchangamano, alijenga haiba ya ushirika kitaifa na kimataifa. Bila shaka kwa haya wapo pia wanaomkumbuka!!
Makada wa CCM maarufu wamekiri hadharani kwamba waliona udhaifu huu lakini walishindwa kuuongelea.Mmoja alisema wazi, "tungeanzia wapi,"kwa maana walikuwa wamezibwa midomo kwa kuwa jambo hili lilikuwa la wakubwa.Kiukweli tumeibomoa CCM kwa mikono yetu wenyewe.
 
Lakini wapinzani waseme nini wakati wao wapo wachache? Kila mwaka ni watanzania husikika wakisema wapinzani hawajakomaa kushika nchi, cha ajabu hao waliokomaa ndiyo hao kila siku wanatutengeneza uoza unaolenda harufu ya uvundo wa ufisadi kwenye jamii yetu. Inawezekana CCM imekomaa kwenye kufanya ufisadi na vitisho kiasi kwamba wananchi wanaiogopa?


Yote uliyosema yanawezekana.
 
Kama Rais John Magufuli anasifiwa kwa kuchukua maamuzi ambayo watangulizi wake walishindwa kuchukua na pia anasifiwa kwa kufanya yale ambayo watangulizi wake walishindwa kufanya. NI kwa nini basi kina John Mnyika walipokuwa wanasema Kikwete ni dhaifu kwa kushindwa kuchukua hatua kwa uharibifu uliofanywa na Mtangulizi wake Mkapa walishutumiwa?

Kwa haya yanayofanywa na Magufuli kama vile kufukuza wafanyakazi hewa, kutaka kubadili mikataba ya madini, kufuta safari za nje, na mengine mengi si dalili kwamba mtangulizi wake alilea mambo yasiyofaa kwa nchi yetu? Wale waliokuwa wanamtetea Kikwete kwamba si dhaifu leo hii bado wanamtetea angalau kwa maneno tu? CCM ina watu wasio na msimamo kabisa!

Si kwamba kuwa Kikwete hana mambo mema alipokuwa Rais. Kwa mfano aliachilia watu wafanye walichoona kinafaa mradi hawavunji sheria, aliendesha siasa za uchangamano, alijenga haiba ya ushirika kitaifa na kimataifa. Bila shaka kwa haya wapo pia wanaomkumbuka!!
Pamoja na hoja zako ambazo ni negative na positive bado huwezi kumuita Kiongozi wa Serikali, Mkuu wa Nchi,Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama kuwa ni Dhaifu.

Kuyaita maamuzi magumu anayoyafanya Dr John Magufuli ni dhana ya kimtizamo tu.
 
Makada wa CCM maarufu wamekiri hadharani kwamba waliona udhaifu huu lakini walishindwa kuuongelea.Mmoja alisema wazi, "tungeanzia wapi,"kwa maana walikuwa wamezibwa midomo kwa kuwa jambo hili lilikuwa la wakubwa.Kiukweli tumeibomoa CCM kwa mikono yetu wenyewe.
Kuzibwa mdomo ni unafiki
 
Ninalia tu nikiona mambo yalivyo hapa Qatar yenye watu 2.7milioni na laki saba ninalia tu
 
Pamoja na hoja zako ambazo ni negative na positive bado huwezi kumuita Kiongozi wa Serikali, Mkuu wa Nchi,Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama kuwa ni Dhaifu.
Kuitwa kiongozi wa nchi dhaifu ni mtazamo tu, kwa nini iwe nongwa!
 
Back
Top Bottom