Kwanini mitihani ya matabibu tu? Mbona ya wauguzi nayo ilivuja na hakuna hatua zilizochukuliwa?

Cashman

JF-Expert Member
Jun 8, 2018
2,293
3,965
Kwanza niwapongeze wale wote walioamua kuwa uchunguzi ufanywe ili kubaini wizi wa mitihani uliotokea kwa watahiniwa wa utabibu. Naamini hatua kali zitachukuliwa dhidi ya wahusika kwani imekuwa kawaida yao kufanya kitendo hiki kwa muda mrefu.

Pamoja na hayo yote, naomba kuuliza, je kwa nini upande wa uuguzi hakuna uchunguzi wowote unaofanyika wakati mitihani yao ilivuja vile vile kama ya utabibu?

Nashauri udhibiti uwe mkubwa kwani hii si mara ya kwanza na imekuwa mazoea hasa kwa kada ya utabibu, ambapo karibu kila mwaka mitihani inavuja na hakuna hatua yoyote inayochukuliwa.
 
Uuguzi ni fani ya kiboya mkuu, nurse mwenye diploma na tabibu mwenye diploma..lakini utashangaa uongozi wa kusimamia kituo anapewa tabibu hata kama ana cheti tu ( certificate) na hawa wote yaani nurse na tabibu wanasoma module ya leadership hii kozi inachukuliwa kama vile ni useless.
 
Una maanisha UE kwa watu wanaosoma medicine imevuja? how can that be possible!
 
Ndio maana utakuta mtu ni mtaalamu wa fani fulani ukimuuliza yahusuyo fani yake hajui kitu, kumbe alifaulu kijanjanja tu akapata ajira, kituko zaidi kiko kwa walimu, wengi wao si wajuzi wa kazi wanazozifanya, ni wababaishaji tu
 
Back
Top Bottom