Kwanini mke haelewani na wifi?

pascaldaudi

JF-Expert Member
Mar 25, 2009
534
96
Wadau ni suala ambalo mie limenisumbua kidogo. Kwa nini wake huwa hawaelewani na wifi zao? Je ni ujinga wa wake? au? Yaani wakati mwingine unaweza kuta mke ni msomi anashindwa kuelewana na wifi zake ambao either ni wadogo au wakubwa hawajaenda shule, why? mwenye experience.
 
Shida zipo pande zote; wadada ambao wannashindwa kuwa-let go kaka zao na kukubali kuwa wameanzisha familia zao.

Kaka (mume) ambaye hana msimamo na hajui what is the right thing to do.

Na Wifi (mke) mbinafsi ambaye hataki ndugu wa mwanaume wawe karibu na mumewe.
 
Ndo mie sitaki wanizoee kabisa
Kwa nini hutaki wakuzoee? Hujui hao wifi zako ni damu moja na mumeo? hii ni kwa mazingira ya kiafrica. Najua nchi za ulaya wao hawana kabisa uhusiano, tena wakati mwingine hata wazazi huwa mtoto akishakua basi hawana muda wa kuwa karibu hata kama mmoja anaishi manzese mwingine ubungo wanaweza kata miaka bila hata hamu ya kuonana. Ila africa siyo hivyo.
 
Ila inakera sana. Bora mtu kutokuoa. Kama wewe hujaoa, mpe exam mkeo ya kuwazoea dada zako.
 
nashukuru Mungu mie na mawifi zangu tunapatana sana, hata mama mkwe pia tunaelewana.
 
Wifi zangu (wake wa kaka zangu) ni rafiki zangu sana hata watu hawaamini ni wifi zangu.
Wifi zangu (dada wa mume) wamegawanyika wapo ambao ni wakorofi na wapo ambao ni rafiki. Wakorofi wanajulikana na njia rahisi kukwepa ugomvi nao ni kuwa mbali nao.
 
Mtu ataacha baba yake na mama yake na kuambatana na mke/mume wake...period!!!!!sasa hapo wifi anatoka wapi kwenye ndoa ya kaka yake? kwa andiko lipi?....ushetani usioonekana kwa kivuli cha ndugu.

Wadau ni suala ambalo mie limenisumbua kidogo. Kwa nini wake huwa hawaelewani na wifi zao? Je ni ujinga wa wake? au? Yaani wakati mwingine unaweza kuta mke ni msomi anashindwa kuelewana na wifi zake ambao either ni wadogo au wakubwa hawajaenda shule, why? mwenye experience.
 
Mtu ataacha baba yake na mama yake na kuambatana na mke/mume wake...period!!!!!sasa hapo wifi anatoka wapi kwenye ndoa ya kaka yake? kwa andiko lipi?....ushetani usioonekana kwa kivuli cha ndugu.

Nadhani wewe ndiye huelewi kwani Yesu Kristu alisisitiza upendo kwa watu wote. Unapomchukia mtu kwa kisingizio cha ndoa si kuwa mtakosa tu baraka bali pia hamuwezi kustawi kiroho (awe muislamu au mkristu).
 
Nadhani wewe ndiye shetani kwani Yesu Kristu alisisitiza upendo kwa watu wote. Unapomchukia mtu kwa kisingizio cha ndoa si kuwa mtakosa tu baraka bali pia hamuwezi kustawi kiroho (awe muislamu au mkristu).

Upendo wa chuki ni sawa na wakati wa kwenda,huko ni kupotea. Upendo furaha na amani, ni sawa na wakati wa kurudi, huko ni kuijua kweli ambayo ndiyo njia....Haya upendo upi huo usio vitendo, Agape, Essos, Phileo,au ule wa Sect?

 
Ila mkuu unaji-contradict mwenyewe. Wewe umeleta uzi acha sisi wadau tuujadili ili ufunguke na kupata mawazo tofauti humu jamvini.

Wadau ni suala ambalo mie limenisumbua kidogo. Kwa nini wake huwa hawaelewani na wifi zao? Je ni ujinga wa wake? au? Yaani wakati mwingine unaweza kuta mke ni msomi anashindwa kuelewana na wifi zake ambao either ni wadogo au wakubwa hawajaenda shule, why? mwenye experience.
 
Pole sana mkuu.

Mara nyingi watu hawa ni ngumu kupatana sana.. (Big reason ni wivu) hasa kwa wale wakubwa na ni kimeo sana kama hawajaolewa.

Yani dada wanashindwa kuelewa kuwa kaka yao ameoa na kwamba kuna mipaka ya kumwa access na ukitaka hali iwe ngumu zaidi ni pale unapo mwignore wife..

Pia kama wife anajipendelea sana talk to her atambue kuwa hao ni wadogo zako na kwa njia moja au nyingine they deserve something from u.

Be very carefull n wise, usiruhusu dada wa run nyumba yako (kundi hili ni mojawapo ya watu wanaoharibu sana ndoa za watu hasa kama baba mwenye nyumba asipokaa kwenye nafasi yake vyema) Kama kuna ishu inayowahusu wao jadili na mkeo kwanza.

Pia kupunguza tatizo wasizoeana yani kila mtu awe na maisha yake.. Kama ni wadogo wanahitaji msaada wasaidiwe wakiwa kwa wazazi au boarding school.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Ila mkuu unaji-contradict mwenyewe. Wewe umeleta uzi acha sisi wadau tuujadili ili ufunguke na kupata mawazo tofauti humu jamvini.

Nimekupata, ila sema nahamasika kuchangia pale ambapo naona sababu iliyotolewa na mchangiaji inakiuka misingi ya ukweli ktk nyanja zote za tamaduni za ubinaadamu. Karibu endelea kuchangia!
 
Pole sana mkuu.

Mara nyingi watu hawa ni ngumu kupatana sana.. (Big reason ni wivu) hasa kwa wale wakubwa na ni kimeo sana kama hawajaolewa.

Yani dada wanashindwa kuelewa kuwa kaka yao ameoa na kwamba kuna mipaka ya kumwa access na ukitaka hali iwe ngumu zaidi ni pale unapo mwignore wife..

Pia kama wife anajipendelea sana talk to her atambue kuwa hao ni wadogo zako na kwa njia moja au nyingine they deserve something from u.

Be very carefull n wise, usiruhusu dada wa run nyumba yako (kundi hili ni mojawapo ya watu wanaoharibu sana ndoa za watu hasa kama baba mwenye nyumba asipokaa kwenye nafasi yake vyema) Kama kuna ishu inayowahusu wao jadili na mkeo kwanza.

Pia kupunguza tatizo wasizoeana yani kila mtu awe na maisha yake.. Kama ni wadogo wanahitaji msaada wasaidiwe wakiwa kwa wazazi au boarding school.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
neggirl, nimekuelewa. Ila sasa chanzo cha chuki ndiyo mi nashindwa kuelewa. Mimi kama mwanaume unaweza kukuta nawapenda sana wadogo za mke wangu, wawe wa kike au kiume. Ila kwa wanawake hii inakuwa tabu. Mfano, kama mke akijua unawasaidia wadogo zako haswa wa kike roho inamuuma sana, tena anakuwa anaona eti hatuwezi wasaidia wote, anakuwa na ile roho mbaya ile mbaya ya kutu kabisa. Sasa mi kinachonitatiza, kwa nini wawe vile?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom